Muda ni protocol ya usafiri kwenye msiba wa Malkia, kila kiongozi angetumia usafiri wake kungekuwa na foleni

Muda ni protocol ya usafiri kwenye msiba wa Malkia, kila kiongozi angetumia usafiri wake kungekuwa na foleni

Ila kweli kwa zile nyuzi na comments za jana, sisi weusi tuna shida sana sana. Yaani Raisi wa Ujerumani kapanda basi na raia wake wala hawana shida. Waziri mkuu wa New Zealand, Raisi wa Italia, Raisi wa EU n.k... vile vile na huoni malalamiko yoyote. Ndio utajua wengi hatuna exposure, tuna uelewa mdogo, tunapenda ufahari. Hizi ni dalili za udumavu wa akili na sababu kubwa ni lishe duni kabla na baada ya kuzaliwa na wakati wa makuzi yetu.
Siyo kwamba watu hawana exposure au udumavu wa akili.Tatizo hapa ni hawa viongozi wa afrika na matumizi mabaya ya fedha za umma.mfano Rais kuwa na msafara wa magari zaidi ya 40 ya nini sasa tena v8.Ukiangalia ulaya wao hawana hiyo mbwembwe,misafara yao haizidi magari kumi.yaani Nchi tajiri zinatumia rasilimali vizuri kuliko viongozi wa afrika ndiyo maana nchi ulizozitaja kama ufaransa nk wananchi wake hawajawaponda viongozi wao tofauti na na wa huku afrika
 
MARAIS WA AFRIKA KUPAKIWA KWENYE BUS NI DHIHAKA?

Na Abbas Mwalimu
(0719258484).

Jumatatu tarehe 19 Septemba, 2022.

Kumekuwa na mijadala mingi kuhusu viongozi wa Afrika kupakiwa kwenye usafiri (bus) wa gari moja wakati wakielekea kwenye ibada ya mazishi Westminster Abbey.

Swali ni je walikuwa viongozi wa nchi za Afrika pekee?

Kwa nini matukio makubwa au mikutano hutumia mabasi?

Kimsingi hawakuwa viongozi wa Afrika pekee waliopanda kwenye mabasi bali viongozi wengi walioalikwa walitumia mabasi.

Tukumbuke kuwa tukio lile lilikutanisha Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali na Wawakilishi zaidi ya 500 kutoka nchi na taasisi mbalimbali duniani hivyo maandalizi ya usafiri yalihitaji kuratibiwa vizuri.

Kimsingi baadhi ya viongozi waliopanda mabasi ni Waziri Mkuu wa Ireland Micheál Martin, Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese, Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern, Mfalme Abdullah II wa Jordan na mkewe Malkia Rania.

Aidha wengine waliopanda mabasi ni Rais wa Malaysia Agong Al-Mustafa Billah Shah, Rais wa Singapore Halimah Yacob, Mfalme wa Japan Naruhito, Rais wa Poland Andrzej Duda, na Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier.

Vilevile, Mfalme Carl XVI Gustaf wa Sweden na mkewe Silvia, Malkia Margrethe II wa Denmark, Mfalme Felipe na Malkia Letizia wa Hispania, Rais wa Italia Sergio Mattarella, Rais wa Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen, Mfalme Harald wa Norway na mkewe Malkia Sonja nao walipanda mabasi.

Matukio makubwa kama mikutano au msiba kama ule wa Malkia Elizabeth II ambao ulikutanisha viongozi wengi njia rahisi ya kuwafikisha katika tukio kwa muda uliopangwa ni kutumia usafiri wa pamoja.

Tufahamu kuwa matukio ya namna ile yanaongozwa na itifaki (protocol) na miongoni mwa mambo muhimu katika protocol ni muda.

Sasa tujiulize kama kila kiongozi angepangiwa muda wake na msafara wake (motorcade) hali ya msongamano ingekuwaje?

Ni muda gani ungetumika kukamilisha idadi ya viongozi wote kufika Westminster Abbey?

Hatudhani kuwa muda wa ibada ya mazishi ungeathiriwa na misafara ya viongozi?

Ifahamike kuwa katika matukio kama lile na yafananayo na lile utaratibu wa usafiri, malazi na usafiri huratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi husika.

Katika muktadha huu suala la usafiri wa viongozi wa nchi na serikali liliratibiwa Ofisi ya Masuala ya Kigeni, Jumuiya ya Madola na Maendeleo (Foreign, Commonwealth and Development Office/ FCDO) ya Uingereza.

Utaratibu huu hufanyika ili kurahisisha usalama wa viongozi mbalimbali duniani kwa wakati mmoja na hii ni kwa sababu itifaki na usalama wa viongozi ni mambo yanayoenda pamoja na kamwe hayawezi kutenganishwa.

Hii si mara ya kwanza kwa viongozi kupakiwa kwenye mabasi kwa sababu hata katika Mkutano wa Jumuiya ya Madola mwaka 2018 (CHOGM2018) uliofanyika London na Windsor viongozi kutoka nchi zaidi ya 54 walipakiwa kwenye mabasi kwenda na kurudi kwenye mikutano kwa siku zote za mikutano.

Hayo yamekuwa yakifanyika hata Tanzania pia labda kwa bahati mbaya wengi huwa hawafuatilii.

Hivyo si dhihaka kama wengi wanavyodhani bali ni sehemu ya utaratibu katika kurahisisha usalama wa viongozi.

Zaidi, kitendo hiki cha kuwapatia usafiri mmoja viongozi hutoa nafasi kwa viongozi kuyasoma mazingira ya nchi au eneo husika na wao kupata muda wa kuchanganyika na kubadilishana mawazo ambapo kitendo hicho huitwa poding.

Wenu:

Abbas Mwalimu
(Facebook|Instagram|Twitter|Clubhouse).

+255 719 258 484.

Uwanja wa Diplomasia
(Facebook|WhatsApp).
View attachment 2362139View attachment 2362140View attachment 2362141
Kwani viongozi wahusika wamelalamika? Shida watanzania ni wanafki sana utafikiri wanawajali viongozi wao wakati kila siku wanamtukana mama yetu humu mtandaoni. Hata hivyo uongozi ni utumishi ni kupata fursa ya kutafuta ubwana mkubwa, kuwa wa pekee. Bahati nzuri Mungu anawapaga uongozi wa juu watu wanyenyekevu km Rais wetu.
 
Wananchi wana hasira jamani sio kwa kule kufoka kuna mambo viongozi wetu huwa wanafanya hawajali ..wanafanya wanavojisikia na majibu wanayotoa pia huwa yanawauzi wananchi ndio matokeo yake hayo.
 
Mkuu, sasa ukiweka mawaziri wote ndani ya bus moja kisha likatokea la kutokea hauoni kama unaweza kukuta tunapoteza serikali nzima within fraction of a second?

Lakini hao marais waliolanda bus moja hata likitokea la kutokea kila nchi inakuwa imepoteza Rais mmoja mmoja tu. Kumbuka mawaziri wote ni marais watarajiwa.

NB: Siombei jambo lolote baya kwa viongozi wetu na hata wa nchi jirani. Mungu tunakuomba uepushie mbali wote warudi salama.
Nakuelewa mkuu, ila tatizo la v8 hapa Tz unalionaje, hatuwezi kua na njia mbadala wa kumpunguza gharama za uendeshaji wa serikali, kweli lipo Jambo umeliongea hapo nimekuelewa,

Je haiwezekani waziri na naibu wake kwenda kwenye kikao na gari MOJA nzuri ila ambayo sio v8,

Najua mawaziri lazima kutembelea Miradi mbali mbali kwenye Mikoa tofauti, na ikumbukwe KILA mkoa yapo magari ya serikali , vipi waziri akiwa na ziara mfano Kigoma, akapanda ndege mpaka kigoma, hawezi pewa usafiri katika mkoa husika na kukamilisha ziara yake , na kupanda ndege kurudi, au ni lazima ungurumisha li v8 from Dom to kigoma,
 
Ila kweli kwa zile nyuzi na comments za jana, sisi weusi tuna shida sana sana. Yaani Raisi wa Ujerumani kapanda basi na raia wake wala hawana shida. Waziri mkuu wa New Zealand, Raisi wa Italia, Raisi wa EU n.k... vile vile na huoni malalamiko yoyote. Ndio utajua wengi hatuna exposure, tuna uelewa mdogo, tunapenda ufahari. Hizi ni dalili za udumavu wa akili na sababu kubwa ni lishe duni kabla na baada ya kuzaliwa na wakati wa makuzi yetu.
Uko sahihi kabisa. Ukuaji duni ukihusisha kwashiakor akili nzuri utaipata. Alikuwa anatutukana Prof Ngware chuo kikuu cha Dar Es Salaam kuwa tulianza kujifunza kula mayai kwa pesa za Boom wakati watoto wake walikuwa wanakula kila siku tusingekuwa na akili sawa na watoto wake. Kuna ukweli.
 
Hii ndo ilikua hoja ,na ndo maana mjadala umekua mkubwa, watu wasijifiche kwenye kichaka Cha kuita watu sijui wajinga, watu wanaelewa why wanahoji na why imekua story, hasa KWa viongonzi watokao afrika
Na kwanini mhoji nyie watu weusi na akili yenu nyeusi wakati wazungu na akili zao hawahoji. Hamuoni hata aibu? Mna akili ndogo km K ya mjusi
 
Machawa ya mama yanajitahidi kuficha aibu
 
Ila kweli kwa zile nyuzi na comments za jana, sisi weusi tuna shida sana sana. Yaani Raisi wa Ujerumani kapanda basi na raia wake wala hawana shida. Waziri mkuu wa New Zealand, Raisi wa Italia, Raisi wa EU n.k... vile vile na huoni malalamiko yoyote. Ndio utajua wengi hatuna exposure, tuna uelewa mdogo, tunapenda ufahari. Hizi ni dalili za udumavu wa akili na sababu kubwa ni lishe duni kabla na baada ya kuzaliwa na wakati wa makuzi yetu.
Kama hukuwaelewa waleta nyuzi useme wakufafanulie walimaanisha nini. Mimi si mmojawapo lakini nyuzi zào zilikuwa na maana kubwa Sana. Ni mwwndelezo wa maoni yao kuhusu matumizi mabaya ya fedha za Umma kwenye misafara. Mwezi uliopita baadhi ya Watanzania walilalamikia wingi wa magari ya misafara kwenye ziara za viongozi wa kitaifa. Msafara wa Rais Samia kwenda Kyela ulikuwa na magari ya kifahari zaidi ya 70 yenye high fuel consumption level, kilichoongeza msafara ni idadi kubwa ya Mawaziri kwenda kwenye ziara eti kutoa ufafanuzi wa masuala yanayohusu wizara zào wakati na wao wametoka huko kwenye ziara wakiwa Peke yao hata mwezi haujaisha. Wakifika eneo la Mkutano Waziri anapewa dakika 2 kuongea Yale Yale anayokuja kuongea Rais. Kichekesho zaidi kilikuja kwenye msafara wa Waziri wa fedha eti anakwenda kuwasilisha bajeti ya serikali akiwa na msafara mkubwa wa pikipiki 3 na magari utadhani ni msafara wa Makamu wa Rais.
Leo Rais amefika Ulaya amepanda basi la pamoja na wenzake lakini ameshindwa kukemea matumizi Makubwa ya Mawaziri na Wakuu wa mikoa na wilaya wanaofanya ziara Kwa misafara mikubwa isiyo na tija. Tumesikia kelele za Watanzania kuhusu ununuzi wa magari ya kifahari wa zaidi ya mil.500 Kwa Gari, lakini Waziri anainuka na kujibu "Waziri hawezi kupanda pick up". Yaani ukitoa pick up magari mengine yaliyobaki yanauzwa mil.500+?
Kwa hili la Marais kipandishwa basi si ajabu Kwa Marais wazungu, lakini Kwa Marais Waafrika liwe funzo Kwa jinsi wanaoishi maisha ya kifahari huku Wananchi wao wakiwa Hohe hahe.
 
Yani mkuu we ACHA tu, utakuta mawaziri wote wanajua kwamba tarehe flan ni kikao Cha Baraza la mawaziri, na kitafanyika ikulu Dodoma, na wote wanaishi kwenye nyumba za serikali Dodoma, ila utashanga v8 60 plus zote zipo ikulu, inashindikana nini kusanywa na basi hapo Dodoma nakwenda kwenye kikao? au waziri hawezi chukua bajaji na kuwai hapo chamwino kwenye kikao, akifanya HIVYO anapungukiwa nini
Akili za kiafrika bado sana
 
Kama hukuwaelewa waleta nyuzi useme wakufafanulie walimaanisha nini. Mimi si mmojawapo lakini nyuzi zào zilikuwa na maana kubwa Sana. Ni mwwndelezo wa maoni yao kuhusu matumizi mabaya ya fedha za Umma kwenye misafara. Mwezi uliopita baadhi ya Watanzania walilalamikia wingi wa magari ya misafara kwenye ziara za viongozi wa kitaifa. Msafara wa Rais Samia kwenda Kyela ulikuwa na magari ya kifahari zaidi ya 70 yenye high fuel consumption level, kilichoongeza msafara ni idadi kubwa ya Mawaziri kwenda kwenye ziara eti kutoa ufafanuzi wa masuala yanayohusu wizara zào wakati na wao wametoka huko kwenye ziara wakiwa Peke yao hata mwezi haujaisha. Wakifika eneo la Mkutano Waziri anapewa dakika 2 kuongea Yale Yale anayokuja kuongea Rais. Kichekesho zaidi kilikuja kwenye msafara wa Waziri wa fedha eti anakwenda kuwasilisha bajeti ya serikali akiwa na msafara mkubwa wa pikipiki 3 na magari utadhani ni msafara wa Makamu wa Rais.
Leo Rais amefika Ulaya amepanda basi la pamoja na wenzake lakini ameshindwa kukemea matumizi Makubwa ya Mawaziri na Wakuu wa mikoa na wilaya wanaofanya ziara Kwa misafara mikubwa isiyo na tija. Tumesikia kelele za Watanzania kuhusu ununuzi wa magari ya kifahari wa zaidi ya mil.500 Kwa Gari, lakini Waziri anainuka na kujibu "Waziri hawezi kupanda pick up". Yaani ukitoa pick up magari mengine yaliyobaki yanauzwa mil.500+?
Kwa hili la Marais kipandishwa basi si ajabu Kwa Marais wazungu, lakini Kwa Marais Waafrika liwe funzo Kwa jinsi wanaoishi maisha ya kifahari huku Wananchi wao wakiwa Hohe hahe.
Chawa hawawezi kuelewa hii mantiki miaka mia moja,ila hicho ulichokielezea ndio uhalisia wa hoja
 
Hata Mimi siwapendi mambo yao, lakini huwezi kunitowa akili ya kutofautisha msiba na official state visit.

Hao wote Leo wanakwenda Marekani UN, fuatilia mapokezi yao utaona tofauti ya protocol ilivyo.

Tusiache mioyo yetu ikajaa chuki ya kupitiliza.
Si kama ile chuki uliyonayo kwa Magufuli?
 
Kama hukuwaelewa waleta nyuzi useme wakufafanulie walimaanisha nini. Mimi si mmojawapo lakini nyuzi zào zilikuwa na maana kubwa Sana. Ni mwwndelezo wa maoni yao kuhusu matumizi mabaya ya fedha za Umma kwenye misafara. Mwezi uliopita baadhi ya Watanzania walilalamikia wingi wa magari ya misafara kwenye ziara za viongozi wa kitaifa. Msafara wa Rais Samia kwenda Kyela ulikuwa na magari ya kifahari zaidi ya 70 yenye high fuel consumption level, kilichoongeza msafara ni idadi kubwa ya Mawaziri kwenda kwenye ziara eti kutoa ufafanuzi wa masuala yanayohusu wizara zào wakati na wao wametoka huko kwenye ziara wakiwa Peke yao hata mwezi haujaisha. Wakifika eneo la Mkutano Waziri anapewa dakika 2 kuongea Yale Yale anayokuja kuongea Rais. Kichekesho zaidi kilikuja kwenye msafara wa Waziri wa fedha eti anakwenda kuwasilisha bajeti ya serikali akiwa na msafara mkubwa wa pikipiki 3 na magari utadhani ni msafara wa Makamu wa Rais.
Leo Rais amefika Ulaya amepanda basi la pamoja na wenzake lakini ameshindwa kukemea matumizi Makubwa ya Mawaziri na Wakuu wa mikoa na wilaya wanaofanya ziara Kwa misafara mikubwa isiyo na tija. Tumesikia kelele za Watanzania kuhusu ununuzi wa magari ya kifahari wa zaidi ya mil.500 Kwa Gari, lakini Waziri anainuka na kujibu "Waziri hawezi kupanda pick up". Yaani ukitoa pick up magari mengine yaliyobaki yanauzwa mil.500+?
Kwa hili la Marais kipandishwa basi si ajabu Kwa Marais wazungu, lakini Kwa Marais Waafrika liwe funzo Kwa jinsi wanaoishi maisha ya kifahari huku Wananchi wao wakiwa Hohe hahe.
Nilielewa sana mkuu, wapo waliokuwa na mtazamo kama ulivyosema. Ila kuna nyuzi nyingi tu zilikuwa zinalaumu sana na hata kutoa lugha kali kwa waliojaribu kufafanua tena kwa vielelezo. Ninawaongelea hawa ambao walikuwa wakali kwelikweli kwa wote walioonekana kutetea utaratibu wa viongozi wetu kutumia mabasi, tna wakidai tumedhalilishwa sana, nilipata muda wa kupitia karibu nyuzi zote kwenye hili sakata.
Asante kwa ufafanuzi
 
Uko sahihi kabisa. Ukuaji duni ukihusisha kwashiakor akili nzuri utaipata. Alikuwa anatutukana Prof Ngware chuo kikuu cha Dar Es Salaam kuwa tulianza kujifunza kula mayai kwa pesa za Boom wakati watoto wake walikuwa wanakula kila siku tusingekuwa na akili sawa na watoto wake. Kuna ukweli.

Mkuu ukifuatilia survey iliyofanywa na kituo cha chakula na lishe Tanzania (Tanzania Food and Nutrition Centre-TFNC), Takribani 32% ya watoto chini ya miaka mitano wana utapiamlo mkali (Severe/acute undernourished) na mikoa inayoongoza kwa kilimo ndio ina tatizo hili sana.

Nutrition and Food Security Situation in Tanzania
Nutrition and Food Security Situation According to the 2018 SMART survey, 32 percent of children under five years are stunted, which is a significant decrease from 35 percent in 2014. The most affected regions with a prevalence of stunting exceeding 40 percent were Ruvuma (41 percent), Iringa (47 percent), Rukwa (48 percent), Kigoma (42 percent), Njombe (54 percent), and Songwe (43 percent). In Zanzibar, stunting rates ranged from 20–24 percent in Stone Town and Unguja North, respectively. Between 2014 and 2018, a significant decrease of the prevalence of stunting was observed in Dodoma, Morogoro, Pwani, Lindi, Tabora, Kagera, Mwanza, and Katavi (MoHCDGEC, MoH, TFNC, NBS, OCGS, and UNICEF 2018).

According to the 2015–2016 DHS-MIS, 5 percent of children under five are wasted. Wasting is more common in Zanzibar than in Tanzania Mainland (7 percent versus 4 percent) and is very high in Kusini Pemba (9 percent), Kaskazini Pemba (9 percent), and Kusini Unguja (8 percent). In Tanzania, 14 percent of children under five are underweight (too thin for age). At the other extreme, 4 percent are overweight. Rates of stunting, wasting, and underweight generally decrease as maternal education increases. All three nutritional status indicators are highest among children in the lowest wealth quintile and lowest among children in the highest wealth quintile (MoHCDGEC, MoH Zanzibar, NBS, OCGS, and ICF 2016).

Fifty-nine percent of infants under six months are exclusively breastfed in Tanzania. Exclusive breastfeeding declines rapidly with age; only 27 percent of infants aged four to five months are exclusively breastfed compared with 84 percent of infants aged zero to one month and 59 percent of infants aged two to three months. Complementary feeding practices are inadequate, with only 10 percent of breastfed children 6–23 months receiving a minimum acceptable diet, which has a major impact on growth and development (MoHCDGEC, MoH Zanzibar, NBS, OCGS, and ICF 2016). A recent presentation shows that 59 percent of the Tanzanian population cannot afford a nutritionally adequate diet (TFNC and WFP 2017).

Early childbearing also contributes to malnutrition in Tanzania. By age 19, 57 percent of adolescent girls had begun childbearing in 2015–2016, which is an increase from 44 percent in 2010 (MoHCDGEC, MoH, NBS, OCGS, and ICF 2016; NBS and ICF Macro 2011). Tanzania is also experiencing the double burden of malnutrition, with 28 percent of women and 4 percent of children under five years suffering from overweight and obesity (MoHCDGEC, MoH Zanzibar, NBS, OCGS, and ICF 2016).

Source: https://www.usaid.gov/sites/default/files/documents/Copy_of_tagged_Tanzania-Nutrition-Profile.pdf
 
Siyo kwamba watu hawana exposure au udumavu wa akili.Tatizo hapa ni hawa viongozi wa afrika na matumizi mabaya ya fedha za umma.mfano Rais kuwa na msafara wa magari zaidi ya 40 ya nini sasa tena v8.Ukiangalia ulaya wao hawana hiyo mbwembwe,misafara yao haizidi magari kumi.yaani Nchi tajiri zinatumia rasilimali vizuri kuliko viongozi wa afrika ndiyo maana nchi ulizozitaja kama ufaransa nk wananchi wake hawajawaponda viongozi wao tofauti na na wa huku afrika
Sawa mkuu ila 32% ya watoto chini ya miaka mitano wana udumavu mkali kabisa (Severe/acute undernourished)
 
Wanakuwa "salama" zaidi wakiwa nje kuliko nyumbani,Tanzania!!!

Ushawahi kushuhudia msafara ,wakiwa nchini? Ama unaishi "ughaibuni"?
Nimekuwa nikishuhudia misafara kila siku. Ungepata wasaa wa kupitia nyuzi zote kuhusu hiyo mada ungeona kuna tatizo mahali. Yaani kuna watu mpaka wanatukana. Nilimsikia Waziri mkuu wa New Zealand akisifia na kusema hata mawaziri wake anawa encourage kutumia usafiri nafuu.
Kiufupi kuna watu wametoa povu kwelikweli na kuna wengine pia walisupport kilichotokea.
 
Shida ni kwamba kwanini wakirudi nyumbani msafara unakuwa na magari 80+,kwanini yasipatikane mabasi mawili na magari manne madogo kwenye Convoy??
Hilo ni tatizo kubwa sana na hata comments nyingi tu zilikuwa zinaliongelea hilo. Pengine ni genetical make up yetu, kiufupi sijui haswa sababu halisi zaidi ya ulimbukeni, ubinafsi, tamaa, kutokujali unaowaongoza n.k....
Huku kwetu mtu akiwa kiongozi anaona wote anaowaongoza ni swekeni tu na hatuna mfumo wa kuwawajibisha au wao kuwajibika. Limekuwa ni kama gang of wolves (genge la mbwa mwitu tu)
 
Hatutaki kuelewa sisi tunachojua wamewekwa kama abiria😂
 
Back
Top Bottom