Mtu anayejenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege (columns), ni imara kweli?

Mtu anayejenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege (columns), ni imara kweli?

Kwa sababu hilo jengo limejengwa iringa haimaanishi jengo linaweza jengwa sehem yeyote hapa duniani.

Kinacho detarmine sustainability ya jengo sio "limesha wahi kujengwa iringa" bali ni nature ya udongo pamoja structural design iliyo fanywa na injinia (namaanisha injinia sio fundi wa mtaani).
Mkuu ubarikiwe. Umenifungua sana macho
 
Unasema uzoezi je ni uzoefu gani na wa nani?

Na huo uimara wa kuta ya chini unaupimaje ili kukiridhisha ni imara? Unaweza kutupa kipimo chake ili na sisi tujue ni imara?

Je hiyo nguzo kutoka chini inatofauti gani na ujenzi kwa kutumia columns?

Ujue unapojenga nyumba ya kuishi watu unaongelea uhai wa watu mkuu!!
Ni kweli mkuu. Asante
 
Inawezekana kabisa... nimejenga gorofa 1 bila kutumia nondo, matofali ya chini ni ya inch 6 na yamelazwa.. nyumba ni imara haina nyufa zozote.. mwaka wa 15 sasa
 
Kuna Eng. Mkali humu.. hataki kabisa mambo ya kuhisi inawezekana.
 
Shida sio ghorofa tatu hata 10 wenda ukajenga! Swali ni je kuna scientific/engineering logic behind hilo jibu?

Na ndio mana kwenye posti yangu ya awali nilimshauri ajiridhishe hilo kutoka kwa injinia!

Maana siku hilo ghorofa likianguka tujue tunaanzia wapi sio aje atuambie aliambiwa ajenge tu bila colums!
Mim makubaliano na mapendekezo yako kwamba kila ujenzi lazima mtalaamu ahusishwe ktk hatua zote muhimu kutokana aina ya jengo na eneo linakojengwa .Ni kwel tofali zinaweza kujenga mpaka ghorofa 4 to maximum ili mradi tu wazingatie ubora wa materials na aina ya udongo .mfano mzuri ni ghorofa polisi ufundi kilwa road dsm na Jeshi pale mwenge.
 
Unaweza kujenga, ila tu inabidi ulaze tofari na hizo tofari unazolaza inabidi ziwe na compression strength ya 4.5 yaani (atleast mfuko mmoja wa cement 42.5 itoe tofari 25) ambapo tofari moja uwa ni Tsh 1800 ziwe cured na zimekaa siku 21 tokea kufyatuliwa, usitumie tofari ya Tsh 1000/1200. Pia hapo hapo partitions za vyumba vya chini visizidi span ya mita 4 bila kuwa na ukuta.
Kuongezea tu hapa, ghorofa bila nguzo zinaitwa kitaalamu (load bearing structures) na zile za nguzo zinaitwa (frame structures). Ni vizuri kujiridhisha kwa kusoma na kuwafata wataalaam na sio washinda katika mitandao
 
Samahanini wadau naomba kujua hivi kujenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege zile. Uimara wake ukoje?

Engineer anadai kwa aina ya udongo ukiwa na matofali imara yakajengwa kwa kulaza inatosha.

Ni kweli inaweza kuwa imara? Eneo ni tambarare.

Naombeni mawazo yenu
Tofautisha ghorofa na nyumba zilizobebana! Pale Goba walijenga nyumba zilizobebana wakadhani wanajenga ghorofa!

Hata mchwa wanaweka nguzo kwenye zile basement zao!
 
1. Huyo injinia umejiridhisha ni injinia kweli?

Maana siku hizi hata darasa la saba au watu wenye diploma za ujenzi wanajiita mainjinia. Kujirisha mwambie akupe muhuri wake wa ERB kama asipokupa mwambie cheti na uhakikishe kiwe cha degree ya civil engineering.

2. Je hilo jengo ghorofa ngapi?

3. Je kuna structural analysis yeyote aliyo fanya ili kuthibitisha anachosema? Kama anayo amekupa? Je kama amekupa ina muhuri wa mhandisi aliye sajiliwa na bodi ya wahandisi Tanzania?

4. Je huyo injinia wako alikushauri ufanye soil analysis ili kujua nature ya udongo kabla hajaja na hilo jibu alilo kupa?

Naomba nijibu maswali yote ili tuendelee.
Cha kwanza ulicho feli ni kuamini katika degree hapo ndipo ulipo feli na nikaudharau uzi wako wote na ujuzi wako wa kwenye madaftari.
 
Unaweza kujenga, ila tu inabidi ulaze tofari na hizo tofari unazolaza inabidi ziwe na compression strength ya 4.5 yaani (atleast mfuko mmoja wa cement 42.5 itoe tofari 25) ambapo tofari moja uwa ni Tsh 1800 ziwe cured na zimekaa siku 21 tokea kufyatuliwa, usitumie tofari ya Tsh 1000/1200. Pia hapo hapo partitions za vyumba vya chini visizidi span ya mita 4 bila kuwa na ukuta.
Kuongezea tu hapa, ghorofa bila nguzo zinaitwa kitaalamu (load bearing structures) na zile za nguzo zinaitwa (frame structures). Ni vizuri kujiridhisha kwa kusoma na kuwafata wataalaam na sio washinda katika mitandao
Wewe umejibu kitaalam kabisa 100%
 
Salaam

Naombeni msaada kuhusu hizo nguzo za geti.
Naambiwa na kijana wa zege kuwa wakati fundi anajenga hapo hizo nguzo kuwa hawakuchimba msingi mrefu kwenda chini na hana hakika kama waliweka kitako chini.

Bahati mbaya fundi alikimbia kabla ya kazi kukamilika na pia hapatikani kwa simu.
Sasa naombeni msaada wa kitaalamu hapo nifanye nini??
Je nivunje hizo nguzo zisukwe upya ama tufanyie ukarabati ili kuweza kuziimarisha hizo nguzo.

Mimi nipo mbali nashindwa kusimamia kwa ukaribu ujenzi.

Tafadhali naomba maoni yenu ya kitaalamu

Trendz
Upepo wa Pesa Equation x
IMG-20220102-WA0000.jpeg
 
Samahanini wadau naomba kujua hivi kujenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege zile. Uimara wake ukoje?

Engineer anadai kwa aina ya udongo ukiwa na matofali imara yakajengwa kwa kulaza inatosha.

Ni kweli inaweza kuwa imara? Eneo ni tambarare.

Naombeni mawazo yenu
Kwa jengo la gorofa moja hakuna tatizo. Isipokuwa uzingatie uimara wa tofali na msingi. Pia nguzo baadhi ya sehemu zenye uwazi mpana jengo la chini au ground floor zinatakiwa ili kuweka uimara wa jengo la juu.
 
Salaam

Naombeni msaada kuhusu hizo nguzo za geti.
Naambiwa na kijana wa zege kuwa wakati fundi anajenga hapo hizo nguzo kuwa hawakuchimba msingi mrefu kwenda chini na hana hakika kama waliweka kitako chini.

Bahati mbaya fundi alikimbia kabla ya kazi kukamilika na pia hapatikani kwa simu.
Sasa naombeni msaada wa kitaalamu hapo nifanye nini??
Je nivunje hizo nguzo zisukwe upya ama tufanyie ukarabati ili kuweza kuziimarisha hizo nguzo.

Mimi nipo mbali nashindwa kusimamia kwa ukaribu ujenzi.

Tafadhali naomba maoni yenu ya kitaalamu

Trendz
Upepo wa Pesa Equation x
View attachment 2067495

Kazi ya nguzo (column) ni kusafirisha loads(mzigo) kwenda ktk ground na kazi ya kitako (Footing) ni kupunguza presha ya udongo inayotokana na mzigo uliobebwa juu.
1. Nguzo zako hazina mzigo wowote uliobebwa juu
2.Kuna aina tofauti za columns na sio kila column lazima iwe na footing.
3. Ukiangalia vizuri ktk picha umetuma kuna beam iliungwa na nguzo ya geti inamaana geti lako halitacheza.
4. Kwa rangi ya udongo wako ninaoona hapo yani wala usipate stress sana kuwa zitadondoka labda tu hiko kibonde kiwe kina erosion hapo utakuwa na tatizo.

Kwa ushauri soma Vizuri nilichoandika number 3
IMG_7144.jpg
 
Samahanini wadau naomba kujua hivi kujenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege zile. Uimara wake ukoje?

Engineer anadai kwa aina ya udongo ukiwa na matofali imara yakajengwa kwa kulaza inatosha.

Ni kweli inaweza kuwa imara? Eneo ni tambarare.

Naombeni mawazo yenu
Kuna perception 2 hapa.
1. Kama hatumii nguzo (column) atalazimika kufanya Walls transformation kutoka non load bearing to load bearing walls kitu ambacho economically itakugharimu sana.
2. Kama atatumia nguzo (column) hapa load transformation itakuwa controled na column at the same place walls zitabaki kuwa material ya kawaida.
Ushauri: Ujenzi wowote wa holera huleta unafuu wa muda mfupi na hasara ya muda mrefu. You have to design the stated building and checked before implementations
Thanks
 
Kazi ya nguzo (column) ni kusafirisha loads(mzigo) kwenda ktk ground na kazi ya kitako (Footing) ni kupunguza presha ya udongo inayotokana na mzigo uliobebwa juu.
1. Nguzo zako hazina mzigo wowote uliobebwa juu
2.Kuna aina tofauti za columns na sio kila column lazima iwe na footing.
3. Ukiangalia vizuri ktk picha umetuma kuna beam iliungwa na nguzo ya geti inamaana geti lako halitacheza.
4. Kwa rangi ya udongo wako ninaoona hapo yani wala usipate stress sana kuwa zitadondoka labda tu hiko kibonde kiwe kina erosion hapo utakuwa na tatizo.

Kwa ushauri soma Vizuri nilichoandika number 3
View attachment 2068574
Ahsante mkuu Trendz
Hapo juu ya nguzo kuna slab nyembamba alafu na tofali zimelazwa 40.

Je kuna namna ya kuimarisha hizo nguzo ziwe imara mara dufu?
Mimi huwa sipendi vitu vya wasiwasi.
 
Acha kucomplicatisha maisha, unahitaji detailed structural analysis umetoa hela??
Mtu kauliza amejibiwa shida iko wapi??

Anyways, Hakuna shida, mimi ni engineer tena structural na nina muhuri kabisa wa ERB.

Nasema hivi, INAWEZEKANA TENA BILA SHIDA YEYOTE KUJENGA JENGO HATA LA GHOROFA TATU BILA KUTUMIA COLUMNS.

Ukiwa na tofari za kuchoma itakuwa nzuri zaidi kuliko hizi za block za mtaani.

Maana tofari za kuchoma constantly zina bearing capacity kubwa ukilinganisha na za block ambazo nyingi ni za michongo
Ila hata hizo tofali za kuchoma dio hizi za USWAHILINI labda ziwe kana ziler ZA NYANKALI - DODOMA
 
Back
Top Bottom