MUHIMU: Tuma maoni yako ya Rasimu ya Katiba Mpya, Mabaraza ya CHADEMA

MUHIMU: Tuma maoni yako ya Rasimu ya Katiba Mpya, Mabaraza ya CHADEMA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo kinaanza rasmi kuendesha Mabaraza ya Katiba, ambapo wananchi wote watashirikishwa kujadili na kutoa maoni yao juu ya Rasimu ya Katiba Mpya, kwa njia mbalimbali kama ifuatavyo;






====================

[TABLE="width: 942"]
[TR]
[TD]S/N
[/TD]
[TD]IBARA
[/TD]
[TD]MAPENDEKEZO YA CHAMA (CHADEMA)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]1.[/TD]
[TD]2 Eneo la Jamhuri ya. Muungano[/TD]
[TD]Neno Tanzania Bara liondolewe na kuandika Tanganyika kila palipo na neno Tanzania Bara.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2.[/TD]
[TD]4(1) Lugha ya Taifa[/TD]
[TD]Lugha ya Taifa itakuwa Kiswahili na miswada/sheria zote zitaandikwa kwayo pamoja na lugha zingine[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]3.[/TD]
[TD]5 Tunu za Taifa[/TD]
[TD]Viongozwe vipengele hivi demokrasia ya vyama vingi, utawala wa sheria,uwazi na haki za binadamu.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]4.[/TD]
[TD]6(2) Daftari la wapiga kura[/TD]
[TD]Liwe mahali ambapo kila raia akifikisha miaka 18 ana andikishwa wakati wowote.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]5.[/TD]
[TD]17&85 watumishi wa umma.[/TD]
[TD]Mishahara ya watumishi wote wa umma pamoja Rais ijulikane.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]6.[/TD]
[TD]32 (2) haki ya kuandamana[/TD]
[TD]Kila mtu ana haki kwa amani na bila kubeba siraha kukusanyika/kuandamana kuzuia njia na kuwasilisha malalamiko.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]7.[/TD]
[TD]35(e) kugoma[/TD]
[TD]Kugoma au kusitisha nguvu kazi yake mahali pa kazi.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]8.[/TD]
[TD]47 Haki ya kumiliki rasilimali[/TD]
[TD]Iongezwe ibara mpya ya 48 haki ya kumiliki rasilimali za asili zote Ardhi, Madini, mafuta na gesi, maji na misitu na wanyama pori.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]9.[/TD]
[TD]60 (7)nyongeza[/TD]
[TD]Kiongozwe kifungu cha 7 Maadili na miiko ya uongozi na utumishi wa umma, Haki za binadamu na wajibu wa raia. Tume huru ya Taifa ya uchaguzi.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]10.[/TD]
[TD]Serikali tatu (3)[/TD]
[TD]Kuwepo serikali ya Muungano, serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]11.[/TD]
[TD]75(d) Uchaguzi wa rais.[/TD]
[TD]Umri wa mgombea urais uwe miaka kumi na nane[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]12.[/TD]
[TD]83(i) kinga dhidi ya mashtaka ya Rais.[/TD]
[TD]Wakati wowote Rais akiwa madarakani na baada ya kuacha kushika madaraka aweze kushtakiwa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]13.[/TD]
[TD]105 (2) (b) wabunge wa kuteuliwa[/TD]
[TD]Kipengele hiki kifutwe na badala yake iwe wabunge 20 watakaochaguliwa kutokana na uwiano wa kura zilizopigwa kwa vyama vya siasa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]14.[/TD]
[TD]117(i) (a) Mgombea Ubunge[/TD]
[TD]Umri wa mgombea ubunge uwe miaka 18 na si 25 kama inavyopendekezwa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]15.[/TD]
[TD]123(2) uwajibikaji wa mbunge.[/TD]
[TD]Hii ifutwe na kuongeza :mbunge aliyependekezwa na chama cha siasa atapoteza ubunge wake ikiwa atafukuzwa au kuvuliwa uanachama wa chama chake cha siasa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]16.[/TD]
[TD]123(3) mbunge kuhama/kujiunga na chama cha siasa.[/TD]
[TD]Kuongeza ibara ndogo :endapo mbunge kwa ridhaa yake atajiondoa au kujivua uanachama wa chama cha siasa au kujiunga na chama kama alikuwa mgombea huru basi atapoteza sifa ya kuwa mbunge.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]17.[/TD]
[TD]124 adhabu kwa mbunge[/TD]
[TD]Kuondoa kabisa ibara hiyo na badala yake iseme wananchi wa jimbo au kata watakuwa na haki ya kuwaondoa madarakani kwa sababu na kwa kufuata utaratibu na sheria.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]18.[/TD]
[TD]182 Tume Huru ya uchaguzi.[/TD]
[TD]Kuongeza wajumbe wa vyama vya Mawakili na vyama vya siasa.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]19.[/TD]
[TD]184 Tume Huru ya Uchaguzi[/TD]
[TD]Watumishi wote wa Tume Huru ya uchaguzi wasiwe watumishi wa serikali.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]20.[/TD]
[TD]234 Mkurugenzi wa usalama wa Taifa.[/TD]
[TD]Ateuliwe baada ya kuthibitishwa na Bunge[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]21.[/TD]
[TD]Nyongeza[/TD]
[TD]Kuanzishwa kwa mchakato wa katiba ya Tanganyika, kuundwa TUME ya Katiba ya Tanganyika.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Maoni yangu kwa baadhi ya Mapendekezo ya CDM;

32 (2) haki ya kuandamana

Kila mtu ana haki kwa amani na bila kubeba siraha kukusanyika/kuandamana kuzuia njia na kuwasilisha malalamiko.
Maoni.

Badala yake Ibara ya 9 ya Maoni yangu napendekeza kuongeza na itaisomeka;
9.-(1) Mtu au kikundi cha watu hakitachukua au kushikilia mamlaka ya nchi (Serikali, Bunge na Mahakama) isipokuwa kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Kitendo chochote kinachokiuka masharti ya Ibara ndogo ya (1) ni batili na ni kitendo cha uhaini isipokuwa Maandamano yoyote ya Amani ya Umma ya kudai haki au kuondoka madarakani kwa maamlaka ya Nchi hayatachukuliwa kuwa ni Uhaini.
(3) Wakati wote wote wa maandamano ya Amani ya Wananchi, Mamlaka ya Nchi haitachukua wala kutumia Nguvu ya dola kuyazima au kuvuruga maandamano isipokuwa inaweza kuyapinga Maandamano kwa kufungua shauri Mahakamani ya juu au kuitisha Kikao cha dharua cha Bunge ilikupata Uamuzi wa hatua itakayochukuliwa.
(4) Kwa vyovyote vile na wakati wote wote ule wa Maandamano ya Amani ya Wananchi itakuwa ni marufuku kwa washiriki au mshiriki kuwa na silaha ya aina yoyote.

35(e) kugoma

Kugoma au kusitisha nguvu kazi yake mahali pa kazi.


Maoni ; Hapana kwa mapendekezo haya; Ukiangalia 35(4) inatosha kulinda haki hiyo na hapa waheshimiwa wanatakiwa wawe na dhamira safi.



(4) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu haki za wafanyakazi na utaratibu utakaowezesha wafanyakazi kutumia haki zao.




60 (7)nyongeza

Kiongozwe kifungu cha 7 Maadili na miiko ya uongozi na utumishi wa umma, Haki za binadamu na wajibu wa raia. Tume huru ya Taifa ya uchaguzi.

Hapa nadhani kuna makosa ya kiuandishi maana Nyongeza inayorejewa tayari ina mambo saba; NYONGEZA [Imetajwa katika Ibara ya 60]
Mambo ya Muungano
________________
1. Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
3. Uraia na Uhamiaji;
4. Sarafu na Benki Kuu;
5. Mambo ya Nje;
6. Usajili wa Vyama vya Siasa; na
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
ambayo inaweka masharti mapya katika sheria nyingine.

8. Maadili na miiko ya uongozi na utumishi wa umma, Haki za binadamu na wajibu wa raia naTume huru ya Taifa ya uchaguzi.
Itakuwa jambo la Maana kama Taifa tukaweka pembeni Usiasa na harufu yoyote ya masilahi ubinafsi katika zoezi hili.
 
Mkuu Tumaini Makene

More Updates;

71.-(1) Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba hii, na sheria za nchi, Rais atakuwa na wajibu wa kufuata na kuzingatia ushauri atakaopewa na mamlaka za nchi, na endapo hakubaliani na ushauri aliopewa sharti atoe sababu katika Baraza la Mawaziri kuhusu

sababu ya kutokubaliana na ushauri aliopewa.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), Rais hatalazimika kuufuata ushauri aliopewa ambao unakwenda kinyume au kukiuka masharti ya Katiba au haukuzi wala kuhifadhi maslahi ya taifa na wananchi walio wengi.

Maoni;

71.-(1) Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba hii,na sheria za nchi, Rais atakuwa na wajibu wa kufuata na kuzingatia ushauri atakaopewa na mamlaka za nchi, na endapo hakubaliani na ushauri aliopewa sharti atoe sababu katika Baraza la Mawaziri kuhusu sababu ya kutokubaliana na ushauri aliopewa.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), Rais hatalazimika kuufuata ushauri aliopewa ambao unakwenda kinyume au kukiuka masharti ya Katiba au haukuzi wala kuhifadhi maslahi ya taifa na wananchi walio wengi.
(3)Hata hivyo Raisi atalazimika kufuata na kutekeleza amri ya Mahakama au Uamuzi utakaotokana na Maamuzi ya Bunge yaliyofikiwa kwa upigaji kura ya Siri kwa Mujibu wa Kanuni zilizopo za Bunge la Muungano kwa Wakati huo.


72.-(1) Endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi kumudu kazi zake kwa sababu ya maradhi ya mwili au akili, linaweza kuwasilisha kwa Jaji Mkuu azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe kwamba Rais, kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili, hawezi kumudu kazi zake.

(2) Baada ya kupokea azimio lililowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Jaji Mkuu atateua bodi ya utabibu ambayo itachunguza suala hilo na kumshauri Jaji Mkuu ipasavyo.

(3) Jaji Mkuu anaweza, baada ya kutafakari ushauri na ushahidi wa kitabibu, kuwasilisha kwa Spika hati ya kuthibitisha kwamba kutokana na maradhi ya mwili au akili, Rais ameshindwa kumudu kazi zake, na iwapo Jaji Mkuu hatabatilisha hati hiyo ndani ya siku saba kutokana na Rais kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa kwamba kiti cha Rais kiwazi, na masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (5) na (6) yatatumika.

(4) Bodi ya utabibu itakayoteuliwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (3) itajumuisha watu wasiopungua watatu watakaoteuliwa kutoka miongoni mwa madaktari bingwa wanaotambuliwa na sheria inayohusu madaktari ya Tanzania.
(5) Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi, kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au akili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na kushika madaraka ya Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika Ibara ya 76.
(6) Mara tu baada ya kuapishwa, au kwa vyovyote vile ndani ya kipindi kisichozidi siku kumi na nne tangu alipoapishwa, Rais:
(a) baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka;au
(b) baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi naUsalama wa Taifa, kwa Rais aliyetokana kwa utaratibu wa mgombea huru,atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zaidi ya asilimia hamsini ya Wabunge wote.


Maoni;


72.-(1) Endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi kumudu kazi zake kwa sababu ya maradhi ya mwili au akili, linaweza kuwasilisha kwa Jaji Mkuu azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe kwamba Rais, kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili, hawezi kumudu kazi zake.
(2) Baada ya kupokea azimio lililowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Jaji Mkuu atateua bodi ya utabibu ambayo itachunguza suala hilo na kumshauri Jaji Mkuu ipasavyo.

(3) Jaji Mkuu anaweza, baada ya kutafakari ushauri na ushahidi wa kitabibu, kuwasilisha kwa Spika hati ya kuthibitisha kwamba kutokana na maradhi ya mwili au akili, Rais ameshindwa kumudu kazi zake, na iwapo Jaji Mkuu hatabatilisha hati hiyo ndani ya siku saba kutokana na Rais kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa kwamba kiti cha Rais kiwazi, na masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (5) na (6) yatatumika.

(4) Bodi ya utabibu itakayoteuliwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (3) itajumuisha watu wasiopungua watatu watakaoteuliwa kutoka miongoni mwa madaktari bingwa wanaotambuliwa na sheria inayohusu madaktari ya Tanzania.

(5) Endapo kiti cha Raisi kitakuwa wazi kutokana na kufariki dunia , kujiuzulu, kupoteza sifa za kuendelea kuwa Raisi, kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au akili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Raisi, na wakati huo Raisi amekwisha kaa madarakani kwa zaidi ya miaka Mitatu basi Makamu wa Rais ataapishwa na kushika madaraka ya Rais kwa muda uliobaki katika kipindi hiki cha miaka mitano kama atatimiza sifa zifuatazo;

(a) (a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii na sheria za nchi;

(b) ni mwenye akili timamu;

(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano;

(d) wakati wa kuteuliwa ana umri usiopungua miaka Thelathini na Tano;

(e) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;

(f) Imani au mtazamo wake si wa mrengo wa kuligawa Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;

(g) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;

(h) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;

(i) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai linalohusu kukosa uaminifu; na

(j) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya uteuzi wake hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

(6)Isipokuwa kama kiti cha Raisi kitakuwa wazi kwa matatizo au taratibu yoyote chini ya Katiba hii na kwamba Raisi huyu hajatimiza miaka Mitatu kuwa madarakani tangu aapishwe kushika madaraka ya Uraisi basi Spika wa Bunge atakaimu nafasi ya Uraisi kwa Siku Tisini na Tume ya uchaguzi itaitisha Uchanguzi Mkuu wa Uraisi na Ubunge kabla siku Sitini hazijaisha toka Spika wa Bunge akaimu nafasi ya Uraisi .

(7) Tume ya uchaguzi itatakiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi na washindi wa nafasi za Ubunge na Raisi ndani ya wiki moja toka siku ya uchaguzi na wateule kuapishwa na kushika madaraka husika kabla ya Siku Tisini haizijaisha toka siku Spika wa Bunge alipoanza kukaimu madaraka ya Uraisi kwa mujibu wa ibara ya 72;(6) ya Katiba hii.

(8) Kwa Raisi aliyetokana na ibara ya 77;(2) ya Katiba hii na kwamba nafasi ya Raisi imekuwa wazi kwa mujibu wa Ibara ya 72;(5) ya Katiba hii au kama Makamu wa Raisi amekosa sifa basi, Baraza la Mawaziri chini ya Uwenyeketi wa Makamu wa Raisi itashauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa;

(a) kumteua Mtu mwenye sifa atakayeshika Madaraka ya Uraisi miongoni mwa Mawaziri

(b) Baada ya uteuzi huu kupeleka jina la aliyeteuliwa kwa Spika wa Bunge kwa ajili ya udhibitisho wa Bunge na idadi ya kura za Wabunge lazima iwe zaidi ya asilimia hamsini ya Wabunge wote.


74.-(1) Rais atachaguliwa na wananchi kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na kwa mujibu wa sheria za nchi.

(2) Nafasi ya madaraka ya Rais itakuwa wazi na uchaguzi wa Rais utafanyika baada ya Rais kumaliza muda wake wa kuwa madarakani kwa mujibu wa Katiba hii.
(3) Endapo kutatokea jambo lolote kati ya mambo yafuatayo, hakutakuwa na Uchaguzi wa Rais na badala yake nafasi hiyo itajazwa na Makamu wa Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, yaani:
(a) Rais kujiuzulu;
(b) Rais kupoteza sifa za kuchaguliwa katika nafasi ya madaraka ya Rais;
(c) Rais kushtakiwa Bungeni na kuondolewa katika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii;
(d) ikithibitika kwamba Rais hawezi kumudu nafasi ya madaraka ya Rais; au
(e) Rais kufariki dunia.

Maoni


74.-(1) Rais atachaguliwa na wananchi kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na kwa mujibu wa sheria za nchi.
(2) Nafasi ya madaraka ya Rais itakuwa wazi na uchaguzi wa Rais utafanyika baada ya Rais kumaliza muda wake wa kuwa madarakani kwa mujibu wa Katiba hii.
(3) Endapo raisi amekaa madarakani zaidi ya miaka Mitatu na ikatokea jambo lolote kati ya mambo yafuatayo, hakutakuwa na Uchaguzi wa Rais na badala yake nafasi hiyo itajazwa na Makamu wa Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, yaani:
(a) Rais kujiuzulu au kupoteza sifa za kuchaguliwa.
(b) Raisi kushtakiwa Bungeni na kuondolewa katika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii;
(d) ikithibitika kwamba Rais hawezi kumudu nafasi ya madaraka au;
(e) Rais kufariki dunia.


75. Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ikiwa:

(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii na sheria za nchi;
(b) ni mwenye akili timamu;
(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano;
(d) wakati wa kugombea, ana umri usiopungua miaka arobaini;
(e) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii;
(f) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(g) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea huru;
(h) sera zake au sera za chama chake si za mrengo wa kuligawa Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;
(i) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;
(j) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;
(k) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai linalohusu kukosa uaminifu; na
(l) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.


Maoni;
75. Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ikiwa:
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii na sheria za nchi;
(b) ni mwenye akili timamu;
(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano;
(d) wakati wa kugombea ana umri usiopungua miaka Thelathini na Tano;
(e) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii;
(f) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(g) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea huru;
(h) sera zake au sera za chama chake si za mrengo wa kuligawa Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;
(i) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;
(j) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;
(k) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinailinalohusu kukosa uaminifu; na
(l) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.


76.-(1) Mtu ambaye ni Rais anaweza kuchaguliwa tena kushika kiti hicho kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
(2) Mtu hatakuwa na sifa ya kugombea na kuchaguliwa zaidi ya vipindi viwili katika nafasi ya madaraka ya Rais.
(3) Mtu aliyewahi kuwa Rais wa Tanzania Bara au Zanzibar hatapoteza sifa za kugombea na kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa sababu aliwahi kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa Tanzania Bara au Rais wa Zanzibar.
(4) Endapo mtu aliyekuwa anashika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais, atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 72 kwa kipindi kisichozidi miezi thelathini na sita, mtu huyo anayo haki ya kugombea nafasi ya madaraka ya Rais katika uchaguzi
wa Rais utakaofuata.
(5) Mtu aliyechaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Ibara ndogo ya (4), atahesabiwa kuwa ameshika nafasi ya madaraka ya Rais katika vipindi viwili na hataruhusiwa kugombea nafasi ya madaraka ya Rais katika kipindi kingine.

Maoni

76.-(1) Mtu ambaye ni Rais anaweza kuchaguliwa tena kushika kiti hicho kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

(2) Mtu hatakuwa na sifa ya kugombea na kuchaguliwa zaidi ya vipindi viwili katika nafasi ya madaraka ya Rais.

(3) Mtu aliyewahi kuwa Raisi au Makamu wa Raisi wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 hana sifa za kugombea na kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(4)Mtu aliyewahi kuwa Raisi wa Tanganyika au Zanzibar hatahesabiwa kuwa hana sifa kwa sababu tu aliwahi kuwa Raisi wa Tanganyika au Zanzibar.
(5) Endapo mtu aliyekuwa anashika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais, atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 72 kwa kipindi kisichozidi miezi Ishirini na Nne mtu huyo anayo haki ya kugombea nafasi ya madaraka ya Raisi katika uchaguzi wa Raisi utakaofuata.
(6) Mtu aliyechaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Ibara ndogo ya (5), atahesabiwa kuwa ameshika nafasi ya madaraka ya Raisi katika vipindi viwili na hataruhusiwa kugombea nafasi ya madaraka ya Rais katika kipindi kingine.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Mwendelezo;
78.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), endapo mtu yeyote aliyeshiriki kama mgombea nafasi ya madaraka ya Rais katika Uchaguzi wa Rais hakuridhika na matokeo ya uchaguzi huo, anaweza kuwasilisha malalamiko katika Mahakama ya Juu kupinga matokeo wa Rais yaliyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi.
(2) Malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais yatawasilishwa Mahakama ya Juu ndani ya muda wa siku saba baada ya siku ya kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais.
(3) Mahakama ya Juu itasikiliza na kutoa uamuzi wa shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais katika kipindi cha siku kumi na nne tangu kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (2) na uamuzi huo utakuwa wa mwisho.
(4) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (3), Mahakama ya Juu inaweza kutoa uamuzi bila kutoa sababu za uamuzi na sababu hizo zikatolewa ndani ya kipindi kisichozidi siku thelathini tangu siku ya kutoa uamuzi.
(5) Iwapo Mahakama ya Juu itaamua kuwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais si halali, Uchaguzi wa Rais utarudiwa ndani ya siku sitini baada ya uamuzi kutolewa.

Maoni;

78.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), endapo mtu yeyote aliyeshiriki kama mgombea nafasi ya madaraka ya Raisi katika Uchaguzi wa Rais hakuridhika na matokeo ya uchaguzi huo,
anaweza kuwasilisha malalamiko katika Mahakama ya Juu kupinga
matokeo wa Rais yaliyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi.
(2) Malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais yatawasilishwa Mahakama ya Juu ndani ya muda wa siku saba baada ya siku ya kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais.
(3) Mahakama ya Juu itasikiliza na kutoa uamuzi wa shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais katika kipindi cha siku kumi na nne tangu kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (2) na uamuzi huo utakuwa wa mwisho.
(4) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (3), Mahakama ya Juu inaweza kutoa uamuzi bila kutoa sababu za uamuzi na sababu hizo zitatolewa ndani ya kipindi kisichozidi siku thelathini tangu siku ya kutoa uamuzi.
(5) Iwapo Mahakama ya Juu itaamua kuwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais si halali, Uchaguzi wa Rais utarudiwa ndani ya siku sitini baada ya uamuzi kutolewa.
(6) Kwa ajili ya usimamizi bora wa Katiba hii kama itatokea pingamizi Mahakamani dhidi ya matokeo ya Uchaguzi wa Uraisi utakaotokana na masharti ya Ibara ya 72(7) ya Katiba hii basi; Spika wa Bunge ataendelea kukaimu nafasi ya Uraisi kwa mujibu wa Katiba hii hadi hapo Mahakama itakapotoa Uamuzi na kwa vyoyote vile hadi Raisi halali atakapoapishwa kwa mujibu wa Katiba hii.



79.
-(1) Rais Mteule ataapishwa na Jaji Mkuu na atashika nafasi ya madaraka ya Rais mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote, hatashika madaraka kabla ya kupita siku thelathini kutoka siku matokeo ya Uchaguzi

wa Rais yalipotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi au siku ya kuthibitishwa na Mahakama ya Juu.
(2) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, Rais Mteule atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa muda wa miaka mitano tangu siku alipochaguliwa kuwa Rais.
(3) Rais atashika nafasi ya madaraka ya Rais hadi-
(a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika nafasi ya madaraka ya Rais;
(b) siku ambapo atafariki dunia;
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

Maoni;

79.-(1) Rais Mteule ataapishwa na Jaji Mkuu kiapo cha uaminifu, kuilinda, kuisimamia na kutekeza ibara za Katiba hii kwa manufaa ya Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .
(2)Raisi Mteule atashika nafasi ya madaraka ya Rais mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote, hatashika madaraka kabla ya kupita siku thelathini kutoka siku matokeo ya Uchaguzi wa Rais yalipotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi au siku ya kuthibitishwa na Mahakama ya Juu.
(3) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, Raisi atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa muda wa miaka mitano tangu siku alipoapishwa /kuapa kuwa Rais.
(4) Rais atashika nafasi ya madaraka ya Rais hadi-
(a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika nafasi ya madaraka ya Rais;
(b) siku ambapo atafariki dunia;
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.


81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, au sheria iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo, Rais anaweza, baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa, kutangaza hali ya hatari au hali ya kuzingirwa kwa eneo fulani la Jamhuri ya Muungano au katika sehemu yake yoyote.
(2) Rais anaweza tu kutangaza kuwa kuna hali ya hatari iwapo-
(a) Jamhuri ya Muungano iko katika vita;
(b) kuna hatari hasa kwamba Jamhuri ya Muungano inakaribia kuvamiwa na kuingia katika hali ya vita;
(c) kuna hali halisi ya kuvurugika kwa amani katika jamii au kutoweka kwa usalama wa jamii katika Jamhuri ya Muungano au sehemu yake yoyote kiasi kwamba ni lazima kuchukua hatua
za pekee ili kurejesha amani na usalama;
(d) kuna hatari dhahiri na kubwa, kiasi kwamba amani katika jamii itavurugika na usalama wa raia kutoweka katika Jamhuri ya Muungano au sehemu yake yoyote ambayo haiwezi kuepukika
isipokuwa kwa kutumia mamlaka ya pekee;
(e) karibu kutatokea tukio la hatari au tukio la balaa au la baa ya kimazingira ambalo linatishia jamii au sehemu ya jamii katika Jamhuri ya Muungano; au
(f) kuna aina nyingineyo ya hatari ambayo kwa dhahiri ni tishio kwa usalama wa nchi.
(3) Endapo inatangazwa kwamba kuna hali ya hatari katika Jamhuri ya Muungano au eneo lolote la Jamhuri ya Muungano, Rais atawasilisha nakala ya tangazo hilo kwa Spika wa Bunge ambaye, ndani ya siku zisizozidi kumi na nne tangu kutolewa kwa tangazo hilo, ataitisha mkutano wa Bunge ili kulijulisha Bunge juu ya taarifa ya hali ya hatari iliyotangazwa na Rais.
(4) Bunge linaweza kutunga sheria itakayoweka masharti kuhusu nyakati na taratibu ambazo zitawawezesha baadhi ya watu wenye kusimamia utekelezaji wa mamlaka ya Serikali katika sehemu mahsusi za Jamhuri ya Muungano kumuomba Rais kutumia madaraka aliyopewa na Ibara hii kuhusiana na yoyote kati ya sehemu hizo endapo katika sehemu hizo, kunatokea lolote kati ya hali zilizotajwa katika aya ya (c), (d) na (e) za Ibara ndogo ya (2) na hali hiyo haivuki mipaka ya sehemu hizo, na pia, kwa ajili ya kufafanua utekelezaji wa mamlaka ya Serikali wakati wa hali ya hatari.
(5) Tangazo la hali ya hatari lililotolewa na Rais kwa mujibu wa Ibara hii litakoma kutumika iwapo litafutwa na Rais.
(6) Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka juu ya ufafanuzi au utekelezaji wa masharti ya Ibara hii, masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge na ya sheria nyingine yoyote inayohusu utangazaji wa hali ya hatari kama ilivyotajwa katika Ibara hii, yatatumika tu katika sehemu ya Jamhuri ya Muungano ambapo hali hiyo ya hatari imetangazwa.


Maoni;
81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, au sheria iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo, Rais anaweza, baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa, kutangaza hali ya hatari au hali ya kuzingirwa kwa eneo fulani la Jamhuri ya Muungano au katika sehemu yake yoyote.

(2) Rais anaweza tu kutangaza kuwa kuna hali ya hatari iwapo-
(a) Jamhuri ya Muungano iko katika vita;
(b) kuna hatari hasa kwamba Jamhuri ya Muungano inakaribia kuvamiwa na kuingia katika hali ya vita;
(c) kuna hali halisi ya kuvurugika kwa amani katika jamii au kutoweka kwa usalama wa jamii katika Jamhuri ya Muungano au sehemu yake yoyote kiasi kwamba ni lazima kuchukua hatua
za pekee ili kurejesha amani na usalama;
(d) kuna hatari dhahiri na kubwa, kiasi kwamba amani katika jamii itavurugika na usalama wa raia kutoweka katika Jamhuri ya Muungano au sehemu yake yoyote ambayo haiwezi kuepukika
isipokuwa kwa kutumia mamlaka ya pekee;
(e) karibu kutatokea tukio la hatari au tukio la balaa au la baa ya kimazingira ambalo linatishia jamii au sehemu ya jamii katika Jamhuri ya Muungano; au
(f) kuna aina nyingineyo ya hatari ambayo kwa dhahiri ni tishio kwa usalama wa nchi.

(3) Endapo inatangazwa kwamba kuna hali ya hatari katika Jamhuri ya Muungano au eneo lolote la Jamhuri ya Muungano, Rais atawasilisha nakala ya tangazo hilo kwa Spika wa Bunge ambaye, ndani ya siku zisizozidi kumi na nne tangu kutolewa kwa tangazo hilo, ataitisha mkutano
wa Bunge ili kulijulisha Bunge juu ya taarifa ya hali ya hatari iliyotangazwa na Rais.

(4) Bunge linaweza kutunga sheria itakayoweka masharti kuhusu nyakati na taratibu ambazo zitawawezesha baadhi ya watu wenye kusimamia utekelezaji wa mamlaka ya Serikali katika sehemu mahsusi za Jamhuri ya Muungano kumuomba Rais kutumia madaraka aliyopewa na
Ibara hii kuhusiana na yoyote kati ya sehemu hizo endapo katika sehemu hizo, kunatokea lolote kati ya hali zilizotajwa katika aya ya (c), (d) na (e) za Ibara ndogo ya (2) na hali hiyo haivuki mipaka ya sehemu hizo, na pia,kwa ajili ya kufafanua utekelezaji wa mamlaka ya Serikali wakati wa hali ya hatari.

(5) Tangazo la hali ya hatari lililotolewa na Rais kwa mujibu wa Ibara hii litakoma kutumika iwapo litafutwa na Rais.

(6) Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka juu ya ufafanuzi au utekelezaji wa masharti ya Ibara hii, masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge na ya sheria nyingine yoyote inayohusu utangazaji wa hali ya hatari kama ilivyotajwa katika Ibara hii, yatatumika tu katika sehemu ya Jamhuri

ya Muungano ambapo hali hiyo ya hatari imetangazwa.

(7)Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka Maandamano ya Wananchi yaliyorejewa na yaliyotimiza masharti yaliyomo katika ibara ya (9) ya Katiba hii hayatahesabiwa/kuchuliwa kuwa ni kitendo cha hali ya hatari na Mamlaka yoyote au na Raisi.



82.-(1) Rais kwa mamlaka ya Mkuu wa Nchi, anayo mamlaka ya:

(a) kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia kwa kosa lolote mbele ya Mahakama dhidi ya Jamhuri ya Muunganokwa masharti maalum kama yatakavyoainishwa katika sheria iliyotungwa na Bunge; au
(b) kubatilisha adhabu ya kifo kuwa adhabu ya kifungo cha maisha.
(2) Masharti ya Ibara hii yatatumika kwa mtu aliyehukumiwana kuadhibiwa akiwa Zanzibar na kwa adhabu zilizotolewa Zanzibar kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge inayotumika Zanzibar, hali kadhalika, masharti hayo yatatumika kwa mtu aliyehukumiwa na kuadhibiwa Tanzania Bara kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge inayotumika Tanzania Bara.
(3) Kwa madhumuni ya Ibara hii, kutakuwa na Kamati ya Taifa ya Ushauri ambayo itakuwa na wajibu wa kumshauri Rais kuhusu kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mahakamani na anatumikia adhabu.
(4) Utaratibu wa namna ya utekelezaji wa madaraka kwa mujibu wa Ibara hii, muundo, majukumu na utendaji kazi wa Kamati ya Taifa ya Ushauri vitaainishwa na sheria itakayotungwa na Bunge.


Maoni;
82.-(1) Rais kwa mamlaka ya Mkuu wa Nchi, anayo mamlaka ya:
(a) kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia kwa kosa lolote mbele ya Mahakama dhidi ya Jamhuri ya Muungano kwa masharti maalum kama yatakavyoainishwa katika sheria iliyotungwa na Bunge; au
(b) kubatilisha adhabu ya kifo kuwa adhabu ya kifungo cha maisha.
(2) Masharti ya Ibara hii yatatumika kwa mtu aliyehukumiwa na kuadhibiwa chini ya Mahakama za Jamhuri ya Muungano akiwa Zanzibar au Tanganyika na kwa adhabu zilizotolewa Zanzibar au Tanganyika kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muunagao inayotumika Zanzibar na Tanganyika.
(3) Kwa madhumuni ya Ibara hii, kutakuwa na Kamati ya Taifa ya Ushauri ambayo itakuwa na wajibu wa kumshauri Rais kuhusu kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mahakamani na anatumikia adhabu.
(4) Utaratibu wa namna ya utekelezaji wa madaraka kwa mujibu wa Ibara hii, muundo, majukumu na utendaji kazi wa Kamati ya Taifa ya Ushauri vitaainishwa na sheria itakayotungwa na Bunge.
(5) Raisi wa Jamhuri ya Muungano hataingilia au kutoa msamaha kwa wafungwa/mfungwa aliyehukumiwa na kuadhibiwa chini ya Sheria na Mahakama ya Washirika wa Muungano .



Kinga dhidi ya mashtaka ya Rais


83.-(1) Wakati Rais akiwa madarakani, hatashitakiwa wala mtu yeyote hataendesha mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.
(2) Wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini
kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.

(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana na kura ya kutokuwa na imani na Rais, haitakuwa halali kwa mtu kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo alilofanya wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.


Maoni;
Kinga dhidi ya mashtaka ya Rais

83.-(1) Wakati Rais akiwa madarakani, hatashitakiwa wala mtu yeyote hataendesha mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

(2) Wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini
kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.

(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Raisi kutokana na kura ya kutokuwa na imani na Rais, haitakuwa halali kwa mtu kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo alilofanya wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

(4)Hata hivyo ibara hii haitazuia mtu au taasisi yoyote kufungua shauri Mahakamani dhidi ya Raisi akiwa madarakani au baada ya kuwa ameacha madaraka kwa taratibu yoyote ile kama anakutuhumiwa kutenda kosa iliyo kinyume na haki na uhuru wa binadaamu au kosa lolote lililotendeka kinyume na Miiko ya Uongozi wa Umma chini ibara ya (20) ya Katiba hii.


Copy; Mnyika Zitto Mzee Mwanakijiji Invisible

Itaendelea;
 
maoni yangu
a) kuwe na serikali moja tu na iitwe TANZANIA .. zanzibar iwe mkoa au jimbo ....

b) Elimu iwe kipaumbele cha kwanza kabisa cha nchi hii
 
Katiba ikataze kabisa kwa kiongozi yeyote wa utumishi wa umma kuanzia Rais mpaka ngazi ya chini kabisa yaani diwani, kupata huduma hizi katika sekta binafsi bali wapate katika sekta za umma yaani;- afya na elimu.
 
Ratiba ya leo, Agosti 22, 2013, Mikutano ya Mabaraza Huru ya CHADEMA, kujadili na kutoa maoni yako kwenye Rasimu ya Katiba Mpya ni kama ifuatavyo;

Timu ya Mwenyekiti Freeman Mbowe, baada ya kumaliza katika wilaya za Mkoa wa Katavi na Rukwa, leo imeingia mkoani Mbeya, itafanya mikutano;

Vwawa, Tunduma, Ileje, Kyela, Tukuyu kisha Mbeya mjini.

Timu ya Katibu Mkuu, Dkt. Slaa baada ya Jeshi la Polisi kuwanyima wananchi wa Lindi na Mtwara, haki na wajibu wa kikatiba, kujadili mstakabali wa nchi yao, leo itakuwa mkoani Pwani, itafanya mikutano;

Utete, Ikwiriri, Kibiti, na kisha Mkuranga.

Jitokeze kushiriki moja kwa moja Mabaraza Huru ya Rasimu ya Katiba Mpya.

Wengine, tuendelee kutoa maoni yetu kupitia ujumbe mfupi kwenye namba 0789248224 au kwa njia ya email;chademamaoni@gmail.com
 
Asantenj watu wa Sumbawanga kwa kutumia fursa, kutimiza haki na wajibu wenu wa kikatiba, kutoa maoni kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, Mabaraza Huru ya CHADEMA.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377181397.605117.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377181397.605117.jpg
    83.1 KB · Views: 28
  • ImageUploadedByJamiiForums1377181480.958110.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377181480.958110.jpg
    93.5 KB · Views: 33
Wananchi wa Sumbawanga, kazi na dawa...
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377182463.129449.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377182463.129449.jpg
    103.3 KB · Views: 35
Neno pasipo kuathiri sheria nyingine kama linavyotumika kwenye rasimu liondolewe kabisa kwenye katiba mpya ijayo na neno sheria zingine zitakazotungwa na bunge liondolewe kabisa,na katiba mpya ijayo ibahnishe wazi kuhusu nani awe boss
 
Wananchi wa Mbeya mjini, wakishiriki kutoa maoni yao kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, Mabaraza Huru ya CHADEMA
 
Ni kweli yote yaliyopo humo ndani ni ukweli yapunguzwe ama kuongezwa. kwani watawala wamekuwa wababe sana.
 
Maeneo ya Mbinga na Songea, Mbamba Bay na Ludewa, asanteni kwa kushiriki kutoa maoni yenu kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, Mabaraza Huru ya CHADEMA!

Pichani, Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, akiwahutubia wakazi wa Mbinga leo.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377274607.526478.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377274607.526478.jpg
    145 KB · Views: 69
Mwananchi, Thadei Ngaizo mmoja wa wakazi wa Ludewa, akitoa maoni yake
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377274702.151875.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377274702.151875.jpg
    96.6 KB · Views: 72
Kamanda Lissu akiwahutubia wana Mbinga leo, Mabaraza ya Wazi ya Katiba Mpya.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377274845.209987.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377274845.209987.jpg
    132.2 KB · Views: 61
Songea leo. Asanteni wana wa Ruvuma. Nafasi yenu katika historia ya mapambano ya uhuru wa kwanza iko pale pale. Bila shaka nafasi mliyoitumia leo, ni mchango wenu mkubwa katika uhuru wa pili.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1377275198.794517.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377275198.794517.jpg
    103.7 KB · Views: 52
  • ImageUploadedByJamiiForums1377275222.624662.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1377275222.624662.jpg
    98.5 KB · Views: 59
Naunga mkono mapendekezo ya CHADEMA 100% Lakini napenda kuongeza mambo machache yafuatayo:
I.Itamkwe Rais pamoja na familia yake waweza kushtakiwa wakati wowote inapothibitika ametenda/wametenda kinyume cha sheria!

2.Kati ya hivi vyeo viwili PM na makamu wa Rais kimoja kifutwe.

3.RCs na DCs vifutwe

4.Kila Mwananchi apate gawio kutokana na raslimali za Taifa.

5.Marufuku viongozi kutibiwa nje.

6.Misafara wa viongozi ipunguzwe spidi, kwani wanakimbia nini?
 
No. 2: Lugha ya Taifa. Ziwe mbili, yaani Kiswahili na Kiingereza. Ni muhimu sana.

No. 10: Serikali tatu. Ndiyo, lakini KATIBA IWE MOJA, ili kila kiongozi aape kulinda katibu hiyo hiyo moja. Vipengele vya namna ya serikali zote tatu zitakavyofanya kazi na kushirikiana viwe kwenye katiba moja.

Kulinda urithi wa Watanzania: Katiba mpya iseme wazi kwamba shughuli yoyote ya kuvuna mali ya urithi kama madini lazima iwe mali ya Watanzania kwa asilimia 51 au zaidi. Kwa uchafu uliopo sasa, our Tanzanite is exported from Kenya, marketed in South Africa and polished in India.
 
Mkuu Tumaini Makene, / Kurugenzi ya Habari


Mchakato maoni dhidi ya Rasimu ya Katiba 2013 unaendelea;

84.-(1) Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara hii.

(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama itadaiwa kwamba Rais ametenda mojawapo ya makosa yafuatayo:
(a) ukiukwaji mkubwa wa masharti ya Katiba hii;
(b) makosa makubwa ya jinai;
(c) kuzuia kwa namna yoyote ile yeyekuchunguzwa kwa mujibu wa Ibara hii;
(d) uhaini;
(e) rushwa;
(f) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha nafasi ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(g) kupuuza au kukataa kutekeleza uamuzi au amri halali za Mahakama; au
(h) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka kanuni za maadili au miiko ya uongozi;
(3) Bunge halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais isipokuwa tu kama-
(a) haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge; na
(b) taarifa ya maandishi, iliyotiwa saini na kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini na tano ya Wabunge wote itawasilishwa kwa Spika siku kumi na nne kabla ya
kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni.
(4) Taarifa itakayowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (3)(b) itafafanua makosa aliyoyatenda Rais, na itapendekeza kuwa Tume ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze tuhuma zilizotolewa dhidi ya Rais.
(5) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyotiwa saini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuwasilisha hoja yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja
kuiwasilisha mbele ya Bunge na kisha Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano, lipige kura juu ya hoja ya kuunda Kamati ya Uchunguzi.
(6) Endapo hoja ya kuunda Kamati ya Uchunguzi itaungwa mkono na Wabunge wasiopungua asilimia sabini na tano ya Wabunge wote, Spika atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati ya Uchunguzi.
(7) Kamati ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya Ibara hii, itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa Mwenyekiti wa Kamati;
(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Bara;
(c) Jaji Mkuu wa Zanzibar; na
(d) wajumbe wengine sita watakaoteuliwa na Spika.
(8) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamatiya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini na nafasi ya madaraka ya Rais yatatekelezwa na Makamu wa Rais hadi Spika atakapomfahamisha Rais juu ya Azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
(9) Ndani ya siku saba baada ya Kamati ya Uchunguzi kuundwa,itachunguza na kuchambua mashtaka dhidi ya Rais, pamoja na kumpatia Rais fursa ya kujieleza, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Kudumu za Bunge.
(10) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile katika muda usiozidi siku tisini, Kamati ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika.
(11) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi,taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Kudumu za Bunge.
(12) Baada ya taarifa ya Kamati ya Uchunguzi kuwasilishwa,Bunge litaijadili taarifa hiyo na kutoa fursa kwa Rais kujieleza, na kisha,kwa kura za Wabunge wasiopungua asilimia sabini na tano ya Wabunge wote, Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais ama
yamethibitika au hayakuthibitika.
(13) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika nafasi ya madaraka ya Rais, Spika atamfahamisha Rais na juu ya Azimio la Bunge na Rais atakuwa ameondolewa madarakani na Makamu wa Rais ataapishwa mara moja kushika madaraka ya Rais.
(14) Endapo Rais ataacha kushika nafasi ya madaraka ya Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya uzeeni, posho wala kupata haki au nafuu nyingine anazopewa Rais au mtu aliyekuwa Rais kwa mujibu wa Katiba au sheria za nchi.

Maoni;

Vipengele vingine vyote kwenye ibara hii vina mashiko kwa mtazamo wangu ispokuwa hizi;

Bunge kumshtaki Rais
84.-(1) Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara hii.


(7) Kamati ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya Ibara hii, itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa Mwenyekiti wa Kamati;
(b) Jaji Mkuu wa Tanganyika;

(c) Jaji Mkuu wa Zanzibar; na
(d) wajumbe wengine sita miongoni mwa wabunge watakaoteuliwa na Spika na mmoja miongoni mwao sharti awe Mwenyeketi au Makamu wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
(13) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika nafasi ya madaraka ya Rais, Spika atamfahamisha Rais na juu ya Azimio la Bunge na Rais atakuwa ameondolewa madarakani na Masharti ya Katiba hii yanayosimamia utaratibu wa Makamu wa Rais kuwa Raisi yatazingatiwa ilikuwezesha Makamu wa Raisi kushika madaraka ya Raisi


85.-(1) Rais atalipwa mshahara na malipo mengineyo kama yatakavyoainishwa na Tume ya Utumishi wa Umma na atakapostaafu atapokea malipo ya uzeeni na stahili nyingine kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

(2) Mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais hayatapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii.
Maoni;

Maslahi ya Rais
85.-(1) Mshahara ,malipo ya Uzeeni na malipo mengineyo ya Raisi yataainishwa na kupendekezwa na Tume ya Utumishi wa Umma na kuthibitishwa na Bunge na muda wote yatakuwa yakilipwa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais baada yakuthibitishwa na Bunge hayatapunguzwa akiwa Raisi au baada ya kuwa amestaafu au kujiuzulu kwa mujibu wa Katiba hii isipokuwa yanaweza kuboreshwa na maboresho yatafuata utaratibu wa ibara 85;(1) ya Katiba hii.

88.-(1) Mtu hatateuliwa kugombea au kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama anazo sifa za kuchaguliwa kama Rais.
(2) Chama chochote au mtu yoyote anayekusudia kugombea kiti cha Urais kama mgombea huru hatazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au Rais wa Tanzania Bara.
(3) Makamu wa Rais hatakuwa na wadhifa mwingine wowote wa kiserikali uliotajwa katika Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge.
(4) Endapo mtu ambaye ni Rais wa Tanzania Bara au Rais wa Zanzibar anateuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais ataacha kiti cha Rais wa Tanzania Bara au cha Rais wa Zanzibar, kadri itakavyokuwa.
Maoni

88.-(1) Mtu hatateuliwa kugombea au kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama anazo sifa za kuchaguliwa kama Rais.

(2) Chama chochote au mtu yoyote anayekusudia kugombea kiti cha Urais kama mgombea huru hatazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au Rais wa Tanganyika.
(3) Makamu wa Rais hatakuwa na wadhifa mwingine wowote wa kiserikali uliotajwa katika Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge.
(4) Endapo mtu ambaye ni Raisi wa Tanganyika au Rais wa Zanzibar anateuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais ataacha kiti cha Rais wa Tanganyika au cha Rais wa Zanzibar, kadri itakavyokuwa.
(5) Katiba za Washirika wa Muungano itaweka Masharti yatakayozingatiwa na Raisi wa Tanganyika au Zanzibar ambaye/ambao wakati wanateuliwa /anateuliwa au kupendekeza kuwa mgombea wa Uraisi wa Muungano au kuwa Makamu ni Raisi ambaye Muda wake wa kukaa Madarakani kwa mujibu wa Katiba ya Washirika Muungano hujaisha Kisheria.
90.-(1) Makamu wa Rais atashika nafasi yamadaraka ya Makamu wa Rais siku hiyo hiyo Rais anaposhika madaraka.
(2) Makamu wa Rais aliyeteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 72 ataapa na kushika madaraka yake baada ya uteuzi wake kuthibitishwa na Bunge.
(3) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, mtu aliyechaguliwa, au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 72 kuwa Makamu wa Rais, bila ya kuathiri masharti mengine ya Ibara hii, atashika kiti cha Makamu wa Rais kwa muda wa miaka mitano tangu alipochaguliwa kuwa Makamu wa Rais.
(4) Makamu wa Rais atashika kiti hicho hadi-
(a) muda wake utakapokwisha;
(b) akifariki dunia akiwa katika madaraka;
(c) atakapojiuzulu;
(d) atakapoapishwa kuwa Rais baada ya nafasi ya madaraka ya Rais kuwa wazi;
(e) atakapotiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai linaloonyesha utovu wake wa uaminifu;
(f) atakapoapishwa Rais mwingine kushika nafasi ya madaraka ya Rais pamoja na Makamu wake;
(g) atakapoondolewa madarakani baada ya kushtakiwa Bungeni kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii;
(h) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais vinginevyo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

Maoni;

Pamoja na maoni Ibara hii nadhani mrejeo uliotajwa kwenye nyukundu ni makosa ya kiufundi;

90.-(1) Makamu wa Rais atashika nafasi yamadaraka ya Makamu wa Rais siku hiyo hiyo Rais anaposhika madaraka.
(2) Makamu wa Rais aliyeteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 72 ataapa na kushika madaraka yake baada ya uteuzi wake kuthibitishwa na Bunge .
(3) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, mtu aliyechaguliwa, au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 87 kuwa Makamu wa Rais, bila ya kuathiri masharti mengine ya Ibara hii, atashika kiti cha Makamu wa Raisi kwa muda wa miaka mitano toka alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Makamu wa Raisi.
(4) Makamu wa Rais atashika kiti hicho hadi-
(a) muda wake utakapokwisha;
(b) akifariki dunia akiwa katika madaraka;
(c) atakapojiuzulu;
(d) atakapoapishwa kuwa Rais baada ya nafasi ya madaraka ya Rais kuwa wazi kwa mujibu wa Ibara ya 72 ya Katiba hii.
(e) atakapotiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai linaloonyesha utovu wake wa uaminifu;
(f) atakapoapishwa Rais mwingine kushika nafasi ya madaraka ya Rais pamoja na Makamu wake;
(g) atakapoondolewa madarakani baada ya kushtakiwa Bungeni kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii;
(h) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais vinginevyo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

91.-(1) Bunge litakuwa na madaraka ya kumshtaki Makamu wa Rais kwa utaratibu unaotumika kumshtaki Rais kwa mujibu wa Katiba hii, isipokuwa kwamba, hoja yoyote ya kumshtaki Makamu wa Rais itatolewa tu iwapo:

(a) Rais amewasilisha hati kwa Spika inayoeleza kwamba Makamu wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi za madaraka ya Makamu wa Rais;
(b) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha nafasi ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano au kiti cha Makamu wa Rais; au
(c) anadaiwa kutenda kosa lolote kati ya makosa yanayoweza kusababisha Rais kushtakiwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba hii, isipokuwa kwamba, haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.

(2) Masharti mengine kuhusu utaratibu wa kumshtaki Rais yatatumika wakati wa kumuondoa madarakani Makamu wa Rais.

(3) Ikitokea kwamba kiti cha Makamu wa Rais ki wazi kutokana na masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (1), kifo au kujiuzulu basi mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote ndani ya siku zisizozidi kumi na nne baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura za Wabunge walio

4) Masharti mengine yote ya Ibara ya 84 yatatumika pia kuhusiana na Makamu wa Rais isipokuwa tu kwamba Makamu wa Rais aliyeondolewa tena madarakani chini ya Ibara ndogo ya (3), hatakuwa na sifa tena za kushika nafasi ya Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Tanzania Bara wala Rais wa Zanzibar.

(5) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika nafasi ya madaraka ya Makamu waRais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya uzeeni, posho wala kupata haki au nafuu nyinginezo anazopewa Makamu wa Rais au mtu aliyekuwa Makamu wa Rais kwa mujibu wa Katiba au sheria za nchi.


Maoni;

91.-(1) Bunge litakuwa na madaraka ya kumshtaki Makamu wa Rais kwa utaratibu unaotumika kumshtaki Rais kwa mujibu wa Katiba hii, isipokuwa kwamba, hoja yoyote ya kumshtaki Makamu wa Rais itatolewa tu iwapo:
(a) Rais amewasilisha hati kwa Spika inayoeleza kwamba Makamu wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi za madaraka ya Makamu wa Rais;
(b) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha nafasi ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano au kiti cha Makamu wa Rais; au
(c) anadaiwa kutenda kosa lolote kati ya makosa yanayoweza kusababisha Rais kushtakiwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba hii,isipokuwa kwamba, haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.
(2) Masharti mengine kuhusu utaratibu wa kumshtaki Rais yatatumika wakati wa kumuondoa madarakani Makamu wa Rais.
(3) Ikitokea kwamba kiti cha Makamu wa Rais kiwazi kutokana na kifo au kujiuzulu basi, mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote ndani ya siku zisizozidi kumi na nne baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua mtu mwenye sifa kuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo lazima uzithibitishwe na Bunge kwa kura za Wabunge walio wengi.
(4) Masharti mengine yote ya Ibara ya 84 yatatumika pia kuhusiana na Makamu wa Rais na kwamba Makamu wa Rais aliyeondolewa madarakani chini ya masharti ya Katiba hii, hatakuwa na sifa tena za kushika nafasi ya kuwa Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Tanganyika wala Rais wa Zanzibar.

(5) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika,hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya uzeeni, posho wala kupata haki au nafuu nyinginezo anazopewa Makamu wa Rais au mtu aliyekuwa Makamu wa Rais kwa mujibu wa Katiba au sheria za nchi.
 
Mimi napendekeza serikali 3 sababu ni wazi,Tunahitaji watanganyika tuwe na mahali huru pa kujadiliana mambo yetu bila kuingiliwa na wazanzibari kama ilivyo sasa.Wao wana baraza lao ambalo watanganyika hawaruhusiwi kuwepo.Bunge la muungano lina mapungufu mengi kwani kwa muundo wa sasa ndilo pia bunge la Tanganyika kichekesho.Nauliza bunge la muungano lina sura mbili yaani la Tanganyika na la Muungano.Mapungufu ninayoona sasa ni kwamba wakati wakijadili jambo au bajeti ya mambo ya Muungano sawa lakini wanapokuwa wanajadili mambo au wizara zisizokuwa za Muungano mbona wabunge toka Zanzibar hawatoki nje? hili ndio tatizo kubwa na suluhu ni serikali tatu.Kama hii ikishindikana basi mwafaka ni serikali moja na hii ikishindikana basi Muunfgano bora ufie mbali.
 
Samahani: Leo nimewasikia wenzetu wakijivuna kukusanya maoni ya wanachama 2,500,000 kwa ajili ya maboresho ya rasimu ya Katiba. Ningependa kujua mpaka sasa kwa SMS hali ipoje kwa mabaraza ya Chadema, E-mail, JF, nk.
Ningefurahi kujua hayo ili kujua position yetu. sorry kama wazo langu litakuwa si muafaka
 
Back
Top Bottom