Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali...
CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili...

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama...

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia...kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi...

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Wakubwa, hoja zetu ni nzito kweli.

Ila kwa namna CCM Rais ndiye mkiti wa Chama, katibu mkuu wa chama ni mteule wa Rais bila shaka inafahamika Rais akiamua kurea term ya pili kwa utamaduni wa CCM wataotoa form moja tu, na mchezo mzima unaisha.

Ambacho kinafahamika, Spika Job hana nia ya 2025 labda kama alikuwa mshenga wa mwingine? Je, Job ni mshenga wa nani mpaka hii "homa ya 2025" imempata mapema kiasi hiki?

Nikikumbuka Bunge la Spika Samuel Sitta au Big Sam, likikuwa na joto sana na kama ingekuwa ni enzi ya Big Sam, basi Madam SSH angeteseka sana; maana mzee yule sio tu angetoa kauli ila angeunda Kamati Teule kujua kulikoni chunguni?

Nakubaliana kabisa na ushauri wako, kuwa politics na diplomacy vinaendana, ni kama vile US na Russia wanakaa meza moja ila kila mmoja anakuwa na interest zake.

Ikitokea Executive branch akai-pin down Legislative branch kwa sababu ya "argument" na homa za 2025, bila shaka kama nchi tutakuwa tuna-set precedence ambao sio nzuri.

By the way, Mhe. SSH alitaka watu wafunguke na wapumue, na hoja ya Job mpaka sasa bado haina majibu, kwa kuwa tozo zilipitishwa ili tujenge mashule, mkopo wa 1.3 Tril mbona unafanya kazi za tozo?

So far, tunampongeza mama SSH kwa kukopa ili ku-push madarasa yajengwa haraka ili wanetu wasome, japo nadhani kuna haja ya kuongeza wanalimu na learning materials ili kujifunza kuwe na uwiano mzuri darasani na access ya learning materials ikiwepo.

Mijadala ni afya hasa kama ni mjadala wa wazi, na mikopo ni mizuri kama imelenga kujenga nchi kama ule wa 1.3Tril, suala ambalo ni vema wasaidizi wa madam SSH wakaja mbele, ni kuweka wazi fedha za tozo zimekuwa allocated kufanya nini maana tulipata mkopo usio na riba na tume-solve tatizo ili wanetu wakute kuna vyumba vya madarasa.

Mwisho, wizara ya fedha ndio inakopa kwa niaba ya serikali na Waziri wa kisekta asitake "kutuzuga" kuwa mwananchi hatalipa, ifahamike tu, hatakuja mtu kugonga mlango wa nyumba ila wananchi tutalipa kwa namna moja au nyingine, hivyo basi kwenye threshold ya fursa ya kukopa, tusifikirie tu kuwekeza kwenye majenzi, tukopo ili kukuza uzalishaji ambao return on Investment ni ya haraka, na multiplier effect yake inapimika na inaongeza cash flow.

Tukope ili kuongeza ukwasi TIB, TADB ili tusibaki tuna-import basics kama mafuta ya kula, sukari, mashuka ya hospitali, surgical cotton and bandages ila tuzifanye bank hizi zitukopeshe Watanzania kwa dhamana ya serikali, tuzalishe finished consumable goods snd service za kuuza sokoni, kwa namna hiyo tunaongeza tax base na watu wenye misuli ya ku-service mikopo pale inapo-mature.

Siku njema, tuendelee kujadiliana kwa staha, tusiraruane.
 
Yaani unalinganisha tuhuma za Rais kutaka kusababisha nchi kupigwa mnada, tena tuhuma zilizotolewa hadharani, na tuhuma za kitoto kama za akina Makamba ambazo ziliongelewa behind the scene?! Hivi kama sio uvunjaji privacy uliokuwa unafanywa na Magufuli, wewe na wenzako mngefahamu akina Makamba waliongea nini dhidi yaJPM?

Ukweli kabisa, mwanzoni hili suala niliona ujinga lakini jana baada ya kuona video ya Ndugai akizungumzia hilo suala la mikopo, unaona wazi hoja yake was more than issue ya mikopo ambayo hakuwahi hata siku moja kuizungumzia wakati wa JPM ambae alikopa sana!!

Namnukuu Ndugai

"Lakini fikiria, nyinyi ndo wasomi. Kwa mfano Mama juzi ameenda kukopa 1.3 Trillion. Deni. Na tuna majengo hivi sasa, ya madarasa, vituo vya afya, ambavyo yanajengwa, kwa tozo. Hivi ipi bora. Sisi Watanzania wa miaka 60 ya uhuru kuzidi kukopa na madeni, au tubanane banane hapa hapa tujenge wenyewe bila ya madeni haya makubwa makubwa yasiyoeleweka? Ni lini sisi tutafanya wenyewe? And how? Tutembeze bakuli? Ndiyo heshima?

Tukishakopa tunapiga makofi. Sisi wa kukopa kila siku? Tukasema pitisha tozo. Anayetaka, asiyetaka, pitisha tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? yuko wapi huyo mjomba? Tukapitisha. Sasa 2025 mtaamua. Mkitoa waliopo, sawa; waje ambao kazi yao itakuwa kwenda kukopa.

Endapo hiyo ndo namna ya ku-run nchi. Hivi sasa deni letu ni 70 Trillion. Hivi nyie si wasomi? Is that healthy? Kuna siku nchi itapigwa mnada hii."

Sasa ukiangalia hiyo nukuu ni kwamba Ndugai karusha mawe yake kwa SSH personally na wala sio kama taasisi! Yaani SSH anaenda kuchukua mikopo isiyoeleweka inayoweza kusababisha nchi kupigwa mnada!

Sasa kwa nafasi ya Speaker, tena mbae u-spika wake umetokana na ubunge wake, nini hapo tafsiri yake kama si kwamba hakubaliani na SSH, tena kwa jambo serious!? Yaani ameonesha hadharani kwamba SSH ni rais wa ovyo! Sasa kama anajua rais ni mtu wa ovyo anayeiweka nchi kwenye rehani, busara si ilikuwa kuachia madaraka ili aendelee kupiga spana?

Ninachokiona kwa Ndugai, he's not happy na SSH, na inawezekana anaona kama SSH amepunguza nguvu aliyokuwa nayo Magu ya kuifanya Dodoma kuwa Capital City ki ukweli ukweli!

Kuna nchi ushawahi kuona imepigwa mnada?..

Suala la Tozo wananchi walipiga sana kelele na kuilaumu sana serikali mpaka Rais kuitwa BI TOZO....sasa bila shaka wataelewa mhusika ni nani..

Kukopa sio dhambi, ila tu uwe na unakopa kwa mipango au ukijua namna sahihi ya kulipa either kupitia kodi hizo hizo unazotoza raia au kupitia uzarishaji mali ndani ya rasilimari zilizopo..

Kumbe kuna mtu alikuwa anakopakopa sana na Ndugai alikuwepo kwanini hakuwahi kuyasema haya bali anakuja kusema wengine hapa utaona naye ni muoga na mnafiki tu..
 
Kwanini amebugi? Au kwasababu Rais ambae ni mwenyekiti wa chama ndie alipendekeza jina la job kugombea uspika? Hivi hatuoni haja ya kuwa na spika asiye na chama
Haja ya kuwa na spika asiye na Chama ipo na haikwepeki.

Lakini tatizo kubwa sana sana ni kitu hiki TABAKA LA WATAWALA

Tuiondoe hiyo kwanza
 
Ambayo aliyakataa Samia yana msingi wa kikatiba km ukopaji kinyemela na kupelekwa fedha nyingi Zanzibar kinyume na katiba,agree to disagree ni kwenye mambo yasiyovunja katiba tu na siyo haya ya upendeleo
Weka vifungu vilivyovunjwa, weka data hapa sio empty words.
 
Rais aambiwe anaipeleka nchi yake mnadani anyamaze? Kweli? Huyo atakuwa siyo Rais wa nchi.
Hili sidhani kwamba litaishia kwa Ndugai tu, lazima itakuwepo safisha safisha.
 
Kwa taarifa tu ni kwamba Ndugai alishaongea sana na mama private lakini hawaku-match interests,ivyo option ya Ndugai ilikuwa ni kupitia public lakini bahati mbaya uku kwenye public nako alishanyea kambi kitambo kwa matendo yake ya uongozi mbaya ivyo ana maadui wengi ndani na nje.

Ndugai angeinvest kwa wananchi na kupendwa na kuheshimika hii vita mama angeshindwa asubuhi tu
Ubuyu wa Babu Issa.

Wazee wa taharuki mnajifanya kuyajua mengi sana kana kwamba nyie ndo wazee wa protocals za hao viongozi.

Tulieni, subirini meza kupinduka
 
Yaani unalinganisha tuhuma za Rais kutaka kusababisha nchi kupigwa mnada, tena tuhuma zilizotolewa hadharani, na tuhuma za kitoto kama za akina Makamba ambazo ziliongelewa behind the scene?! Hivi kama sio uvunjaji privacy uliokuwa unafanywa na Magufuli, wewe na wenzako mngefahamu akina Makamba waliongea nini dhidi yaJPM?

Ukweli kabisa, mwanzoni hili suala niliona ujinga lakini jana baada ya kuona video ya Ndugai akizungumzia hilo suala la mikopo, unaona wazi hoja yake was more than issue ya mikopo ambayo hakuwahi hata siku moja kuizungumzia wakati wa JPM ambae alikopa sana!!

Namnukuu Ndugai

"Lakini fikiria, nyinyi ndo wasomi. Kwa mfano Mama juzi ameenda kukopa 1.3 Trillion. Deni. Na tuna majengo hivi sasa, ya madarasa, vituo vya afya, ambavyo yanajengwa, kwa tozo. Hivi ipi bora. Sisi Watanzania wa miaka 60 ya uhuru kuzidi kukopa na madeni, au tubanane banane hapa hapa tujenge wenyewe bila ya madeni haya makubwa makubwa yasiyoeleweka? Ni lini sisi tutafanya wenyewe? And how? Tutembeze bakuli? Ndiyo heshima?

Tukishakopa tunapiga makofi. Sisi wa kukopa kila siku? Tukasema pitisha tozo. Anayetaka, asiyetaka, pitisha tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? yuko wapi huyo mjomba? Tukapitisha. Sasa 2025 mtaamua. Mkitoa waliopo, sawa; waje ambao kazi yao itakuwa kwenda kukopa.

Endapo hiyo ndo namna ya ku-run nchi. Hivi sasa deni letu ni 70 Trillion. Hivi nyie si wasomi? Is that healthy? Kuna siku nchi itapigwa mnada hii."

Sasa ukiangalia hiyo nukuu ni kwamba Ndugai karusha mawe yake kwa SSH personally na wala sio kama taasisi! Yaani SSH anaenda kuchukua mikopo isiyoeleweka inayoweza kusababisha nchi kupigwa mnada!

Sasa kwa nafasi ya Speaker, tena mbae u-spika wake umetokana na ubunge wake, nini hapo tafsiri yake kama si kwamba hakubaliani na SSH, tena kwa jambo serious!? Yaani ameonesha hadharani kwamba SSH ni rais wa ovyo! Sasa kama anajua rais ni mtu wa ovyo anayeiweka nchi kwenye rehani, busara si ilikuwa kuachia madaraka ili aendelee kupiga spana?

Ninachokiona kwa Ndugai, he's not happy na SSH, na inawezekana anaona kama SSH amepunguza nguvu aliyokuwa nayo Magu ya kuifanya Dodoma kuwa Capital City ki ukweli ukweli!
Kwa kasi ya ukopoji ya mama na akili yake ilivyo ya kukosa kiasi kwenye hesabu za kukopa basi kufikia 2025 mama atakuwa kakopa kuliko maraisi wote toka raisi wa kwanza hadi wa tano combine maana mama kakopa til11 ndani ya miezi 9 tu tena inaonekana hiyo ndiyo aliyo bahatika kupata maana yake kama angepata zaidi hata til40 kwa mwaka angekopa ndiyo nikasema mama anaongoza nchi kwa kupractise upumbavu kukopa kuna mahesabu
 
My opinion anyway, there could be something fishy sported a far from presidentia advisory committee kumisslead Rais kwa manufaa yao, unajua hata mikopo inaweza kutumika kupata pesa za kupambania vita ya Urais 2025? Ni mtazamo wa kichokozi tu
Mikopo haikwepeki kwa sababu walioishika dunia wanalazimishia hilo.

Msipokopa leo, mnaua uchumi wa ulaya na majinamizi yanayotukamua.

Kikubwa mikopo itumike kwa usahihi na tuwe na open forums za kujadili mwenendo wa uchumi wetu.

Sasa Job alikuwa anatafuta milleage na tunajua kabisaa hana viwango hata vya kuwa mbunge.

Mtu anatoa boko kisha akimulikwa anakimbilia kichaka cha ukabila. Ni kufilisika kisiasa na kiakili
 
Ile ilikuwa kazi wale wenyeviti wa CCM mikoa waliyopewa kumpinga Ndugai ndio maana jana wakaitwa ikulu kupongezwa kwa kazi nzuri waliyoifanya.

Hapo ukiangalia vizuri utaona Samia binafsi ameshaanza kujipanga kwa 2025, ila hataki wengine wajipange, akiulizwa anakimbilia najenga nchi, huu ni uongo, anacheza na akili za wajinga.

Sasa nawashauri wote waanze kujipanga kwa 2025 hii nchi haina haja ya kuwa na Rais wala Spika, inaweza kujiendea tu, kila siku tunalia umasikini, hakuna maji safi na salama wakati hawa miaka yote wapo tu hawajui wanachofanya, bora wapigane niangalie vita yao.
Acha chuki za wazi kwa Rais, je meko aliruhusu wengine kujipanga?nini kilimtokea Benard membe?Hili ni kwa viongozi wote wa Africa, ni dhuruma ngapi Ndugai alishiriki kuwatendea wengine awamu ya 5?, eti wabunge wachague moja kumpigia rais au spika kura ya kutokuwa na imani, kwa rais hicho ni kitu kigumu sana.Ila kama mama akitaka spika atoke anaweza, kwa siasa zetu hizi, ni dakika tu, kwani watu wanaangalia tu upepo!!huo sio mgogoro wa bunge na serikali bali ni Ndugai na serikali.
 
Hivi umesikiliza hatua kwa hatua alichoongea Ndugai?! Yaani badala ya yeye kuilaumu serikali lakini ametupa makonde yake kwa Samia personally, na wala sio kama taasisi!!
Upo sahihi.

Dhambi ya kupitisha tozo kandamizi inaanza na Job.

Wengine watafuatia
 
Wale wabunge wana nafasi nzuri sana kwenye kuamua hili suala, ni either wapige kura ya kutokuwa na imani na Samia au kutokuwa na imani na Ndugai, kwao kuendelea kukaa kimya ni unafiki wasilete habari ya kulinda chama zaidi ya kulinda interests za nchi.

Kuwa na mihimili miwili isiyoelewana ni tatizo, kwa sababu yote hufanya kazi kwa kushirikiana, na kwa namna fulani inategemeana. Naona Samia ameaminiwa kwa kauli yake ya anajenga nchi hataki watu wamharibie, huu kwangu ni usanii tu.

Wakati yeye ndie aliekuwa wa kwanza kuwaambia wanawake wenzie 2025 ni zamu yao, kama alidhani alikuwa anapiga umbea kwenye kikao cha wanawake wenzie ajue wanaume walijua vita ndio imeshatangazwa, sasa apigane asijifiche kwenye kisingizio cha najenga nchi na kutaka kutumbua mawaziri wanaojipanga, anawaonea.
Mawaziri ni wasaidizi wake anahamua yeye nan hamteue nan hamuache
 
hili ni suala muhimu sana kama Taifa kulizingatia..Taifa limekuwa la siasa kila siku..Watu wanawaza urais muda wote..
Mkuu kwa vast of resources available on our motherland, tungekuwa na mijadala ya namna gani tukope kwa kuongezea uwezo bank za maendeleo ili Tz iwe major exporter basics consumable kwa Mozamboque, Malawi, Congo, Burundi, Rwannda, Uganda, Kenya, Madagascar ili kusisimua uchumu, kukuza ajira ili hata hao wanaosoma kwenye hayo madarasa wakitoka shule kuwe na avenue ya wao kuja kuwa producers.

Ila sana, mhhh.

Mungu tusaidie sana, kuna pahala akili yetu hatujaishughulisha vya kutosha.
 
Wale wabunge wana nafasi nzuri sana kwenye kuamua hili suala, ni either wapige kura ya kutokuwa na imani na Samia au kutokuwa na imani na Ndugai, kwao kuendelea kukaa kimya ni unafiki wasilete habari ya kulinda chama zaidi ya kulinda interests za nchi.

Kuwa na mihimili miwili isiyoelewana ni tatizo, kwa sababu yote hufanya kazi kwa kushirikiana, na kwa namna fulani inategemeana. Naona Samia ameaminiwa kwa kauli yake ya anajenga nchi hataki watu wamharibie, huu kwangu ni usanii tu.

Wakati yeye ndie aliekuwa wa kwanza kuwaambia wanawake wenzie 2025 ni zamu yao, kama alidhani alikuwa anapiga umbea kwenye kikao cha wanawake wenzie ajue wanaume walijua vita ndio imeshatangazwa, sasa apigane asijifiche kwenye kisingizio cha najenga nchi na kutaka kutumbua mawaziri wanaojipanga, anawaonea.
Kwa katiba ya ccm ni ngumu kumpinga Mwenyekiti ana nguvu kuliko chama
 
Si mtego mgumu...lakini ni mtego mkali... CCM kwa miaka yote imejitahidi sana kukwepesha na wakati mwingine kuahirisha milongas ya mihimili.

Kuanzia wakati wa Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere na mjadala wa Uafrika na Uraia wa Tanzania hadi huu wa mkopo na Tozo wa Rais Samia. Migongano iliepushwa kwa kuzungumza kichama.

Sasa hivi kichama vitu haviendi na visingefika alipofikisha Rais Samia, kukataa msamaha alioomba Ndugai. Samia angeweza kutoa kauli ya kusamehe kama aliyotoa mtangulizi wake kwa waliomkosea wakati ule (mnakumbuka ya Kinana?). Mambo yangeisha kiutu uzima kwa kupiga picha na kunywa chai.

Spika ni mtu mzito sana Kikatiba...Rais ni mzito zaidi..hawapimani. Spika hana hata chipukizi wa kumlinda na mshale..Rais anaamuru majeshi.

Lakiki Samia yuko tayari kuandika historia ya kuwa Rais aliyemlazimisha Spika wa chama chake kujiuzulu kwa jambo la mitazamo midogo yenye kutofautiana kisera? Ni kweli tunataka kumuona Ndugai anatoka lango la Ikulubakitembea anageukageuka nyuma akijifuta jasho?

Kama Rais ni taasisi na Spika ni taasisi kama ilivyo kwa Jaji Mkuu. Tusiingie mtego huu. Wa kutegua ni Samia na si Ndugai.

Hekima itatamalaki? Ya nani?
Ndugai alipokuwa anasema watu watachagua Kati ya mikopo na kujibana bana kwenye uchaguzi wa 2025 alikuwa na maana gani?
 
Now you are back.
We missed you bro.

Hoja hii makini sana.

Samia ameshatishwa na tetesi zinazoenea kwa kasi hivyo ameona wacha aoneshe makali kidogo..
Wazee wakiondoka jukwaa linamiss hekima kubwa sana.....
Alilolifanya linaonyesha wepesi wa kihisia , sasa angeambiwa Idd Amini ame amevamia taifa ndio angeweza hiyo vita ya moto kama vita ya propaganda tu anashindwa kuhema?
 
Kosa kuu la kiufundi la Ndugai ni kuomba Msamaha.

Ila Kosa kuu zaidi la kiufundi ni alilofanya Samia kumsema Ndugai kiasi kile, au kwa maana nyingine ni kutangaza vita na adui asiyejua idadi yake.

Samia amedanganywa sana Kuwa Rais ndio Kila kitu, amesahau Bunge likiamua linaweza Kuifanya Serikali isifanikiwe kwa lolote kwa chochote.

Samia anasahau kwenye kamati kuu watu wake wa uhakika ni 2 tu labda na Wazanzibar wenzake, Bado Kwenye mkutano mkuu wa CCM hajui wapo wangapi.

Samia alidokeza Kuwa akina Ndugai walitaka hii serikali iitwe ya Mpito, Kama Ndugai aliamini anaweza kuipeleka hiyo hoja Bungeni basi, Sio wa kupuuzwa hata kidogo.

Hawa wenyeviti mikoa ni watu wasiotakiwa kumpa imani Rais.

Samia anatakiwa ajue Tanzania nzima 80% hawako tayari kuongoza na Rais Mwanamke..

Mwisho nisingependa Ndugai ajiuzulu, ila anoeshe makucha yake sasa
Huna akili ndyg mnapenda kuwa na matumaini hewa yan mtu anaepokea report za ushushu toka tiss na mi ashindwe na huyo ndugai serious kabisa
 
Hii busara ilitakiwa ianze kwa Supika kwenda kumuona Rais na kumpa dokezo kiuongozi, kwenda public na kuhoji huku ukikebehi "nchi itapigwa mnada" zaidi ya hapo unasema wataamua 2025 mkitaka kuweka wa kukopakopa, huku kulikuwa ni kupungukiwa busara kwa hali ya juu.

Na retaliation yake ndio hii watu msije kumuona Rais amekosea kumjibu public kwasababu yeye aliongea public basi naye acha ajibu public ndio waende huko ndani wakamalizane, hauwezi kuharibu image ya mwenzako yeye akae amekuangalia tuu.
Umeandika vizuri iwe musigazi (wewe mvulana).Nimeshakupa like
 
Back
Top Bottom