Mtu huyu akisimama na mgombea wa CCM mwaka 2025, ni lazima CCM tuangukie pua

Mtu huyu akisimama na mgombea wa CCM mwaka 2025, ni lazima CCM tuangukie pua

Kwani ushauri hutolewa kwa namna gani mkuu?
Ndo kwanza naingia humu, bado nina maluweluwe. Ngoja nitulie kwanza, maanake naona kuna mengi ya kujadili kati yetu.
Nimeweka mstari wa nyongeza katika bandiko hilo ulilojibu sasa hivi. Tafadhali nenda kausome.
 
Ndo kwanza naingia humu, bado nina maluweluwe. Ngoja nitulie kwanza, maanake naona kuna mengi ya kujadili kati yetu.
Nimeweka mstari wa nyongeza katika bandiko hilo ulilojibu sasa hivi. Tafadhali nenda kausome.
Ok mkuu ubarikiwe sana kwa kujibu hoja kielimu zaidi tofauti na baadhi ya wachangiaji wengine wanaojibu hoja in somehow.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Ndugu wana JF wenzangu na watanzania wenzangu, ili chama cha CCM kiweze kushindwa katika uchaguzi mkuu wa 2025 au 2030, yanahitajika mambo matatu.

1) Kwanza: kinahitajika chama imara cha upinzani chenye sera nzuri, zinazoeleweka na kutekelezeka. Chama hicho kiwe na sura ya kitaifa, kiwe na viongozi wakweli, wenye maono na misimamo thabiti ya kuikomboa nchi. Kiwe na mifano hai ya utekelezaji wa sera zake kupitia chama husika ili kiweze kuaminika machoni mwa watanzania wengi.
a) Sio mtu useme chama chetu kina misingi ya demokrasia wakati mwenyekiti wa chama ambacho kingekuwa mfano wa demokrasia hiyo ana miaka 20 madarakani.​

b) Sio mtu useme chama chetu ni cha maendeleo, wakati wanaoendelea katika chama ni mwenyekiti wa chama taifa na genge lake, huku chama chenyewe kikiwa hakina hata ofisi ya kufanyika mkutano wa ndani.​

c) Sio mtu useme chama chetu kitasimamia utawala bora na haki, huku ndani ya chama chenyewe hakuna anaeweza kuongelea lolote mbele ya mwenyekiti wa chama au makamu wake.​

2) Pili: Anahitajika kuchaguliwa mgombea ambae hana makandokando ya uongo, uoga, unafiki na mwenye uwezo wa kweli wa kusimamia sera za chama chake bila kuyumbishwa na mtu yoyote iwe ndani ya chama au nje ya chama.

a) Sio kiongozi anakuwa na kauli za kilaghailaghai kwa maslahi yake binafsi ya kisiasa, na kiuongozi (kama tunavyoona hapo chini pichani) bila kujali madhara yatokanayo na ulaghai huo. Mtu wa aina hii ni ngumu kuchaguliwa maana watanzania wa sasa sio wale wa 2001, kule Zanzibar ambapo watu walikufa, kujeruhiwa na kufungwa, huku muhusika aliepiganiwa (aliekuwa katibu mkuu wa chama, na mgombea wa upinzani) akiwa Saudia Arabia kula tende na maswaiba zake. Mgombea akiwa hana msimamo thabiti wa kusimamia sera au hoja zake mwenye, basi hata Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Marekani ikija kusimamia uchaguzi bado ataangukia pua tu.​

3) Tatu: Tume huru isiyoegemea upande wowote wa kisiasa. Tume iwe na viongozi kutoka vyama mbali mbali vya kisiasa na kiraia ili kujenga sura ya utaifa katika tume hiyo.

Ni hayo tu ninayoyaona mimi, katika kuijenga Tanzania bora zaidi ya kesho.

Asanteni sana.

View attachment 2319901View attachment 2319903View attachment 2319904View attachment 2319911View attachment 2319912
Crap
 
Kwani zito ni mpinzani?
Ni mpinzani wa makaratasi, ila kiroho ni miongoni mwa wapinzani butu waliotengenezwa na mfumo ili kuihadaa dunia kuwa Tanzania kuna demokrasia ya vyama vingi. Na matokeo yake misaada inayotumwa kwa ajili ya kukuuza na kuimarisha demokrasia hiyo inaliwa na wajanja wachache walio serikalini, CCM na Upinzani. Kama hautojali rudi juu kidogo kasome post namb #20 utaelewa nilichoandika hapa.
 
Ndo kwanza naingia humu, bado nina maluweluwe. Ngoja nitulie kwanza, maanake naona kuna mengi ya kujadili kati yetu.
Nimeweka mstari wa nyongeza katika bandiko hilo ulilojibu sasa hivi. Tafadhali nenda kausome.
Unaweza pia pitia post namb #20 kwa kaufafanuzi fulan. Just thinking tu maana moyo wa mtu msitu. Na ni Mungu pekee anaejua yaliopo mioyoni mwetu.
 
Mkuu ukisoma post yangu namb #20 utaelewa tu kwamba matukio mengi yanaweza kuwa ya kutengenezwa ili watu wavute mpunga kwa njia ambazo mimi na wewe hatuzijui. Tusikimbilie kuamini kila linalosemwa na mwanasiasa kwani tumeshajifunza mengi kupitia kauli zao.
Mfano chukulia 2008 mwanasiasa anakwambia Lowasa ni fisadi na ushahidi anao, afu 2015 mwanasiasa huyo huyo anakwambia Lowasa sio fisadi, kama kuna mtu ana ushahidi na ufisadi wake basi apeleke ushahidi huo polisi nk. Nafikiri Lissu anaweza kuwa mpinzani wa kweli ndo maana yalimkuta yaliomkuta. Na kamwe mpinzani wa kweli ni ngumu kupewa nafasi ya juu (mwenyekiti) kuongoza chama, maana anaweza kubadili maelewano yaliopangwa na waanzilishi wa system ya vyama vingi.
Ndiyo hii uliyonirejea (refer)?

Hapana, bado tunapishana sana.
Ila najuwa unastahili kupewa maelezo ya kina katika kupishana kwetu, na muda huo sasa hivi haupo. Nitaangalia njia ya kuja hapa tena kueleza tunavyopishana.
 
sisiemu kuanguka hilo swala litoe kichwani na wakianguka wametaka wao wenyewe hvi unaijua sisiemu ww sio watu wa nchezo kwenye swala a nani aiongize nchi
 
Ndiyo hii uliyonirejea (refer)?

Hapana, bado tunapishana sana.
Ila najuwa unastahili kupewa maelezo ya kina katika kupishana kwetu, na muda huo sasa hivi haupo. Nitaangalia njia ya kuja hapa tena kueleza tunavyopishana.
Ok mkuu, sisi wote tupo hapa kwa ajili ya kujadili namna ya kulijenga taifa lenye kesho nzuri kwa vizazi vyetu. Ni tofauti na wanasiasa ambao 98% wapo kwa ajili ya kuijenga kesho nzuri yao na ya vizazi vyao. Huku wakituhadaa sisi wafuasi wao wa vyama kuwa wanatusaidia kutujengea kesho yetu.
 
Inshaallah. Ki ukweli kuna watu wameshaichoka CCM, ila sasa hawaoni mbadala wa chama cha kuitoa CCM madarakani. Vyama vyote ukivichunguza havina tofauti na CCM mpaka inafikia kipindi watu wanahisi huenda huu upinzani ulitengenezwa maalum na CCM ili kuihadaa dunia kuhusu demokrasia nchini. Kwahiyo misaada inayoletwa na mabeberu kwa ajili ya kukuza na kuimarisha demokrasia inaliwa na wajanja wachache walio ndani ya serikali, CCM na upinzani butu.
Hakuna lililo la maana zaidi kuliko kuiondoa CCM kwenye madaraka wakati huu. CCM kung'ang'ania kutawala kwa mabavu kwa kutumia vyombo vya dola haihitaji kuwepo na chama chenye sera bora zaidi kama uwezo wa kuondoa mkandamizaji inawezekana.

Kipaumbele kwa Tanzania sasa hivi ni kuiondoa CCM, mambo ya sera na mengine yatafuata baadae.
This is how serious it has become.
 
Hakuna lililo la maana zaidi kuliko kuiondoa CCM kwenye madaraka wakati huu. CCM kung'ang'ania kutawala kwa mabavu kwa kutumia vyombo vya dola haihitaji kuwepo na chama chenye sera bora zaidi kama uwezo wa kuondoa mkandamizaji inawezekana.

Kipaumbele kwa Tanzania sasa hivi ni kuiondoa CCM, mambo ya sera na mengine yatafuata baadae.
This is how serious it has become.
Mkuu kuiondoa CCM bila kujua huyo atakaeiondoa CCM atakuja na sera au mikakati gani ya kuijenga nchi, ni sawa na mtu anaeacha kazi bila ya kuwa na plan ya kazi nyingine.

Wakati nchi za magharibi zinaivamia Libya, kuna walibya wengi walifurahia uvamizi ule wakiamini kuwa ndio ilikuwa njia ya wao kuanza kuishi maisha kama wanayoishi wazungu huko ulaya na amerika.
Sasa hivi miaka 10 baada ya Gadafi kung'olewa na kuuwawa, walibya wale wale wanajuta na kutamani utawala ule wa Gadafi ungeendelea tu kulikoni huu uliopo sasa ambao kwao ni majanga makubwa. Hivyo hivyo kwa nchi nyingine kama Iraq, Sudan kusini, kaskazin nk.

Kwahiyo mkuu kusema tu CCM itoke bila kujua huyo atakaeingia baada ya kutoka atakuwa na mikakati gani ni kujivika kitanzi ambacho hapo baadae yakija kutukuta ya zaidi ya haya yanayofanywa na CCM tutashindwa kukitoa shingoni. Malawi kila siku wanabadili vyama lkn hali inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku, halikadhalika Zambia pia.

Wanasiasa ni kama wacheza mpira. Anapokuwa nje ya uwanja atakwambia dah ingekuwa mimi ndo niko uwanjani mechi hii ningefunga hata magoli kumi.
Lakini ukimuingiza acheze hana la maana atalofanya mpaka mechi inaisha.
 
Mkuu kuiondoa CCM bila kujua huyo atakaeiondoa CCM atakuja na sera au mikakati gani ya kuijenga nchi, ni sawa na mtu anaeacha kazi bila ya kuwa na plan ya kazi nyingine.
Bado huelewi ninachosema.

Hakuna kipaumbele Tanzania kuliko kuondoka kwa CCM madarakani.
Hicho ndiyo kipaumbele zaidi vingine vyote sasa hivi.

Unapopata dharura na kutaka kuondoka kwenye dharura huna anasa ya kupanga hayo mengine yafuatayo. Hayo yatakuja baada ya kuondokana na dharura.

Sasa kama bado huelewi ninachosema hapa, hutaki kuelewa na hutaelewa kamwe hata nikiandika na wino wa dhahabu.
 
Wakati nchi za magharibi zinaivamia Libya, kuna walibya wengi walifurahia uvamizi ule wakiamini kuwa ndio ilikuwa njia ya wao kuanza kuishi maisha kama wanayoishi wazungu huko ulaya na amerika.
Sasa hivi miaka 10 baada ya Gadafi kung'olewa na kuuwawa, walibya wale wale wanajuta na kutamani utawala ule wa Gadafi ungeendelea tu kulikoni huu uliopo sasa ambao kwao ni majanga makubwa. Hivyo hivyo kwa nchi nyingine kama Iraq, Sudan kusini, kaskazin nk.
Nilijua toka mwanzo unapolalia na mada yako hii.
Unaleta mifano ya ajabu sana katika mjadala usiohusiana kabisa na hiyo mifano.

Ngoja nimalizane nawe kwa kukueleza kuwa haijalishi CCM iliyopo sasa inaondoka vipi, na haina maana kuwa mageuzi hayawezi kutokea huko huko ndani ya CCM.
 
Kwahiyo mkuu kusema tu CCM itoke bila kujua huyo atakaeingia baada ya kutoka atakuwa na mikakati gani ni kujivika kitanzi ambacho hapo baadae yakija kutukuta ya zaidi ya haya yanayofanywa na CCM tutashindwa kukitoa shingoni. Malawi kila siku wanabadili vyama lkn hali inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku, halikadhalika Zambia pia.

Wanasiasa ni kama wacheza mpira. Anapokuwa nje ya uwanja atakwambia dah ingekuwa mimi ndo niko uwanjani mechi hii ningefunga hata magoli kumi.
Lakini ukimuingiza acheze hana la maana atalofanya mpaka mechi inaisha.
Ni dhahiri toka mwanzo wewe ni mfaidika wa uozo huu wa CCM iliyopo sasa. Najaribu kujikumbusha michango yako ya huko nyuma. Nikikumbuka vizuri ni kama tuliwahi kujibizana kwa kiasi juu ya misimamo yako hapa hapa JF.
 
Ni mpinzani wa makaratasi, ila kiroho ni miongoni mwa wapinzani butu waliotengenezwa na mfumo ili kuihadaa dunia kuwa Tanzania kuna demokrasia ya vyama vingi. Na matokeo yake misaada inayotumwa kwa ajili ya kukuuza na kuimarisha demokrasia hiyo inaliwa na wajanja wachache walio serikalini, CCM na Upinzani. Kama hautojali rudi juu kidogo kasome post namb #20 utaelewa nilichoandika hapa.
Nimekuelewa mkuu.
 
Bado huelewi ninachosema.

Hakuna kipaumbele Tanzania kuliko kuondoka kwa CCM madarakani.
Hicho ndiyo kipaumbele zaidi vingine vyote sasa hivi.

Unapopata dharura na kutaka kuondoka kwenye dharura huna anasa ya kupanga hayo mengine yafuatayo. Hayo yatakuja baada ya kuondokana na dharura.

Sasa kama bado huelewi ninachosema hapa, hutaki kuelewa na hutaelewa kamwe hata nikiandika na wino wa dhahabu.
Nimekuelewa vizuri mkuu. Lakini hili ni wazo lako pengine na wenzako, sio wazo la watanzania wote including myself.

Nchi yoyote ikiwemo Tanzania huwa na makundi matatu ya kuamua mustakabali wa nchi kupitia demokrasia. Makundi hayo ni 👇
1) Kuna kundi ambalo huwa upande wa chama tawala. Lenyewe humpigia kura mtu aliepitishwa na chama chao ili agombee uraisi, ubunge, udiwani nk, haijalishi mgombea ana sifa nzuri au mbaya.
2) Kuna kundi ambalo huwa upande wa vyama vya upinzani. Kundi hili nalo pia huwapigia kura watu waliopitishwa na vyama vyao ili wagombee uraisi, ubunge, udiwani nk. Haijalishi wagombea hao wana sifa nzuri au mbaya.
3)Kundi la mwisho hili halina chama au linachama lkn huwa linamchagua mtu kwa kufuata tu sifa za mtu alie katika kinyang'anyiro cha uraisi, ubunge, udiwani nk.

Sasa unaposema kuwa CCM inahitajika kutoka hata sasa hivi bila kujali chama au mtu atakaeingia baada ya CCM kutoka madarakani, sikupingi maanake huo ni mtizamo wako wewe na wenzako. Ila kuna mtizamo wangu mimi na wenzangu ambao baada ya kuangalia aina ya upinzani uliopo nchini, na sifa, matendo au tabia za wagombea mbali mbali wa uraisi, ubunge na udiwani waliopitishwa na vyama vyao kugombea nafasi hizo nchini. Sisi kwa mtanzamo wetu tunaona ni afadhali mara 70 CCM iendelee kubaki kuliko wao kuingia ikulu. Maana tabia zao hazina tofauti na zile za CCM au pengine ni zaidi ya zile za CCM. So huwezi kusema kuwa mimi siipendi harufu ya mkojo nyumban kwang, lkn wakati huo huo unaona sawa tu kuishi katika nyumba ambayo nyuma ya dirisha kuna shimo la choo linalotema harufu ya kinyesi. So hapo ndio tunapopishana. Katika CCM kuna mafisadi, waongo, wachumia tumbo na wanafiki, na katika upinzani vyama vyote kuna mafisadi, waongo, wanafiki na wachumia tumbo.
 
Inshaallah. Ki ukweli kuna watu wameshaichoka CCM, ila sasa hawaoni mbadala wa chama cha kuitoa CCM madarakani. Vyama vyote ukivichunguza havina tofauti na CCM mpaka inafikia kipindi watu wanahisi huenda huu upinzani ulitengenezwa maalum na CCM ili kuihadaa dunia kuhusu demokrasia nchini. Kwahiyo misaada inayoletwa na mabeberu kwa ajili ya kukuza na kuimarisha demokrasia inaliwa na wajanja wachache walio ndani ya serikali, CCM na upinzani butu.
Alphonce mawazo Yuko wapi??nani alimuua Mwangosi??Tume huru ya Uchaguzi Iko wapi??nani alizuia Mali za Lowasa na kuzitoza Kodi kubwa??nani Alivuruga Uchaguzi 2019/20??kwa nini wakiunga mkono juhudi,lazima wapewe vyeo??senseless person will not and never see oppression for opposition
 
Nimekuelewa vizuri mkuu. Lakini hili ni wazo lako pengine na wenzako, sio wazo la watanzania wote including myself.

Nchi yoyote ikiwemo Tanzania huwa na makundi matatu ya kuamua mustakabali wa nchi kupitia demokrasia. Makundi hayo ni 👇
1) Kuna kundi ambalo huwa upande wa chama tawala. Lenyewe humpigia kura mtu aliepitishwa na chama chao ili agombee uraisi, ubunge, udiwani nk, haijalishi mgombea ana sifa nzuri au mbaya.
2) Kuna kundi ambalo huwa upande wa vyama vya upinzani. Kundi hili nalo pia huwapigia kura watu waliopitishwa na vyama vyao ili wagombee uraisi, ubunge, udiwani nk. Haijalishi wagombea hao wana sifa nzuri au mbaya.
3)Kundi la mwisho hili halina chama au linachama lkn huwa linamchagua mtu kwa kufuata tu sifa za mtu alie katika kinyang'anyiro cha uraisi, ubunge, udiwani nk.

Sasa unaposema kuwa CCM inahitajika kutoka hata sasa hivi bila kujali chama au mtu atakaeingia baada ya CCM kutoka madarakani, sikupingi maanake huo ni mtizamo wako wewe na wenzako. Ila kuna mtizamo wangu mimi na wenzangu ambao baada ya kuangalia aina ya upinzani uliopo nchini, na sifa, matendo au tabia za wagombea mbali mbali wa uraisi, ubunge na udiwani waliopitishwa na vyama vyao kugombea nafasi hizo nchini. Sisi kwa mtanzamo wetu tunaona ni afadhali mara 70 CCM iendelee kubaki kuliko wao kuingia ikulu. Maana tabia zao hazina tofauti na zile za CCM au pengine ni zaidi ya zile za CCM. So huwezi kusema kuwa mimi siipendi harufu ya mkojo nyumban kwang, lkn wakati huo huo unaona sawa tu kuishi katika nyumba ambayo nyuma ya dirisha kuna shimo la choo linalotema harufu ya kinyesi. So hapo ndio tunapopishana. Katika CCM kuna mafisadi, waongo, wachumia tumbo na wanafiki, na katika upinzani vyama vyote kuna mafisadi, waongo, wanafiki na wachumia tumbo.
Mtaji mkubwa wa ccm ni ujinga wa watanzania walio wengi huko vijijini.huko Hadi mtendaji wa kata ni kama rais.wakipewa kofia na t-shirt wanaridhika.only that
 
Back
Top Bottom