Muda ni protocol ya usafiri kwenye msiba wa Malkia, kila kiongozi angetumia usafiri wake kungekuwa na foleni

Hii ndo ilikua hoja ,na ndo maana mjadala umekua mkubwa, watu wasijifiche kwenye kichaka Cha kuita watu sijui wajinga, watu wanaelewa why wanahoji na why imekua story, hasa KWa viongonzi watokao afrika
Kabisa mkuu,utashangaa akirudi bongo ataenda kupokewa na viongozi 50 airport kila mmoja na V8 lake,kwa nini wasipakiwe kwenye basi
 
Ni.ngumu mtanzania kumuelewesha. Ubaya watanzania tuna jiona tuna jua kila kitu. Mimi sijaona kosa lolote kwa viongozi wetu na mataifa mengine kupanda bus. Ukichoandika mkuu umeelezea vzr. Kama watu hawatakuelewa basi wana mtindio tu wa ubongo. Sio kila jambo la.kubisha. Viongozi zaidi ya 500 wote na misafara yao au hata na gari moja moja aisee pasingetosha kwa kweli
 
Ume quote vizuri " ujuaji" ni tatizo linakuja kwa kasi hapa nchini
 
Walisha wahi kuja Marais hata 10 kwa wakati mmoja hapa kwetu?
Unaukumbuka mkutano wa Sulivan kipindi cha JK,
AICC arusha huwa inajaza mikutano ya AU marais zaidi ya 50
Tuje nchini mawaziri siku ya msiba wa Jpm kwa nini hawakupakizwa kwenye mabasi,hatupingi mabasi bali tunataka wayatumie hata huku
 
Kabisa mkuu,utashangaa akirudi bongo ataenda kupokewa na viongozi 50 airport kila mmoja na V8 lake,kwa nini wasipakiwe kwenye basi
Halafu barabara zote zitafungwa na njia nzima watatapakaa maaskari wenye silaha nzito nzito utadhani wanaenda vitani.

Ni wachache sana wataelewa kwa nini maRais wetu kupakiwa kwenye basi kumekuwa gumzo. Miunguwatu kwenye basi!
 
Shida ni kwamba kwanini wakirudi nyumbani msafara unakuwa na magari 80+,kwanini yasipatikane mabasi mawili na magari manne madogo kwenye Convoy??
 
Halafu barabara zote zitafungwa na njia nzima watatapakaa maaskari wenye silaha nzito nzito utadhani wanaenda vitani.

Ni wachache sana wataelewa kwa nini maRais wetu kupakiwa kwenye basi kumekuwa gumzo. Miungumtu kwenye basi!
Naona akili zenu zimeathiriwa na mazingira tuliyopo, na mazoea, ni kama vile hamkuwahi kudhania iko siku mtamuona Rais kwenye bus!.

Kama mngejua Samia yupo nchi nyingine, yenye sheria na taratibu tofauti, sidhani kama mngeshangaa kwake kupandishwa bus.

Binafsi ningeshangaa Samia kupandishwa bus, kama ingefanyika hivyo ndani ya hizi nchi zetu zinazofanana tabia ambazo marais wao walikuwa kwenye bus moja na Samia.

Simply mnachotetea nyie, ni kama vile mlitaka Rais wetu akavunje sheria na taratibu za wengine, ambapo naamini kama angefanya hivi, mngesema pia.
 
Halafu barabara zote zitafungwa na njia nzima watatapakaa maaskari wenye silaha nzito nzito utadhani wanaenda vitani.

Ni wachache sana wataelewa kwa nini maRais wetu kupakiwa kwenye basi kumekuwa gumzo. Miunguwatu kwenye basi!
Kama hawajapata cha kujifunza hawatajifunza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…