Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Mtego Aliojitegea Rais Samia, nani atauvunjilia?

Kujiuzulu ni kukubali kushindwa, na akijiuzulu anawapa oppornent(s) wake point za kiulani (kuwa alikua sahihi)
... CCM walivyo washenzi watamzushia majina huyo! Hakuna jina baya ambalo Ndugai hatapewa; wanaweza kumwita hata Nduli such that hadi kizazi kijacho kitakuwa na image mbaya sana ya Nduli Ndugai kumbe alikuwa na maoni ya kawaida tu!
 
Kwa Hali ulivyo sioni namna ya ndugai kuendelea kuwa spika kwa Hilo lililotokea, anapaswa kujiuzulu au kuondolewa.Mama kakataa msamaha wake
Anaweza akajiuzulu na ikampa heshima kubwa kuliko kuendelea kumlamba miguu muimba taarabu na mpaka inna viganjani ni aibu, hata akitaka kugombea 2025 hatutamuelewa kuliko akijiuzulu halafu aje 2025,
 
Wale wabunge wana nafasi nzuri sana kwenye kuamua hili suala, ni either wapige kura ya kutokuwa na imani na Samia au kutokuwa na imani na Ndugai, kwao kuendelea kukaa kimya ni unafiki wasilete habari ya kulinda chama zaidi ya kulinda interests za nchi.

Kuwa na mihimili miwili isiyoelewana ni tatizo, kwa sababu yote hufanya kazi kwa kushirikiana, na kwa namna fulani inategemeana. Naona Samia ameaminiwa kwa kauli yake ya anajenga nchi hataki watu wamharibie, huu kwangu ni usanii tu.

Wakati yeye ndie aliekuwa wa kwanza kuwaambia wanawake wenzie 2025 ni zamu yao, kama alidhani alikuwa anapiga umbea kwenye kikao cha wanawake wenzie ajue wanaume walijua vita ndio imeshatangazwa, sasa apigane asijifiche kwenye kisingizio cha najenga nchi na kutaka kutumbua mawaziri wanaojipanga, anawaonea.
Tunatikiwa tufikie viwango vya USA, Bunge liongozwe na chama kingine na urais ushikiliwe na chama kingine tofauti na kazi iweze kuendelea
 
Ngoja ma-CCM yaparuane, si huwa yanajifanya hayajui umuhimu wa katiba mpya isiyo na mawaa yenye clear separation of powers kati ya mihimili ya dola.
Kwa hiyo kwenye katiba nzuri viongozi Wakuu wa mihimili huwa awapalulani?
 
Nadhani issue wanayoona maCCM wenyewe si kupishana kauli bali ni uchaguzi 2025...
 
Tatizo kiongozi mkubwa akikosolewa kwa hoja inaonekana ni uadui, ni lini tutabadilisha mtazamo.

Mh Raisi S.S.Hassan na yeye angepaswa kujibu kwa hoja, na wala asidhani ni uadui.

Siasa zetu bado sana.

Halafu sio kwamba mtu kama spika wa bunge hajui nini kingetokea baada ya kauli hio, lakini ameomba msamaha as if aliteleza, lakini ukweli ni kwamba jamaa ametimiza adhma yake kwa kufikisha ujumbe, na tayari hatujui huo ujasiri ni akina nani wapo nae.

Pia sioni haja Ndugai kuomba msamaha, amefanya kinachopaswa, kwa kuomba msamaha anadhihirisha na kuaminisha umma wa wa Tanzania kwamba kumkosoa raisi ni kosa na ni mwiko na haipaswi.
 
Ya Ndugai yalikuwa maoni yake ambayo kila mtu ana haki yake.

Yakajibiwa kwa marungu na kumpelekea Ndugai kuomba yaliyopita yasiwe ndwele.

Maombi ya Ndugai yametupwa kwa kejeli.

Tulipo sasa ni hapa:

Msamaha kubutuliwa, Ndugai aungwe mkono

Aluta Continua.

Vita ni vita, Mura!
Kwa cheo cha Ndugai anapoongea kitu kupitia media maneno yake yanachukuliwa Spika kasema sio mnywa kahawa kasema
Kwa hiyo lazima ujue kuna tofauti kubwa Kati ya Ndugai na Mtanzania wa kawaida katika maneno watakayosema
 
Kitendo cha Ndugai kuretreat kimemmaliza nguvu kabisa. Hiyo imemfanya Maza awe comfortable kama alivyoonyesha jana.

Lakini alichokifanya Maza jana nalo ni kosa la kiufundi kwa kutangaza vita hadharani. Kama anajaribu kufanya Kimagufuri akumbuke kuwa yeye siyo Magufuli.

Kwa vile kisha likoroga basi ajiandae vizuri kujihami. Hasa baada ya kufumua hilo baraza. Nategemea Wanawake wataongezwa ili kumpa nguvu.
 
Mawazo yangu ni kwamba Ndugai asijiuzulu unless kuna tishio la usalama wake.

Ningependa kushuhudia upigaji wa kura ya kutokuwa na imani naye Kupitia kura ya siri.

Ningependa Wananchi tufahamu msimamo wa wabunge wetu kuhusu hii mitazamo miwili tofauti ya viongozi hawa wakuu

Vinginevyo ni jambo zuri kuona namna sumu waliyoitengeneza wenyewe kwa ajili ya kuwaua wapinzani wao sasa inawatafuna wenyewe.
 
Tatizo Ndungai ameomba msamaha kinafiki sana,

Na mbaya zaidi anakana kile alichoongea na kusingizia watu wame edit,

Sasa kama mtu anakana kitu kilicho wazi na anaomba msamaha,

Huo msamaha anaomba kwa kosa lipi?
Nadhani watu wanamiss kwanini Ndugai kaomba msamaha...si kwa sababu alikosea
 
Wale wabunge wana nafasi nzuri sana kwenye kuamua hili suala, ni either wapige kura ya kutokuwa na imani na Samia au kutokuwa na imani na Ndugai, kwao kuendelea kukaa kimya ni unafiki wasilete habari ya kulinda chama zaidi ya kulinda interests za nchi.

Kuwa na mihimili miwili isiyoelewana ni tatizo, kwa sababu yote hufanya kazi kwa kushirikiana, na kwa namna fulani inategemeana. Naona Samia ameaminiwa kwa kauli yake ya anajenga nchi hataki watu wamharibie, huu kwangu ni usanii tu.

Wakati yeye ndie aliekuwa wa kwanza kuwaambia wanawake wenzie 2025 ni zamu yao, kama alidhani alikuwa anapiga umbea kwenye kikao cha wanawake wenzie ajue wanaume walijua vita ndio imeshatangazwa, sasa apigane asijifiche kwenye kisingizio cha najenga nchi na kutaka kutumbua mawaziri wanaojipanga, anawaonea.
Ila ikumbukwe lile bunge ni la watu wa mwenda zake, japo wanasiasa hawaaminiki.

Pia, tujiulize yale Ni mawazo binafsi tu ya Ndugai au kuna kundi liko nyuma yake.

Ila tumekosea Sana kuwa na Rais Mzanzibari kuja kuitawala Tanganyika. Sisi Ni mateka wa Rais amabaye ni raia wa nchi jirani.

Nasikia DP Naye ana vinasaba vya Kirundi.

Tanganyika imetekwa. Itajinasuaje 2025 au kabla?
 
Mawazo yangu ni kwamba Ndugai asijiuzulu unless kuna tishio la usalama wake.

Ningependa kushuhudia upigaji wa kura ya kutokuwa na imani naye Kupitia kura ya siri.

Ningependa Wananchi tufahamu msimamo wa wabunge wetu kuhusu hii mitazamo miwili tofauti ya viongozi hawa wakuu

Vinginevyo ni jambo zuri kuona namna sumu waliyoitengeneza wenyewe kwa ajili ya kuwaua wapinzani wao sasa inawatafuna wenyewe.
Hili ni suala la Rais na chama...Ndugai amuache Rais na Mwenyekiti amuambie wazi kuwa hana Imani ya kufanya kazi naye..hapo atatakiwa kujiuzulu. Asimfanyie Rais kazi.
 
Kwani Ndungai akiachia hayo madaraka kuna shida gani, unadhani Mh. SSH atataka kuongea na huyo mhusika tena, ki uhalisia huwezi kuishi na nyoka ndani ya nyumba yako ukawa salama. Muhimu ni kukikata kichwa mapema tu.
Unyoka wa Ndugai uko wapi?

Ule ujumbe wake?
 
Back
Top Bottom