Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

KUTOKA KWA VYANZO MBALIMBALI, Huu ni mtiririko wa matukio ya Mauji hayo.

NACHINGWEA.....
Kijana mmoja ambaye ni mkazi wa NACHINGWEA, LINDI ambaye pia anajihusisha na biashara ya madini, mwishoni mwa mwaka uliopita yaani 2021, alipata bahati ya kupata madini yenye thamani kadhaa, hali hii ilimpelekea kupata connection moja na mzungu ambaye alimuuzia madini hayo na kupata Dola za kimarekani Elfu kadhaa.

Mara baada ya kupata kiasi hicho cha fedha, ilibainika wazi kuwa asingeweza badilisha pesa zile ktk wilaya ya Nachingwea, hivyo akaona bora aende MKOANI MTWARA ambako ndio makao makuu ya benki karibia zote kwa Mikoa ya Kusini. Mkoa ambao pia wanapatikana ndugu zake kadhaa pia ambapo mjomba wake anayejishughilisha na ukatishaji wa tiketi za magari katika stendi ya Mkanaledi Mjini hapo.

Mkoani MTWARA...
Mara baada ya kuwasili mjini hapo, alimjulisha Mjomba wake huyo juu ya kile kilichompeleka hapo ili awe msaada wake. Hapo wakachagua Benki ya NMB kwenda kubadilishia Fedha hizo.

NMB MTWARA....
Mara baada ya kufika benki hapo, alipokelewa na Mhudumu wa benki mmoja wa kike, ambapo alimshughulikia kama mteja mpaka kufanikisha kupata fedha zinazokadiriwa kufikia au kuvuka mil 70 za Tanzania.

TATIZO LINAANZA....
Mara baada ya kuchukua Fedha hizo, mhudumu huyo wa NMB alimuuliza kijana yule kuwa anataka kurudi LINDI siku ile ile, ambapo alijibiwa na kijana huyo kuwa ndio anataka kurudi kwao.
Hapa sasa yule mhudumu wa BENKI akamshauri yule kijana asiondoke na pesa zote zile kwa siku ile, ni bora atafute Lodge nzuri apumzike ili kesho yake aweze kuondoka kwa amani zaidi. Kijana yule alikubali na kwa ugeni wake akaamua kumuuliza Mhudumu yule ni Lodge ipi nzuri kwake, ndipo akaelelezwa na akaenda huko ambapo pia alimjulisha mjomba wake.

[emoji117][emoji117][emoji117] INASEMEKANA SASA YULE MHUDUMU WA NMB ALIWATONYA MAMWELA (POLISI) KUWA KUNA ISHU YA PESA NDEFU NA MUHUSIKA YULE YUPO LODGE FULANI MJINI PALE.

LODGE....
Mara baada ya kuwasili Lodge hiyo, hapo ndipo tatizo lilianza rasmi, usiku alifuatwa na Polisi kadhaa ambapo walimtishia na kuchukua vitu vyake vyote. Waliondoka nae mpaka kituo kikuu cha polisi mjini hapo. Huku akipewa masharti ya kuwa akiulizwa kwanini amekamatwa aseme alikuwa anendesha pikipiki hivyo alivunja sheria za barabarani. Inasemekana sasa alipewa Laki moja aondoke na atarudi tar 6 mwezi huu. Lakini inasemekana askari wale kutokana na tamaa zaidi ya fedha walimchukua mpaka NACHINGWEA na wakamchukulia pesa zake zingine na kumuacha.

ANARUDI KITUONI...
Kama alivyoambiwa arudi kituoni hapo, alirudi kituoni hapo akiwa na mjomba wake ambapo sasa alikuja kufuata vitu vyake alivyoporwa ikiwa sambamba na pesa zake. Mara baada ya kufika askari wale walimchukua kwa madai wanaenda kumhoji. Wakati huo mjomba wake akiwa nje ya kituo hiko akimsubiri mpwawe huyo.
Dakika zikapita, masaa yakapita, hatimaye siku ikaisha bila kumuona mpwa wake huyo.

Siku ya pili, mjomba alirudi polisi kujua hasa mpwa wake alikopelekwa, lkn hakupata majibu sahihi. Hali hii ilipelekea kutoa taarifa NACHINGWEA na hapo familia ikaenda kwa Mkuu wa wilaya ya NACHINGWEA ili wapatiwe msaada wa kumpata ndugu yao huyo. Taarifa zilifika mbali zaidi ambapo sasa uchunguzi ulifanyika kubaini nini tatizo halisi.

YAGUNDULIKA KUUAWA...
Watoa taarifa wanadai ikagundulika kuwa kumbe alichukuliwa na kwenda kuuawa tena kwa kupigwa sindano ya Sumu, kisha mwili wake kwenda kufukiwa kusikojulikana.

ASKARI WASAKWA WAKAMATWA.
Maafisa waandamizi wa Polisi mkoani hapo wamekamatwa wapo gereza laLILUNGU mjini hapo, MKUU WA KITUO, OC-CID na askari kadhaa, pia yupo askari amekimbia lkn taarifa zinadai pia mhudumu wa NMB anasakwa kuunganishwa kwenye kesi hiyo ya kikatili zaidi.

Askari mmoja ajiua...
Inasemekana mara baada ya kesi hii kujulikana, basi askari mmoja wapo mara baada ya kukamwatwa na kuwekwa mahabusu alijiua kwa kujinyonga kwa kutumia shati lake.

Hadi sasa bado familia hawajakabidhiwa mwili wa kijana wao.
KUTOKA KWA WASIMULIAJI WA MKONI MTWARA NA VYANZO VYA HABARI KAMA ITV, MWANANCHI NK
 
Waandishi wa habari walitaka kupata Maelezo ya kilichosababisha mfanyabiashara wa madini afariki akiwa mikononi mwa polisi lakini IGP Sirro akasema yeye yuko kwenye ziara ya Waziri hivyo ni vema waandishi hao wakamuuliza Waziri.

Source: ITV habari
Polisi wameanza kuchezea kesi, aliyejinyonga mahabusu ni afisa wao, hapo mahabusi alikuwa peke yake? Mahabusu imekuwaje na mazingira ya mtu kujinyonga? Haki ya huyu mfanyabiasha itapotea tusipoliangalia ili suala, wanatengeneza story sasa
 
Kwa ufupi Siro anatakiwa aachie ngazi huwa anawatetea sana Polisi waovu
 
kuna police alikuwa anaitwa Benadi kama sikosei.kikosi chao kilikuwa na askari kazaa pale Morogoro ila nisingependa kuwataja.
hawa police walikuwa wakifanya unyang'anyi wa kiujambazi kwa wa2 wengi sana.Ila uyu benad ambae aliingia kazini kwa kipaji cha kucheza mpila alipatwa na shida ya kuifiwa na mke wake.Ila cjajuwa kilichomuuwa mkewe.
kutokana na kifo cha mkewake ambae alikuwa anafanya kazi SUA uyu askari akaamuwa kuokoka.
Sasa basi katika kuokoka kwake ilimbidi aanze kutubu matendo yote ambayo alikuwa wakiyafanya.
Apo ndio alikuwa anaamuwa kuyasema adhalani matendo ambayo alikuwa wakiyafanya na askali wenzake.siwezi kuelezea sana mambo ambayo walikuwa wakiyafanya ila hayatofautiani na aya waliyofanya askali wa mtwala akina Zombe.
Mwisho waliamua kutangaza kama yule askali amechanganyikiwa na wakampeleka dodoma milembe ila bado mshikaji alikoamaa na msimamo wake na kuamuwa kuandika vijalada kuutangazia uma kwa matendo yao waliyokuwa wakiwafanyia rahia hasa wafanya biashala wenye hela.
Mwisho kabisa uyu askali walimkuta amejinyonga ila kwanye mazingila yanaonyesha kuwa aliuwawa ila kwakuwaa upelelezi wanafanya wao hivyo walifanikiwa kumpoteza.
Kati ya maaskari waliobaki ni yule ambae niliona you tube amejitengenea kabuli.Nazani damu za wasio na hatia zishaanza kumtafuna...
Nazani damu za watu wasio na hatia.. 76 nazani anaitwa.
naomba nisiongee sana maana zama za jiwe bado zinaendelea...Matendo yanayo tendeka sasa c mageni kwenye idala hii😭😢!!!
m
Fanyia kazi R na L
 
KUTOKA KWA VYANZO MBALIMBALI, Huu ni mtiririko wa matukio ya Mauji hayo.

NACHINGWEA.....
Kijana mmoja ambaye ni mkazi wa NACHINGWEA, LINDI ambaye pia anajihusisha na biashara ya madini, mwishoni mwa mwaka uliopita yaani 2021, alipata bahati ya kupata madini yenye thamani kadhaa, hali hii ilimpelekea kupata connection moja na mzungu ambaye alimuuzia madini hayo na
Story kama ya Jamal Khashoggi
 
Wewe ni polisi? Au baba yako ni polisi acheni dhuluma na ujambazi.
Wewe sio spokesperson wangu,soma to understood mkuu,tatizo langu ni chanzo cha habari hii,siliamini na sitokuja kuliamini gazeti la Mwananchi.
 
Imenikumbusha 14 January ya mwaka 2006 Zombe na kina Bageni walipowauwa kinyama wale jamaa wanne Sabinus Chigumbi na nduguze na jamaa yangu Juma Ndugu aliyekuwa IT driver wa miaka hiyo na dereva tax pale Magomeni.
 
Waandishi wa habari walitaka kupata Maelezo ya kilichosababisha mfanyabiashara wa madini afariki akiwa mikononi mwa polisi lakini IGP Sirro akasema yeye yuko kwenye ziara ya Waziri hivyo ni vema waandishi hao wakamuuliza Waziri.

Source: ITV habari
Sirro bure kabisa.
Juzi vijana wake wa Traffic wsmekamatwa na TAKUKURU wakila rushwa mchana kweupe.
Hakuwa na la kusema.
Leo vijana wake wanaua na kupora, hana la kusema.
Sirro is useless.
 
KUTOKA KWA VYANZO MBALIMBALI, Huu ni mtiririko wa matukio ya Mauji hayo.

NACHINGWEA.....
Kijana mmoja ambaye ni mkazi wa NACHINGWEA, LINDI ambaye pia anajihusisha na biashara ya madini, mwishoni mwa mwaka uliopita yaani 2021, alipata bahati ya kupata madini yenye thamani kadhaa, hali hii ilimpelekea kupata connection moja na mzungu ambaye alimuuzia madini hayo na kupata Dola za kimarekani Elfu kadhaa.

Mara baada ya kupata kiasi hicho cha fedha, ilibainika wazi kuwa asingeweza badilisha pesa zile ktk wilaya ya Nachingwea, hivyo akaona bora aende MKOANI MTWARA ambako ndio makao makuu ya benki karibia zote kwa Mikoa ya Kusini. Mkoa ambao pia wanapatikana ndugu zake kadhaa pia ambapo mjomba wake anayejishughilisha na ukatishaji wa tiketi za magari katika stendi ya Mkanaledi Mjini hapo.

Mkoani MTWARA...
Mara baada ya kuwasili mjini hapo, alimjulisha Mjomba wake huyo juu ya kile kilichompeleka hapo ili awe msaada wake. Hapo wakachagua Benki ya NMB kwenda kubadilishia Fedha hizo.

NMB MTWARA....
Mara baada ya kufika benki hapo, alipokelewa na Mhudumu wa benki mmoja wa kike, ambapo alimshughulikia kama mteja mpaka kufanikisha kupata fedha zinazokadiriwa kufikia au kuvuka mil 70 za Tanzania.

TATIZO LINAANZA....
Mara baada ya kuchukua Fedha hizo, mhudumu huyo wa NMB alimuuliza kijana yule kuwa anataka kurudi LINDI siku ile ile, ambapo alijibiwa na kijana huyo kuwa ndio anataka kurudi kwao.
Hapa sasa yule mhudumu wa BENKI akamshauri yule kijana asiondoke na pesa zote zile kwa siku ile, ni bora atafute Lodge nzuri apumzike ili kesho yake aweze kuondoka kwa amani zaidi. Kijana yule alikubali na kwa ugeni wake akaamua kumuuliza Mhudumu yule ni Lodge ipi nzuri kwake, ndipo akaelelezwa na akaenda huko ambapo pia alimjulisha mjomba wake.

[emoji117][emoji117][emoji117] INASEMEKANA SASA YULE MHUDUMU WA NMB ALIWATONYA MAMWELA (POLISI) KUWA KUNA ISHU YA PESA NDEFU NA MUHUSIKA YULE YUPO LODGE FULANI MJINI PALE.

LODGE....
Mara baada ya kuwasili Lodge hiyo, hapo ndipo tatizo lilianza rasmi, usiku alifuatwa na Polisi kadhaa ambapo walimtishia na kuchukua vitu vyake vyote. Waliondoka nae mpaka kituo kikuu cha polisi mjini hapo. Huku akipewa masharti ya kuwa akiulizwa kwanini amekamatwa aseme alikuwa anendesha pikipiki hivyo alivunja sheria za barabarani. Inasemekana sasa alipewa Laki moja aondoke na atarudi tar 6 mwezi huu. Lakini inasemekana askari wale kutokana na tamaa zaidi ya fedha walimchukua mpaka NACHINGWEA na wakamchukulia pesa zake zingine na kumuacha.

ANARUDI KITUONI...
Kama alivyoambiwa arudi kituoni hapo, alirudi kituoni hapo akiwa na mjomba wake ambapo sasa alikuja kufuata vitu vyake alivyoporwa ikiwa sambamba na pesa zake. Mara baada ya kufika askari wale walimchukua kwa madai wanaenda kumhoji. Wakati huo mjomba wake akiwa nje ya kituo hiko akimsubiri mpwawe huyo.
Dakika zikapita, masaa yakapita, hatimaye siku ikaisha bila kumuona mpwa wake huyo.

Siku ya pili, mjomba alirudi polisi kujua hasa mpwa wake alikopelekwa, lkn hakupata majibu sahihi. Hali hii ilipelekea kutoa taarifa NACHINGWEA na hapo familia ikaenda kwa Mkuu wa wilaya ya NACHINGWEA ili wapatiwe msaada wa kumpata ndugu yao huyo. Taarifa zilifika mbali zaidi ambapo sasa uchunguzi ulifanyika kubaini nini tatizo halisi.

YAGUNDULIKA KUUAWA...
Watoa taarifa wanadai ikagundulika kuwa kumbe alichukuliwa na kwenda kuuawa tena kwa kupigwa sindano ya Sumu, kisha mwili wake kwenda kufukiwa kusikojulikana.

ASKARI WASAKWA WAKAMATWA.
Maafisa waandamizi wa Polisi mkoani hapo wamekamatwa wapo gereza laLILUNGU mjini hapo, MKUU WA KITUO, OC-CID na askari kadhaa, pia yupo askari amekimbia lkn taarifa zinadai pia mhudumu wa NMB anasakwa kuunganishwa kwenye kesi hiyo ya kikatili zaidi.

Askari mmoja ajiua...
Inasemekana mara baada ya kesi hii kujulikana, basi askari mmoja wapo mara baada ya kukamwatwa na kuwekwa mahabusu alijiua kwa kujinyonga kwa kutumia shati lake.

Hadi sasa bado familia hawajakabidhiwa mwili wa kijana wao.
KUTOKA KWA WASIMULIAJI WA MKONI MTWARA NA VYANZO VYA HABARI KAMA ITV, MWANANCHI NK
Askari aliekimbia ni Zabroni ndio mtu wao wa connection, mara nyingi anakaa kwenye Bar ya shooters akichunguza nani ana pesa za kutosha na kuwatonya kundi lake la kigaidi.
 
Bila kukagua vyeti vya shule tutazidi kuangamizwa raia na hawa police.
 
Back
Top Bottom