Muna Love ajutia kufanya upasuaji wa kutengeneza mwili wake

Hii ishu ya mastaa wa Bongo kufanya upasuaji wa miili yao imekuwa kama fasheni lakini ni wapuuzi hawa hawajui madhara ya hiyo kitu.

Nilikuwa nasoma alichoandika Muna Love kuwa anajutia alichokifanya, ngoja kwanza nimnukuu:

“Achaneni na surgery. Msifanye nitakuja kuwaeleza vitu vingi ninavyopitia. Nampenda Yesu nawapenda."

Kwanza namsikitikia na ninamuonea huruma kwa kuwa wakati mwingine ni ulimbukeni wa kutoelewa nini wanachokifanya.

Wasanii na mastaa wetu wa Bongo wana tamaa ya kuiga mambo mengi ya nje ambayo wakati mwingine hayana kichwa wala miguu.

Najua wapo wengi tu wanaofanya michezo kama hiyo, inawezekana sasa hivi hawaonekani kwa kuwa wapo bahati ilikuwa kwao hawajapata madhara ya mapema ila ipo siku wataibuka wengi tu kama alivyofanya Muna Love.

Mtu mwingine ambaye nina wasiwasi naye ni Irene Uwoya, nikiutamza ule mdomo wake hasa wa chin, kiukweli siuelewei kabisaaaaaa

Labda nakosea lakini nahisi kuna kitu kafanya kuuogeza huo mdomo, na kwa kuwa sasa hivi ana hela anaweza kuona poa tu na anao uwezo wa kufanya ‘service’. Kama hauniamini kautazama mdomo wa Uwoya ulivyo kwa sasa.
 
Yeah, Kuna watu wako Duniani,, Bwana Yesu kawaacha wapitie maisha Fulani. Ili wengine wajifunze[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kaongeza lips
 
Haya warembo wetu igeni ya mzungu mpaka mchoke…
 
Mchuma janga hula mwenyewe iwapo wakwao walimshauri akapuuza.
 
Hivi huyu Muna ndo nani kwani? Ni mwanamuziki? Muigizaji?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…