Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

Tatizo la watu wamejipa hisia kinyume na uhalisia,yani humu mitandaoni jinsi mtu anavyoelezea maisha ya Tz ni kana kwamba hapakaliki kiasi kwamba imefikia mtu kuwa hana cha kupoteza ameshakata tamaa kabisa na ndiyo maana haoni cha kupoteza hata ikija vita,ugaidi au mlipuko wotewote tu wa maradhi. Ila sasa mtu huyo huyo aliyekataa tamaa kiasi hicho ndiye ambae hata kwenda kwenye maandamano anaogopa virungu vya polisi,sasa hapo utajiuliza huyu mtu aliyekata tamaa ya maisha kiasi haogopi hata vita anaanzaje kuogopa virungu vya polisi wakati maisha anayopitia ni mabaya zaidi ya vita,ugaidi na hata Corona?

Jibu ni kwamba huyu mtu amejipa hisia ambazo hazitoki kwenye uhalisia na ndiyo maana anaishia kupiga kelele mitandaoni tu maana ana vingi vya kupoteza kwenye maisha halisi. Mtu aliyekataa tamaa ya maisha kwa kufanyiwa uonevu anawezaje kutulizwa kwa mkwara tu wa polisi?
 
Stupid topic from Paskali

Why it's stupid?

Mi naona ni topic ya maana sana

Hivi huyo aliyeombea gonjwa lije anafikiri Serikali ndio itakayoathirika?

Au ndugu zake pamoja naye waweza kufa?

Kwa namna tulivyo watanzania hatuna haja ya kuombea gonjwa hili hata Kama tunaichukia Serikali vipi.....wao watajikinga na wanaweza wasichukua hatua za muhimu na kwani tutawafanyaje? Si tutapiga tu kelele Kama tunavyoendelea kupiga?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema ni wajinga sana, unafikir huo ugonjwa ukija ndio mtapata ridhaa ya kwenda ikulu ama?

Alafu unafikiri atakae umia ni nani? Ni wewe na bibi, mama, dada, na babu zako kule kijijini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kwahiyo two wrongs justify rights?

Kwamba kwakuwa watu wanafanya mabaya basi tuombee mabaya yatupate.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Corona ni hatari ikiingia kwetu maana kula yetu inategemea lazima utoke na ukitoka lazima upande daladala mbanano kama wote.
 
Mimi pia siwapendi CCM, lakini siwezi kufikia hatua ya kijinga kiasihicho.

Mtuanaewaza ujinga kama huo ni alie na mawazo ya kushindwa wakati wote.
Hana njia mbadala, naninamfananisha na wale wanaojitoa muhanga kujilipua.

Ni mtu muoga mlopokaji.

Hata kama nichuki, ikifikia kumuombea mwenzako afe, then na wewe nikama yeye.
Tofauti ni kwamba wewe hujapata nafasi tu ya kuonyesha ubayawako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali!!
Upo sahihi kuja na bandiko hili.
Mwenzetu ametereza kidogo.
Soma waamuzi 16:1-22.
Watu wakionewa sana huwazia wabaya wao mabaya na ikibidi wafe pamojana nao.

Paskali, Mambo maovu wanayotendewa wananchi mmeyalea Sana na kuyashangili bila kufikiri kuwa hawa watu wanaoonewa au wanaonyimwa haki zao Wana mioyo ya nyama au wananyongo,( wanasikia maumivu)

Paskali!
Watu wanaponyimwa haki zao wanaumia,wewe unaposhangilia ni sawa na kuweka chumvi kwenye vidonda vyao
KWAHIYO HUPASWI KUTOA LAWAMA.

PASKALI MAYALLA
UNGULI WAKO UENDANE NA
1. HEKIMA
2. BUSARA
3. MAARIFA
4. WELEDI,
Tatizo unaangalia mwisho wa neno lakini huangali mwanzo neno.
Kutereza kwa mwenzetu kunatokana na maumivu aliyonayo ya kukandamizwa haki zake. ASILAUMIWE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani hujui kuna kitu kinaitwa detox! Corona ni kama detox tu kuondoa bad cells na poisons mwilini. Lakini kwa bahagi mbaya few good cells nazo inabidi ziende na maji!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…