Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Mchawi hela mkuu, shule nyingi ambazo mitaala wamebase kwenye GCSE Ada zao sio za nchi hii. Niliona mwanang mmoja alikua abasoma Haven of Peace (HOPAC) maburungutu aliyokua analipiwa ada aisee Acha tu

Sent from my Redmi Note 8 Pro using JamiiForums mobile app
 
Wazazi/ walezi wengi wanapenda watoto wao wasome shule bora. Lakini changamoto inakuja kwenye gharama kubwa za kusoma kwenye hizo shule.
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Hahaaa.mkuu wabongo tunaakili zetu za kuzaliwa nazo.hivi unaweza amaini kuna masela wanashika vitengo mhiumu sana huko nchi za wenzetu lakini walimaliza hapa hapa bongo shule hizi hizi za serikali.Yaana nazungumzia kwamba walijifunza kingereza kwa kiswahili"leo tutajifunza kuhusu nauni......,nani anaweza kunitajia mifano miwili ya nauni?...anaandika ubaoni NOUN".Yaani walianza kingereza kama somo moja darasa la 4,na masomo yote ya kingereza fomu one.
Tusikate sana taamaa .hizo IST,ukiwa na mihela tuu,unakuwa tayari umeshaijua kwamba iko.Ila ukikosa huo uwezo mpeleke mtoto shule yoyote ile na mkazanie atatoboa tuu.
 
Mbona wengine tumesoma hizi hizi shule za sirikali, tena shule ya msingi kijijini kwa babu kuongea kilugha mwanzo mwisho lakini tumefanikiwa kupata scholorship kusoma Masters na PhD kwenye international universities ambazo zipo kwenye world ranking ya 10 bora, what happened?

Ww unapenda tu kubishana lakini mkuu hapo juu yupo sahihi.
 
Nationalism is an infantile disease. It is the measles of mankind

- Albert Einstein.

Siko hapa kwenye squabbles za Wakenya na Watanzania.

Najieleza tu.

Watanzania tuna lugha yetu tunaelewana wenyewe.

Hii inawezekana East Africa nzima ipo, lakini Tanzania nimeona sana. Labda kwa sababu ndipo nilipozaliwa na kuishi sana.

Haya ni baadhi ya matatizo, haijalishi mtu ana elimu vipi, mara nyingi sana yanajitokeza.

1. Kuongea bila kumaliza sentensi. Kuanzia mtoto mpaka rais, si ajabu kukuta mtu anaongea, halafu anaachia sentensi inaelea hewani bila kuimalizia. Sasa sijui ni aina mahsusi ya mawasiliano au ni mapungufu.

2. Kuongea katika namna ambayo mawazo hayana mpangilio. Mawasiliano bora yanajali mpangilio. Hoja inaanza kutambulishwa, maana za kiini cha hoja zinanyambulishwa, halafu maelezo mengine yanafuata. Tanzania si ajabu mtu akarukia mwisho wa hoja hata bila ya kuitambulisha.

3. Watu kuchukulia kirahisi tu kwamba mtu mwingine anajua wanachozungumzia kama wanavyojua wao. Hili linachangia sana tatizo namba 2 hapo juu.

4. Kujadili mambo kwa ushabiki, mahaba na hashuo badala ya kuangalia hoja. Watu wanachukua upande kama ushabiki wa timu za Simba na Yanga, halafu, baada ya hapo, watafanya kila hila upande wao uonekane ndio bora. Bila kujali hoja. Iwe kwenye siasa, dini, kujadili nchi, na kadhalika. Hapa utakutana na logical non sequitur zote, ad hominem attacks zote, deus ex machina zote, ili mradi mtu ashinde mjadala tu.

5. Non verbal communication. Hili ni janga la kitaifa. Unaweza kukuta rais anahutubia taifa, hapo hapa anajishika pua kama anataka kupenga makamasi.

6. Mikingamo katika dhana. Jana nilikuwa namsikiliza jamaa mmoja shabiki wa timu ya soka ya Yanga. Anasems anataka mambo yawe fair, Yanga ipewe nafasi ibebwe kwa sababu Yanga ilipigania uhuru wa nchi. Yani hapo hapo anasema anataka mambo yawe fair, hapo hapo anasema anataka Yanga ipendelewe. Haoni contradiction hapo. Kauli kama hizi kwa Watanzania si kitu cha ajabu. Hata siasa zetu za "Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction. Ujamaa maana yake ni kutegemeana, na kutegemeana ni kinyume cha kujitegemea, hivyo "Ujamaa" na "Kujitegemea" ni vitu vinavyopingana. Sisi tunaona sawa tu.

7. Kukosa uwazi. Mawasiliano ya Watanzania wengi yametawaliwa na hila na kukosa uwazi. Ama kwa sababu wengi hawana uwezo wa kuchambua hoja na kuiwakilisha vyema, ama kwa sababu hata wenye uwezo wa kukwambia kitu ambacho wanaona hutakipenda, huenda kujipendekeza, kutaka suluhu ya uongo, kueleza mambo yao kama utani na dhihaka, na kadhalika. Kwa Watanzania wengi ni bora akukubalie jambo bila ridhaa ya kweli, halafu akusengenye pembeni, kuliko akuambie ukweli na kukukatalia jambo mbele yako.

8. Kasumba/Generalization/Stereotyping.
Watanzania wakitaka kuoa wengi wanaanza kuuliza "kabila fulani tabia zao zipi?". Hili tatizo la ukabila hata Kenya lipo, tena zaidi.Bora yetu, huko hata kuoana makabila tofauti nafikiri bado ni mzozo. Ila Tanzania watu wanaishi kwa kukariri sana na labda kwa kiasi fulani kuna mantiki, lakini imezidi sana. Mpaka inaharibu mawasiliano. Kwa sababu mtu kabla hajawasiliana na kujua ukweli kashaweka dhana Wachaga wezi.
Kuna hotuba moja ya rais Magufuli aliletewa kesi ya Mchaga akasema nyie mlitegemea nini, huyo mtu ni Mchaga, akimaanisha kuwa walitakiwa wajue Wachaga ni wezi. Halafu nchi hiyo hiyo kuna watu wanajisifia kinafiki haina ukabila. Yani kwa watu wengine ukiwa unaishi nje wewe ni beberu tu. Cha ajabu, wewe beberu wakipata matatizo wanakufuata kukuomba msaada! Hapa tqtizo la kasumba limechanganyika na tatizo la namba 6 la contradiction. Wao wanaona sawa tu.

9.Kutotaka kujifunza. Watanzania wengi unaweza kuona mtu kakosea, ukamsahihisha. Tena kwa heshima tu, iki asikisee tena sehemu mbaya zaidi. Mwenzako anakwambia "Si umeelewa tu?". Yeye ukweli kwamba kakosea na anatakiwa kujifynza si kitu muhimu. Anakulazimisha wewe uwe umeelewa hata alipokosea.

10. Uzalendo wa kijinga. Watanzania wengi serikali inawapiga, inawatukana, inawanyanyasa. Lakini wanaitetea bado kwa "cognitive dissonance" ya " my country, wrong or right".

Si Watanzania wote walio hivyo. Tuna watu sharp wengi. Watu wanafunguka macho. Upinzani unakua.

Lakini naona kama majority ndiyo wako hivyo. Kibaya zaidi wengine wengi ni watoto wa mjini ambao walitakiwa kujua zaidi.

Before you gleefully gang on us with vitriolic schadenfreude, let it be known that I am a country agnostic equal opportunity offender and I can dish the same ten point harangue on Kenya.
Umenipa mambo mengi Sanaa.
 
Mkuu umemaliza kila kitu hapa.
Na mada imeishia hapa atakayeendelea kukubishia hapa huyo ana matatizo.
Angalia maisha anayoishi msanii TID yale ndio mfano wa watoto waliosoma kwenye shule hizo.
TID hajasoma international school , amesema shabaan Robert ni English medium ya kawaida
 
Nadhani hujamuelewa mtoa mada amesema int schools zinafundisha analytical skills, creativity, reasoning , logic nk
Amesema tuachane na exam based schools
Kupata A haimaanishi ndio unaakili Sana .
Tunatakiwa tuachane na Mambo ya kuangalia mtoto kwenye mtihani kapata A na kutunga mitihani ambayo haimsaidii mtoto ku reason Wala kuwa mbunifu na kujua jinsi ya kutatua matatizo yake (problkem solving)

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Sasa bila mtihani tutajuaje kama ameelewa?

Shule za internationali ni ujinga mwingine tu wa kuendelea kuamini hao wenye mitaala yao.
Binafsi natamani kuona watoto wafundishwe vitu vilivyo katika mazingira yetu,na vitu ambavyo vinaendesha ulimwengu.
Mf watoto wajifunze
Kilimo kwa vitendo
Uvuvi
Ufugaji
Stadi za kazi
Tehama nk
Hivi viwe kwa vitendo zaidi na sio kukalilishana.

Shule zitengwe kama ilivyokuwa awali,yani shule za
Kilimo
Biashara
Tech nk.
Mtoto ajifunze kitu kimoja tangu kidato cha kwanza,sio anzie kidato cha tano kama tufanyavyo.hii itawafanya wabobee kwenye fani husika tangu awali,hili litawafanya wawe wabunifu zaidi,

Mambo ya shule za kimataifa nao ni aina ta ujinga
 
Nationalism is an infantile disease. It is the measles of mankind

- Albert Einstein.

Siko hapa kwenye squabbles za Wakenya na Watanzania.

Najieleza tu.

Watanzania tuna lugha yetu tunaelewana wenyewe.

Hii inawezekana East Africa nzima ipo, lakini Tanzania nimeona sana. Labda kwa sababu ndipo nilipozaliwa na kuishi sana.

Haya ni baadhi ya matatizo, haijalishi mtu ana elimu vipi, mara nyingi sana yanajitokeza.

1. Kuongea bila kumaliza sentensi. Kuanzia mtoto mpaka rais, si ajabu kukuta mtu anaongea, halafu anaachia sentensi inaelea hewani bila kuimalizia. Sasa sijui ni aina mahsusi ya mawasiliano au ni mapungufu.

2. Kuongea katika namna ambayo mawazo hayana mpangilio. Mawasiliano bora yanajali mpangilio. Hoja inaanza kutambulishwa, maana za kiini cha hoja zinanyambulishwa, halafu maelezo mengine yanafuata. Tanzania si ajabu mtu akarukia mwisho wa hoja hata bila ya kuitambulisha.

3. Watu kuchukulia kirahisi tu kwamba mtu mwingine anajua wanachozungumzia kama wanavyojua wao. Hili linachangia sana tatizo namba 2 hapo juu.

4. Kujadili mambo kwa ushabiki, mahaba na hashuo badala ya kuangalia hoja. Watu wanachukua upande kama ushabiki wa timu za Simba na Yanga, halafu, baada ya hapo, watafanya kila hila upande wao uonekane ndio bora. Bila kujali hoja. Iwe kwenye siasa, dini, kujadili nchi, na kadhalika. Hapa utakutana na logical non sequitur zote, ad hominem attacks zote, deus ex machina zote, ili mradi mtu ashinde mjadala tu.

5. Non verbal communication. Hili ni janga la kitaifa. Unaweza kukuta rais anahutubia taifa, hapo hapa anajishika pua kama anataka kupenga makamasi.

6. Mikingamo katika dhana. Jana nilikuwa namsikiliza jamaa mmoja shabiki wa timu ya soka ya Yanga. Anasems anataka mambo yawe fair, Yanga ipewe nafasi ibebwe kwa sababu Yanga ilipigania uhuru wa nchi. Yani hapo hapo anasema anataka mambo yawe fair, hapo hapo anasema anataka Yanga ipendelewe. Haoni contradiction hapo. Kauli kama hizi kwa Watanzania si kitu cha ajabu. Hata siasa zetu za "Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction. Ujamaa maana yake ni kutegemeana, na kutegemeana ni kinyume cha kujitegemea, hivyo "Ujamaa" na "Kujitegemea" ni vitu vinavyopingana. Sisi tunaona sawa tu.

7. Kukosa uwazi. Mawasiliano ya Watanzania wengi yametawaliwa na hila na kukosa uwazi. Ama kwa sababu wengi hawana uwezo wa kuchambua hoja na kuiwakilisha vyema, ama kwa sababu hata wenye uwezo wa kukwambia kitu ambacho wanaona hutakipenda, huenda kujipendekeza, kutaka suluhu ya uongo, kueleza mambo yao kama utani na dhihaka, na kadhalika. Kwa Watanzania wengi ni bora akukubalie jambo bila ridhaa ya kweli, halafu akusengenye pembeni, kuliko akuambie ukweli na kukukatalia jambo mbele yako.

8. Kasumba/Generalization/Stereotyping.
Watanzania wakitaka kuoa wengi wanaanza kuuliza "kabila fulani tabia zao zipi?". Hili tatizo la ukabila hata Kenya lipo, tena zaidi.Bora yetu, huko hata kuoana makabila tofauti nafikiri bado ni mzozo. Ila Tanzania watu wanaishi kwa kukariri sana na labda kwa kiasi fulani kuna mantiki, lakini imezidi sana. Mpaka inaharibu mawasiliano. Kwa sababu mtu kabla hajawasiliana na kujua ukweli kashaweka dhana Wachaga wezi.
Kuna hotuba moja ya rais Magufuli aliletewa kesi ya Mchaga akasema nyie mlitegemea nini, huyo mtu ni Mchaga, akimaanisha kuwa walitakiwa wajue Wachaga ni wezi. Halafu nchi hiyo hiyo kuna watu wanajisifia kinafiki haina ukabila. Yani kwa watu wengine ukiwa unaishi nje wewe ni beberu tu. Cha ajabu, wewe beberu wakipata matatizo wanakufuata kukuomba msaada! Hapa tqtizo la kasumba limechanganyika na tatizo la namba 6 la contradiction. Wao wanaona sawa tu.

9.Kutotaka kujifunza. Watanzania wengi unaweza kuona mtu kakosea, ukamsahihisha. Tena kwa heshima tu, iki asikisee tena sehemu mbaya zaidi. Mwenzako anakwambia "Si umeelewa tu?". Yeye ukweli kwamba kakosea na anatakiwa kujifynza si kitu muhimu. Anakulazimisha wewe uwe umeelewa hata alipokosea.

10. Uzalendo wa kijinga. Watanzania wengi serikali inawapiga, inawatukana, inawanyanyasa. Lakini wanaitetea bado kwa "cognitive dissonance" ya " my country, wrong or right".

Si Watanzania wote walio hivyo. Tuna watu sharp wengi. Watu wanafunguka macho. Upinzani unakua.

Lakini naona kama majority ndiyo wako hivyo. Kibaya zaidi wengine wengi ni watoto wa mjini ambao walitakiwa kujua zaidi.

Before you gleefully gang on us with vitriolic schadenfreude, let it be known that I am a country agnostic equal opportunity offender and I can dish the same ten point harangue on Kenya.
Nyongeza:

Kusoma na kushindwa kuelewa ulichokisoma.

Hili tatizo huna hata haja ya kwenda mbali. Humu humu tu JF kila siku watu wanasoma vitu lakini hawaelewi walichokisoma.

Sijui huko shuleni walikuwa wanajibu vipi maswali ya insha; ile unasoma insha halafu ukimaliza kusoma unajibu maswali yahusianayo na insha uliyoisoma.

Ni kipimo kizuri sana kupimia uwezo wa mtu wa kusoma na kukielewa alichokisoma.

Imani potofu.

Imagine mtu ana PhD yake tena katika mambo ya sayansi halafu papo hapo anaamini katika uchawi.

Like, seriously?

Unakutana na mdada mtanashati kabisa. Kasoma ana Master’s yake [chagua fani] halafu anaamini katika habari za kwenda kwa mganga wa kienyeji kutafuta dawa ya mapenzi.

Akienda kwa mganga huko, mganga anampeleka baharini huko. Anamwambia avue nguo halafu aoge maji ya bahari.

Wakimaliza huko baharini, anamrudisha nyumbani na makorokoro ya ajabu ajabu akimwambia ndo sijui dawa ya kumtuliza mume or whatever other nonsense.
 
Sasa bila mtihani tutajuaje kama ameelewa?

Shule za internationali ni ujinga mwingine tu wa kuendelea kuamini hao wenye mitaala yao.
Binafsi natamani kuona watoto wafundishwe vitu vilivyo katika mazingira yetu,na vitu ambavyo vinaendesha ulimwengu.
Mf watoto wajifunze
Kilimo kwa vitendo
Uvuvi
Ufugaji
Stadi za kazi
Tehama nk
Hivi viwe kwa vitendo zaidi na sio kukalilishana.

Shule zitengwe kama ilivyokuwa awali,yani shule za
Kilimo
Biashara
Tech nk.
Mtoto ajifunze kitu kimoja tangu kidato cha kwanza,sio anzie kidato cha tano kama tufanyavyo.hii itawafanya wabobee kwenye fani husika tangu awali,hili litawafanya wawe wabunifu zaidi,

Mambo ya shule za kimataifa nao ni aina ta ujinga
Hayo NI mawazo yako
Na mtoa mada nae ametoa mawazo yake
Raha ya kuishi hapa duniani NI kutofautiana kimawazo na ndio maana kunakuwa na maendeleo

Hatuwezi watu wore kuwa na mtazamo mmoja

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Mtoto akifeli IST ni sawa na mtu umechana mkeka,tena sio umechana bali ni Umeurarua mkeka,Unaletewa taaarifa na uongozi mwanao anatakiwa arudie mwaka mzima,mwaka ambao ADA na makorokoro yote ni 23.5M - 25M Hii kama sio kurarua mkeka ni nini?

Mtu anaeweza somesha mtoto International ni yule mwenye income ya not less of 20M per month,yani kama kwa mwezi huna income hiyo internatinal isikilize tu humu JF tuki iongelea na kuipgia story.

Hamna ubishi kwamba huko ndipo penye ELIMU huko kote wala sibishi na sidhani kama kuna mende yeyote humu ataeweza kubisha,swala lililopo mezani ni Dooooo hapa tunaongelea Doooo wajua nini maana ya Dooo wewe,sio dooor ya mlango naongelea Doooo....hehehehe

Nitavimba sana town,ntakua na kiburi sana ila kiburi cha kusomesha international sijafikia na nadhani hata muda huo ukifika wanangu nao watakua washamaliza kusoma,hebu msinipe stress zingine mimi Pale maromboso nafasi zipo pananitosha vizuri tu,st patrick ipo panantosha vizuri tu acha akadanganywe huko huko na walimu sina namna.

ila international wajuba ni story zingine ishu sio kumiliki Mercedes-Benz Maybach Exelero ishu ni kuihudumia hii ndinga,ishu sio ADA ishu ni zile vi cost vya hapa na pale,kubabeki unaweza jikuta unaimba Mwambie Farao nimeokoka kwenye kundi la alshabaab wewe mwenyewe yani.

Mkuu hawa watu hawana bei za 23 to 25 bei zao ni balaa
 

Attachments

  • CE7E49BA-640E-4E44-B174-240515740993.jpeg
    CE7E49BA-640E-4E44-B174-240515740993.jpeg
    128.7 KB · Views: 6
Watu wengine wabishi tu. hata kama TID angesoma IST akaharibikiwa, hawezi kutumika kusema kuwa international schools hazifai.
TID hajasoma international school , amesema shabaan Robert ni English medium ya kawaida
 
mkuu fatilia vizuri sababu za wao kusoma hapa....kumbuka ili kuweza kuwa qualified kusoma nje kutokea International schools lazima upitishwe na CIA (Cambridge International Assessment) tena hiyo ni hatua ya pili baada ya kupita AS inayofanywa sana na walimu wa hapohapo shuleni... So unaweza kuwa na expectation ya kusoma nje ila ukakosa vigezo ukaamua kusoma hapahapa..

Mimi kuna alumn wa miaka 2 iliyopita ninaowajua walisoma shuleni hapa 80 wote wameenda vyuo vya nje na waliofail wengine wanapiga kazi office za wazee wao wengine wanasoma hapa bongo....

Ila pia unaweza soma PYP, MYP kwa primary au ukafanikiwa vuka hadi olevel na alevel wanaotumia IGCSE ukamaliza alafu uchumi ukawa mbaya home, ukaenda shule za kawaida as long as unaufaulu mzuri.....

So ni kweli wanaosoma bongo wapo ila wachache sana na wanakuwaga na sababu 2 tu kukatwa na CIA au uchumi bro
Nilivyokuelewa ni km vile wanakuwa tayari ni watu kutoka Royal families kwa hiyo mambo ya connection za masomo ya nje ya nchi zipo nje nje,Maana kwa mtu km mimi Kapuku eti nimejichanga changa tuhela twangu twa kahawa au korosho nikajipinda nikampeleka shule hizo za kiinternational bila connection sidhani km mwanangu anaweza kufika ktk vyuo hivyo vya Mamtoni,kwangu ni km naota .
 
Tofauti huwezi kuiona chuo. Utaiona mnapomaliza chuo. Ndo utajua nani wa kimataifa nani wa Mtakatifu Kayumba.
Unataka kusema kwenye competition ya ajira,wale wa International watapa ajira kiurahisi kuliko wa Kayumba hata km GPA za wale wa St.Kayumba ni nzuri kuliko za wale wa International??
 
Tajiri namba moja wa Tanzania bwana Mo kasoma shule gani?? Mo amesoma International School of Tanganyika (IST)

Watu wote tunahangaika kutafuta hela/utajiri. Sasa kama tajiri namba moja kasoma IST unataka kutulinganishia na nani mwingine??
Nimemjibu mdau humu kwamba wanaosoma shule hizo wengi huwenda kusimamia miradi ya familia au kupewa nafasi kwenye mashirika ya serikali kama wazazi au ndugu ni watu wa serikali
Mfano Ni huo uliotoa lakini suala la kukuza vipaji siliafiki sana

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Sio vizuri kwenye mada nzuri kama hii kuweka siasa ila utanisamehe.....Tundu Lissu na Cahadema ndio vinara wa ujinga huu wa kuwa wanajua kiingereza ndio wasomi sana!
Aliongea hivyo wapi na lini?,Au ni chuki tu?
 
Nadhani hujamuelewa mtoa mada amesema int schools zinafundisha analytical skills, creativity, reasoning , logic nk
Amesema tuachane na exam based schools
Kupata A haimaanishi ndio unaakili Sana .
Tunatakiwa tuachane na Mambo ya kuangalia mtoto kwenye mtihani kapata A na kutunga mitihani ambayo haimsaidii mtoto ku reason Wala kuwa mbunifu na kujua jinsi ya kutatua matatizo yake (problkem solving)

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo Sisi akina Uchebe wa St.Kayumba hatuna creativity, reasoning na logic?.
 
Haijaishi umesoma Mpaka level gani foundation ndio kila kitu Nina uhakika reasoning yako and analytical skills zako ni tofauti kabisa na wale watoto wa Breibum na IST
Tatizo wengi mko brainwashed na hicho mnachoita reasoning na analytical skills ambacho kimsingi ni kutekwa kifikra, namaanisha huyo anayekufundisha huko IST sijui na international school gani huko hataki uwe huru kifikra ndo maana anakuingizia ideology za ushoga na unaona ni kitu kizuri kabisa, simply because ameshakuteka kifikra. Wengi mmekwama hapo kwenye ndoto kwamba mtoto wangu akisoma IST atakuwa katibu mkuu wa UN kwa sababu ana analytical na reasoning skills, then what! hivi kuna binadamu hata kama hajakanyaga darasani ambaye hawezi kufanya reasoning na analyisis? labda kama ubongo wake umekufa.
 
Back
Top Bottom