Mtoto wa Zachary Kakobe: Mfikishieni salamu baba yangu namtafuta, sijaonana naye kwa Miaka 20, nikienda Kanisani sipati nafasi ya kumuona

Mtoto wa Zachary Kakobe: Mfikishieni salamu baba yangu namtafuta, sijaonana naye kwa Miaka 20, nikienda Kanisani sipati nafasi ya kumuona

Kwa umri wake miaka 43 ni mtu mzima haki yake lazima ipate approval ya mzazi na mzazi hata akitaka kumwona mwanawe kwake mtoto akiwa na umri huo lazima huyo mtu mzima mwanawe mwenye miaka 43 atoe approval kuwa mzazi ruksa njoo nione sio kushinikiza kuwa mimi mzazi lazima nije kwako mwanangu jitu zima miaka 43
Ni maoni yako binafsi
 
Mwana mpotevu alipokelewa na baba yake japo alikuwa amemkosea, hata huyu anastahili msamaha kama kweli alikosea.
Mwana mpotevu hakwenda kuomba msamaha akiwa kalewa na kupuliza bangi kama huyo wa Kakobe tofautisha
 
Mwana mpotevu hakwenda kuomba msamaha akiwa kalewa na kupuliza bangi kama huyo wa Kakobe tofautisha
Mchungaji mwema hawezi kuacha hata kondoo mmoja apotee kisa eti kuna wengine 99 wamebaki.
 
kwani ni mtoto wa nje ya ndoa? na je kama ni nje ya ndoa mama yake yupo wapi?
 
Si aende jpili kanisani kama waumini wengine ahakikishe siku hiyo baba ake yupo asubiri muda wa kutoa ushuhuda anaenda mbele aelezee kila kitu kinachomsumbua anakuwa ameshaonana na baba yake tayari
 
Huyo baba yake angekua choka mbaya huyo mtoto angekumbuka kumtafuta?
 
Kwa umri ule au ulevi wake ?
Ila haibadilishi ukweli kuwa ni mwanaye
Mtoto ni mtoto Pombe ni kila Mtu anakunywa na miaka 40 sio Mingi anabidi kutunzwa na kupewa haki zake za kutunza utu wake

Mchungaji mwema hawezi kuacha hata kondoo mmoja apotee kisa eti kuna wengine 99 wamebaki
 
I see,ni kweli kabisa huyu ni Mtoto wa Askofu Kakobe,kaka wa Sifa,Ezekiel na mwingine mdogo..wakiishi Knyama mtaa wa Marehemu Mzee Kambangwa na Kusaga Ndege,..
Hebu Mzee wetu Askofu Kakobe,rudisha MOYO,kijana anaonekana kujirudi,msamehe na muonyeshe njia..
Kijana anaitafuta miaka 50
 
Zee la miaka 43 linataka lilelewe na baba shenzi
 
Pengine kweli mtoto wake, ila nafikili kuhusu kuonekana Kama ni mzee pengine nae labda mwenzetu hapo zamani alipita pita kwenye kamnyweso kale ka kienyeji....pengine lakini!!
 
Hilo toto zima hilo miaka 43 liache kunyanyapaa huyo mzee Kakobe

Kama hataki kuonana naye aendelee na maisha hilo toto zee liache kunyanyapaa Mzee Kakobe nyumbani kwake na Kanisani liendelee na maisha yake yakikubali sawa yakigoma sawa si ya kwake na ndiyo aliyoyachagua zaidi ya miaka 20 iliyopita

Aendelee na maisha yake
Nadhani sasa unapambana na hisia zako.

Jipe muda uelewe undani wa hili suala. Mimi binafsi nimejiridhisha nimefika hadi kanisani hapo na kuweza kupata ukweli wa hili.

Nimefanikiwa pia kupata clue ya majirani wa familia pale Kijitonyama karibu na Mabatini alipokuwa anaishi mzee Kakobe.

Pia nimekuwa connected na jamaa walioshuhudia malezi ya huyo (hilo) mtoto unayetamani akaozee jela leo.

Kiufupi ni kuwa Askofu Kakobe hana sababu za kumkataa. Lakini unganisha dots kuwa hata wadogo zake wanamnyanyapaa hawana issue naye. Hapo ndipo mtu mwenye akili ya kupambanua anapata picha tatizo lipo wapi.

Kwa nini haujoulizi kuwa mbona hilo (huyo) totohamtafuti mama Askofu bali anataka tu kuzungumza na baba yake?

Unapokurupuka kukimbia mjusi bafu la.uswazi tena unatoka bila taulo hakuna ambaye atakuelewa unachokikimbia bali watapima uwezo wako wa akili na tukio la kukurupuka bila kujisitiri.

Jifunze kutafakari unaweza kuisaidia akili kufanya kazi hata once in your lifetime
 
Back
Top Bottom