Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.
Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...
Yaani unalinganisha tuhuma za Rais kutaka kusababisha nchi kupigwa mnada, tena tuhuma zilizotolewa hadharani, na tuhuma za kitoto kama za akina Makamba ambazo ziliongelewa behind the scene?! Hivi kama sio uvunjaji privacy uliokuwa unafanywa na Magufuli, wewe na wenzako mngefahamu akina Makamba waliongea nini dhidi yaJPM?

Ukweli kabisa, mwanzoni hili suala niliona ujinga lakini jana baada ya kuona video ya Ndugai akizungumzia hilo suala la mikopo, unaona wazi hoja yake was more than issue ya mikopo ambayo hakuwahi hata siku moja kuizungumzia wakati wa JPM ambae alikopa sana!!

Namnukuu Ndugai

"Lakini fikiria, nyinyi ndo wasomi. Kwa mfano Mama juzi ameenda kukopa 1.3 Trillion. Deni. Na tuna majengo hivi sasa, ya madarasa, vituo vya afya, ambavyo yanajengwa, kwa tozo. Hivi ipi bora. Sisi Watanzania wa miaka 60 ya uhuru kuzidi kukopa na madeni, au tubanane banane hapa hapa tujenge wenyewe bila ya madeni haya makubwa makubwa yasiyoeleweka? Ni lini sisi tutafanya wenyewe? And how? Tutembeze bakuli? Ndiyo heshima?

Tukishakopa tunapiga makofi. Sisi wa kukopa kila siku? Tukasema pitisha tozo. Anayetaka, asiyetaka, pitisha tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? yuko wapi huyo mjomba? Tukapitisha. Sasa 2025 mtaamua. Mkitoa waliopo, sawa; waje ambao kazi yao itakuwa kwenda kukopa.

Endapo hiyo ndo namna ya ku-run nchi. Hivi sasa deni letu ni 70 Trillion. Hivi nyie si wasomi? Is that healthy? Kuna siku nchi itapigwa mnada hii."

Sasa ukiangalia hiyo nukuu ni kwamba Ndugai karusha mawe yake kwa SSH personally na wala sio kama taasisi! Yaani SSH anaenda kuchukua mikopo isiyoeleweka inayoweza kusababisha nchi kupigwa mnada!

Sasa kwa nafasi ya Speaker, tena mbae u-spika wake umetokana na ubunge wake, nini hapo tafsiri yake kama si kwamba hakubaliani na SSH, tena kwa jambo serious!? Yaani ameonesha hadharani kwamba SSH ni rais wa ovyo! Sasa kama anajua rais ni mtu wa ovyo anayeiweka nchi kwenye rehani, busara si ilikuwa kuachia madaraka ili aendelee kupiga spana?

Ninachokiona kwa Ndugai, he's not happy na SSH, na inawezekana anaona kama SSH amepunguza nguvu aliyokuwa nayo Magu ya kuifanya Dodoma kuwa Capital City ki ukweli ukweli!
 
Ndugai alikosea yes alikosea laakin kuomba msamaha kakosea Zaid.

Alitakiwa kuendelea kuvimba tu kama msamaha ange omba sirini sio public.

Kama itatokea hatokuwa kwenye nafasi yake kesho jaambo ambalo kitamumiza zaidi ni kuomba msamaha na bado hujasamehewa, kujishusha Halafu haujathaminiwa hii huumiza sana.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...
Tatizo Ndungai ameomba msamaha kinafiki sana,

Na mbaya zaidi anakana kile alichoongea na kusingizia watu wame edit,

Sasa kama mtu anakana kitu kilicho wazi na anaomba msamaha,

Huo msamaha anaomba kwa kosa lipi?
 
Hii busara ilitakiwa ianze kwa Supika kwenda kumuona Rais na kumpa dokezo kiuongozi, kwenda public na kuhoji huku ukikebehi "nchi itapigwa mnada" zaidi ya hapo unasema wataamua 2025 mkitaka kuweka wa kukopakopa, huku kulikuwa ni kupungukiwa busara kwa hali ya juu...
Kwani siku anaongea kuhusu mikataba hakulidhika kumnanga mpaka arudie?
 
Waendelee wasiendelee....?

Kiitikio= Waendeleee...!

Makofi tafadhari...pwa, Pwa, Pwa, Pwa
 
Ile kazi wale wenyeviti wa CCM mikoa walipewa ndio maana jana wakaitwa ikulu kupongezwa kwa kazi nzuri waliyoifanya.

Hapo ukiangalia vizuri utaona Samia binafsi ameshaanza kujipanga kwa 2025, ila hataki wengine wajipange, akiulizwa anakimbilia najenga nchi, huu ni uongo anacheza na akili za wajinga.

Sasa nawashauri wote waanze kujipanga kwa 2025 hii nchi haina haja ya kuwa na Rais, inaweza kujiendea tu, kila siku tunalia umasikini, hakuna maji safi na salama, hawa miaka yote hawajui wanachofanya bora wapigane tu niangalie vita yao.
Hivi katika wale wenyeviti waliongea kuna ata mmoja aliongea jambo la maana kweli la kuisumbua hoja ya Ndugai? Alafu at the end eti Rais anawapongeza kwa kipi?
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Kosa kuu la kiufundi la Ndugai ni kuomba Msamaha.

Ila Kosa kuu zaidi la kiufundi ni alilofanya Samia kumsema Ndugai kiasi kile, au kwa maana nyingine ni kutangaza vita na adui asiyejua idadi yake.

Samia amedanganywa sana Kuwa Rais ndio Kila kitu, amesahau Bunge likiamua linaweza Kuifanya Serikali isifanikiwe kwa lolote kwa chochote.

Samia anasahau kwenye kamati kuu watu wake wa uhakika ni 2 tu labda na Wazanzibar wenzake, Bado Kwenye mkutano mkuu wa CCM hajui wapo wangapi.

Samia alidokeza Kuwa akina Ndugai walitaka hii serikali iitwe ya Mpito, Kama Ndugai aliamini anaweza kuipeleka hiyo hoja Bungeni basi, Sio wa kupuuzwa hata kidogo.

Hawa wenyeviti mikoa ni watu wasiotakiwa kumpa imani Rais.

Samia anatakiwa ajue Tanzania nzima 80% hawako tayari kuongoza na Rais Mwanamke..

Mwisho nisingependa Ndugai ajiuzulu, ila anoeshe makucha yake sasa
 
Back
Top Bottom