Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Status
Not open for further replies.
Karibu sana mkuu!Gonga Balimi zako ukiwa na tahadhari sana kwa sababu ikitokea matope linakochwea hilo Jua yaka-overflow, Balimi itageuka kuwa msiba.
Ha ha ha Mkuu, hayo matope kidogo yana uwalakini, ila siyo vyema ku-block mind zetu, ngoja wanazuoni waje kutuambia hayo matope yana maana gani kiarabu isije ikawa ndiyo ile michezo ya kimjini
 
Unamkumbuka yule mwanafasafa wa kirumi aliyeuwawa na kanisa katoliki kwa kusema dunia ni duara na siyo flat?
Kurudi kwenye swali lako ni kwamba Quran haisomwi kama riwaya za kufikirika bali ipo kwa mafumbo ambayo huhitaji kusherehewa na kutafsiriwa kwa kutumia vitabu vingine na wanazuoni wasomi.
Vitu kama hivi mkuu ni beyond your tiny capabilities kuelewa..
Mfano " tumemuumba Adam kwa udongo.." kwa tiny brain yako utadhani Allah alikuwa na washirika.
Just let it go hii sio riwaya ya Eric Shigongo

Kwa hiyo, hapo kwa aya hiyo,sio Jua linaongelewa hapo? Ni nini hasa Mungu alikuwa anamaanisha kwa kumueeleza Muhammad kwamba Jua huzama katika matope meusi? Na vitabu gani hivyo ambavyo ndio Mungu kwavyo anatoa ufafanuzi? Na je hivyo vitabu,vinavyofafanua hayo mafumbo aliyokuwa Mungu anampatia Muhammad, navyo aliviandika Mungu au nani? Kama aliandika Mungu vilipokelewa na nani? Je,navyo vilipokelewa na Muhammad kwa kupitia malaika Gabriel? Na kama vitabu hivyo vya ufafanuzi havikupokelewa na Muhammad, vinaaminikaje? Na kama vitabu hivyo vya ufafanuzi havikuandikwa na Mungu vinaaminikaje kama ndio vyenye ufafanuzi wa ukweli?
 
Sawa sawa mkuu.Kuna mambo mengi sana tumeelezwa isivyo.Hili la Jua ni cha mtoto.Kuna masuala nitayaleta kadri ya muda utakavyoturuhusu ambayo tukiyaacha yaendelee kuaminiwa na kufundishwa namna yanavyofundishwa,tutakaokuwa tunapata hasara ni sisi wanadamu na sio Muhammad au Yesu Kristu.
Napenda sana uelewa wa kiwango hichi. Mambo mengi tumeaminishwa sivyo.
 
kwanza"" ni umbumbu"" kukaa na"kuamini kuwa Jua linatua kwenye ""matope " wakati"" inafamika kuwa linajoto Kali ""na kuunguza""", hayo matope"" mpka muda huu jamani"" si yangekuwa"" yameshaungua na udongo wake ""kuwa"" kma"" tofari la"" kuchoma""

wanao"" amini ""mafundisho", Ya dini",, ni watu " ambao ",wameamua " kuwa " wapumbavu" kifikira
 
na kule Roma ilikuwa unafungiwa sakramenti au kufukuzwa kabisa kuwa muumini kama ungetamka kuwa "dunia inalizunguka jua" pia wanasayansi wa kanisa waliamini dunia ni kama meza hivi ambapo unaweza kutembea hadi mwisho ambapo kuna "korongo" kubwaa!
Sasa hivi kanisa linapambana na utafiti na majaribio ya stem cell, maana siku akitengezwa binadamu kwenye maabara ndio utakuwa mwisho wa mafundisho ya "dhambi ya asili"

Sijawahi kuiamini hii misahafu na waandishi wake! Japo mimi ni mkatoliki kanisani huwa naenda kama " social activity" na sio kuitafuta mbingu.
Umenichekesha sana.
 
Wanajukwa:

Dunia yetu inaendelea kushika kasi katika suala la Sayansi na Tekinolojia.Kwa siku za hivi karibuni,wanasayansi wamegundua kuweza kutengeneza Moyo kwa kutumia stem cells,ikiwa ni hatua katika kuelekea kutengeneza moyo wa binadamu,hali ambayo itasaidia katika kukabiliana na matatizo ya Moyo yanayowakabili wanadamu,kwa kiasi kikubwa, yale ambayo uhusisha mwanadamu kupoteza maisha, kwa sababu tu Moyo wa mgonjwa husika hauna repair au hauwezi kubadilishwa.Miaka kama kumi hivi iliyopita,wanasayansi walikuwa wamefanikiwa kutengeneza Moyo wa panya kwa kutumia hizo stem cells.

Kumbe,kwa tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika sehemu mbalimbali duniani,ama ardhini au angani,zote zinalenga katika kuboresha maisha ya mwanadamu na hata kuongeza siku za kuishi kwake.Historia inao watu wengi sana ambao wamejihusisha na Sayansi kwa nyakati tofuati tofauti.

Leo,ninataka tumuangalie Mtume Muhammad kwa namna alivyoweza kujihusisha na suala la Sayansi kwa kile kinachosemwa ni kwa msaada wa Mungu.Kurani neno la Mungu;maneno ambayo Mungu akiisha kuyaandika huko Mbinguni, alikuwa anampatia Malaika Gabriel na malaika Gabriel akampatia Mtume Muhammad katika Nyakati tofauti tofauti na Muhammad kuyaweka katika maandishi,lakini kwa namna ya pekee,kwa mara ya kwanza kabisa ikiwa ni katika Pango lililoko katika Mlima Hira, Jabal an-Nour,huko Makka,ambako inadaiwa Mtume Muhammad alipokea ufunuo huo, kwa matatizo sana kwa sababu ya kutojua kwake kusoma na kuandika,Malaika Gabrieli alijikuta anamkaba.

Kwa njia ya ufunuo wa Kurani,tunafunuliwa mambo mengi ya Kisayansi ambamo Muhammad anatujuza jinsi mambo yalivyo.Kwa leo, ninawaletea jambo moja tu.Nalo ni juu ya namna Jua linavyokuchwa na kadri Mungu atakavyotujalia tutayaangazia na mambo mengine.


Kurani kupitia Sura al-Kahf (18: 83-86), inaeleza kwamba Jua huchwea katika chemchemu ya matope meusi mazito(dark Muddy spring):

“83-Na wanakuuliza khabari za Dhul- Qarnaini. Waambie: Nitakusimulieni baadhi ya hadithi yake.84 -Sisi tulimtilia nguvu katika ardhi na tukampa njia za kila kitu.85 - Basi akaifuata njia. 86 - Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika chemchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.”

Wakati Muhammad akiwa ametupasha ukweli huo ambao aliandikiwa na Mungu, Ukweli wa kisayansi umebainisha kwamba Jua ni kubwa zaidi na lenye joto kali kuliko dunia.Na ikitokea kwamba Dunia inakaribiana na Jua,basi dunia itayeyuka kutokana na joto kubwa la Jua.

Ukweli mwingine,ambao pia Sayansi imetupatia ni kwamba Jua halitembei bali sayari mbalimbali ndio hulizunguka,ikiwemo Sayari yetu ya Dunia. Historia inaonyesha kwamba mtu wa kwanza kugusagusa habari za kuwa Jua lilikuwa halizunguki alikuwa ni Aristarchus (310-230KK).

Aristarchus alikuwa ni mwana-Astronomia wa Kigriki.
Yeye aliamini dunia ilikuwa katikati ya Mfumo wa Jua(Solar system) na sayari zingine (ikijumuishwa na nyota ambazo zilikuwa zimefungwa katika nafasi fulani) ndio zilizokuwa zikilizunguka Jua.

Hata hivyo, baadaye mwanasayansi,Aristarchus, alikuja kugundua kuwa sio dunia iliyokuwa katikati ya Mfumo wa Jua, bali ni Jua na hivi kwamba ni Dunia na sayari zingine ndizo zilikuwa zikilizunguka Jua.Ugunduzi wa namna hii ulipatikana miaka mingi sana (takribani karne tatu hivi) kabla hata ya Yesu Kristu kuzaliwa na karne tisa kabla ya Muhammad kuzaliwa.

Mwanasayansi mwingine pia aliyekuja na mtizamo tofuati na wa Muhammad (kwa kadri ya ufunuo kutoka kwa Mungu) ni Jean Buridan (1300-1359/61). Huyu) anafahamika kama Mwanafalsafa Mashuhuri sana katika Ufaransa.Buridan alikuwa Mwalimu katika Kitivo cha Sanaa cha Chuo Kikuu cha Paris kwa kupindi chote cha maisha yake ya kitaaluma akimakinika hasa hasa katika masuala ya Logiki (Logic) na kazi za mwanafalsafa Aristotle.

Ni Bridan aliyeanzisha wazo juu ya kiitwacho Copernican Revolution katika Ulaya.Hili ni fundisho lililoleta mwangaza kutoka kuamini kwamba dunia ilikuwa imesimama sehemu moja katika ulimwengu na kwamba Jua ndio lilikuwa linaizunguka dunia (Geocentrism) hadi kueleweka kwamba kumbe Jua ndilo limesimama wakati dunia na sayari zingine zikilizunguka (Heliocentrism).

Kumbe, sasa kwa uchache,kwa mawazo ya hao wanasayansi wawili,tunapata picha kwamba Muenendo wa Jua kuchomoza na kutua sio jambo lililoanza wakati wa Muhammad.Na kama suala la Sayansi ya Mfumo wa Jua lilianza mapema kabla ya Yesu na Muhammad kuzaliwa, yeye Muhammad alipopewa ufunuo na Mungu, hakuweza kujiuliza iwapo ufunuo huo wa Mungu inakuwaje unapingana na ukweli wa mambo?Katika kutafakari ufunuo huu wa Mungu kwa Muhammad, nimejikuta nina maswali yafuatayo,ambayo naomba yatuongoze katika kujadili suala hili.Ni muhimu kujadili kwa sababu pengine Dunia inatufundisha vitu ambavyo havipo.Hivi kweli Mungu anaweza kumueleza Muhammad mambo ya uongo?Maswali mengine ambayo bila shaka hata wewe unaweza kujiuliza ni haya:

1. Hiyo Chemchemi ya matope mazito na meusi iko hapa duniani?Na kama haipo hapa duniani iko angani? Na kama iko angani iko sehemu gani?


2. Huyo Dhul-Qarnaini alikuwa ni kiumbe wa namna gani huyo aliyepewa uwezo wa kuona Jua linavyotumbukia katika matope?


3. Pamoja na kwamba wakati wakati wa Muhammad, labda Sayansi ya kwamba Jua halizunguki, isipokuwa dunia ndio hulizunguka Jua, ilikuwa haijafika katika maeneo ya ardhi ya Arabia, bado hata vizazi vya zamani sana havikupata kuwa na uelewa kama huo wa Muhammad kuwa Jua lilikuwa linatua matope meusi! Je,ilikuwaje katika Vizazi vyote hivyo hapo katikati(ikiwemo na Yesu mwenyewe ambaye Muhammad anamuelezea kama aliyekuwa na uwezo wa kufinyanga wanasesere na kuwapulizia uhai na wakawa ndege kamili), kabla ya Muhammad, akakosekana mtu mwenye uelewa wa kuliona Jua likizama katika matope meusi tofauti? Hivi wewe kwa sayansi hii ya Muhamma juu ya Jua kuchwea katika matope meusi haikupelekei kujiuliza yafuatayo:

· Je, Muhammad kusema mambo ambayo hakuwa nayo uthibitisho ilikuwa ni kutafuta tu kuonekana kwamba Mungu amempa ufunuo wa kipekee juu ya ulimwengu?


· Je, vizazi ya Kiarabu na dunia kwa ujumla baada ya kugundua kwa tafiti za kisayansi, ambazo zimethibitisha kuwa Jua huzungukwa na sayari mbalimbali, ikiwemo Sayari yetu ya dunia, vimuoneje, Muhammad na Uislamu kwa ujumla?


· Je,wanadamu wa vizazi vyote vinavyofahamu kuwa Jua halijawahi kuzama katika matope ama meusi,bluu au meupe, visimuamini Muhammad katika mambo mengine aliyoyasema au vimuchukulie kama mtu aliyekuwa anajaribu kupiga ramli ya jinsi mambo yalivyo?

Lakini swali la mwisho kabisa ambalo nitaomba ujiulize ni hili:Je,Ni kwa nini hadi leo baada ya kugundulika kuwa Jua halizami na wala halizunguki,ni kwa nini hadi sasa aya hiyo iko imesalia katika Kurani?Je,ni nani anasema uongo kati ya Mungu na wanasayansi juu ya suala la Jua?

Karibu kwa mjadala ili tupate kujua ukweli kwa faida ya maendeleo ya Dunia yetu.
Dini nyingi zina hadithi nyingi za kale zisizokuwa na ukweli, primitive mythologies
 
Tatizo kubwa ni AIBU, waumini wanaona aibu kukiri ukweli kwamba wamedanganywa!
hahaaaa ""wamedanganywa " muda mrefu sana ",so wanashindwa",kuachana " na imani zao " kwakuwa wanaogopa kuchekwa na wenzao""

juzi " nilikuwa " namueleza" jamaa " yangu",hizi Habari" aiseee"" alipanick sana "alifikia stage yakuniita" mimi " mtu mbaya
 
Ndugu usipotoshe Qur'an Kwa kuitafsiri wewe utakavyo!!!

(18:86) until when he reached the very limits where the sun sets,63 he saw it setting in dark turbid waters;64 and nearby he met a people. We said: "O Dhu al-Qarnayn, you have the power to punish or to treat them with kindness."65
63. “The setting place of the sun” does not mean the place of the setting of the sun. According to Ibn Kathir, it means that he marched to the west conquering one country after the other till he reached the last boundary of the land, beyond which there was ocean.

Lugha asili ya Kurani ni Kiarabu.Unalikubali hilo? Wewe umetumia tafsiri ya Kiingereza na mimi nimetumia tafsiri ya Kiswahili.Je,unataka kusema tafsiri ya Kiswahili siyo sahihi ila ya kiingereza ndio iko sawa? Je,kwa nukuu hiyo ya Kiswahili, ni wapi mimi nimekosea? Je,ni mimi niliyetafsiri Kurani katika lugha ya Kiswahili kuonyesha alichokiongea Muhammad?
 
hahaaaa ""wamedanganywa " muda mrefu sana ",so wanashindwa",kuachana " na imani zao " kwakuwa wanaogopa kuchekwa na wenzao""

juzi " nilikuwa " namueleza" jamaa " yangu",hizi Habari" aiseee"" alipanick sana "alifikia stage yakuniita" mimi " mtu mbaya

Huyo rafiki yako kama alikuona mbaya ni kwa sababu hafahamu mambo mengi.Hili la Jua ni cha mtoto.Ninawaomba wanazuoni wa kiislamu wajipange sawa sawa.Kuna hoja tunaomba majibu yake yasiyoacha shaka.
 
Ndugu usipotoshe Qur'an Kwa kuitafsiri wewe utakavyo!!!

(18:86) until when he reached the very limits where the sun sets,63 he saw it setting in dark turbid waters;64 and nearby he met a people. We said: "O Dhu al-Qarnayn, you have the power to punish or to treat them with kindness."65
63. “The setting place of the sun” does not mean the place of the setting of the sun. According to Ibn Kathir, it means that he marched to the west conquering one country after the other till he reached the last boundary of the land, beyond which there was ocean.

Wewe unasema mimi napotosha.Sawa unaweza kuniambia Muhammad alimaanisha nini kusema kwamba Mungu alimuambia kuwa maziwa ya Ng'ombe hutokea katikati ya Mavi na damu yake?
 
Ha ha ha Mkuu, hayo matope kidogo yana uwalakini, ila siyo vyema ku-block mind zetu, ngoja wanazuoni waje kutuambia hayo matope yana maana gani kiarabu isije ikawa ndiyo ile michezo ya kimjini
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Weweeeee hatariii Sana
 
Mud sijawahi kumwelewa kabisa, kuna mahali anasema alienda mbinguni go and return.

Hayo yote tutayaleta humu hadi yapatiwe majibu.Sasa wameanza kuhamisha magoli kwa kusema kwamba Kurani haisomwi kama vitabu anavyoandika Shigongo.Sawa, lakini mbona hawatuonyeshi hivyo vitabu vya kufafanulia hayo ambayo yameandikwa kwa mafumbo na Mungu?
 
So, if Muhammad in moving and finally viewing the boundary,was that enough for him to conclude that what he was seeing was the dark muddy spring onto which the Sun had set in?
 
Ha ha ha Mkuu, hayo matope kidogo yana uwalakini, ila siyo vyema ku-block mind zetu, ngoja wanazuoni waje kutuambia hayo matope yana maana gani kiarabu isije ikawa ndiyo ile michezo ya kimjini
hahaaaa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom