Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Hahiitaji kusoma IST ndio uweze kurithi mali za baba na kuzisimamia
Kwan hapa watu wanaongelea kwamba ukisoma IST ndo utaweza kusimamia mali za wazaz

Watu wameonyesha product ya IST ambayo ni tajir nmba moja Tanzania swala ni tumeangalia nn IST imeitengeneza na nini imezalisha na hicho ndo tumekitumia kwa Mo
 
Mkuu umetoka nje ya mada kabisa,habari za wivu zinatoka wapi tena ongea mada iliyopo mezani.
Mo karithi utajiri kwa baba yake kitu ambacho hata darasa la 7 pia anaweza kufanya kama kwa kuna mali.
Sawa tutajie hao darasa la 7 waliorithi mali za baba zao na wakawa the richest person in Tz na the youngest billionaire in Africa...usiongee general statement zisizo na data.!.usiwe kama wale wanaosema wasio soma wana maisha mazuri kuliko waliosoma but wakiambiwa walete data wanarukaruka
 
Hizo ni kazi za kufanywa na serikali yako kwa kuweka mazingira rafiki,we unataka afanye mtoto wa mwenzako aliyejipinda...acha iwe faida kwake na kwa familia yake, we lia na serikali yako
Kama hii ndio reasoning na analytical skills ya mliopita international schools, basi aliyesema hamuwezi kusoma science, nyie mnaenda kuwa maDJ wa muziki hajakosea
 
Nadhani serikali ijaribu kubuni mfumo mzuri utakaojengea wanafunzi ufahamu na uelewa wa kusoma na kuweza kutatua changamoto za mazingira yetu
siku watakayothubutu kufanya ivi na madarakani watang'oka kitu ambacho wao hawataki kukisikia.....
 
nilipomuuliza mate wangu wa chuo anawalipia shs ngapi wanawe pale IST akanimbia shilingi milioni 17 tuu kwa mwaka, pumzi ikakataa kabisaaaa hapo hapo nikagundua hapa duniani kuna watu na viatu…………..
 
Mbona wengine tumesoma hizi hizi shule za sirikali, tena shule ya msingi kijijini kwa babu kuongea kilugha mwanzo mwisho lakini tumefanikiwa kupata scholorship kusoma Masters na PhD kwenye international universities ambazo zipo kwenye world ranking ya 10 bora, what happened?
Usingekuwa hapa muda huu

Amini maneno yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sina tu pesa,laiti Kama ningekuwa nazo Hakika wanangu wangesoma hizi shule...
 
Mkuu huko IST hawanaga zile barua za "Mzazi unakumbushwa kumalizia karo ya mwanao"
 
Hongera, maana umekuwa mzalendo. Jamii yetu imezungukwa na watu (wakulima, wafugaji, wavuvi) wanaoishi katika umasikini mkubwa. Je hizi elimu za IST zimewasaidia hawa watu wetu kuondoka kwenye umasikini? Kujieleza na confidence ni vitu vizuri sana, lakini elimu bora inatakiwa ijikite kwenye kuleta maendeleo ya watu katika jamii yetu na siyo mtu mmoja tu binafsi.
Natamani wanaosifia sana hizo international schools na wao kusoma Universities za nje ya nchi na kuishi huko watuletee mifano ya watu waliotoka hizo shule na kwa jinsi gani wamekuwa msaada/ role models kwa watu wetu wa Tanzania.
Je tunahitaji skills gani kuwasaidia wakulima na wafugaji wetu ambao ndio majority. Tunahitaji watu wa kwenda majukwaani na kwenye makongamano na kuongea kingereza/ kiswahili kizuri? Je ili vijana wetu waweze kujiajiri hapa Tanzania wanahitaji skills gani?
Hebu tuache haya mambo ya kurithiswa/ kuaminishwa na wakoloni tuwaze nje ya Box. Tunahitaji skills zipi za kuwatoa watu wetu kweye umasikini, wazalishe kwa ubora na ufanisi na kupata masoko ya bidhaa zao? Skills gani za kuwawezesha vijana kujiajiri?
Andiko lingekuwa zuri sana kama wangesema muasisi wa kampuni kama ASAS, Tanga milk, Shambani milk, alisoma IST kwa sasa anamiliki kiwanda cha bidhaa za maziwa. Ananunua maziwa kiwa wafugaji pia kaajiri waTanzania kadhaa kwenye processing, distribution na marketing. Hizo habari za exposure za kuishi na kufanya kazi nje ya nchi ni fursa zilizopo kwa vijana wachache sana na hazina trickle down effects kwa waTanzania walio wengi.

Je hao wanaosoma Kayumba wana msaada gani Kwa hao wakulima na wafugaji??

Kama hao wa IST Wana msaada kwao binafsi na familia zao..je Hilo sio Jambo jema??

Hao kina ASAs ni exceptional cases hata
Huko USA wanaofanikiwa kuanzisha biashara na kuajiri wengine ni asilimia moja tu..

Dhana ya elimu Bora isipimwe na uwezo wa kuajiri wengine
Mradi hawarudi kuwa mzigo Kwa jamii basi elimu imewasaidia
 
Tatizo hizo shule zenyewe katuletea huyo mzungu unayembeza,


Kakufundisha kusoma na kuandika na una type kupitia device yake...then unataka uvimbe eti elimu yao ni kuwa brainwashed ,ha ha haaa kweli dunia haiishiwi vituko
Hiki ndo namaanisha kwamba upo brainwashed, kabla wazungu wakoloni hawajaja afrika walikuwa hawaishi? na waliishi vp, kama hawakuwa na reasoning na analytical capability mnazotafuta sasa kwa wazungu.
 
Tatizo mtu mweusi yuko brainwashed na fikra kwamba hakuna anachoweza hadi asomeshwe na mzungu au asome shule za wazungu. Na hii ndo imefanya wazungu wametu-undermine karibu kila sekta ya maisha toka miaka mingi sana. Sasa wewe umekiri kwamba you among a few best students, lakini bado unajidharau kwamba bila kufundishwa reasoning na analysis na mzungu bado wewe si kitu!
unaijua taasisi inaitwa MENSA?
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Ila ukishindwa peleka English Media za ukweli angalau
 
Back
Top Bottom