Mtu mmoja akiwa bilionea, watu elfu moja huwa masikini

Mtu mmoja akiwa bilionea, watu elfu moja huwa masikini

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Utajiri ni hali ya kuwa na mali au pesa nyingi . Mara nyingi utajiri hupimwa kwa wingi wa pesa alizonazo mtu mfano , kiwango kikianzia milioni 100 mtu huyo huitwa milionea, kikianzia milioni 1000 mtu huyo huitwa bilionea, Mtu mwenye utajiri huitwa TAJIRI na mtu asiye na utajiri (mali au pesa nyingi) huitwa MASIKINI.

Unyonyaji ni kitendo cha kukamua pesa au mali za watu wengine. Kwa maana hiyo tunaweza kusema tajiri ni mtu anaye kamua pesa au mali za mtu mwingine kwa lengo la kujinufaisha, ukamuaji unaweza kuwa ni halali kisheria au unao vunja sheria, ktk maada hii nitazungumzia ukamuaji usiovunja sheria.

Mfano: Kijiji A kikiwa na upungufu wa chakula mfano mahindi, mimi nikaenda kijiji B ambacho kinamahindi mengi, nikanunua kwa shilingi 5 kila gunia, nikarudi kijiji A nikawauzia kwa shilingi 10 kila gunia, nitakua nimekamua shilingi 5 kwa kila gunia.

Mfano: Nikizalisha juisi moja kwa gharama ya shilingi 1, nikamuuzia mwenye kiu kwa shilingi 5, ninakua nimekamua shilingi 4. Kumbuka katika mifano yote miwili hakuna mahali ambapo sheria imevunjwa.

Ili nitengeneze Shilingi 100 inabidi niwauzie watu wasiopungua 20 ktk mfano namba moja, kiuhalisia kila mtu anakuwa amenipa shilingi 5 ni sawa na kusema amepoteza shilingi tano.
Ili mtu yeyote apate pesa ni lazima mtu mwingine apoteze pesa. Tajiri akipata juwa kuna masikini kapoteza, mtu yeyote akipata juwaa kuna mtu kapoteza.

(15).PNG

Ni kama vile mzani jinsi unavyofanya kazi

Ukitengeneza bilionea mmoja unakuwa umetengeneza masikini elfu moja
127934837-chalk-board-sketch-of-scales-concept-of-balance-between-rich-and-poor-1.jpg



Kanuni haidanganyi, inafanya kazi popote pale duniani, inaleta matokeo yale yale

Nawasilisha


 
Mkuu wanasema utajiri ni Tabia kwamba ukichukua utajiri wote duniani ukaugawa sawa baada ya muda flani maji yanajitenga na mafuta

Waliokuwa matajiri wanarudi kuwa matajiri na wale wa dagaa za mia mia wanarudi huko.

Ko kuna watu watakamuliwa tu hata wafanyaje maana wameumbwa hivyo
 
Kiongozi,

Hivi Kwa uelewa wako wanaonunua vitu ni masikini tu?

Unachambua mada ya kiuchumi kwa kutumia theory za Physics; huwa mambo hayako hivyo.

Naona unakiu ya kujua hiyo tafuta mtu mwenye taaluma ya Uchumi atakusaidia na utafaidika
 
Kiongozi,
Hivi Kwa uelewa wako wanaonunua vitu ni maskini tu?
Unachambua mada ya kiuchumi kwa kutumia theory za Physics; huwa mambo hayako hivyo.
Naona unakiu ya kujua hiyo tafuta mtu mwenye taaluma walau kidogo ya Uchumi akausaidie
WORLD BANK ikiikopesha TANZANIA shilingi 5 kwa makubaliano ya kurejesha shilingi 7, inakuwa imekamua shilingi mbili,

Unahitaji degree ya uchumi kuelewa hii principle?

Kosoa kwa kutumia uchumi unaousema nikueleweshe
 
Kwa hiyo unataka watu wasiwe matajiri?..

Kuna watu hata ukitaka wasiwe matajiri tabia zao tu zitawafanya wawe matajiri tu, kuna watu hata ukitaka wasiwe masikini tabia zao tu watakuwa masikini...

Sasa wewe unalala masaa 14 kwa siku na mwenzio analala masaa 4 kwa siku hayo mengine yote anapiga kazi mnataka wawe sawa.. kuna mtu akipanda kitandani ule muda wa kutafuta usingizi anapanga mipango tu mpaka analala, wewe ule muda unachati na michepuko + umbea facebook unataka muwe sawa..

Kuna watu risk taker wanazama kwenye mashimo migodini huko, wengine sasa hivi wako deep sea wanapambana na wimbi, wengine wanapishana na risasi, wengine wameweka bond kila mali zao, wengine wamekopa madeni kila kona, wengine wamebet mamilioni ya hela halafu tuwe sawa na wewe NEVER....
 
WORLD BANK ikiikopesha TANZANIA shilingi 5 kwa makubaliano ya kurejesha shilingi 7, inakuwa imekamua shilingi mbili,

Unahitaji degree ya uchumi kuelewa hii principle?

Kosoa kwa kutumia uchumi unaousema nikueleweshe

kwanini nawewe ukakope world bank wakati una ardhi ina rutuba kila mahala na madini tele....ukilima ukaenda kuuza huko bangladesh kwa superprofit huko world bank utaenda kufanya nini...

Huko world bank kuna hela za wanaume zinatafuta wazembe wasiofanya kazi kama nyie mpewe bure mkatumie...
 
kwa hiyo unataka watu wasiwe matajiri?..

kuna watu hata ukitaka wasiwe matajiri tabia zao tu zitawafanya wawe matajiri tu, kuna watu hata ukitaka wasiwe masikini tabia zao tu watakuwa masikini...
Point yangu ni kwamba kuna haja ya kutumia hii principle kujinufaisha kiuchumi,

Mimi nimeeleza tu sijapinga popote pale
 
kwanini nawewe ukakope world bank wakati una ardhi ina rutuba kila mahala na madini tele....ukilima ukaenda kuuza huko bangladesh kwa superprofit huko world bank utaenda kufanya nini...

Huko world bank kuna hela za wanaume zinatafuta wazembe wasiofanya kazi kama nyie mpewe bure mkatumie...
Swali lako ni pana sana, kiufupi kuna wachache wananufaika huku wengi wakizidi kuwa masikini
Rejea issue ya gas ya mtwara
 
Kwa hiyo unataka watu wasiwe matajiri?..

Kuna watu hata ukitaka wasiwe matajiri tabia zao tu zitawafanya wawe matajiri tu, kuna watu hata ukitaka wasiwe masikini tabia zao tu watakuwa masikini...
Hamna tabia inayokufanya kuwa tajri bali ni vyanzo vyako vya mapato

Mfano ukipewa laki ukiwekeza vzuri itaendelea kuwepo. Na ukienda kununua jens ndo itakuwa imeisha hyo
 
Hamna tabia inayokufanya kuwa tajri bali ni vyanzo vyako vya mapato

Mfano ukipewa laki ukiwekeza vzuri itaendelea kuwepo. Na ukienda kununua jens ndo itakuwa imeisha hyo
Kiufupi ni kwamba ukitaka kuwa tajiri tafuta watu uwakamue pesa kwa njia iliyo halali.

Mfano ulioutoa, unakuta huyo anayekuuzia jeans kwa laki unakuta yeye kainunua kwa elfu kumi na tano, kwa haraka haraka anakua amekukamua 75
 
kama unachokisema mleta mada ni sahihi basi nchi kama USA yenye mabilionea wengi si ungekuta ina masikini wengi kuliko hata TZ[emoji23][emoji23]
 
kama unachokisema mleta mada ni sahihi basi nchi kama USA yenye mabilionea wengi si ungekuta ina masikini wengi kuliko hata TZ[emoji23][emoji23]
US wajanja, wao wanakamua nchi zingine wanapereka kwao, mfano wanamakampuni ya kuchimba mafuta, gesi na madini, wao wakichimba wanakukatia 3% kinachobaki wanapereka kwao,

Huoni kule afghanstan wanajeshi wao walikaa miaka 10?
 
Hivi ni kweli ukiwa na milioni 100 ww ni milionea?na ukiwa na milioni 1000 eti ww ni bilionea?,
 
SI KWELI.

KABLA YA UWEPO WA FEDHA WALIKUWEPO MATAJIRI NA MASIKINI.

Tafsiri ya utajiri sio pesa bali ni uwezo wa akili wa kutawala rasilimali zinazokuzunguka kulinganisha na viumbe wengine.

Mtoto wa Masai anatawala watoto wa ng'ombe na baba zao si kwa sababu ni milionea ila uwezo wake wa akili upo juu kulinganisha na ng'ombe.

Utajiri ungekuwa ni pesa ungerithishwa daima, hakuna matajiri wangeibuka kutoka katika masikini.

Utajiri ni uwezo wa akili, Pesa ni matokeo ya kuwa tajiri au masikini. Kabla ya kuwa na pesa matajiri na masikini walikuwepo.
 
Back
Top Bottom