Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Kosa kuu la kiufundi la Ndugai ni kuomba Msamaha.

Ila Kosa kuu zaidi la kiufundi ni alilofanya Samia kumsema Ndugai kiasi kile, au kwa maana nyingine ni kutangaza vita na adui asiyejua idadi yake.

Samia amedanganywa sana Kuwa Rais ndio Kila kitu, amesahau Bunge likiamua linaweza Kuifanya Serikali isifanikiwe kwa lolote kwa chochote.

Samia anasahau kwenye kamati kuu watu wake wa uhakika ni 2 tu labda na Wazanzibar wenzake, Bado Kwenye mkutano mkuu wa CCM hajui wapo wangapi.

Samia alidokeza Kuwa akina Ndugai walitaka hii serikali iitwe ya Mpito, Kama Ndugai aliamini anaweza kuipeleka hiyo hoja Bungeni basi, Sio wa kupuuzwa hata kidogo.

Hawa wenyeviti mikoa ni watu wasiotakiwa kumpa imani Rais.

Samia anatakiwa ajue Tanzania nzima 80% hawako tayari kuongoza na Rais Mwanamke..

Mwisho nisingependa Ndugai ajiuzulu, ila anoeshe makucha yake sasa
Unaonekana unaongea kishabiki ndugu.

1) Nani kakwambia Mama hawajui maadui zake na idadi yao?? Unamchkulia poa???

2) Yaani wewe hujui kwamba Rais ndio kila kitu ndani ya nchi hii. Kweli hujui hilo?? Unaikumbuka kesi ya uamsho??? Iliishaje???

3) Kwenye kamati kuu watu wa Mama ni wawili tu?? Like seriously? Huoni kama kuna Wazanzibari mpaka huko Njombe na Ilemela??

4) Ndugai ni wa kupuuzwa na hana nguvu yoyote mnayotaka kumpa. Walimtanguliza kikatuni chao slow slow akagonga mwamba chap kwa haraka, na hakuna yeye na genge lake walichoweza kufanya.

5) Nani aliekwambia wenyeviti mikoa sio watu wanaotakiwa kumpa imani Mheshimiwa rais?? Uliwaona Jana Ikulu?? Hivi wewe ulikuwa umekaa kwa upande gani pale??

6) Haya maneno ya watu hawako tayar kuongezwa na mwanamke ni ujinga tu. Huu ni mwaka sasa unamalizika na Mama ndie Rasi wetu

7) Mtu wenu hana namna zaidi ya kuachia ngazi tu. Sio suala la wewe kupenda au kutokupenda. Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Amir jeshi mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama na ni MWENYEKITI WA Chama Cha mapinduzi.
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Mi nadhani mama kaona hana nafasi 2025 kwa sababu ya utamaduni wa chama chake kuwa mgombea urais anatoka bara na makamu zanzibar.kwahiyo kaamua kulipuka na ikiwezekana aaache legacy flani kwenye kipindi chake.Pia Ndugai ana damu ya kunguni.
 
Wale wabunge wana nafasi nzuri sana kwenye kuamua hili suala, ni either wapige kura ya kutokuwa na imani na Samia au kutokuwa na imani na Ndugai, kwao kuendelea kukaa kimya ni unafiki wasilete habari ya kulinda chama zaidi ya kulinda interests za nchi.

Kuwa na mihimili miwili isiyoelewana ni tatizo, kwa sababu yote hufanya kazi kwa kushirikiana, na kwa namna fulani inategemeana. Naona Samia ameaminiwa kwa kauli yake ya anajenga nchi hataki watu wamharibie, huu kwangu ni usanii tu.

Wakati yeye ndie alikuwa wa kwanza kuwaambia wanawake wenzie 2025 ni zamu yao, kama alidhani alikuwa anapiga umbea kwenye kikao cha wanawake wenzie ajue wanaume walijua vita ndio imeshatangazwa, sasa apigane asijifiche kwenye kisingizio cha najenga nchi na kutaka kutumbua mawaziri waliojipanga, anawaonea.
Ukiisoma katiba vizuri kabisa utabaini kuwa hata huyo ndugai na wabunge wake hawana uwezo wa kumtoa rais madarakani
 
Now you are back.
We missed you bro.

Hoja hii makini sana.

Samia ameshatishwa na tetesi zinazoenea kwa kasi hivyo ameona wacha aoneshe makali kidogo..
Hivi umesikiliza hatua kwa hatua alichoongea Ndugai?! Yaani badala ya yeye kuilaumu serikali lakini ametupa makonde yake kwa Samia personally, na wala sio kama taasisi!!
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Msamaha alitakiwa aseme kweli,sio kusema klipu iliundwaundwa,kwamba kakusema hayo na aombe msamaha,wa nini?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
CCM ktk uchaguzi wa ndani wa 2017 iliingiza madodoki ya kutosha ili kuweka mazingira ya team za ushindi...

Kisha madodoki hayo mkaja kuwaita WAJUMBE NUKSI walipovunja rekodi ya rushwa kwenye teuzi za ndani ya chama kuelekea uchafuzi mkuu 2020.

Jobo na wenzake hawakustahili hata kuwa wabunge kwa sababu hawana merits za kushika nafasi hizo.

Kikubwa ni kwamba, nchi imekosa muelekeo inayumba kwa sababu tumetengeneza TABAKA la watawala.

Mimi sioni tija kwenye huu mtanange lakini kwa mujibu wa Katiba yetu ya Nchi, ni wazi Spika amebugi step
My opinion anyway, there could be something fishy sported a far from presidentia advisory committee kumisslead Rais kwa manufaa yao, unajua hata mikopo inaweza kutumika kupata pesa za kupambania vita ya Urais 2025? Ni mtazamo wa kichokozi tu
 
CCM ktk uchaguzi wa ndani wa 2017 iliingiza madodoki ya kutosha ili kuweka mazingira ya team za ushindi...

Kisha madodoki hayo mkaja kuwaita WAJUMBE NUKSI walipovunja rekodi ya rushwa kwenye teuzi za ndani ya chama kuelekea uchafuzi mkuu 2020.

Jobo na wenzake hawakustahili hata kuwa wabunge kwa sababu hawana merits za kushika nafasi hizo.

Kikubwa ni kwamba, nchi imekosa muelekeo inayumba kwa sababu tumetengeneza TABAKA la watawala.

Mimi sioni tija kwenye huu mtanange lakini kwa mujibu wa Katiba yetu ya Nchi, ni wazi Spika amebugi step
Kwanini amebugi? Au kwasababu Rais ambae ni mwenyekiti wa chama ndie alipendekeza jina la job kugombea uspika? Hivi hatuoni haja ya kuwa na spika asiye na chama
 
Wakati ndugai anashinikiza asad atoke kisa tu alihoji matumizi ya fedha za matibabu mlishangalia, nionavyo mimi ndugai ana mengi aliliyoyafanya hadi kufikia kwenye tozo na mikopo, maana mama alisema eti rais wa mpito aliyekuwa anaratibu haya ni nan? Kimsingi rais kashaonesha kwamba hamtaki ndugai na huyo jiwe alikuwa anasamehe anawataka asiowataka alikuwa anafurusha na wengine hadi leo hawajulikana walipo. Hivyo hapa ndugai avune alichopanda
Uko na point ila ina sononesha kwa mustakabali mpana muhimu wafunike Kombe shetani apite nchi ni kubwa kuliko sisi sote. Nimewaza kipumbavu kama mnyama Twiga.
 
Rais is everything in TZ tuczidanganye nafsi zetu
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
 
Ushawahi sikia Samuel Sitta anaomba msamaha kwa mkuu mwenzie wa muhimili! (enzi hizo alikua JK)

Kwa kifupi Job Ndugai kakosea alitakiwa aendelee kuvimba, yeye ni muhimili tofauti, na inashangaza mwanaume gani anakuwa mwepesi mwepesi kuomba msamaha tena kwa she!
Anavimbaje wakati wenye mamlaka na kadi yako ya chama ndio wanaokupiga madongo hadharani kweupeee...kifupi Jobo hana pa kutokea....that is why KATIBA mpya ndio solution ya hizi mambo.
 
Hii busara ilitakiwa ianze kwa Supika kwenda kumuona Rais na kumpa dokezo kiuongozi, kwenda public na kuhoji huku ukikebehi "nchi itapigwa mnada" zaidi ya hapo unasema wataamua 2025 mkitaka kuweka wa kukopakopa, huku kulikuwa ni kupungukiwa busara kwa hali ya juu.

Na retaliation yake ndio hii watu msije kumuona Rais amekosea kumjibu public kwasababu yeye aliongea public basi naye acha ajibu public ndio waende huko ndani wakamalizane, hauwezi kuharibu image ya mwenzako yeye akae amekuangalia tuu.
Kwa taarifa tu ni kwamba Ndugai alishaongea sana na mama private lakini hawaku-match interests,ivyo option ya Ndugai ilikuwa ni kupitia public lakini bahati mbaya uku kwenye public nako alishanyea kambi kitambo kwa matendo yake ya uongozi mbaya ivyo ana maadui wengi ndani na nje.

Ndugai angeinvest kwa wananchi na kupendwa na kuheshimika hii vita mama angeshindwa asubuhi tu
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Kuna uwezekano wapo wengi nyuma ya Ndugai akitumika kama chambo tu, na Rais hupewa taarifa zote nyeti kwani vyombo vyote vipo chini yake.

Kaamua kumuanzishia ugomvi Ndugai ili aweze kufanya kazi kwa uhuru zaidi.

Kumbuka hii n nchi ya “mfumo dume” wapo baadhi hawaamini mpaka dakika hii kuwa nchi inaongozwa na rais mwanamke.
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Mimi nina maoni tofauti, juu ya hili swala la hii mihimili miwili! Wakati wa JPM, ilisemekana bunge ni dhaifu na lawama zilikuwa zinaelekezwa kwa JPM. Sasa utawala wa Rais Samia, unataka kuonyesha bunge siyo dhaifu na Rais haingilii bunge (yaani kuna utawala wa sheria) - lakini tutaaminije? Ili kutuaminisha, basi zengwe hili la Spika likazaliwa. Players katika zengwe hili ni wao kwa wao, yaani CCM na mihimili husika.
Na nia kubwa, ni kuonyesha Muhimbili wa serikali haugandamizi wa bunge - Nafikiri zoezi limefanikiwa.
 
Kwa taarifa tu ni kwamba Ndugai alishaongea sana na mama private lakini hawaku-match interests,ivyo option ya Ndugai ilikuwa ni kupitia public lakini bahati mbaya uku kwenye public nako alishanyea kambi kitambo kwa matendo yake ya uongozi mbaya ivyo ana maadui wengi ndani na nje.

Ndugai angeinvest kwa wananchi na kupendwa na kuheshimika hii vita mama angeshindwa asubuhi tu
Wewe ile busara ya let us agree to disagree hauitambui kwahiyo ukipishana na kiongozi mwenzako ni unamuanika hadharani.
 
Yaani unalinganisha tuhuma za Rais kutaka kusababisha nchi kupigwa mnada, tena tuhuma zilizotolewa hadharani, na tuhuma za kitoto kama za akina Makamba ambazo ziliongelewa behind the scene?! Hivi kama sio uvunjaji privacy uliokuwa unafanywa na Magufuli, wewe na wenzako mngefahamu akina Makamba waliongea nini dhidi yaJPM?

Ukweli kabisa, mwanzoni hili suala niliona ujinga lakini jana baada ya kuona video ya Ndugai akizungumzia hilo suala la mikopo, unaona wazi hoja yake was more than issue ya mikopo ambayo hakuwahi hata siku moja kuizungumzia wakati wa JPM ambae alikopa sana!!

Namnukuu Ndugai

"Lakini fikiria, nyinyi ndo wasomi. Kwa mfano Mama juzi ameenda kukopa 1.3 Trillion. Deni. Na tuna majengo hivi sasa, ya madarasa, vituo vya afya, ambavyo yanajengwa, kwa tozo. Hivi ipi bora. Sisi Watanzania wa miaka 60 ya uhuru kuzidi kukopa na madeni, au tubanane banane hapa hapa tujenge wenyewe bila ya madeni haya makubwa makubwa yasiyoeleweka? Ni lini sisi tutafanya wenyewe? And how? Tutembeze bakuli? Ndiyo heshima? Tukishakopa tunapiga makofi. Sisi wa kukopa kila siku? Tukasema pitisha tozo. Anayetaka, asiyetaka, pitisha tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? yuko wapi huyo mjomba? Tukapitisha. Sasa 2025 mtaamua. Mkitoa waliopo, sawa; waje ambao kazi yao itakuwa kwenda kukopa. Endapo hiyo ndo namna ya ku-run nchi. Hivi sasa deni letu ni 70 Trillion. Hivi nyie si wasomi? Is that healthy? Kuna siku nchi itapigwa mnada hii."

Sasa ukiangalia hiyo nukuu ni kwamba Ndugai karusha mawe yake kwa SSH personally na wala sio kama taasisi! Yaani SSH anaenda kuchukua mikopo isiyoeleweka inayoweza kusababisha nchi kupigwa mnada!

Sasa kwa nafasi ya Speaker, tena mbae u-spika wake umetokana na ubunge wake, nini hapo tafsiri yake kama si kwamba hakubaliani na SSH, tena kwa jambo serious!? Yaani ameonesha hadharani kwamba SSH ni rais wa ovyo! Sasa kama anajua rais ni mtu wa ovyo anayeiweka nchi kwenye rehani, busara si ilikuwa kuachia madaraka ili aendelee kupiga spana?

Ninachokiona kwa Ndugai, he's not happy na SSH, na inawezekana anaona kama SSH amepunguza nguvu aliyokuwa nayo Magu ya kuifanya Dodoma kuwa Capital City ki ukweli ukweli!
Paragraph ya mwisho umebashiri ukweli Ndugai akerwa na safari za Dodoma to Dar kila siku
 
Back
Top Bottom