Mtoto wa Zachary Kakobe: Mfikishieni salamu baba yangu namtafuta, sijaonana naye kwa Miaka 20, nikienda Kanisani sipati nafasi ya kumuona

Mtoto wa Zachary Kakobe: Mfikishieni salamu baba yangu namtafuta, sijaonana naye kwa Miaka 20, nikienda Kanisani sipati nafasi ya kumuona

Miaka 43 mbona amekomaa hivyo Kama ana miaka 60! Inaonekana anateseka sana wakati baba yake ni bilionea! Kakobe aache kunyanyasa watoto kwa kujifanya Mungu mtu.. yaani mtoto wako mwenyewe akija nyumbani hawezi kuingia mpaka aandike barua! Hatari sana
 
Katika pitapita zangu mitandaoni, nimekutana na makala hii inayohusu mahojiano aliyoyafanya huyu jamaa anaitwa Frank ambaye anasema ni mtoto wa Mchungaji Zachary Kakobe, nimeona si vibaya nikishea hapa inawezekana kama ni kweli basi ujumbe umfikie kwa urahisi mtumishi kwa kuwa najua JF ni platform kubwa na inafika mbali.

@@@@

Naitwa Frank Zachary Kakobe, mimi ni mzaliwa wa Tuliani, Wilayani Mvomelu Mkoani Morogoro, nilisoma Elimu ya Msingi Mwenge Mwaka 1986 hadi 1993 baada ya hapo nikaenda Real High School ipo Thiker Nchini Kenya

Baada ya hapo nikasomea masuala ya kompyuta nikapata Diploma katika chuo cha Techno Brain, sijui sasa hivi kinaitwaje.

Nina umri wa miaka 43, nina Watoto watatu na baada ya kuhitimu masomo yangu nilifanya kazi kadhaa za kiufundi.

Nia yangu ya kujitokeza kuzungumza hapa ni baba yangu apate taarifa juu ya uwepo wangu, tangu nilipoachana naye miaka 17 hadi 20 iliyopita, nimejaribu mara kadhaa kumtafuta kwa njia nyingi kupata mawasiliano naye lakini imekuwa ngumu.

Nimewahi kukaa pale Kanisani zaidi ya wiki sijaonana naye, nilipowaona viongozi wa Kanisa lake wakaniambia niandike barua ndio nitafanikiwa kumuona, nikafanya hivyo kwa kuandika barua za zaidi ya 300 lakini sijafanikiwa.

Nimetuma SMS za simu nyingi tu lakini hakuna mafanikio, ninachokumbuka nimewahi kukutana naye mara kadhaa akiwa anaingia kwenye gari nikawa naishia kumsalimia “Shikamoo Baba”, basi baada ya hapo inaishi hivyohivyo.

Nimeshaenda nyumbani Mbezi Beach lakini sijafanikiwa kuonana naye, hata wiki mbili zilizopita nilienda nikakutana na mlinzi ambaye akaniambia niandike barua.

Nikawa najiuliza niandike barua tena? Akaniambia ndio utaratibu, nikajiuliza niandike barua kuingia nyumbani!
View attachment 2546433
Nakiri kuwa hali ya mazingira kama hayo ikanifanya niwe mlevi, mara kadhaa nikawa nalewa licha ya kuwa mimi sipendi pombe.

Kuna muda nilikuwa nalewa kisha naenda Kanisani kumtafuta baba yangu kutokana na mawazo, nilikuwa nalala hapohapo Kanisani lakini hakuna mafanikio.

Sijui kuna ukuta upi uliotokea kati yangu na baba hadi anifanyie yote hayo, nakumbuka mara ya mwisho kupata mrejesho ilikuwa wakati nahitaji vyeti vya Watoto, nilituma SMS zaidi ya 80, ndipo nikajibiwa kuwa nifike getini nikachukue hivyo vyeti.

Nilienda na nikasaini kisha baada ya hapo sijawahi kupata mrejesho wowote.

Nilikuwa kimya muda mrefu, lakini nimeamua kufunguka na kumtafuta, mimi sina madai yoyote kuhusu baba, kwamba ndani ya miaka yoye hiyo ambayo sijamuona nadai kitu fulani, Hapana.

Unajua yeye ndiye kanilea kuanzia nikiwa mdogo nina miaka mitatu.

Kuhusu ukaribu wa wadogo zangu na mimi haupo, sijui wanapokaa wala wao hawajui ninapokaa na wala sijawahi kukaribishwa wala kushirikishwa kama familia licha ya kuwa mimi ndio nilikuwa ninawalea kwa kuwa walinikuta kaka yao.

Naamini barua ambazo nimekuwa nikituma inawezekana zinamfikia au hazimfikii, hivyo nimeamua kutumia nafasi hii kuweka wazi ili kama kuna ukuta upo kati yetu uweze kubomoka.

Matatizo katika familia yapo na ni kawaida kutokea, sijajua tatizo lililopo kati yangu mimi na yeye (Kakobe), kiasi kwamba kumekuwa na ukuta huo mkubwa.

Mfano mimi sinywi pombe kwa starehe, lakini imetokana na mawazo na kuathirika kisaikolojia, pia kwa kuwa nimeathirika kimaendeleo basi hata familia yangu pia imeathirika kwa njia moja au nyingine.

Baba yangu ni mtumishi na ninajua ana upendo sana, naamini haya mambo anaweza kuyatatua watu wakasameheana kama kulikuwa na shida.

Pia nina dada yangu anaitwa Mage ambaye naye hajaonana na baba kwa muda mrefu inawezekana zaidi hata ya ilivyo kwangu.

Chanzo: OnTV
Hapa kuna mambo ya kujifunza passively:

Kulingana na yatokanayo.

1: Watoto kulelewa na wazazi/jamiii kwa kadri ya maadili mema.

2: Watoto kufuata maadili kwa kadri ya maelekezo ya wazazi na jamii.

3: Watoto wanapoamua kukisanua na kufuata yao, wahakikishe wanamaanisha. Usisuburi baadae huruma ya jamii na maandiko.

Maana kuna wakati ujuaji wa mtoto unaweza kumpa uchizi mpaka kifo mzazi/wazazi au watoto kuifanya safari ya mwisho ya mzazi.

NB: Yaliyoko kati yao wayajua wenyewe na baba yao wa sirini. Kama yaweza kusameheka au la ni jukumu lao. Usiubebe mzigo unaokuzalishia zambi zaidi.
 
Kwa hiyo unataka kusema kuwa hata wewe umekaza pumb* ukaachana na bababyako?

Kama baba yupo hai, kwa nini asimtafute?

Hataki kulelewa maana amesema alishalelewa naye bali anataka kuzungumza naye. Hofu yenu ni kuwa atadai mali
Mm sio kukaza pumbu tu hadi dushe that's why sitegemei mtu chini ya jua zaidi ya Mungu pekee ili kuweza kuishi.
Mm ni mstaafu sasa nakula pensheni tu + stahiki zangu.
Huyo anamtafuta baba yake ili aweze kuishi imagine kama angekuwa anamtafuta baba yake just kumsalimia tu na amehangaika mara zaidi ya mamia kwanini asiachane naye?
Huyo anataka Kitonga toka kwa baba yake trust me..))))
 
nilisoma Elimu ya Msingi Mwenge Mwaka 1986 hadi 1993 baada ya hapo nikaenda Real High School ipo Thiker Nchini Kenya

Baada ya hapo nikasomea masuala ya kompyuta nikapata Diploma katika chuo cha Techno Brain, sijui sasa hivi kinaitwaje.

Nina umri wa miaka 43,
Hesabu zinagoma! Miaka 43 ina maana kazaliwa 1980, kaanza standard One akiwa na Miaka sita? Kwa miaka ile ilikua ngumu
 
Katika pitapita zangu mitandaoni, nimekutana na makala hii inayohusu mahojiano aliyoyafanya huyu jamaa anaitwa Frank ambaye anasema ni mtoto wa Mchungaji Zachary Kakobe, nimeona si vibaya nikishea hapa inawezekana kama ni kweli basi ujumbe umfikie kwa urahisi mtumishi kwa kuwa najua JF ni platform kubwa na inafika mbali.

@@@@

Naitwa Frank Zachary Kakobe, mimi ni mzaliwa wa Tuliani, Wilayani Mvomelu Mkoani Morogoro, nilisoma Elimu ya Msingi Mwenge Mwaka 1986 hadi 1993 baada ya hapo nikaenda Real High School ipo Thiker Nchini Kenya

Baada ya hapo nikasomea masuala ya kompyuta nikapata Diploma katika chuo cha Techno Brain, sijui sasa hivi kinaitwaje.

Nina umri wa miaka 43, nina Watoto watatu na baada ya kuhitimu masomo yangu nilifanya kazi kadhaa za kiufundi.

Nia yangu ya kujitokeza kuzungumza hapa ni baba yangu apate taarifa juu ya uwepo wangu, tangu nilipoachana naye miaka 17 hadi 20 iliyopita, nimejaribu mara kadhaa kumtafuta kwa njia nyingi kupata mawasiliano naye lakini imekuwa ngumu.

Nimewahi kukaa pale Kanisani zaidi ya wiki sijaonana naye, nilipowaona viongozi wa Kanisa lake wakaniambia niandike barua ndio nitafanikiwa kumuona, nikafanya hivyo kwa kuandika barua za zaidi ya 300 lakini sijafanikiwa.

Nimetuma SMS za simu nyingi tu lakini hakuna mafanikio, ninachokumbuka nimewahi kukutana naye mara kadhaa akiwa anaingia kwenye gari nikawa naishia kumsalimia “Shikamoo Baba”, basi baada ya hapo inaishi hivyohivyo.

Nimeshaenda nyumbani Mbezi Beach lakini sijafanikiwa kuonana naye, hata wiki mbili zilizopita nilienda nikakutana na mlinzi ambaye akaniambia niandike barua.

Nikawa najiuliza niandike barua tena? Akaniambia ndio utaratibu, nikajiuliza niandike barua kuingia nyumbani!
View attachment 2546433
Nakiri kuwa hali ya mazingira kama hayo ikanifanya niwe mlevi, mara kadhaa nikawa nalewa licha ya kuwa mimi sipendi pombe.

Kuna muda nilikuwa nalewa kisha naenda Kanisani kumtafuta baba yangu kutokana na mawazo, nilikuwa nalala hapohapo Kanisani lakini hakuna mafanikio.

Sijui kuna ukuta upi uliotokea kati yangu na baba hadi anifanyie yote hayo, nakumbuka mara ya mwisho kupata mrejesho ilikuwa wakati nahitaji vyeti vya Watoto, nilituma SMS zaidi ya 80, ndipo nikajibiwa kuwa nifike getini nikachukue hivyo vyeti.

Nilienda na nikasaini kisha baada ya hapo sijawahi kupata mrejesho wowote.

Nilikuwa kimya muda mrefu, lakini nimeamua kufunguka na kumtafuta, mimi sina madai yoyote kuhusu baba, kwamba ndani ya miaka yoye hiyo ambayo sijamuona nadai kitu fulani, Hapana.

Unajua yeye ndiye kanilea kuanzia nikiwa mdogo nina miaka mitatu.

Kuhusu ukaribu wa wadogo zangu na mimi haupo, sijui wanapokaa wala wao hawajui ninapokaa na wala sijawahi kukaribishwa wala kushirikishwa kama familia licha ya kuwa mimi ndio nilikuwa ninawalea kwa kuwa walinikuta kaka yao.

Naamini barua ambazo nimekuwa nikituma inawezekana zinamfikia au hazimfikii, hivyo nimeamua kutumia nafasi hii kuweka wazi ili kama kuna ukuta upo kati yetu uweze kubomoka.

Matatizo katika familia yapo na ni kawaida kutokea, sijajua tatizo lililopo kati yangu mimi na yeye (Kakobe), kiasi kwamba kumekuwa na ukuta huo mkubwa.

Mfano mimi sinywi pombe kwa starehe, lakini imetokana na mawazo na kuathirika kisaikolojia, pia kwa kuwa nimeathirika kimaendeleo basi hata familia yangu pia imeathirika kwa njia moja au nyingine.

Baba yangu ni mtumishi na ninajua ana upendo sana, naamini haya mambo anaweza kuyatatua watu wakasameheana kama kulikuwa na shida.

Pia nina dada yangu anaitwa Mage ambaye naye hajaonana na baba kwa muda mrefu inawezekana zaidi hata ya ilivyo kwangu.

Chanzo: OnTV
Wako wengi aende Same atawakuta ndugu zake
 
Inaonekana huyu kijana Kuna vitu waliudhiana na Mzee wake..Kuna wazee wengi Sana walishawakataa na kuwafukuza watoto wao kisa Tabia zao au ukorofi wa mama zao...ila Kwa maelezo inaonekana huyu ni mtoto wake kabisa sio fake.....Mzee kakobe inaonekana hawa watoto aliwazaa kabla ya kupata wokovu au watoto wa ujana..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Kumbe Ni wa kwakwe

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Sasa kama una maisha yako na hakutaki kwanini umtafute?

Pili yaani baba yako na mama yako akukatae? Labda ni mtoto wa nnje mama kakobe anakaza

Apambane na maisha tu amuombe Mungu amsaidie apate fedha aache mambo ya kujikomba
 
Kwa nini unasema hivyo? Inawezekana matatizo tu ndio yanamfanya mtoto aonekane mzee zaidi
Nadhani Pombe ndo zimeleta athari lakini I hope atasaidiwa na mzee wake Pombe sio nzuri Sana kwa wanaume.
 
I see,ni kweli kabisa huyu ni Mtoto wa Askofu Kakobe,kaka wa Sifa,Ezekiel na mwingine mdogo..wakiishi Knyama mtaa wa Marehemu Mzee Kambangwa na Kusaga Ndege,..
Hebu Mzee wetu Askofu Kakobe,rudisha MOYO,kijana anaonekana kujirudi,msamehe na muonyeshe njia..
Miaka 43 anamwonyesha njia gani jitu zima hilo

Limtafute mzee kwa adabu tena za hali juu likiwa limeacha tabia zote mbovu lisije mdhuru Mzee Kakobe


Liandike tu linaishi wapi Mzee Kakobe atakuja kulifuata huko siku akijisikia lakini sio kwenda kumsumbua Kanisani au nyumbani na kwenda vyombo vya habari

Hana adabu
 
I see,ni kweli kabisa huyu ni Mtoto wa Askofu Kakobe,kaka wa Sifa,Ezekiel na mwingine mdogo..wakiishi Knyama mtaa wa Marehemu Mzee Kambangwa na Kusaga Ndege,..
Hebu Mzee wetu Askofu Kakobe,rudisha MOYO,kijana anaonekana kujirudi,msamehe na muonyeshe njia..
Njia anayotumia si sahihi anamnyanyapaa baba yake Mzee Kakobe
 
Amani iwe kwenu.
Katiba pitapita zangu nimekutana na hii clip ya Youtube inayoonesha Mtoto wa Askofu Kakobe akizungumza mahusiano na madhila anayopitia baina yake na baba yake yaani Askofu Kakobe. click hiyo link hapo uweze kuona mwenyewe umsikie.
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
Mtoto wa Askofu Kakobe aibuka na kusema
☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️☝️

Yesu katika mafundisho yake alitoa mfano wa Mchungaji na Kondoo aliyepotea ambapo aliselezea kuwa mwanakondoo mmoja alipotea hivyo mchungaji aliacha kondoo 99 zizini na kwenda kumtafuta mmoja aliyepotea. Inawezekana mfano huo usijenge dhana ya hili jambo la kifamilia.

Biblia takatifu katika Kitabu cha Luka 15: 11 - 32

Luka 15:11
Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili;

Luka 15:12
yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake.

Luka 15:13

Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.

Luka 15:14

Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji.

Luka 15:15

Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.

Luka 15:16

Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu.

Luka 15:17

Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.

Luka 15:18

Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;

Luka 15:19

sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.

Luka 15:20

Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.

Luka 15:21

Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.

Luka 15:22

Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;

Luka 15:23

mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;

Luka 15:24

kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.

Luka 15:25

Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.

Luka 15:26

Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?

Luka 15:27

Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima.

Luka 15:28

Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi.

Luka 15:29

Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;

Luka 15:30

lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.

Luka 15:31

Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.

Luka 15:32

Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.

Huu mfano unahusu kwa sehemu kinachoendelea kati ya Askofu Kakobe na Mtoto wake ambaye amesimama kutafuta uso wa baba yake kwa miaka inayokaribia 20.


Naamini kwa neema ya Mungu kila jambo litawezekana kwa kumtukuza Mungu
Usipotoshe maandiko kwa Issue ya mtoto wa Kakobe

Mwana mpotevu alienda kwa baba yake nyumbani tena akiwa na akili timamu huyo anasema amekuwa akienda hadi kanisani akiwa kalewa njwiii kutaka kuonana na baba yake kanisani anataka nini? Kwenda kalewa kanisani ambako baba yake anahudumu ? Kumwaibisha au kumharibu kisaikolojia apate presha are madhabahuni aanze ugomvi wa mirathi au nini? Lengo la kwenda kalewa kanisani kama sio kuharibu huduma ya baba yake mzazi ni nini?

Kwa hili nadimama na Kakobe mtoto alichofanya school na sio mtoto ana miaka 43 na ana watoto na kasema uchumi wake umeyumba kwa hiyo anataka Mzee Kakobe ampe sadaka za kanisani kwa nguvu na shinikizo?

Anachofanya ni kitendo cha unyasasaji wazee next time akifika akamatwe apelekwe polisi Mzazi akigoma kukuona ukiwa na miaka 43 sio kesi hutakiwi ku.force uhusiano

Baba kasema sikutaki to hell kila mtu aendelee na maisha yake


Wanasheria kanisani akija hapo.kanisani mpelekeni polisi awekwe ndani na mburuzeni mahakamani kwa kufanya fujo kanisani na kunyanyasa mzazi wake

Hata kama Mzee Kakobe hataki mpelekeni Polisi na mahakamani
 
Pombe ni nzuri ila ni mbaya kama ukiinywa ili ikuondolee mawazo .

Frank ni kijana wake kakobe hii ni kwa mujibu wa maneno yake yeye tulipokuwa tunakunywa gambe bukoba miaka ya tisini na kitu .

Ilikuwa ni ziara ya mzee wake huko kagera kulifungua kanisa la Full gospel lililopo pale Hamugembe miaka hiyo ndiyo nikiwa bar fulani nikapata kujuana na kijana na kunieleza kuwa ni mtoto wa Kakobe na pia amekuja kwenye uzinduzi wa hilo kanisa kipindi iko mimi nikiwa kwenye shughuli zangu .

Tukapoteana na kijana nikaja kumuona tena Dodoma mwaka 2014 akiwa ni mtangazaji katika kituo cha redio fulani .

Tukapata wasaa wa kunywa kama kawaida ila hakuwa kachoka kama nionavyo leo, ila baada ya pale sijaonana naye tena wala sikuwa na mawasiliano naye sababu sikuwa na kazi wala bond na yeye kwa lolote zaidi ya kulewa .

Ni hapo nilijua kuwa kweli kuwa mtoto wa mtumishi sio kuwa mtakatifu .

Ila kwa kawaida nahisi ni mwanaye kweli japo watakuwa walitibuana na mzee wake .

Kakobe mpokee mwanao wenzako wanatafuta watoto hawapati
 
Back
Top Bottom