Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Suala kubwa ni kubadili mentality ya watoa huduma wetu, waone kuwa tunahitajiana wote. Si kuwa shirika halina shida bali wateja ndo wanaohitaji shirika zaidi.

Kama ulivyojitokeza na kutoa majibu hapa, inaonyesha utayari wa kutoa huduma kwa mteja. Hongera kwako.

Pamoja na matatizo yetu ya kutojitosheleza kwa mahitaji kutoka kwenye shirika, kutoa jibu mwafaka kwa wakati bila kona kona/njoo kesho/ nenda kwa huyu naye anakurudisha pale au maelezo halisia ni muhimu kwa mhitaji.

Nakuja PM
 
TANESCO ya sasa sio ya zamani na ya kesho inaonesha dira ya mabadiliko makubwa sana kwenye utoaji wa huduma, tunakuhakikishia kuwa kwa huduma zetu zimeboreshwa sana na wateja wamekuwa wakionesha hilo. Hebu twende kwa data au taarifa kamili ya wapi unapendekeza paboreshwe zaidi ili ufurahie huduma zetu
Hakuna kitu tanesco ni ile ile watu tumejaza form kuanzia 2020 na hatujaunganishiwa umeme cha ajabu jirani anajenga hata mwezi bado na umeme unawaka, Bora mkae kimya tu ni vile hakuna mbadala
 
Hakuna kitu tanesco ni ile ile watu tumejaza form kuanzia 2020 na hatujaunganishiwa umeme cha ajabu jirani anajenga hata mwezi bado na umeme unawaka, Bora mkae kimya tu ni vile hakuna mbadala
Tafadhali onesha namba ya simu uliyoandika kwenye maombi yako ya umeme kwa hatua zaidi, Tupo kukuhudumia
 
Je ulijibiwa ambavyo haujaridhika ofisi gani? Nani alikujibu na alikujibuje? Tafadhali tupatie namba yako ya simu na siku uliyojibiwa tufatilie
Mikwala tu[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Police namba moja,mjinga mmoja wa saiba kituo kimoja yaani nimeibiwa Simu anataka laki moja kwanza.....yule nilichukua namba zake pale kwenye shati,dawa yake inachemka......
 
Mikwala tu[emoji16][emoji16][emoji16]
Tunamaanisha TANESCO tupo vizuri na kama unachangamoto yeyote tafadhali ilete tusaidiane kuitatua, TANESCO ni yenu, ni mali ya uma mnawajibu wa msingi wa kuisaidia kuwahudumia vema kwa kutoa taarifa sahihi, ushauri nk
 
TANESCO wafanyakazi wao ni miungu watu kabisa,ni ngumu shirika kupata faida maana watu wake wote ni majizi huku wakishirikiana na vishoka kupata hela........yaani kishoka anakuwa na details zote za ofisini.........
 
Tunamaanisha TANESCO tupo vizuri na kama unachangamoto yeyote tafadhali ilete tusaidiane kuitatua, TANESCO ni yenu, ni mali ya uma mnawajibu wa msingi wa kuisaidia kuwahudumia vema kwa kutoa taarifa sahihi, ushauri nk
Vizuri? Tanesco ni kichefuchefu kabisa
 
Tafadhali onesha namba ya simu uliyoandika kwenye maombi yako ya umeme kwa hatua zaidi, Tupo kukuhudumia
Nimesha fanya hivyo mara kazaa na sijaona mabadiriko,cha kukwambia tu Tanesco pale Chanika magengeni hakuna wanachofanya ukiwa na hela Leo Leo unajaza form na unafungiwa umeme,
 
TANESCO wafanyakazi wao ni miungu watu kabisa,ni ngumu shirika kupata faida maana watu wake wote ni majizi huku wakishirikiana na vishoka kupata hela........yaani kishoka anakuwa na details zote za ofisini.........
Asante sana kwa tuhuma nzuri kwa kuwa zinatusaidia kujua pa kuboresha, tafadhali tujulishe ni wapi, lini na nani alikufanyia hayo? Tafadhali onesha namba yako ya simu tukusikilize

Ushauri wetu unapokutana na viashiria ulivyodai hapo juu toa taarifa kwa uongozi au TAKUKURU hakuna mteja anayepaswa kupata changamoto yeyote ile kwa kulazimishwa kufanya malipo kwenye huduma ambazo ni wajibu wake kuzipata

Ahsante kwa ushirikiano
 
Nimesha fanya hivyo mara kazaa na sijaona mabadiriko,cha kukwambia tu Tanesco pale Chanika magengeni hakuna wanachofanya ukiwa na hela Leo Leo unajaza form na unafungiwa umeme,
Leo utayaona njoo Pm tupo kukusikiliza na kukuhudumia
 
Asante sana kwa tuhuma nzuri kwa kuwa zinatusaidia kujua pa kuboresha, tafadhali tujulishe ni wapi, lini na nani alikufanyia hayo? Tafadhali onesha namba yako ya simu tukusikilize

Ushauri wetu unapokutana na viashiria ulivyodai hapo juu toa taarifa kwa uongozi au TAKUKURU hakuna mteja anayepaswa kupata changamoto yeyote ile kwa kulazimishwa kufanya malipo kwenye huduma ambazo ni wajibu wake kuzipata

Ahsante kwa ushirikiano
Labda wewe ndio unaweza kuwa mfanyakazi Bora Tanesco maana unajibu kwa wakati
 
Nimesha fanya hivyo mara kazaa na sijaona mabadiriko,cha kukwambia tu Tanesco pale Chanika magengeni hakuna wanachofanya ukiwa na hela Leo Leo unajaza form na unafungiwa umeme,
achana naye uyo kwanza ni roboti, pili yuko HQ anakula kiyoyozi, na kutapika nadharia kibao
ilihali uhalisia wa field haujui, huku akibwatuka eti tuko vizuri
 
achana naye uyo kwanza ni roboti, pili yuko HQ anakula kiyoyozi, na kutapika nadharia kibao
ilihali uhalisia wa field haujui, huku akibwatuka eti tuko vizuri
Je unalalamikia nini? Onesha taarifa kamili tukuhudumia

Jina

Eneo

Simu

Wilaya

Hayo mengine hayana haja ya kusema au kuandikwa kwa kuwa hayana tija kwa nchi yetu
 
Nimesha fanya hivyo mara kazaa na sijaona mabadiriko,cha kukwambia tu Tanesco pale Chanika magengeni hakuna wanachofanya ukiwa na hela Leo Leo unajaza form na unafungiwa umeme,
Mkuu Dada yangu mmoja amejenga maeneo yale,alihangaika miezi 6 nikamwambia atumie kirainishi,Laki moja tu...umeme ukaingia ndani ya siku 3, halafu TANESCO anasema tupo vizuri wakati walishaoza kitambo
 
Back
Top Bottom