Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Mtazamo: Taasisi na mashirika ya Serikali ambayo yana huduma mbovu kwa wateja Tanzania

Ni kweli wanapenda kuchangisha Hela ya mafuta/ nauli, wakati mafuta ni ya serikali na wanalipwa na serikali. Ila dawa Yao ni kuandaa ushahidi na kuwaripoti makao makuu Dodoma
Inakera mno chief, mbaya zaidi wanakuja hapa majukwaani wanajifanya hawajui yanayoendelea.
 
Mimi nasimamia ujenzi sehemu nyingi ndani ya Dar.

Wanapokuja kufunga mita, gar yao inabeba kazi nyingi na hao vibarua wao sijui vishoka wanaitwa. Dereva anaweza akawaacha vibarua point A, kisha wengine awaache point B, ni kama umbali wa mita mia mbili, yaani viwanja viwili vya mpira,na gari inafika kabisa.

Sasa cha ajabu unaombwa uchangie ela ya mafuta ili gari ifike kwako wakufungie umeme. Kuna mambo ya kipuuzi mno, yanakera haswa. Tukianza kuyaandika haya ni kuinua hasira zetu tu.
Tunashukuru kwa pongezi je unaweza kutusaidia namba ya simu mliyopiga mkaambiwa mtoe hela? Tunaomba tufatulie tujue na kuchukua hatua
0718851650;
na Kuna huyu anajiita MANAGER 0737739835.
 
Inakera mno chief, mbaya zaidi wanakuja hapa majukwaani wanajifanya hawajui yanayoendelea.
Tafadhali toa ushiirikiano kwa huduma bora unataka tuanzie wapi bila wewe kutoa taarifa?
 
TANESCO ya sasa sio ya zamani na ya kesho inaonesha dira ya mabadiliko makubwa sana kwenye utoaji wa huduma, tunakuhakikishia kuwa kwa huduma zetu zimeboreshwa sana na wateja wamekuwa wakionesha hilo.

Hebu twende kwa data au taarifa kamili ya wapi unapendekeza paboreshwe zaidi ili ufurahie huduma zetu
🤣🤣🤣🤣
 
Tunamaanisha TANESCO tupo vizuri na kama unachangamoto yeyote tafadhali ilete tusaidiane kuitatua, TANESCO ni yenu, ni mali ya uma mnawajibu wa msingi wa kuisaidia kuwahudumia vema kwa kutoa taarifa sahihi, ushauri nk
Sema wewe upo vizuri na sio tanesco. Tanesco inawafanyakazi wengi na sio wote wanafanya kazi zao ipasavyo na ndo hao tunakumbana nao kwenye huduma mbovu kila siku. TANESCO ingekuwa vizuri usingeona malalamiko hapa.
 
Unauhakika alimpa nani? Tafadhali milango ipo wazi akidhibitisha hili hatua zinachukulowa mara moja.

Tuache kutoa tuhuma za uongo ambazo hazina taarifa
Msingiziwe ili iweje? Kwamba tunawaonea wivu?
 
Taarifa itatolewa kwenye uzi wenu. Huu uzi ni kwaajili ya kutaja mashirika yenye huduma mbovu na mmeibuka washindi jipongezeni.

Mmetukatia umeme bila taarifa huku arusha mnarudisha saa ngapi?
Je ni Arusha sehemu gani
 
Huu ni mtazamo wangu kutokana na uzoefu wangu wa kupitia huduma mbali mbali katika mashirika hayo kwangu naona Hawa WATANO Wafuatao kwao mteja ni "boya" na Wala sio mfalme
5. TRA
4. Polisi
3. Maji
2. Nida
1. Tanesco

Kama umewahi kwenda ofisi hizo hapo juu utaona jinsi unavyopokelewa mpaka kuhudumiwa mpaka unajisemea moyoni..
'kungekuwa na mbadala ningeenda"

Anyway ni mtazamo tu..
Naomba kote mpinge ila sio hapo kwa Tanesco🤣🤣
Nunua Viwanja vyenye hati ndo utajua wengine
 
Ni aina ya watu wanaoishi kwenye jamii ndiyo huakisi aina ya watu kwenye kila nyanja. Unategemea watu aina gani kwenye jamii yetu hii ya watu wa ovyo ovyo?
 
Back
Top Bottom