Uchaguzi 2020 Mtu timamu hawezi kushangilia matokeo haya

Uchaguzi 2020 Mtu timamu hawezi kushangilia matokeo haya

nia yenu mnataka watu wafe amani itoke.
Tunajua tangu mwezi wa 8 mwaka huu polisi walikuwa wanafanya mazoezi ya ziada kwa ajili ya kuja kupiga watu kwenye uchaguzi huu.
Swali la msingi Kama hamtaki upinzani Tanzania uchaguzi mnafanya wa nini?
Miaka yote polisi wanajiandaakuelekea uchaguzi, tena 2015 walinunua kabisa na magari ya maji ya washawasha. Hakuna kigeni chochote mwaka huu walicholalamikia ambacho hakijawahi kutokea huko nyuma, ni namna Upinzani ulivojipanga kudhibiti hizo mbinu maana zipo siku zote na kila siku wanazilalamikia, sio leo wala jana hayo malalamiko ndugu.
 
Ndio imeshakuwa tiyari ushangilie usishangilie ushindi kwa CCM , nadhani muda wa matusi umeisha sasa

sent from HUAWEI
Siyo ushindi ni uporaji madaraka CCM wamebaka sanduku la kura
 
Kituo chenye wapiga kura 125,239 (registered voters) msimamizi anatangaza wamepiga kura 437,980, hata wizi hauko hivyo.

Uchaguzi ambao karibu nusu ya wagombea ubunge nchi nzima aidha wamekamatwa, wanashikiliwa na polisi au kujeruhiwa kwa silaha, utashangiliaje matokeo haya.

Matokeo ya uchaguzi ambao karatasi za kura feki zimezagaa mitaani nchi nzima.

Uchaguzi ambao wakati wa kuhesabu kura polisi wanaingia vituoni wanawatoa mawakala wote wa vyama vingine anabaki wakala wa CCM na msimamizi wa kituo wakihesabu peke yao.

Uchaguzi ambao OCD anaingia kituo cha kupigia kura anakwapua ballot box na kuondoka nalo.

Hata mwana CCM mwenye akili timamu hawezi kushangilia matokeo ya uchaguzi kama huu unaokwenda kuligawa taifa.
Mmeanza uongo baada ya kushindwa?
 
Kuna Mambo mengine unatakiwa kujiongeza mwenyewe.
Kuna faida gani ya kusema Tanzania ni ya VYAMA vingi?.
si Bora vyama vyote vifutwe ibaki ccm tujue MOJA hakuna uchaguzi.
Hakuna vyama vingi kuna ujinga mtupu sasa CCM inaenda kuwa Serikali haramu ya kishetani
 
huu uchaguzi ulikuwa wa kimagumashi tu,haikuwa rahisi kukifungashia virago chama tawala ingekuwa aibu sana,ni safari ndefu kuking'oa madarakani
Si mlikuwa mnasema kabla ya misa ya kwanza kuisha mtakuwa mshatangaza ushindi nyie?
 
Kuna Mambo mengine unatakiwa kujiongeza mwenyewe.
Kuna faida gani ya kusema Tanzania ni ya VYAMA vingi?.
si Bora vyama vyote vifutwe ibaki ccm tujue MOJA hakuna uchaguzi.
Wananchi wana imani na Ccm. Wapinzani watabaki na ofisi zao za vyama wakinywa kahawa.
 
Achana na mtu kama huyo anayefikiri kutumia makalio. JF ingekuwa tunajiunga kwa kiingilio pengine ingetu punguzia wajinga
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Mkuu vipi uko road za sehemu gani muda huu katika harakati za kumng'oa mkoloni mweusi?
 
Hizi habari zinakuja baada ya kushindwa?? Lete na ushahidi otherwise ni porojo tuuuuu
 
Back
Top Bottom