Ni utapeli tu. Wanaoutetea aidha wanafaidika nao au wana upungufu mkubwa wa uelewa wa mambo ya diniKizazi cha sasa hakitaki Uongo na ulaghai.
Fikiria mchungaji anasema utoe sadaka utabarikiwa, au ukitoa sadaka unamtolea Mungu, mpaka hapo hauoni huo ni Utapeli
Zac Poonen ni mhubiri wa kweli. Namkubali sana. Hana ujinga na utapeli wa kutaka pesaNiliwahi kumwambia mchungaji wangu mmoja kuwa paulo mtume aliishi KWA kushona matenti ya matumizi mbali mbali ya majumbani wala hakutegemea SADAKA za watu,na nyie mnapaswa muwe na kazi za kufanya kujikimu!!
Akachukia na KUSEMA eti anajuta kupokea vyote nilivyowahi kumtumia eti ninamsimanga!
Nikaishia kukejeliwa sana na hapo ukawa mwisho wa mawasiliano!!
JAMBO hili nilijifunza TOKA KWA zac poonen mhindi mchungajir wa kikristo huko Bangalore india!baada ya kumsikiliza,mzee HUWA haombi SADAKA KWA wazungu wala mtu YEYOTE yule!
Nilimkubali sana!!
Biblia inasema dini iliyo safi ni kuwaangalia yatima na wajane kwenye shida zao siyo kuwapelekea matapeli pesa zakoHii ni sadaka impendezayo Mwenyezi Mungu
Mungu ni baba wa wote ila kuna matapeli siku hizi yanajifanya yapo karibu zaidi na Mungu eti tuende kwao yakatuombee mahitaji yetu kwa Mungu. Upumbavu wa kiwango cha lami huu!! Kama huwezi kuongea na baba yako ukiwa na shida unategemea ndugu yako akusaidie kuongea nae basi huna uhusiano mzuri na baba yako.Mungu wangu haitaji mtu wa tatu kuniombea
Najiombea mwenyewe na ananijibu
Huu ni ushauri wa Bwana wetu Yesu Kristo
Mathayo 6:5-6
Tena msalipo,msiwe kama wanafiki, kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia,ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, wamekwishapata thawabu yao.
Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Uhakika nilio nao ni kwamba Bwana wangu Yesu Kristo anamjua Mungu vizuri kuliko hawa wachungaji na mapadri
Kwa hiyo nafuata ushauri wa Bwana wangu Yesu Kristo maishani mwangu
Hizo zaka na sadaka zingekuwa zinafanyiwa financial control ndo ungejua watu wanavyozifuja. Utetezi wako hauna mashiko kabisaSasa ukienda kanisani au msikitini ukakuta jengo zuri, viti, meza, viyoyozi,mazuria, vyombo vya mziki na mengineyo
We hujui kuna watu waliwajibika hivo vikapatikana na wewe umefika ukaabudu kwa amani na raha.
Sasa kwanini unaona uzito kutoa sadaka ili wengine wavutiwe kumjua Mungu na kusali katika sehemu nzuri
Mungu anahitaji sadaka na zaka zetu ili injili ihubiriwe
Kuhubiri injili ni gharama
Ili watu wamjue Mungu
Naninatawajika kutoa hizo gharama ili injili iende pote duniani ikiwa sisi waumini tumejawa na kibri hivi
Acha kibri toa zaka na sadaka
Sent using Jamii Forums mobile app
Uongo na ukweli umejificha humohumo. Watu wanafuja pesa na kiasi kidogo tu kinatumika kutangaza "injili"Umenena vyema.
Ili injili iendelee kuhubiriwa ni lazima watu wajitoe.
Basi mpelekee mhitaji moja kwa moja. Zikipitia kwa hawa matapeli hazifiki zote!Mungu ana zihitaji sana hizo pesa, ili kuweza kusaidia watu waja wake wenye shida, Mungu hawezi, kushuka chini akakupa chakula, inabidi atumie rasilimali za kibinadamu kusaidia wanadamu
Sasa kwanini usisaidie watu kitaa waliokuzunguka ? Huoni huo ndio ufanisi ? Kuliko kumpa mtu ili ampe mtu ili atoe msaada ?Mungu ana zihitaji sana hizo pesa, ili kuweza kusaidia watu waja wake wenye shida, Mungu hawezi, kushuka chini akakupa chakula, inabidi atumie rasilimali za kibinadamu kusaidia wanadamu
Mungu ana zihitaji sana hizo pesa, ili kuweza kusaidia watu waja wake wenye shida, Mungu hawezi, kushuka chini akakupa chakula, inabidi atumie rasilimali za kibinadamu kusaidia wanadamu
Ukitaka upate baraka ww toa kwa wenye uhitaji hawa kenge wengine ambao sadaka zikiwa chache wanasimama madhabahuni wanasema sadaka hazitoshi achana nao ni kenge wa blue tu
Wapo wengi sana hujataka tu kufungua macho ukaona mbaliBado nafikiri ni lini nitakuja kumuona kenge wa buluu vile anavyofanana
Swali zuriKuna sehemu umesema Mchungaji au paroko anaweza kuwa Kama dalali Kati yako na Mungu.
Inawezekana vipi Mchungaji akawa karibu zaidi na Mungu kuliko ww? Kwamba ana usafi wa kimwili kukuzidi? Ama ana ushawishi Zaidi mbele ya Mungu?
Sadaka au Dhaka tunazozitoa mm huchukulia kuwa ni michango ya uendeshaji wa Sehemu tunayoabudia. Na kiasi kidogo ni kwaajili ya viongozi wa dini.
Mara nyingi sadaka yangu huitoa kwa watu Baki ninaokutana nao njiani ama niwanunulie chakula, au niwawezeshe kifedha kutokana na Hali halisi niliyoiona na namna nilivyoguswa.
upigaji wa wazi kabisa. Labda iko siku serikali zetu zitaamua kuwakomesha
Hio ni shida yake binafsi na Sio shida ya dini.Utapeli wa hizi dini umeliza watu wengi duniani. Mtu anaamini mpaka anakuwa kama taahira wa kiaina.