Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 2,318
- 8,464
Kuna taarifa kuwa basi la Shule ya King David iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani limepata ajali mbaya iliyopelekea vifo vya wanafunzi na dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa jina moja Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa mika (54-60)
Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.
Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.
======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI
Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.
Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.
Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.
UPDATES: 1130HRS
Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha
RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi
''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''
Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.
Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.
======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI
Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.
Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.
Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.
UPDATES: 1130HRS
Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha
RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi
''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''