Mtu hatoki ndani asubuhi hadi jioni lakini analipa kodi na bills zote kwa wakati

Hiyo ndo shida yenu wanawake kuchunguza maisha ya watu! Usiishi kwa kukariri, huenda ni mtu wa forex trading au blogger...kwanza unapata wapi muda wa kufatilia maisha ya watu!? Umasikini mbaya sana aisee.
 
Watanzania tuna tabia za kishamba na kimasikini sana.
 
Mpaka Leo hii haujui kama Kuna Hela za "kudownload" wewe..............!
 
Mkuu ujinga unakuwa mzigo wakati mwingine,wewe unataka umuone mtu kachafuko nguo kwa rangi,au grisi au tope ndio ujue anafanya kazi au atoke asubuhi na kurudi jioni, watu wanatengeneza pea vyubani huku wamelala kitandani,tena hutengeneza pesa mamilioni,mitandao,simu, laptops ndio ofisi siku hizi,wala huhitaji hata kwenda benki ni msj tu unaingiza pesa, au umesahau kipindi cha UVIKO aka Corona watu walikuwa wanafanya kazi wakiwa majumbani mwao ni sawa na mtu yupo Bongo lakini anafanya kazi na walioko Marekani au Ulaya au Uchina na kwingineko. Tabu ya kuishi uswahilini na nyumba za NHC ndio hizi.
 
Ninachoelewa mzee ukijilinganisha na maisha ya watu utakonda mzee, kuna watu familia zao zimeshawaset vizuri, unakuta mtu kama huyo ana kodi zake kadhaa anapokea za kupewa, ana uhakika wa mwaka mzima, atoke aende wapi?
 
Sikuhizi kuna njia nyingi sana za kupata fedha na kuinua uchumi wako, usikariri zile traditional ways kwamba lazima uingie mzigoni mzima mzima ndio upate pesa

1. Kuna Remote work. Mtu ana ofisi home ni Pc yake tu mchezo umeisha.

2. Freelancers, watu wanatafuta madili, yakitiki ndio wanaenda piga, unahisi wameenda kutembea kumbe mchongoni, na wengine wanapigia online, Upwork etc.
3. Passive investment, watu wengine walijiwekea plans za ku retire mapema, so wamejiwekeza, miradi,hisa, UTT, Hati fungani gawio wanalopata linawatosha.

Ukisoma kitabu cha Millionaire next door utaelewa, kuna watu mnaweza kuwa mnaishi nao kitaa ,but wana ukwasi na hawahtaj kukuonyesha au kukupa ishara.

4. Support, kutoka kwa ndugu, Mpenzi, wazazi etc. humu inahuisha wadangaji piaaa..

5. Matapeli, Kuna watu wanapiga madili ya ku scam watu mitandaon etc.
Maisha ni siri ,watu wana sirii sanaaaaa, siri maana yake ni fumbo huwezi kulijua.
 
Wee mkazi wa Tanga? Mambo hayo ya kuchunguzana Dar hayapo.
 
Acheni tabia zenu za kishenzi kuchunguza maisha ya watu! Acheni roho za kichawi , fanyeni kazi.
 
Mumefahamiana tokea udogoni! Au mumekutana tu ukubwani?
Isije kuwa wakati yeye anahaso wewe ndo kwanza wazazi wanajadili wakapande karanga Ili upatikane.
 
Trading huna haja ya kwenda ppt ni ww na simu yako or kompyuta mpakato na bando lako,unaweza waziwa vitu vya ajabu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…