Maleven

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2019
Posts
689
Reaction score
3,373
  • Uzi huu ni mrefu.
  • Ukichangia naomba ujikite Zaidi katika kutoa maoni yako lakini kukosoa kunaruhusiwa.
Binafsi nadhani maamuzi haya yangechukuliwa mwezi mmoja uliopita pale Waziri Mkuu alipotangaza kuzifunga shule na vyuo, lakini haikuwa hivyo badala yake shule zilifungwa kisha hakukuwa na mpango mkakati madhubuti wa kukabiliana na COVID-19, Zaidi ya makatazo ya kuepuka mikusanyiko na kunawa mikono na maombi. Lakini huu sio muda wa kuendelea kulaumiana zaidi ni wakati wa kupeana mawazo na kushauriana.

Pia bado naamini athari za kiafya kama watakaofariki kutokana na Virusi hivi bado watakuwa wachache kuliko watakaoathirika kutokana na athari za kuwepo ugonjwa huu haswa suala la uchumi na elimu. Hivyo ni lazima kuwe na mpango mkakati wa haswa kuhakikisha kuwa baada ya muda fulani tuwe tumefikia jambo Fulani.

Anyway, binafsi kama ningekuwa na mamlaka ningetumia njia hii kutatua tatizo la hili |Ushauri wangu.

  • Kwanza ni lazima kila mmoja ( Serikali na wananchi kwa ujumla) kuwa na fikra ya kutatua tatizo na siyo kutengeneza faida, waswahili husema hasara roho, pesa makaratasi na zinatafuwa, huu ni wakati wa Serikali na wananchi kujua kuwa nchi iko kwenye vita kubwa sana na inapambana na adui wa ajabu asiyeonekana mwenye madhara lukuki ikiwemo kupoteza maisha na hali mbaya ya uchumi, amapo kama Serikali ni lazima iwe tayari kutumia rasilimali zilizopo katika kunusuru Taifa, rasilimali hizi kama fedha na watu na miundombinu
Nini cha kufanya?

  • Serikali inainishe maeneo ambayo yako hatarishi zaidi katika maambukizi ya virusi vya Corona, naamini yako wazi. Maeneo mengi ya mjini yana muingiliano mkubwa wa watu kutokana na shughuli zao za kiuchumi.

  • Baada ya kuanisha maeneo hayo, viongozi wa mtaa na katika maeneo yalioainishwa wapite wachukue idadi ya watu wote katika mtaa husika wakizingatia mambo yafuatayo:-
    • Idadi ya watu katika nyumba husika (hili nimesikia limefanyika maeneo ya Dar sina uhakika.
    • Hali yao ya kiuchumi
    • Kuchukua mawasiliano wa watu wawili waliopo katika nyumba hiyo na kuacha mawasiliano ya viongozi wawili wa mtaa husika.( namba za simu zenye uhakika).

  • Baada ya hatua ya kuainiasha maeneo na kujua wakazi namba ya wakazi husika na hali zao za kimaisha, Serikali ikishirikiana na wadau, waangize bidhaa muhimu kutoka nje( kwenye upungufu) pia kwa wakati huu Serikali inunue au iongoze vifaa vya kupimia Virusi vya corona Viwepo kwa wingi zaidi visambazwe kila wilaya. Kama nilivyosema huu ni wakati wa kutumia rasilimali tulizonazo katika kupamba na janga hili si wakati wa kuanza kuangalia faida.

  • Hatua ya nne ni Serikali kugawa chakula kwa familia zilizo na uchumi duni ambao hawana uwezo wa kuishi kwa siku ishirini na moja wakiwa ndani. Hatua hii inahitaji unaminifu na uadilifu kwa viongozi wa serikali wanaokadiria hali za kiuchumi za wananchi na pia kwa wananchi ambao watakua wanaeleza uhalisia wa maisha yao ili wasiibebeshe serikali mzingo ambao wanauweza, wasiwakoseshe wale wenye uhitaji na wala wasionewe. Watu wanosihi kijijini wengi chakula wanacho, shida walionayo ni hela ya kusagia mahindi, hela ya sukari chunvi na mafuta ya taa.

  • Hatua ya tano Serikali itangaze lockdown kwa siku ishirini na moja (21) . Hapa wananchi wakiwa tayari wana mahitaji muhimu hasa chakula. Katika kipindi hiki.
    • Serikali itumie vyombo vya usalama katika kuhakikisha watu wanafata utaratibu lakini wawe ni wenye kuelewa kuepuka maafa kama yaliotokea nchi nyingine.
    • Tangazo la kuwa lockdown liwe mapema na watu kufanya maandalizi ikiwa ni pamoja na wale watakao pewa msaada mapema
    • Katoka kipindi hiki cha wiki tatu, kodi za biashara, umeme na maji viwe free kwa ambao luku zao zitaisha basi wasizime, pia wakadirie matumizi ya maji ya wiki tatu wasihesabu katika bili ya maji.
    • Mawasiliano ya karibu ya viogozi wa serikali katika kujua kinachoondelea latika kila kaya, hasa kwa dharura ya wagonjwa na mama wajawazito kuweza kupatiwa uduma.
    • Wale wanaotamulika kama homeless na watoto wa mitaani, watafutiwe sehemu ya kuhifadhiwa( nashauri kwenye walo moja la kambi ya jeshi mana watakua na adabu, au watakapo wekwa wasimamiwe na wanajeshi).
    • Mipaka ifungwe kabisa.

  • Wiki ya pili ya lockdown, yaani siku ya kumi na nne (14), serikali ichukue sampuli ya watu wawili au mmoja kutoka katika kila nyumba, nashauri awe yule anaetoka toka sana( mtafutaji) na yule mtu mzima Zaidi au ambao anaumwa. Lengo na madhumuni ni kua,
    • Kwa kipindi cha wiki mbili kama kama mtu alikua na virusi basi atajulikana.
    • Lengo la kuchukua mtu mzima au yule mgojwa ni kua, mwenye virusi anaweza kua yuko na kinga madhubutu hivyo kwa mtu mzima itasaidia hugundulika mapema.
    • Kuchukua watu wawili au hata mmoja kila nyumba kutasaidia kupunguza utumiaji wa rasilimali katika upimaji. Mfano kama idadi ya watu katika kaya yenye nyumba 300 na watu 2000, then tunapima 300 au 600 (kama wakichukua kila nyumba wawili) badala ya watu 2000.
    • Baada ya kuchukua sampuli kutoka katika kila nyumba, kutegemea na siku watakazo tumia. Kasha nyumba zitakazo kutwa na maambukizi watawekwa katika ungalizi( kutotoka au kuwapeleka katika maeneo maalumu yaliotengwa ) na kui disinfect nyumba.
  • Baada ya kuchukua familia zilizokutwa positive, kutegemea na siku zilizotumika kupima na kupata majibu, na kufanya mapendekezo ya namba saba, the tunaweza kufungua shule na shughuli zikaendelea huku tukiendelea na tahadhali, suala la level seat likendelea, kunawa mikono na uvaaji wa barakoa.

  • Katika kipindi chote hicho , Serikali isisite kufanya utafiti katika jamii mbalimbali kwa asili yao kwa jinsi walivyoweza kupambana na magonjwa ya mfumo wa hela ili kuangalia uwezekano wa tiba mbadala.
Haya ni mawazo yangu ya jinsi ninavyoona jinsi gani ya kuweza kupambana na suala hili.

Amani ya Bwana iwe nanyi wote.


---MICHANGO---







Kwa habari zaidi. soma:

Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga - JamiiForums

Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus) - JamiiForums
 
Pitia taarifa za habari za nchi zilizokumbwa na hili tatizo mkuu, ni hatari sana jinsi Corona inavyosambaa kama moto wa nyika. Kuna baadhi ya nchi hata chakula hakuna, watu wamejifungia ndani na vyakula vya miezi kadhaa na hawatoki nje.

Tafakari maisha ya mtu wa kwetu tanzania, anae ishi kwa kiwango cha chini ya "Sh 2,200/= (Under USD 1$)" kwa siku??? Anaweza vipi kujifungia ndani mwezi mzima wakati chakula cha siku moja hana uhakika wa kupata.

Kama mambo gani nliovutia kwangu mkuu?
 
Acha tulipie uzembe uliosabishwa na serikali toka mwanzo ilishindwa kuonyesha reaction yoyote unashindwa funga mipaka kisa watalii nani bora kati ya mwananchi na mtalii pesa ina thamani kuliko uhai wetu

Nb: Serikali imehusika kwa uzembe ktk hili.
 
acha tulipie uzembe uliosabishwa na serikali toka mwanzo ilishindwa kuonyesha react yoyote unashindw funga mipaka kisa watalii nani bora kati ya mwananchi na mtalii pesa ina thaman kuliko uhai wetu
Nb:serikali imehusika kwa uzembe jtk hili.
Je, uzembe wa kuwa na MAABARA moja tu nchi nzima? Mgonjwa akipatikana Bukoba au sehemu yoyote ya nchi, inabidi damu itumwe Dar halafu wasubiri majibu ya vipimo kwa muda usioeleweka.
 
Mbona hujashauri serikali kusitisha malipo ya mikopo ya nje pamoja na matumizi ya fedha kwenye miradi inayoendelea?

Ushauri wangu ni kuisitisha miradi yote na kujihami kwa kuweka pesa zote za nchi kwenye mfuko wa tahadhari. Mambo yakirejea normal tutaendelea na ujenzi.
 
Wakuu ,habarini poleni na majukumu poleni pia na hili janga la corona ,kiufupi mimi niseme corona sio tishio kubwa ila limekuwa overrated,

Ebu kumbuka lile janga la dengue ebu assume dengue ingewapata wazungu au wachina wangekuwa katika hali gani?

Katika kufikiri tu mi nadhani hao mabwana wana weak immune system na pia nadhani dengue is more serious than corona.

Kumbuka hata kipindi cha kujenga railway uko marekani walitumia watu weusi maana ngozi nyeupe they are very weak hata malaralia ambayo asilimia kubwa huku kwetu ni kama homa ya kawaida wenzetu wakipata inakuwa tragedy

Yani corona ni ugonjwa ambao unapata nafuu kwa kujitenga mwenyewe ndani ya siku kadhaa !!! Na pia ni ugonjwa ambao unawakumba wazee sana sana 50+

Wanasema watoto na vijana asilimia kubwa wanaweza hata wasioneshe dalili japokuwa ugonjwa huo wanao mimi nadhani ni kwakua tu maambukizi yake niyakasi na haraka ndo maana umepewa promo ila sio janga kubwa kiivyo cha msingi ni kuzingatia kunawa na sabuni mara kwa mara ,kuvaa mask na gloves ,kuepuka misongamano hutaisha fastaa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waafrika tulifahuru hesabu za kurahisisha tu😂
Ngoja zije za kugawa na kutoa hapo tutajua how serious Corona it is!
 
Yani structure za Virus huwa complicated compared na bacteria na amoeba. Sijui ili kututisha? mstructure wa HIV ulikua unaniboa kuchora Advance.
 
Na Elius Ndabila
0768239284

Ni dhahiri kuwa kwa sasa ugonjwa wa Corona ndio habari ya dunia. Corona imekuwa tishio eneo kubwa la dunia kutokana na kasi yake ya kuenea, madhara yake kwa jamii na tiba yake kutogunduliwa hadi sasa. Ni ugonjwa ambao utaathiri uchumi wa dunia hasa ikizingatiwa kwamba ripoti ya dunia mwaka jana baada ya mkutano uliofanyika Ufaransa ya G7 walisema uchumi unakua kwa asilimia 2.9 na mwaka huu ulikadiriwa kufikia asilimia 3.3 yaani ongezeko la asilimia 0.4.

Hata hivyo Wataalamu wa mambo ya uchumi duniani wanadai kuwa majanga kama mlipuko wa magonjwa ni chanzo kikubwa cha kuzuia kukua kwa uchumi. Wataalamu wanakiri kuwa endapo tiba ya Corona haitatikanika haraka tutegemee mtikikisiko mkubwa wa uchumi duniani.

Ushauri wangu kwa serikali ya Tanzania, pamoja na kuanza kuchukua hatua kali za kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu kwa watu wengi basi inapaswa kuchukua hatua zingine kali za kulinda uchumi wa ndani. Mimi siyo mchumi ninatambua wachumi wanaaeza kuja kunipinga kwa hoja, si mbaya. Ombi langu kwa Serikali ni kuwa isitishe miradi yote mikubwa inayoendelea nchini ambayo haina matokeo ya haraka. Ninaamini miradi mikubwa hasa iliyoshikwa na wageni ingesimamishwa kwanza kupisha ugonjwa huu. Hii inawezekana ikasaidia ku save fedha kuliko sasa wakiendelea hizo fedha watazipeleka nchini kwao na tutakosa fedha za kigeni.

Ninaamini Corona si ugonjwa wa Mungu, ni ugonjwa ambao sababu kubwa ni vita ya kiuchumi na vita ya kushindanisha teknolojia. Kuna vita kubwa kati ya mataifa makubwa duniani. Wakati mwingine ili kudhoofisha uchumi wa nchi nyingine yapo mataifa yanaweza kutengeneza magonjwa ili kufifisha uchumi wa Taifa jingine. Siyo siri kuwa kwa sasa China ndiyo nchi inayofanya biashara kubwa duniania. Unapoivuruga China unaivuruga ni Afrika ambayo inategemea bidhaa toka China. Leo hakuna Mwafrika anayekwenda kuchukua bidhaa China na viwanda vya china havizalishi. Kitakachokwenda kutokea ni mfumuko wa bei na bidhaa mhimu kuadimika. Wakati bidhaa zinaadimika kama hatua ya kustisha miradi mikubwa haitachukuliwa baadae nchi inaweza kosa fedha za kuagizia bidhaa mhimu toka nje kwa kuwa itakosa fedha za kigeni.

Historia ni mwalimu mzuri, hatuwezi kuipuuza. Historia inatukumbusha kwamba Dunia ilishawahi kubwa na mdororo wa uchumi mwaka 1929-1939, na ilianza kimzahamzaha tu. Baadae wakajikuta mabenki yanakosa fedha, maduka yanakosa bidhaa, kukakawa Na mfumuko wa bei n.k.

Ninadhani sasa ni busara wakati wanasayansi hasa madakitari wakipambana kugundua tiba basi Wachumi nao waje washauri mambo ya kuyazingatia katika kulinda uchumi wa ndani.
 
Umetumia busara na hekima ya juu sana katika kutoa ushauri basi nao wataalam wa mambo ya uchumi waliangalie hili kwa kina wasipuuzie mambo yakajirudia ya mwaka 1929_1939

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeongea vyema ingawa sidhani kama wanahitaji ushauri wako...

#HAWAPANGIWI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…