Mtozi Alloyce Nyanda: Kuna watu wanamtumia Swai kumchafua Sabaya?

Mtozi Alloyce Nyanda: Kuna watu wanamtumia Swai kumchafua Sabaya?

Hadi mwakilishi wa umoja wa mataifa nchini alishangaa number plates zao kutumika na huyo jamaa kwenye tukio la uvamizi na kutaka kumuua Mbowe akiwa Kabeba silaha ya kivita
 
Mama Mama SSH pitia uzi huuu na ikikupendeza huyu jambazi umpumzishe anapostahili huku kesi zikifunguliwa juu yake.
 
Wangemleta mikoa ya wasiovumila kabisa ujinga aliofanya huyu Sabaya.
Sasa angekuwa historia.
Chalamila aliingia Mbeya kwa gia yake, aliambiwa tulia bwana mdogo,
Sasa amekuwa joker.
Mimi nimewashangaa mno wakionewa eti kisa Mkuu wa wilaya aisee...
 
Bwana wako Sabaya akiifanya Hai kama nchi yake, akadharau hata RC sasa unataka aendeelee kufanya Ugaidi? Kafanyieni kitandani sasa awamu hii ya sita hailei magaidi
 
Nimepitia uzi mzima, out of messages 113, nimepata message tatu tu zinazomtetea Sabaya.

Haihitaji rocket science kungamua kwamba Sabaya ni jangili na hafai kuwa kiongozi pia hafai kuishi kwenye jamii, huyu panapomfaa kwa sasa ni jela maana evidence zipo wazi.
 
Kwa siku za hivi karibuni kumeibuka video mbalimbali zikiwemo za baadhi ya viongozi wakifanya matendo yakinyama kwa Raia . Kwa Taifa changa kama letu na kwa mitandao ilivyozagaa video hizi zinaangukia mikononi mwa watoto. Wanapoona namna wazazi wao wanavyonyanyaswa, wanavyoona namna viongozi wanavyotawala, wanavyoona hakuna mzee au Kiongozi katika ngazi ya Taifa anayechukua hatua wanajenga chuki na nchi yao.

Hii siyo njia sahihi yakulea Taifa, hii siyo njia sahihi yakuongoza Taifa, hii siyo njia sahihi yakukuza viongozi, haya ni matendo yakinyama na yanayonajisi Taifa letu.

Kwa picha na video hizi za akina Sabaya timu yake, kwa aina hii ya dharau baina ya wateule wa Rais ni wazi tumefika wakati wa baadhi yetu kuwa slave na wengine kuendelea kuwa slave master.

Ni mtizamo wangu Kama mzazi, mnaosambaza hizi video mwache msiendelee kupandikiza chuki kwa watu. Watawala tulionao wameshaona namna wanavyotawala na wameridhika na aina hii ya kututawala. Please tuvumilie haya machungu bila kuwarithisha watoto wetu, wazazi msiwashirikishe watoto dhambi hii mtawaaribu kifikra na kisaikologia.

Niombe msizisambaze hazina afya kwa ustawi wa nchi yetu, zinatweza Utanzania wetu, zinadhalilisha uchumi wetu na zinafukuza wawekezaji na majirani wema, zinatutenga na Dunia, zinaifanya Tanzania ionekane nchi yenye viongozi katili Duniani na wasioguswa.
 
Nimepitia uzi mzima, out of messages 113, nimepata message tatu tu zinazomtetea Sabaya.

Haihitaji rocket science kungamua kwamba Sabaya ni jangili na hafai kuwa kiongozi pia hafai kuishi kwenye jamii, huyu panapomfaa kwa sasa ni jela maana evidence zipo wazi.
Na hizo tatu moja inahoji kuhusu kuwekwa video hadharani huyu tunamtoa kwenye tatu za kumtetea sabaya.
 
Ndugu yangu ukitaka kumtetea sabaya utaishia kuchafuka mwenyewe. Hata umtoe swai katika masuala aliyowahi kufanya sabaya ni mengi. Muulize nandy alichofanyiwa pale weruweru mountain lodge usiku sabaya akiwa na genge lake.
Alifanyiwa nini mkuu?
 
Back
Top Bottom