Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Status
Not open for further replies.
Sasa kama ni beyond our tiny capabilities kuelewa, hii Quran imeandikwa ili nani aielewe? Au ameandikiwa nani?

Safi kabisa mkuu! Na kama Kurani ni uncomprehensible document kwa binadamu yeye ameelewaje kwamba ni Uncomprehensible? Hiyo aya iko wapi? Na kama haieleweki kwa wanadamu,ni kwa nini Mungu alikuwa anampatia Muhammad kwa nguvu vile, tena kwa kumpiga kiasi kile, kule Pangoni?

Je,huyu jamaa anataka kutuambia kuwa Kurani hadi leo haieleweki kama vile ambavyo Muhammad alishindwa kuielewa wakati ule (hadi Mungu kuamua kumpiga Muhammad kwa njia ya Malaika Gabrieli)?
 
Hao walioamini kwamba Dunia ni kama Meza, huko Roma, walishakiri siku nyingi kwamba walifanya makosa kuamini hivyo.Je,wewe katika hilo la Jua kuchwea kwenye matope,una msimamo gani? Unasemaje sasa,kwamba Mungu ni muongo au sayansi ndiye imesepetuka?Tupe msimamo wako.
hahaaaa halafu utasemaje kwamba sayansi ni uwongo wakati ",unatumia material mbali mbali yanayokurahisishia" kuishi kwako "tena matukio hayo yakiwa nizao la sayansi"",hayo maandishi "Yao" yenyewe" walikuwa hawana uwezo " wakuyahifadhi" kwenye karatasi" mpaka pale Ambapo "wanasaynsi "walipogundua" tech ,, yakuhifadhi maandishi" kwenye vitabu"" so kwanini" wasingemwambia "mungu wao awapatie ujuzi wakufanya "hayo yote" kama "Kweli " hayo madai yao huwa ni yamsingi
 
Daah...huu uzi uko jukwaa sahihi kabisa maana una hoja nzito sana. Kama na kwenye kitabu cha wakristu cha Biblia kuna sentensi inayosema Joshua alisimamisha jua....je huu si ushahidi kuwa Mungu anasema Jua ndilo huzunguka dunia na siyo vinginenvyo?
hahaaa"" nilishamjibu mtoa Mada mmoja hivi ""
 
Safi kabisa mkuu! Na kama Kurani ni uncomprehensible document kwa binadamu yeye ameelewaje kwamba ni Uncomprehensible? Hiyo aya iko wapi? Na kama haieleweki kwa wanadamu,ni kwa nini Mungu alikuwa anampatia Muhammad kwa nguvu vile, tena kwa kumpiga kiasi kile, kule Pangoni?

Je,huyu jamaa anataka kutuambia kuwa Kurani hadi leo haieleweki kama vile ambavyo Muhammad alishindwa kuielewa wakati ule (hadi Mungu kuamua kumpiga Muhammad kwa njia ya Malaika Gabrieli)?
Mkuu akijibu hata hoja mojawapo kati ya hizi unitag
 
Dini nyingi zina hadithi nyingi za kale zisizokuwa na ukweli, primitive mythologies

Swali la Msingi ni kwamba inakuwaje Mungu awaandikie wanadamu hadithi na ngano na kuwaambia kuwa ndiyo matukio halisi? Ina maana Mungu hajui tofauti kati ya Hadithi na tukio halisi?
 
Karibu sana mkuu!Gonga Balimi zako ukiwa na tahadhari sana kwa sababu ikitokea matope linakochwea hilo Jua yaka-overflow, Balimi itageuka kuwa msiba.
Inaonekana mzee una majibu yako tayar na pia unajionyesha kabisa imani yako iko upande gani tayar umeanza kudhihaki kile ulichokiuliza.
Jiulize hivi biblia na quraan inatuambia mtu wa kwanza aliumbwa kwa udongo ambaye ni adamu,wanasayansi wametuambia mtu wa kwanza ametokana na sokwe na fuvu lake limegunduliwa Tanzania sasa hapo mzee wewe una amini lipi labda?
 
Hayo yote tutayaleta humu hadi yapatiwe majibu.Sasa wameanza kuhamisha magoli kwa kusema kwamba Kurani haisomwi kama vitabu anavyoandika Shigongo.Sawa, lakini mbona hawatuonyeshi hivyo vitabu vya kufafanulia hayo ambayo yameandikwa kwa mafumbo na Mungu?
Kweli kabisa, yapo mengi yana changanya sana Mud anasema shetani ni mbaya ila jini kiumbe mzuri hana shida anaweza kushirikiana na binadam bila shida.
 
Wanajukwa:

Dunia yetu inaendelea kushika kasi katika suala la Sayansi na Tekinolojia.Kwa siku za hivi karibuni,wanasayansi wamegundua kuweza kutengeneza Moyo kwa kutumia stem cells,ikiwa ni hatua katika kuelekea kutengeneza moyo wa binadamu,hali ambayo itasaidia katika kukabiliana na matatizo ya Moyo yanayowakabili wanadamu,kwa kiasi kikubwa, yale ambayo uhusisha mwanadamu kupoteza maisha, kwa sababu tu Moyo wa mgonjwa husika hauna repair au hauwezi kubadilishwa.Miaka kama kumi hivi iliyopita,wanasayansi walikuwa wamefanikiwa kutengeneza Moyo wa panya kwa kutumia hizo stem cells.

Kumbe,kwa tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika sehemu mbalimbali duniani,ama ardhini au angani,zote zinalenga katika kuboresha maisha ya mwanadamu na hata kuongeza siku za kuishi kwake.Historia inao watu wengi sana ambao wamejihusisha na Sayansi kwa nyakati tofuati tofauti.

Leo,ninataka tumuangalie Mtume Muhammad kwa namna alivyoweza kujihusisha na suala la Sayansi kwa kile kinachosemwa ni kwa msaada wa Mungu.Kurani neno la Mungu;maneno ambayo Mungu akiisha kuyaandika huko Mbinguni, alikuwa anampatia Malaika Gabriel na malaika Gabriel akampatia Mtume Muhammad katika Nyakati tofauti tofauti na Muhammad kuyaweka katika maandishi,lakini kwa namna ya pekee,kwa mara ya kwanza kabisa ikiwa ni katika Pango lililoko katika Mlima Hira, Jabal an-Nour,huko Makka,ambako inadaiwa Mtume Muhammad alipokea ufunuo huo, kwa matatizo sana kwa sababu ya kutojua kwake kusoma na kuandika,Malaika Gabrieli alijikuta anamkaba.

Kwa njia ya ufunuo wa Kurani,tunafunuliwa mambo mengi ya Kisayansi ambamo Muhammad anatujuza jinsi mambo yalivyo.Kwa leo, ninawaletea jambo moja tu.Nalo ni juu ya namna Jua linavyokuchwa na kadri Mungu atakavyotujalia tutayaangazia na mambo mengine.


Kurani kupitia Sura al-Kahf (18: 83-86), inaeleza kwamba Jua huchwea katika chemchemu ya matope meusi mazito(dark Muddy spring):

“83-Na wanakuuliza khabari za Dhul- Qarnaini. Waambie: Nitakusimulieni baadhi ya hadithi yake.84 -Sisi tulimtilia nguvu katika ardhi na tukampa njia za kila kitu.85 - Basi akaifuata njia. 86 - Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika chemchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.”

Wakati Muhammad akiwa ametupasha ukweli huo ambao aliandikiwa na Mungu, Ukweli wa kisayansi umebainisha kwamba Jua ni kubwa zaidi na lenye joto kali kuliko dunia.Na ikitokea kwamba Dunia inakaribiana na Jua,basi dunia itayeyuka kutokana na joto kubwa la Jua.

Ukweli mwingine,ambao pia Sayansi imetupatia ni kwamba Jua halitembei bali sayari mbalimbali ndio hulizunguka,ikiwemo Sayari yetu ya Dunia. Historia inaonyesha kwamba mtu wa kwanza kugusagusa habari za kuwa Jua lilikuwa halizunguki alikuwa ni Aristarchus (310-230KK).

Aristarchus alikuwa ni mwana-Astronomia wa Kigriki.
Yeye aliamini dunia ilikuwa katikati ya Mfumo wa Jua(Solar system) na sayari zingine (ikijumuishwa na nyota ambazo zilikuwa zimefungwa katika nafasi fulani) ndio zilizokuwa zikilizunguka Jua.

Hata hivyo, baadaye mwanasayansi,Aristarchus, alikuja kugundua kuwa sio dunia iliyokuwa katikati ya Mfumo wa Jua, bali ni Jua na hivi kwamba ni Dunia na sayari zingine ndizo zilikuwa zikilizunguka Jua.Ugunduzi wa namna hii ulipatikana miaka mingi sana (takribani karne tatu hivi) kabla hata ya Yesu Kristu kuzaliwa na karne tisa kabla ya Muhammad kuzaliwa.

Mwanasayansi mwingine pia aliyekuja na mtizamo tofuati na wa Muhammad (kwa kadri ya ufunuo kutoka kwa Mungu) ni Jean Buridan (1300-1359/61). Huyu) anafahamika kama Mwanafalsafa Mashuhuri sana katika Ufaransa.Buridan alikuwa Mwalimu katika Kitivo cha Sanaa cha Chuo Kikuu cha Paris kwa kupindi chote cha maisha yake ya kitaaluma akimakinika hasa hasa katika masuala ya Logiki (Logic) na kazi za mwanafalsafa Aristotle.

Ni Bridan aliyeanzisha wazo juu ya kiitwacho Copernican Revolution katika Ulaya.Hili ni fundisho lililoleta mwangaza kutoka kuamini kwamba dunia ilikuwa imesimama sehemu moja katika ulimwengu na kwamba Jua ndio lilikuwa linaizunguka dunia (Geocentrism) hadi kueleweka kwamba kumbe Jua ndilo limesimama wakati dunia na sayari zingine zikilizunguka (Heliocentrism).

Kumbe, sasa kwa uchache,kwa mawazo ya hao wanasayansi wawili,tunapata picha kwamba Muenendo wa Jua kuchomoza na kutua sio jambo lililoanza wakati wa Muhammad.Na kama suala la Sayansi ya Mfumo wa Jua lilianza mapema kabla ya Yesu na Muhammad kuzaliwa, yeye Muhammad alipopewa ufunuo na Mungu, hakuweza kujiuliza iwapo ufunuo huo wa Mungu inakuwaje unapingana na ukweli wa mambo?Katika kutafakari ufunuo huu wa Mungu kwa Muhammad, nimejikuta nina maswali yafuatayo,ambayo naomba yatuongoze katika kujadili suala hili.Ni muhimu kujadili kwa sababu pengine Dunia inatufundisha vitu ambavyo havipo.Hivi kweli Mungu anaweza kumueleza Muhammad mambo ya uongo?Maswali mengine ambayo bila shaka hata wewe unaweza kujiuliza ni haya:

1. Hiyo Chemchemi ya matope mazito na meusi iko hapa duniani?Na kama haipo hapa duniani iko angani? Na kama iko angani iko sehemu gani?


2. Huyo Dhul-Qarnaini alikuwa ni kiumbe wa namna gani huyo aliyepewa uwezo wa kuona Jua linavyotumbukia katika matope?


3. Pamoja na kwamba wakati wakati wa Muhammad, labda Sayansi ya kwamba Jua halizunguki, isipokuwa dunia ndio hulizunguka Jua, ilikuwa haijafika katika maeneo ya ardhi ya Arabia, bado hata vizazi vya zamani sana havikupata kuwa na uelewa kama huo wa Muhammad kuwa Jua lilikuwa linatua matope meusi! Je,ilikuwaje katika Vizazi vyote hivyo hapo katikati(ikiwemo na Yesu mwenyewe ambaye Muhammad anamuelezea kama aliyekuwa na uwezo wa kufinyanga wanasesere na kuwapulizia uhai na wakawa ndege kamili), kabla ya Muhammad, akakosekana mtu mwenye uelewa wa kuliona Jua likizama katika matope meusi tofauti? Hivi wewe kwa sayansi hii ya Muhamma juu ya Jua kuchwea katika matope meusi haikupelekei kujiuliza yafuatayo:

· Je, Muhammad kusema mambo ambayo hakuwa nayo uthibitisho ilikuwa ni kutafuta tu kuonekana kwamba Mungu amempa ufunuo wa kipekee juu ya ulimwengu?


· Je, vizazi ya Kiarabu na dunia kwa ujumla baada ya kugundua kwa tafiti za kisayansi, ambazo zimethibitisha kuwa Jua huzungukwa na sayari mbalimbali, ikiwemo Sayari yetu ya dunia, vimuoneje, Muhammad na Uislamu kwa ujumla?


· Je,wanadamu wa vizazi vyote vinavyofahamu kuwa Jua halijawahi kuzama katika matope ama meusi,bluu au meupe, visimuamini Muhammad katika mambo mengine aliyoyasema au vimuchukulie kama mtu aliyekuwa anajaribu kupiga ramli ya jinsi mambo yalivyo?

Lakini swali la mwisho kabisa ambalo nitaomba ujiulize ni hili:Je,Ni kwa nini hadi leo baada ya kugundulika kuwa Jua halizami na wala halizunguki,ni kwa nini hadi sasa aya hiyo iko imesalia katika Kurani?Je,ni nani anasema uongo kati ya Mungu na wanasayansi juu ya suala la Jua?

Karibu kwa mjadala ili tupate kujua ukweli kwa faida ya maendeleo ya Dunia yetu.
Hakuna la kujadili hapo! Kwasababu unavyoviita 'sayansi' na 'dini' ni vitu viwili tofauti.
Dini ni imani. Ni hiyari yako kuamini au kutoamini uambiwacho. Na si lazima mtu mwingine aamini uaminicho wewe.
Sayansi ni elimu, maarifa au taaluma. Kupitia elimu umeambiwa na umeelewa kwamba dunia ni sayari inayolizunguka jua, si kinyume chake.
Umeambiwa ukifa utakwenda 'mbinguni' labda umeamini; hata kama hujafa! Kuna la kujadili hapo? Ukishakufa ndio utajua ukweli au uongo wa hilo.
Kwanza kuna wengine wenye imani zao watakuona kama ni mchokozi. Unaweza kujikuta anamlaumu Mungu wako kwamba kwanini 'alikuumba' na kichwa kimoja tu; sio viwili au vinne? Ukitumia akili ya imani utapata jibu kuwa umeumbwa kwa mfano wa Mungu, (usiniulize kama Mungu ni mwanaume au mwanamke!)
Napendekeza huu mjadala wako uupeleke msikitini au kanisani kwa jinsi imani yako ilivyo.
 
Swali la Msingi ni kwamba inakuwaje Mungu awaandikie wanadamu hadithi na ngano na kuwaambia kuwa ndiyo matukio halisi? Ina maana Mungu hajui tofauti kati ya Hadithi na tukio halisi?
Mungu huwa haandiki, hakuwahi kuandika na hataandika kamwe. Wanadamu ndio wanaotunga na kuandika kisha kusema ni Mungu ili utunzi wao ukubalike
 
SANCTUS ANACLETUS usitake kupotosha, hapo Mwenyezi Mungu anaeleza kile DHIL QARNAIN (ALEXANDER THE GREAT ) "alichokiona" kwa udhaifu wake, someni muelewe bana, mbona ipo very clear ? .... 86 - Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika chemchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.”

Kwenye Aya nyingine ya SURAH AN'AM ( 6;78 ) anaeleza alichokiona ( Nabii ) Ibrahim
Na alipo liona jua linachomoza akasema: Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Huyu mkubwa kuliko wote. Lilipo tua, alisema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayo fanyia ushirikina.
So ina maana hapo Qur'ani inasema kuwa Jua ndio Mola mlezi mkubwa wa Ibrahim ?? Na zipo nyingi Aya kama hizo ,
Qur'an huwezi kusoma ukaielewa unavyotaka wewe , uinyofoe aya katikati ( out of context ) mbichi mbichi ikupe tafsiri uonavyo wewe mkuu bila kujua sababu ya kushuka kwake,n.k.
 
Ndugu usipotoshe Qur'an Kwa kuitafsiri wewe utakavyo!!!

(18:86) until when he reached the very limits where the sun sets,63 he saw it setting in dark turbid waters;64 and nearby he met a people. We said: "O Dhu al-Qarnayn, you have the power to punish or to treat them with kindness."65
63. “The setting place of the sun” does not mean the place of the setting of the sun. According to Ibn Kathir, it means that he marched to the west conquering one country after the other till he reached the last boundary of the land, beyond which there was ocean.

So, if Muhammad in moving and finally viewing the boundary,was that enough for him to conclude that what he was seeing was the dark muddy spring onto which the Sun had set in?So who was seeing on the way, the Sun moving towards boundaries,God or Muhammad?

Hivi kwa maelezo yako hayo unaelewa maana ya Kurani? Usitupotoshe kwa kutuletea maana tafsiri nyingine ya Kurani.Kurani maana yake ni maneno aliyoyaandika Mungu kwa mkono wake mwenyewe na kisha kumpatia Malaika Gabrieli (naye bila editing wala addition) akampatia Muhammad.Kwa hiyo,hiyo suala lolote linalosemwa na Muhammad maana yake ni Mungu anasema na sio vinginevyo!
 
Mungu huwa haandiki, hakuwahi kuandika na hataandika kamwe. Wanadamu ndio wanaotunga na kuandika kisha kusema ni Mungu ili utunzi wao ukubalike

Maneno hayo kwamba Mungu ndiye aliandika na kisha kumpatia Muhammad, yako katika Kurani na wala sio yangu, mkuu.Mimi nasaidia tu kueleza kile ambacho Mungu ameshakisema kupitia Kurani.
 
Kweli kabisa, yapo mengi yana changanya sana Mud anasema shetani ni mbaya ila jini kiumbe mzuri hana shida anaweza kushirikiana na binadam bila shida.
nafuu ya shetani nimbaya watu wanaaminishwa Kuwa
anga la blue ni mbingu nawao wanaamimi
 
[color=redûHapa tunajadili ukweli wa Kisayansi juu ya Jua [/color]na ambao unaihusu jamii ya wanadamu.Au wewe Jua halikuhusu na halina faida kwako? Unapendekeza tukafanye mjadala kama huu huko msikitini au kanisani,kwani Mungu Jua linamsaidia nini?
Mie naona unatuletea uongo wa sayansi juu ya juwa.
 
Sawa sawa mkuu.Kuna mambo mengi sana tumeelezwa isivyo.Hili la Jua ni cha mtoto.Kuna masuala nitayaleta kadri ya muda utakavyoturuhusu ambayo tukiyaacha yaendelee kuaminiwa na kufundishwa namna yanavyofundishwa,tutakaokuwa tunapata hasara ni sisi wanadamu na sio Muhammad au Yesu Kristu.
Binafsi elimu dunia nimeisoma na kuilinganisha na elimu ya Mungu. Elimu ya Mungu iko pure na hapana chembe ya uongo. Suala la jua kutozunguka hiyo ni uongo wa kisayansi, kwani kiuhalisia hata kwa kulitazama jua lina Move.
Kwamba dunia ni elliptical sphere, pamoja kung'ang'anizwa nikariri hivyo mpaka leo hii nimekataa na naona kwa macho yangu dunia ni flat, Jua, Mwezi na Nyota zote zinazunguka juu ya uso wa dunia, Jua na mwezi zikiwa na ukubwa sawa na kiwango cha mwanga tofauti lakini Nyota zikiwa ni ndogo kuliko jua na mwezi.
By the way, Jua sio Nyota na wala Nyota sio jua kama sayansi inavyolazimisha.
Zaidi ya hapo vitu vinavyoitwa sayari is just "sci-fi" tu but in reality hakuna kitu kinaitwa sayari angani but kuna Mwezi, Jua, na Nyota.
Drama za NASA hasa ni za kupinga ukweli halisi (ambao hata wao wa Naujua) na kule launch uongo mkuu kwa malengo maalumu kabisa.
Bila Shaka Dunia sio sayari na haijawahi kuwa, tena ni kweli Antarctica sio bara la saba kwa ukubwa bali ni Sio bara kabisa ndio maana hata kwenye bendera ya UN naya USGS halijaoneshwa kwa kwa kuwa sio bara.
Kwa kumalizia ni kwamba sio wanasayansi wote wanaothibisha kuwa jua ni Immovable objects lipo kundi kubwa tu la wanasayansi wa kale na wa kisasa wanaothibisha pasipo chembe ya shaka kuwa dunia ni immovable, na jua, mwezi na Nyota ni movable objects.
So neno la Mungu always linabaki sahihi na la binadamu (hao wanasayansi) uongo wa makusudi wenye nia ovu!!
 
SANCTUS ANACLETUS usitake kupotosha, hapo Mwenyezi Mungu anaeleza kile DHIL QARNAIN (ALEXANDER THE GREAT ) "alichokiona" kwa udhaifu wake, someni muelewe bana, mbona ipo very clear ? .... 86 - Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika chemchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.”

Kwenye Aya nyingine ya SURAH AN'AM ( 6;78 ) anaeleza alichokiona ( Nabii ) Ibrahim
Na alipo liona jua linachomoza akasema: Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Huyu mkubwa kuliko wote. Lilipo tua, alisema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayo fanyia ushirikina.
So ina maana hapo Qur'ani inasema kuwa Jua ndio Mola mlezi mkubwa wa Ibrahim ?? Na zipo nyingi Aya kama hizo ,
Qur'an huwezi kusoma ukaielewa unavyotaka wewe , uinyofoe aya katikati ( out of context ) mbichi mbichi ikupe tafsiri uonavyo wewe mkuu bila kujua sababu ya kushuka kwake,n.k.


Mkuu kaa vizuri sana katika uzi huu kwa maana ukija pupa utakosa mlango wa kutokea! Hapo Mungu anaongeleaje habari za Alexander the Great? Alexander, aongelewe hapo kwa faida ya nani hasa? Mungu alikuwa anamueleza Muhammad habari za Alexander kwa ili Muhammad apate picha gani hasa?

Hivi unafahamu kuwa Alexander the Great aliishi miaka mingi sana kabla ya hata Yesu Kristu kuzaliwa au hata Muhammad?

Mtawala aliyeitwa Aleksanda Mkuu (Alexander the Great) alikuwa ni mtawala(Mfalme) wa Makedonia (336-323 KK).Makedonia ni eneo la kijiografia na kihistoria katika Peninsula ya Balkani, kusini-mashariki mwa bara la Ulaya.Je,ni lini Muhammad aliwahi kufika Makedonia kabla hajazaliwa hadi akaweza kuona jinsi Alexander alivyoliona Jua likizama katika matope?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom