Mume wangu alizaa nje: Nimekuwa na chuki na kusababisha kuchepuka nje ya ndoa

Mume wangu alizaa nje: Nimekuwa na chuki na kusababisha kuchepuka nje ya ndoa

Ni hulka ya jinsia KE hata kwa wanyama,, ndege nk ni vigumu kwa jinsia KE kukubali mtoto wa mwenzake hata kama ni aina moja ya spishi,,,and vise versa!!
 
Hizi nyuzi zipo kimkakati, hawa watakua wazee wa 50/50 wanajaribu kubalance mzani.
Tatizo hoja zao ni mfu, mwisho wa siku mwanamke anaonekana malaya tu.

Siku ukipata mimba huko mume atakutimua.
 
Wewe hukuchepuka kwa sababu ya maumivu ya mumeo kuzaa njee.

In short,unachepuka ili kutimiza malengo/maslahi yako,kwa maneno mengine wewe ni changudoa uliyekaa kikisasa zaidi.
 
Laiti km huyo mtoto angejua unavyomfikiria vibaya angeondoka. Kwa namna ulivyoandika upo tayari kumpa sumu afe wakati yeye hana kosa. Sema sku mumeo akikufuma usiste kutupa hapa mrejesho.
 
mzabzab
Yani broo kuna KE humu zishaanza kuona wivu kisa mwenzao anajenga, hahaha washaanza ooo nyuzi feki kama kawaida .
Yani bro mzabzab
Wanawake wanawivu wa kijinga sana. Eti nyuzi feki hahaha
Atoto
Donatila
Carleen
Wewe hawa sii wnataka wajionyeshe wao malaika tafikiria wao hawachepuki. Sasa sijui sie wanaume tunachepuka na punda?
 
Kayaga Twende, Dawa Ya Moto Ni Moto

Kupanga Ni Kuchagua
Nakushauri Mfate Yule Baba Dodoma Anyooshe Mambo Yako Halafu Zaa Naye
Nawe Upate Kupona Kidonda
 
Ukishindana na mwanaume zitakazoumia ni sehemu zako za siri tu.

Tafuta note duniani ukikuta mke kaolewa na mume zaidi ya mmoja then go ahead.
hebu jaribu Nepal naona kama vile wanao utamaduni huo wa mke mmoja waume wengi
 
mzabzab
Yani broo kuna KE humu zishaanza kuona wivu kisa mwenzao anajenga, hahaha washaanza ooo nyuzi feki kama kawaida .
Yani bro mzabzab
Wanawake wanawivu wa kijinga sana. Eti nyuzi feki hahaha
Atoto
Donatila
Carleen
Carleen hili furushi huwa halikosi hizi nyuzi. Tena wa mwanzo mwanzo kucoment. Na huwa ni mtetezi mkuu. Sijui dots zinaungika😂😂😂😂
 
Miaka kadhaa iliyopita mume wangu alimtambulisha mtoto wa nje katika familia yake ni wa kiume alikuwa ni mtu wa furaha sana na kujisifu kuwa kapata mtoto wa kiume na ndugu zake walimpongeza hasa mtoto alifanana nae. Japo mimi nilibaki na maumivu, kwani nimezaa nae watoto wawili wa kike tuu.
Katika maisha yangu nilipenda kuwa na mwanaume ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu. Ila ijakuwa hivyo. Nimelipokea japo nina maumivu.

Mume wangu ni mtu wa mfumo dume niseme. Akiongea ndani ya nyumba ndo ishakuwa hivyo. Aliniambia tuu mtoto huyu ni wangu na ataishi hapa kama utaki basi waweza ondoka.
Nikasema tuu sawa, basi mtoto tunaishi nae hapa.

Tulijenga nyumba moja tulikuwa tunashirikiana kwa kila kitu kwa sababu mimi nina kazi na mume wangu pia na baadhi ya biashara. Na tulishaanza nyumba nyingine kujenga. Ila nilisimama baada ya tukio hilo lililonipa maumivu.

Nilishangaa sana mume wangu anatabia ya kusema tuu yeye hana uwoga. Anasema kuwa huyu ni mtoto wangu wa kiume ndio atarithi mali zangu kwa kuwa anaendeleza jina langu. Mimi namuangali tuu. Mtoto anapita nae mtaani kwa kujisifu hata mbele ya marafiki zake kwa kuwa mtoto kafananae. Na yeye mali zetu zipo kwa jina lake na mimi hata ushahidi kuwa nimeweka mkono sina ninabaki namuangalia tuu.

Miaka 3 iliyopita kuna kiwanja kimoja aliniachia marehemu Baba kipo kigamboni kule ni kikubwa kiasi. Na mume wangu ajui hiko kiwanja. Ni mimi tu ka ndugu zangu. Sasa nilipigania kuwa niwajengee watoto wangu nyumba pale japo mimi mama yao sina sio tajiri. Nikasema nitapambana tuu. Nilikuwa naweka vipesa vyangu baadhi na kujinyima. Hata pesa ya mume wangu ya matumizi nilikuwa naibana sana.
Biashara zetu na mume wangu nilikuwa nachota kiasi bila mume wangu kujua kabisa.

Nilianza msingi wa nyumba mbili kwenye eneo moja. Nyumba sio kubwa ni vyumba viwili tuu vya kulala, living na dining room, choo na store na jiko. Sio kubwa kivile.

Ilikuwa ngumu sana kwangu kuanza kujenga.
Sasa siku moja nilikutana na Baba mmoja mtu mzima na anamke na watoto wakubwa tuu. Nilikutananae karikoo kwenye nduka moja hivi. Tulizoeana mapaka kupanga nichepuke nae.
Mkewe kuna kipindi nikamjua mpaka nyumbani kwake. Ni Baba mwenye uwezo tuu tena sana.
Mimi ni mwanamke nina mvuto kwa hio niliamini hawezi nikataa yule Baba. Mara nyingi tulikuwa tunakutana kwenye hotel. Nilimueleza shida zangu akasema atanisaidia.

Alinisaidia kumaliza msingi mpaka boma kuisha za vijumba vyangu. Nilijitahidi sana mume wangu asijue kwani yeye namjua reaction yake endapo akijua.

Yule Baba alikuwa ananifurahia sana , ila alikuwa ananionya kuwa kuwa makini mumeo asijue kabisa. Mimi namwambia tuu usijali ni kweli nilijitahidi mume wangu asijue kabisa.
Nilikaanae miaka 2 yote hio niliendelea nae bila my hubby kujua.
Yeye yuko busy na mtoto wake maana namuangali tuu jinsi anavyomuaangaikia. Mwaka jana alinisaidia sana kuwezeka vijumba vyangu.
Ila mwishoni mwa mwaka jana aliamishwa na kwenda Dodoma kikazi na mahusiano na mimi yaliisha.
Nikiri tuu alinisaidia sana yule Baba. Kwa kiasi kikubwa.

Sasa mwaka huu nilikutana na kijana mmoja mgahawa mmoja nilimpenda, nilijitahidi nikapata tukabadilishana namba najua hawezi kunikataa coz mimi ni mzuri najiamini. Niliingia nae kwenye mahusiano. Na sijamwambia kuwa ni mke wa mtu. Japo vijana ni wagumu kutoa pesa ila anajitahidi kiasi chake. Naamini atanisaidia hata kwenye biashara zangu binafsi, coz yeye anaagiza vitu china.

Najua wanaume mnakasilishwa na usaliti kama huu, najua wapo watanitukana na maneno juu. Lkn hata nyinyi ni wasaliti kwa wake zenu, thread zenu za michepuko mnashauriana sana humu jf.

Mume wangu kanipa donda kubwa sana , tena hata aibu anasema huyu ndo mrithi wangu. Yeye ni wale wanaume akisema basi wote mtii.
Namuangali tuu na mwanae.

Sijaleta kama sifa ni matokeo ya maumivu niliyopata sikuwa na hio tabia kabisa.
Mwenye kuleta povu na alete tuu.
Hujamalizia story ya hii hapa eh akawa analeta vitu kutoka china anakupa chuna mama usijali maisha ni magumu ila ndio hivyoo aangalia afya Yako maana ukijifanya unamkomoa basi tu wewe ndio utabakia unashida sio yeye anatamba na mtoto wake
 
Hahahaha Wanawake wanaojionaga wazuri hahaha wanakuaga Wajinga sana kwakweli !!

Wengi wa Wanawake wazuri hawaolewi, wakiolewa ,ujue mwanaume ana Moyo wa uvumilivu sana.


Simnaona Kila Aya anasema "Coz najiamin mie mzuri "😂😂😂
 
Back
Top Bottom