Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Roho ambayo ipo ndani yako ina umbo?
Cha msingi nacho kukusisitiza tambua kwanza utofauti wa Allah na Mungu wa wakristo ,ukisha tambua hilo hutauliza maswali kwa kuweka uelewa wako wa Mungu Allah kwa Mungu mwingine

Allah amesema wazi na scholar wote wa waislamu wanakubali ni physical being , una umbile linashikika

Sema umbile lake ndio hivyo la kutisha , mikono miwili upande mmoja
Nasubiri majibu ya maswali yangu. Kisha tuendelee na hili.
 
Issue sio maswali nataka ukiri kwanza Allah na Mungu wa wakristo ni tofauti ,ndio nitaendelea na majibu , kinyume Cha hapo siwezi kukujibu maana unaleta nature ya physical being (Allah) na nature ya Spirit (Mungu wa wakristo) ambavyo ni vitu viwili tofauti
Kijana naona unaendeleza tabia yako ya kukimbia maswali. Swali nililo anza nalo ni kuwa wapi Yesu alisema yeye ni mwana wa mungu au yeye ni Mungu.

Mkanukuu andiko toka kwa Luka, nikawataka mthibitishe huyo Luka amewahi kumuona Yesu kama hajamuona hayo maneno ameyapata wapi.

Kisha turudi huku.
 
Kama Mna muita nabii issa lakini mnasema hajafaaa mtu gani wa kawaida gani asiyekufa huyo, Yesu ni njia na kweli na uzima
 
Wewe ndio umesema Ndugu yangu kwamna Mungu kazaa. Sasa Yanakuwaje tena maneno yangu

Kama Alizaa kwa Neno Mariam alihusikaje sasa. Si angetamka au kumuumna Yesu kwa Udongo kama Alivyofanya Kwa Adam

Kuna swala ambalo inabidi uelewe.
Wewe unamjua Yesu baada ya kuzaliwa na maria lakini Yesu alikuwepo kabla ya maria. Yeye ndio MWANZO. Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana. Ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
 
Huwezi. Niambie kwamba nabii issa tokea kipindi kile Cha mitume yeye hajafaaa tu Kuna ,halafu eti atarudi Kuna Siri hapo,kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri ya kwamba Yesu Kristo ni mwana wa Mungu it matter of time tu
 
Mungu anateswaa kwa ajili yetu sasa anateswa na Nani na yeye ndio Mungu [emoji28][emoji1787][emoji1787] hapa tulipigwa na kitu kizito
halafu anakuja kutuhukumuu mamaweeeh
Umepewa tahadhari.
Roho asema wazi wazi siku za baadaye watu wengine watatii roho danganyifu nakufuata mafundisho ya pepo
Timotheo4°
 
Ungekua unamjua Yesu usingeuliza hilo swali
Rudi nyuma kasome comments utanielewa

YESU NI MUNGU
Kumbukeni nilivyowambia nitakwenda na nitarudi, kama kweli mnanipenda mngefurahi na kushangilia maana nakwenda kwa baba: na baba yangu ni mkuu kuliko mimi°
Yesu anasema Mungu ni Mkuu kuliko yeye.
 
Kuna Mambo Yapo Ulimwenguni ukiyatafakari kwa Kina hayaingii Akilini ndugu waafrika wenzangu

Kuna Historia katika Vitabu kwamba Mungu alimtoa Mwanae Ili aje Kuikomboa Dunia katika Dhambi (ambazo zipo mpaka Leo)

Ukiangalia kwa Undani Historia hii ya kuzaliwa kwake inatia Shaka sana kabla ya Kujua Majibu ya kuzaliwa kwake inakuja Historia kwamba hana Baba. Kabla hujapata Majibu ya Baba ni nani Inakuja Kwamba ni Uwezo wa Mungu ndio akazaliwa. Yanakuwa Maswali juu ya Maswali

Kumbuka Yusufu na Mariam si kwamba Walikuwa ni Wachumba la hasha bali walikuwa tayari wapo Ndani (wameoana) wanaishi pamoja. Hakuna wachumba Wanaoishi pamoja kwa Utaratibu wa Kuishi. Ukichumbia wewe utakaa kwako na Huyo mchumba atakaa kwao. Kama Waliishi pamoja maana Yake waliweza Kushiriki Tendo la Ndoa yao na Ukifuatilia kwa Makini Yusuf alikuwa Pamoja na Mariam kila Sehemu hakuna Sehemu inayosema Alikuja Kumuoa mariam Ikiwa na Maana Kwamba Tayari alikuwa keshaoa maana yake ule uchumba ulio andikwa Tayari ukayeyuka

Binadamu huzaliwa Kwa Mwanaume na Mwanamke hili halina ubishi. Ila Kuna Kuja Utata wa Hapa Kwamba Yesu alizaliwa bila Mfumo maalumu wa Uzazi wa Baba na Mama ila Roho Mtakatifu kama Wanavyodai (kumbuka Hata Huko india Wapo Watu wenye Hadithi hizi hizi za Kuzaliwa bila Baba)

Sasa Hapa Unajiuliza Maswali. Mungu huyo aliyeweza Kumuumba Mwanadamu wa Kwanza Bila Kutumia mifumo ya Uzazi Inakuwaje leo aje Aanze Kumuumba Binadamu mwingine anayedaiwa ni Mwanae kwa Mifumo ya Uzazi na Akaenda kwa Mariam ambaye alikuwa teyari ana Mume(kumbuka Hapa Mungu hazai na Wala Hakuzailiwa)

Sasa Anamzaa mwanae kupitia Mariam mara Yusufu atake kumkimbia Mariam maana Kuna Siri May be Yusufu aliiona akaona Hapa Nimepigwa na Baada ya Yesu kuzaliwa Yusuf Anapotea Ghafla kwenye Maandiko na Historia yake inaishia Hapo hapo

Mungu anamtoa Mwanae. Anakuja Mnamkataa, mnampiga, mnamtesa anawahubiria mnagoma Kukubali maneno yake mnamfukuza kwenye masinagogo yake, Anaenda Kusali mlimani peke yake, anakusanya wanafunzi wake. Hao wanafunzi nao mnawakataa mnawafukuza. Hivi Mungu hapo anawaogopa Nyie kisa Nini mpak Awafanyie Haya Yote Nyie Viumbe wake

Yaani Mungu mpaka Anatoa Mtoto wake Wa Pekee ili awabembeleze nyie mmrudie Yeye na Mnakataa. Sasa Hapo Mungu Anakuwa na Ule Uwezo na Kutoshindwa Kitu kweli. Kama Kawatumia Mwanae na Mmemgomea kawatumia Manabii na Mitume mmemgomea Tena na hamtaki kumrudia. Hivi Mungu anawalemba Hivyo Ili Iweje

Si kila Mtu anayezaliwa bila Baba Yake basi Baba Yake ndio Mungu. Wachawi wanazini na Binadamu kila Siku na Wachawi hao hao ndio Binadamu wenzenu. Wanawake wanabeba Mimba zingine wasizozijua zimetoka wapi

Basi Mjue Kwamba Hapo Mwenye Enzi Mungu hayupo na Mnaozeshwa Akili zenu ndugu zangu. Kaeni Chini Mtafakari kwa Akili zenu Timamu. Mungu hawezi kufanya hayo Kwa Viumbe wake. Yeye hayupo Hivyo

[emoji3507]Mungu si Mmoja
[emoji3507]Mungu si Wengi
[emoji3507]Mungu si Baba
[emoji3507]Mungu si Mama
[emoji3507]Mungu si Kiumbe
[emoji3507]Mungu hachukii Viumbe
[emoji3507]Mungu hapendi Viumbe wake ila Ana Enzi na Viumbe wake (usijione wewe Kiumbe Mtu unapendwa na Mungu Kuliko Viumbe wake wengine aliowaumba)
[emoji3507]Mungu hakuzaa wala Kuzaliwa

Yachunguzeni maandiko Yenu mtajua kwamba si Maandiko ya kiucha Mungu ila Maandiko ya Viumbe wenye Tamaa

ASANTENI
Acha kupoteza muda kujadili story za Abunwasi. Huyo Yesu hakuwahi kuwepo. Vyanzo vyote huru (visivyofungamana na dini) vya kihustoria vimeonesha wazi hakuna ushahidi wa kushikika wa huyo wanayemuita Yesu na hao wanafunzi wake kuwahi kuwepo hapa duniani.

Kuna wakati tuache kutangliza kuamini (Imani) badala ya kutanguliza kuelewa (Ukweli).
 
Kumbukeni nilivyowambia nitakwenda na nitarudi, kama kweli mnanipenda mngefurahi na kushangilia maana nakwenda kwa baba: na baba yangu ni mkuu kuliko mimi°
Yesu anasema Mungu ni Mkuu kuliko yeye.

Soma kwa kuelewa

Yohana 14:2-10
Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendako mwaijua njia.

Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia? Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.

Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.
 
Kwani nyie hamtendi dhambi?!
Kijana kutoka suala la kumuamini yesu na kutenda dhambi yameingiaje hapa?

m nimekwambia I am a Muslim

jaribu kutafuta swali linaloendana kidogo
 
Sema wakristo wengi hatusomi biblia kikamilifu, matokeo ni kupwaya pale zinapoibuka hoja kinzani kama hizi, unakuta swali moja linaleta majibu 40, na hayajitoshelezi. Tusomeni Biblia na kuielewa vyema wakuu.
Yesu amesoma biblia au alishushiwa injili?
 
Yesu alikufa kwa sababu ya dhambi zetu, kifo chake kilithibitisha kuwa mwanadamu anaweza kudumisha ushikamanifu na Mungu.
Aisee kila mtu atabeba mzigo.wake msijidanganye kabisaaa ety kafa kwa ajili.ya dhambi zetu
Yni uue,uzini,uibe hlf useme kuna mtu kashanitubia dhambi zangu its non sense

Sasa mbona mnaenda makanisani ili msamehewe dhambi zenu? Na ubaya zaidi ety Pastor au Padri ndie anaesamehe dhambi wakati yy hpo anamichepuko kibao

kusema ukweli wakristo jitafakarini bhna mumeingizwa chaka na iyo imani yenu
 
Back
Top Bottom