MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 707
Rais asiwe na mamlaka ya kuteua Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Wilaya, bali viongozi hao (ambao hawatatokana na Wabunge) wagombee nafasi hizo kwa njia ya demokrasia. Wananchi wawapime kwa uwezo wao. Zama za kuletewa mfamasia au mveterinari kuja kuongoza Wizara ya Ndani, n.k., au Mjumbe wa NEC kuja kuwa Mkuu wa Mkoa, ZIMEISHA!
Rais asiruhusiwe kugombea zaidi ya kipindi kimoja cha miaka tano! Kisingizio "sijamaliza kutekeleza ahadi zangu" ni hoja mfu. Pia, kama ilivyo Marekani, Baraza la Mawaziri liwe na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, lakini kumuondoa Rais madarakani kusiathiri uwepo wa Bunge au Baraza la Mawaziri. Uchaguzi wa Rais pekee ndio urudiwe.
Wananchi wawe na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani kwa wabunge wao, uchaguzi urudiwe apatikane mbunge mwenye uwezo. Wananchi wawe na uwezo wa kubadili vigezo vya mbunge wamtakaye jimboni mwao, kila ufikapo uchaguzi mkuu au mdogo, ili apatikane mbunge stahiki.
Rais asiruhusiwe kugombea zaidi ya kipindi kimoja cha miaka tano! Kisingizio "sijamaliza kutekeleza ahadi zangu" ni hoja mfu. Pia, kama ilivyo Marekani, Baraza la Mawaziri liwe na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, lakini kumuondoa Rais madarakani kusiathiri uwepo wa Bunge au Baraza la Mawaziri. Uchaguzi wa Rais pekee ndio urudiwe.
Wananchi wawe na uwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na imani kwa wabunge wao, uchaguzi urudiwe apatikane mbunge mwenye uwezo. Wananchi wawe na uwezo wa kubadili vigezo vya mbunge wamtakaye jimboni mwao, kila ufikapo uchaguzi mkuu au mdogo, ili apatikane mbunge stahiki.