Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Utumishi wa serikalini ungeekua na target au ajira zote za serikali zingekua na mikataba ya muda (lets say 3 years) huku wakiangalia nini ume deliver, nadhani tungekua mbali sana.
Watumishi wa umma wamejisahau sana kutokana na ajira zao kua permanent, na hata wakikosea kwenye ajira zao wanahamishwa tu eneo la kazi.
Ungeandika haya maandishi kwa herufi kubwa.
 
Mkuu Dada yangu mmoja amejenga maeneo yale,alihangaika miezi 6 nikamwambia atumie kirainishi,Laki moja tu...umeme ukaingia ndani ya siku 3, halafu TANESCO anasema tupo vizuri wakati walishaoza kitambo
Unauhakika alimpa nani? Tafadhali milango ipo wazi akidhibitisha hili hatua zinachukulowa mara moja.

Tuache kutoa tuhuma za uongo ambazo hazina taarifa
 
TANESCO ya sasa sio ya zamani na ya kesho inaonesha dira ya mabadiliko makubwa sana kwenye utoaji wa huduma, tunakuhakikishia kuwa kwa huduma zetu zimeboreshwa sana na wateja wamekuwa wakionesha hilo. Hebu twende kwa data au taarifa kamili ya wapi unapendekeza paboreshwe zaidi ili ufurahie huduma zetu
Hahahahahaha
 
Unauhakika alimpa nani? Tafadhali milango ipo wazi akidhibitisha hili hatua zinachukulowa mara moja.Tuache kutoa tuhuma za uongo ambazo hazina taarifa
Aaah haina haja maana Hela ya sister haitarudi na kifupi alishawekewa umeme within 3days baada ya kutoa hela.....na kazi ilifanyika Kwa speed ya 5G
 
Aaah haina haja maana Hela ya sister haitarudi na kifupi alishawekewa umeme within 3days baada ya kutoa hela.....na kazi ilifanyika Kwa speed ya 5G
Acha kuuaminisha ulimwengu taarifa zisizo na ukweli tena za kusikia hii ni sio sahihi kabisa, kama kweli unataarifa kamili njoo PM tufatilie na haki yake aipate
 
Tunamaanisha TANESCO tupo vizuri na kama unachangamoto yeyote tafadhali ilete tusaidiane kuitatua, TANESCO ni yenu, ni mali ya uma mnawajibu wa msingi wa kuisaidia kuwahudumia vema kwa kutoa taarifa sahihi, ushauri nk
1. Unaweza ukapata emergence Tanesco, mfano meter imezingua, umeme kuwaka na kuzima kutokana na nyaya flan hivi kutokaza ktk waya unaoingiza umeme sehemu ya nyumba. Unaenda kutoa taarifa saa 2 asubuh, ila Tanesco wanakuja usiku, tena hapo unakuwa unapiga simu kweli kweli, unapiga kila baada ya lisaa limoja. Imenikuta saana hii.

2. Unalipia umeme leo, anakuja jirani yako analipia umeme miezi minne mbele au hata mwaka, cha ajabu umeme anaanza kupata yeye kabla yako wewe, na hii michezo mnacheza sn, jina la mtu ktk mita flan anaenda kupewa mwingine (Hii nmeshuhudia mwenyewe) mtu alitoa laki nzima akafanyiwa huu mpango, nna jina la huyo mtu mpaka Staff aliyefanya hiyo kaz, huyo staff na namba zake ninazo.

3. Nikupe hongera kwa kujitokeza kujibu hapa JF changamoto za wadau, ila kuna mda unaonekana boya kwa kutetea upuuzi, eti unamwambia mda ataje kituo na majibu aliyopewa, unauliza hivi kwani hizi changamoto ni ngeni kwenu au? Kukubali makosa ni ujinga? Kwani ukisema tu kuwa hili tatizo lipo na tunaomba radhi kwa yanayotokea lakini punde tutatatua changamoto hii, unapungukiwa nini? Usiwe boyaboya broh. Watu tunalala Dar bila fen kisa upuuzi wenu Tanesco, tunatoa malalamiko lakini hamjali, tunakuja kusema hapa mnajifanya kujitetea.
 
Nimesha fanya hivyo mara kazaa na sijaona mabadiriko,cha kukwambia tu Tanesco pale Chanika magengeni hakuna wanachofanya ukiwa na hela Leo Leo unajaza form na unafungiwa umeme,
Usingemtajia eneo, kwani hawajui basiiii? Si basi tu wapo hapa kujifanya kama wanajali lakini hakuna kitu. Huyo mwenyewe anayejibu hapa bila kumshikisha bahasha hawajibiki.
 
Unauhakika alimpa nani? Tafadhali milango ipo wazi akidhibitisha hili hatua zinachukulowa mara moja.

Tuache kutoa tuhuma za uongo ambazo hazina taarifa
Uongo vipi wakati mtu miezi 6 hakusaidiwa ila kilainishi kikafanikisha ndani ya siku tatu? Admin ukweli unaujua ila unataka kuleta Siasa,kifupi watumishi wenu ni miungu watu na bila HELA huwezi kusaidika.........na huo ndiyo ukweli Vishoka waliojazana nje ya ofisi zenu ndiyo wanapokea hizo Hela Kwa niaba ya waliohuko ndani na hao vishoka wanajua A-Z ya mambo yote ya ndani......kama unaona ni uongo nenda tawi lolote achana na kutype hapo kwenye keyboard kajifanye mteja uone balaa lake
 
Labda wewe ndio unaweza kuwa mfanyakazi Bora Tanesco maana unajibu kwa wakati
Usikute kibarua, vibarua hawana uhakika wa ajira permanent, wanapiga kazi saana hawa. Akipata ajira rasmi hutamuona hapa.
 
1. Unaweza ukapata emergence Tanesco, mfano meter imezingua, umeme kuwaka na kuzima kutokana na nyaya flan hivi kutokaza ktk waya unaoingiza umeme sehemu ya nyumba. Unaenda kutoa taarifa saa 2 asubuh, ila Tanesco wanakuja usiku, tena hapo unakuwa unapiga simu kweli kweli, unapiga kila baada ya lisaa limoja. Imenikuta saana hii.

2. Unalipia umeme leo, anakuja jirani yako analipia umeme miezi minne mbele au hata mwaka, cha ajabu umeme anaanza kupata yeye kabla yako wewe, na hii michezo mnacheza sn, jina la mtu ktk mita flan anaenda kupewa mwingine (Hii nmeshuhudia mwenyewe) mtu alitoa laki nzima akafanyiwa huu mpango, nna jina la huyo mtu mpaka Staff aliyefanya hiyo kaz, huyo staff na namba zake ninazo.

3. Nikupe hongera kwa kujitokeza kujibu hapa JF changamoto za wadau, ila kuna mda unaonekana boya kwa kutetea upuuzi, eti unamwambia mda ataje kituo na majibu aliyopewa, unauliza hivi kwani hizi changamoto ni ngeni kwenu au? Kukubali makosa ni ujinga? Kwani ukisema tu kuwa hili tatizo lipo na tunaomba radhi kwa yanayotokea lakini punde tutatatua changamoto hii, unapungukiwa nini? Usiwe boyaboya broh. Watu tunalala Dar bila fen kisa upuuzi wenu Tanesco, tunatoa malalamiko lakini hamjali, tunakuja kusema hapa mnajifanya kujitetea.
Tunashukuru kwa maelezo mazuri, Tunaendelea kukumbushana kuwa tatizo halitatuliwi au kumalizwa kwa taarifa ambayo haijakamilika, sasa TANESCO tuna mifumo mizuri sana kila kinachofanyika kinaonekana hivyo unapotoa tuhuma onesha wilaya gani, Namba ya simu uliyotolea taarifa, tatizo na namba ya taarifa, Tunataka kukuhakikishia kuwa baadhi ya wateja wetu wamekuwa wakitoa taarifa za uongo (Samahani kuandika hivyo) ukifatilia anasema nilisikia au kuona ukifatilia anashindwa kutoa ushirikiano, Mfano search taarifa ya ajali ya mtoto Kyela ambayo wengi mliandika TANESCO vibaya tukafanya uchunguzi mpaka eneo husika hakuna taarifa mpaka serikali ya mtaa, hivyo tunawahi kuwa wazalendo kwa kuisaidia TANESCO kuwahudumia vema.
 
Acha kuuaminisha ulimwengu taarifa zisizo na ukweli tena za kusikia hii ni sio sahihi kabisa, kama kweli unataarifa kamili njoo PM tufatilie na haki yake aipate
Unadhani ni mm tu niliyewahi kuonja joto la jiwe la shirika letu la Umma? Sina haja ya kuja PM maana hakuna asiyejua uozo wa shirika mkuu...
 
Uongo vipi wakati mtu miezi 6 hakusaidiwa ila kilainishi kikafanikisha ndani ya siku tatu? Admin ukweli unaujua ila unataka kuleta Siasa,kifupi watumishi wenu ni miungu watu na bila HELA huwezi kusaidika.........na huo ndiyo ukweli Vishoka waliojazana nje ya ofisi zenu ndiyo wanapokea hizo Hela Kwa niaba ya waliohuko ndani na hao vishoka wanajua A-Z ya mambo yote ya ndani......kama unaona ni uongo nenda tawi lolote achana na kutype hapo kwenye keyboard kajifanye mteja uone balaa lake
Njoo inbox tafadhali onesha uhalali wa taarifa zako tukupatie ufafanuzi maana sisi ni wataalamu na tunaenda na taarifa zilizopo kwako na kwenye mfumo wetu
 
achana naye uyo kwanza ni roboti, pili yuko HQ anakula kiyoyozi, na kutapika nadharia kibao
ilihali uhalisia wa field haujui, huku akibwatuka eti tuko vizuri
Upo sahihi mkuu, jamaa anabwatuka tu, mikwara miiingiiii eti ooh taja sehemu, weka namba ya simu sijui nini na nini, hovyo kabisa wezi hawa.

Mtu unapata emergence mchana, unakuja kusolviwa kesho yake jioni.
 
Upo sahihi mkuu, jamaa anabwatuka tu, mikwara miiingiiii eti ooh taja sehemu, weka namba ya simu sijui nini na nini, hovyo kabisa wezi hawa.

Mtu unapata emergence mchana, unakuja kusolviwa kesho yake jioni.
Tuonesha fact tafadhali ulitoa taarifa lini?namba ya taarifa?ili tukujibu kwa fact vingenevyo hatusaidie kukuhudumia
 
Mkuu Dada yangu mmoja amejenga maeneo yale,alihangaika miezi 6 nikamwambia atumie kirainishi,Laki moja tu...umeme ukaingia ndani ya siku 3, halafu TANESCO anasema tupo vizuri wakati walishaoza kitambo
Wezi saaana hawa, mpaka unajiuliza kwani wanacholipwa hakiwatoshi? Na bado wakikufungia watakuomba 20,000 mara sijui wataomba nini na niniii, kumbuka bado surveyor umpe 30,000 na takataka zingine. Njaa tupu, hawatosheki kabisa na wanachopata, kama hakina maslahi kwanini wasiache?
 
Njoo inbox tafadhali onesha uhalali wa taarifa zako tukupatie ufafanuzi maana sisi ni wataalamu na tunaenda na taarifa zilizopo kwako na kwenye mfumo wetu
Mngeutumia huo utaalamu Kwa weledi mngekuwa mbali sana
 
Back
Top Bottom