Mtu anayejenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege (columns), ni imara kweli?

Mtu anayejenga gorofa bila kusimamisha nguzo za zege (columns), ni imara kweli?

Bwana mhandisi kwanza nikupe pole maana umedandia treni kwa mbele! Ilibidi uelewe mada imeanzia wapi kwanza kabla ya kukimbilia kujibu.

Nilicho andika sio kwamba mimi nataka hizo designs kiasi kwamba uniambie nitoe ela. Hoja iliyo kuwepo ni kwamba tulimshauri mleta mada aombe hivyo vitu kutoka kwa injinia wake. Na sio mimi nilikua naomba. Umeelewa?

Pia umetoa jibu ya kwamba inawezekana kujenga hata ghorofa tatu.

Hili ni jibu ambalo siwezi siwezi lisemea chochote au nikalikubali maana halina any logic ya kuniwezesha mimi kuli prove!

Na ndio maana nikamshauri mleta mada kabla hajachukua ushauri wa injinia wake amuulize kama ana structural design and analysis inayo support jibu alilo pewa!

Then kutokea hapo anaweza fanya maamuzi!

Nadhani umeelewa mkuu!
Wewe kazi yako kupinga tu, maswali mengi Ila huna majibu sahihi...wacha wazoefu na wataalamu wajibu.
 
Unaweza kujenga, ila tu inabidi ulaze tofari na hizo tofari unazolaza inabidi ziwe na compression strength ya 4.5 yaani (atleast mfuko mmoja wa cement 42.5 itoe tofari 25) ambapo tofari moja uwa ni Tsh 1800 ziwe cured na zimekaa siku 21 tokea kufyatuliwa, usitumie tofari ya Tsh 1000/1200. Pia hapo hapo partitions za vyumba vya chini visizidi span ya mita 4 bila kuwa na ukuta.
Kuongezea tu hapa, ghorofa bila nguzo zinaitwa kitaalamu (load bearing structures) na zile za nguzo zinaitwa (frame structures). Ni vizuri kujiridhisha kwa kusoma na kuwafata wataalaam na sio washinda katika mitandao
Asante sana mkuu. Shida ni sehemu gani ya kupata hizo tofali kwa DAR? Fundi niliyemtumia ni mzoefu sana ana age almost 70 na mjenzi toka ujana wake. Nilishangaa kukuta msingi hauna hizo colums siku nafika site namwuliza anasema hakuona haja ya kuweka kwa sababu udongo ni mzuri sana hivyo nitafute tu tofali imara za floor ya kwanza.
Nilishindwa kugombana nae kwa sababu ni mtu mzima sana na amesaidia watu wengi na amejenga magorofa mengi.
Kwa sababu natamani kupata nyumba IMARA natamani kumwomba tuvunje zile sehemu ambazo ni critical tuweke colums.

Nimeshindwa kumwamini anachoniambia maana KILA NYUMBA YA GOROFA NAYOIONA INA COLUMS.

NA NAOMBA NIKIRI KUWA KWENYE UJENZI HUU WA GOROFA SIFAHAMU CHOCHOTE.
Eng. americomend haina shida nipate tu tofali IMARA.
Kwa DAR NAZIPATA WAPI? na pia inweza kuwa gharama kuliko angeniwekea hizo columns.
 
Back
Top Bottom