Mume wa rafiki yangu anatarajia kuoa mke wa tatu wiki ijayo, rafiki yangu hana raha na ndoa yake

Mume wa rafiki yangu anatarajia kuoa mke wa tatu wiki ijayo, rafiki yangu hana raha na ndoa yake

Tuachane Na Hayo, Kwahiyo Vipi dini Utabadili Au Hutabadili? 😡😡
 
Hujanielewa kwanini mnaoa leo kesho talaka halafu mnajaza wanawake nyumba moja??
Kama nilivyomweleza mdau hapo juu kwamba asichanganye kati ya Ukristo na Wakristo; na ndivyo hivyo usichanganye kati ya Uislamu na Waislamu!!

Unaposema "...kwanini mnaoa leo kesho talaka", kwani ndivyo unavyosema Uislamukwamba "oeni leo na kesho acheni" ?! Something tells me huyu bwana/bibi alikuwa sahihi
Iman za watu ukiziingilia utaonekana unawapinga.
hapo kabla, nilidhani you'd clear conscious ya kutaka kuelimishwa kama ambavyo ulidai lakini kwa kuangalia post yako hii:-
Mwambie dini yetu ni mke mmoja , mme mmoja na ndio vizuri sisi sio wajinga sasa wao wanawajaza mwisho karaha bhana .
Heshima nikitu cha bure
nadhani lengo lako ni tofauti kabisa, na kwa bahati mbaya sana, huwa sina interest ya kufanya malumbano ya kiimani, and that being said KWAHERI, and stay blessed!!!
 
Mimi ni mkristo kindakindaki ila huwa naona ndoa za kiislamu ni za kweli hazina unafiki. Ukiona watu wamedumu ndoani basi wamedumu kweli sio hizi za kwetu wanandoa wanafikia hatua ya kuwa maadui kiasi cha kuuana ila wapo tu wanasubiri kifo kiwatenganishe.
Angalizo: sio ndoa zote
 
Wajameni kati ya kitu ninachoogopa ni kubadili dini niwe muislamu.
Na ndoa yao imefunguliwa.
Ipo kirahisi sana .
Unaolewa leo kwa gharama kubwa akimaliza haja zake anakupa talaka tatu.

Hapo mashosti wanakucheka umeachwa unashangaa.
Juzi nilienda kwa shosti yangu kaolewa huu ni mwaka wapili mie nikazani anaraha .
Kumbe nikaraha huyo mwanamme alimsilimisha akawa muislamu .
Halafu akapata watoto naye .

Baada yakupata watoto wakike hao ni mapacha.
Akanza vitimbi akaoa bila ya ridhaa yake.

Akamleta mke wa pili sasa wapo wawili .
Huu ni mwaka watatu yupo humo ndani kwenye chumba chake.
Sasa huyu baba anaoa tena wiki ijayo na atamleta mke ndani.

Hivi shida huwa nini?
Niambieni jamani?
Akaanza vitimbi
Inamaana bado hunaolewa eti


Ndoa ya Aina yeyote ni ndoa Kwa jamii

Lzm ufuate taratibu za kijamii hiyo

Mwanamke nzao ya Kwanza unaazaje kitambi


[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Mie naunguza kbs mafuta
 
Kama ni vitimbi kwenye ndoa... hakuna cha ndoa ya Kiislamu, Kikristo wala Kiyunani!! Sasa mambo yakiwa kitimtim namna hiyo si bura kila mtu ashike hamsini zake kuliko mnaishi nyumba moja wakati hakuna amani?!!

Anyway, hizo taraka zinatolewa ndivyo sivyo lakini msingi wake, ni kuepusha shari baina ya wanandoa, isjie mkafikia hadi kuuana au kudhuriana! Na hadithi inasema wazi kwamba "...talaka ni ruhusa inayochukiza"!

Ni kutokana na hilo, ndo maana mafundisho yanasema, mwanaume ukiona ndoa haivumiliki, basi toa taraka moja; na kama nyumba ni kubwa basi gawaneni upande labda hadi kwisha eda, suluhu kati yenu itakuwa imeshapatikana!!!!

Na lau kama nyumba ni ndogo, basi mwanaume toa taraka kisha mwache ex wako kwenye hiyo nyumba, huenda baada ya muda akili zitakurudia na kuamua kumrejea mke wako!!
Nikikutana na comment yako huwa natoa like kwanza kisha nasoma.

Eda ndio nini, huwa naisikia. Huo utaratibu wa taraka ndio nimeuona hapa ingawa mimi sio Mwislamu lakini sijawahi ona unafuatwa.
 
Hapa unaponda ndoa za kiislamu au unamponda mine wa rafiki yako anataka aoe mwanamke mwingine?
Au unataka kujua taratibu za ndoa za kiislamu zipoje,binafsi sijakuelewa,maana umeandika kwa jazba Sana.
 
Mimi ni mkristo ila katika suala naliunga mkono ni kuoa wake wanne,ina maana yake aisee..suala la talaka naliunga mkono pia..hivi imagine kuna watu wamefunga ndoa za kikristo lakini wana ugomvi usiokoma,mke na mme wanalala vyumba viwili tofauti kwa zaidi ya miaka miwili..hakuna tendo la ndoa wala maelewano tena..wanaishi kwa kuviziana sasa si bora kupeana talaka?
Tukianza na swala la taraka kwa mkiristu ina ruhusiwa sema labda kama umefungwa na mafundisho ya dhehebu lako. Vigezo na masharti kuzingatiwa


Pia suala la kuoa wake wanne nalo lina umuhimu wake,wanaume tumependelewa sana imagine hatuingii P kama wanawake,hatubebi mimba,hatuzai kama wenzetu..sasa ukiwa na mke mmoja kipindi anapitia hayo unafanyaje?mtu akijifungua unashauriwa uache angalau miezi 6,je katika hali ya kawaida inawezekana kweli kwa mtu aliyezoea kufanya mara kwa mara?si ndo chanzo cha usaliti!!ni bora ukiwa na wake wanne unahamia tu..huyu akiwa P unaenda kwa mwingine..huyu akijifungua unahamishia majeshi sehemu nyingine..
Hapa umeongea kibinafsi zaidi vip mkeo nae akisema umruhusu aolewe na mwanaume zaid ya mmoja ili utakapo kuwa kwa mke mwenza nae apate wa kumtiliza midadi zake? Kwenye ndoa kunahitaji uvumilivu sio ubinafsi.
Swala la kujifungua sidhan kama kuna ukwel kuwa usubiri had miezi sita labda kama amepata matatizo ya kiafya.
 
Nikikutana na comment yako huwa natoa like kwanza kisha nasoma.

Eda ndio nini, huwa naisikia. Huo utaratibu wa taraka ndio nimeuona hapa ingawa mimi sio Mwislamu lakini sijawahi ona unafuatwa.
Kwa lugha nyepesi, eda ni muda wa matazimio... it's like grace period ambayo mwanamke anatakiwa kukaa pindi anapoachika au anapofiwa na mumewe!!

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, nadhani ni siku 90. Lengo ni kuhakikisha mwanamke aliyeachika au kufiwa mumewe hakukutwa na mkasa huo wakati akiwa ana mimba changa!!

Which means, kama alikuwa na mimba changa basi hadi kufikisha hizo siku 90 mimba itaonekana na hatimae kufahamika baba halisi wa mtoto mtarajiwa ni yupi!

Kuhusu utaratibu wa talaka, upo sahihi kwa 99%... yaani watu hawaufuati kabisa huo utaratibu licha ya Mtume mwenyewe kusema "...talaka ni ruhusa inayomchukiza Mwenyezi Mungu"!

Kauli hiyo ina maana moja tu: Huwezi kutoa taraka kama zinavyotolewa na Waislamu kwa sababu wamepewa hiyo ruhusa inapoonekana hapana jinsi! Mmejitahidi kutafuta suluhu na imeshindikana, na inaonekana kuendelea kuishi pamoja basi inaweza kuleta matatizo makubwa zaidi!
 
Wewe hakuna aliekulazimisha kuwa muislamu,sisi wenyewe tunatosha hatutaki muhamiaji.
2.unadai rafiki yako alisilimishwa akawa muislamu akaolewa akapata mapacha mume wake akaanza vitimbi, unajua kesi za ndoa hazisikilizwi upande mmoja?
Umemsikiliza rafiki yako tu ukatoa hitimisho mumewe ni mkorofi,
Una uhakika gani?
Mambo ya ndoa ni magumu na nahisi wewe hujaolewa,Kama ungekua na mume usingeandika haya;
Ndoa za kiislamu ziko rahisi kwa kuwa hatutaki unafiki ndani yetu.
Hatutaki kuchomana na magunia ya mkaa,hatutaki kuuana Kama yule jamaa aliemuua mkewe akamfukia kwenye shamba lake la migomba kule mkuranga(nilishuhudia katika kufukua maiti tukiwa na wenzangu)
 
Mimi ni mkristo ila katika suala naliunga mkono ni kuoa wake wanne,ina maana yake aisee..suala la talaka naliunga mkono pia..hivi imagine kuna watu wamefunga ndoa za kikristo lakini wana ugomvi usiokoma,mke na mme wanalala vyumba viwili tofauti kwa zaidi ya miaka miwili..hakuna tendo la ndoa wala maelewano tena..wanaishi kwa kuviziana sasa si bora kupeana talaka?...
Msituingize chaka hakuna mwanaume ambaye yuko mwenyewe tu anashangaa shangaa lazima uwe na kipoozeo msituchore .😎😎
 
Back
Top Bottom