Mungu maana yake ni nini? Au Mungu ni nini?

Mungu maana yake ni nini? Au Mungu ni nini?

Utaelezeaje kitu ambacho hakipo?

Kama sio hadithi hadithi tu na stori uchwara uchwara kama mnavyofanya.
Nikueleze tu kwamba hakuna ambacho hakipo - kila kitu kipo ilimradi akili ipo.

Mfano huu mdogo ukusaidie kujifunza.

Kabla ya uvumbuzi ( sijui hata unajua uvumbuzi ni nini) wa kumputa au simu - kabla ya kuwa na kitu kinachoitwa kumputa au simu leo hilo, neno hilo kumputa au simu halikuwepo.

Unajua nini kitakuwepo miaka 1000 ijayo? Bila shaka jibu lako ni kwamba mimi sitakuwepo hivyo nitawezaje kujua! Basi mfano huu ukufundishe miaka 1000 iliyopita.
 
Nikueleze tu kwamba hakuna ambacho hakipo - kila kitu kipo ilimradi akili ipo.

Mfano huu mdogo ukusaidie kujifunza.

Kabla ya uvumbuzi ( sijui hata unajua uvumbuzi ni nini) wa kumputa au simu - kabla ya kuwa na kitu kinachoitwa kumputa au simu leo hilo, neno hilo kumputa au simu halikuwepo.

Unajua nini kitakuwepo miaka 1000 ijayo? Bila shaka jibu lako ni kwamba mimi sitakuwepo hivyo nitawezaje kujua! Basi mfano huu ukufundishe miaka 1000 iliyopita.
Wewe hata kuandika huwezi una bwabwaja bwabwaja tu..

Wala huelewi hata unacho andika.

Unafanya a lot of logical fallacies kuanza kutaka ziwe fact kumbe hakuna kitu.

Unaruka ruka tu.
 
Aiseeee
Mkuu.

Haiwezekani kushughulikia kitu au jambo ambalo hujui ni nini.

Katika taaluma au elimu yoyote haiwezekani kushughulikia kitu au jambo lolote, bila kujua kitu hicho au jambo hilo maana yake ni nini au ni nini - hiyo ndiyo sayansi, ndiyo logic pia.

Huwezi kuunda kwa mfano, mfumo wa mawazo au maelezo au muongozo uliopangwa ili kuelezea jambo fulani au kitu fulani kama kitu hicho kipo au hakipo; jambo hilo lipo au halipo, kitu hicho ni ukweli au sio ukweli; jambo hilo ni ukweli au sio ukweli ikiwa haujui kitu hicho au jambo hilo ni nini.

Huwezi kuthibitisha kama ni kweli Mungu yupo au hayupo ikiwa hujui Mungu ni nini. Kadhalika huwezi kuthibitisha kuna malaika au hakuna malaika kama hujui malaika maana yake ni nini.

Utaratibu ndivyo ulivyo na hivi ndivyo elimu tunayokwenda kusoma na kujifunza shuleni na vyuoni ilivyo. Sasa labda tutafute utaratibu mwingine nje ya huo wa kupima mambo.
Mkuu unamaanisha Dunia yote hii hawajui Mungu ni nini ndio maana wanashindwa kumchakata kisayansi isipokua wewe tu?

Ni wapi umewahi kuona imetengenezwa scientific theories kuhusu Mungu? Au peponi au malaika nk nk?
Hao Manguli wenyewe wa sayansi walikua na dini zao lakini walijiepusha na kuchanganya imani zao na sayansi

Mungu amefafanuliwa kinaga ubaga kwenye scriptures.
Kwa mujibu wa maandiko (Tanakh, Bible,Quran)Mungu hafananishwi wala kulinganishwa na chochote..... NI KUFURU.
Njia zake sio njia zetu wanadamu.......... Halafu wewe unataka tuanze kumtengenezea NADHARIA?
Sasa kama na wewe umekuja na Mungu wako mpya ambaye hatumjui ni nini au nani na anayeweza kuchakatwa kisayansi basi utupe hizo data zake tuzichakate..... Ila Mungu wa kwenye scriptures tajwa ameelezwa wazi kabisa ni nani na kwanini katuumba na anataka tufanye nini na hachunguziki

Theory za kisayansi hazitengenezwi from nowhere au kwa mtu kusema tu kuna kitu fulani halafu sayansi ianze kutengene nadharia based na ulichoropoka tu....... science doesn’t work that way mkuu.
Nadharia Zinatangenezwa pale physical data(accessible) zilizo kusanywa zinapokua hazitoshelezi kutoa hitimisho ndio inatengenezwa NADHARIA
Big Bang imetengenezwa baada ya ku access data zilizopo ambazo ni kila kitu kilichopo duniani na angani, zikachakatwa ikatengenezwa Bing Bang.
Nadharia ya Solar system ilianza kwa kukusanya data za sayari zingine zilizo kua accessible kwa darubini hadi ilipokuja kuwa proven..... haikuanza kwa Hadithi za alfa ulela wa ulela

Sayansi inachakata kitu ambacho ni accessible kujua ukweli wake au kutengeneza nadharia.

Sasa huyo Mungu unaanza kukusanya data gani? Unapata wapi data za kuchakata kujua malaika? Kwa kusoma Wagalatia 2? au sijui Surat inayosema ukifa unampigania Mungu utapewa mabikra 72 wa kuzagamua peponi?
 
Inawezekana, kwa upande mmoja vitabu vitakatifu na mapokeo kama msingi mkuu wa mafundisho ya dini vimeibua maswali mengi kwa baadhi ya watu kuhusu Mungu.

Na kwa upande mwingine, Ukana Mungu ambao msingi wake ni kutokuwa na uelewa wa kina wa mambo na elimu ya vitu umewavutia watu wengi katika mwelekeo huo kwa sababu ya kutokujua kama ambavyo ilivyo pia kwa wafuasi wengi wa dini.

Kile kinachoweza kuonekana kama kutoelewana - wengine wakikubali kuna Mungu na wengine wakikana hakuna Mungu, kimeendelea hata wakati ambao kuna ukuaji mkubwa wa maarifa ya sayansi na teknolojia. Na kwa kweli ni kama, kwa baadhi wasio na uelewa wa imani na sayansi, na walio na uelewa wa imani na sayansi, sayinsi imeimarisha mwelekeo wao.

Si kweli kwamba sayansi haibainishi kweli za akili, yaani kweli zilizotufikia kwa njia ya imani: mfano kuna Mungu na tokeo la uhai na ulimwengu, kwanini kuna ouvu duniani, nini hutokea baada ya kifo, nakadhalika.

Hatahivyo, pamoja na sayansi kuweka wazi mambo mengi ya imani (dini), ni dhahiri watu wengi bado hawajaelewa, na hivyo wanajiuliza:-

Je , ni kweli Mungu yupo au hayupo? Au Je, ni kweli Mungu yupo mahali pote (omnipresent)? Je, Mungu anauwezo wote (omnipotent)? Je, Mungu anajua yote, ana ujuzi wote; ana maarifa yote (omniscience)?

Na kama ni kweli! Kwa nini Mungu ambaye ni upendo, anauwezo wote, anajua yote, ana maarifa yote, ana nguvu na mamlaka yote, aumbe na aruhusu dunia ambayo inawezekana uovu kufanyika?

Kimsingi mjadala huu au maswali hayo hayawezi kuwa na maana au kujibika kama hatujui msingi wa neno Mungu, (au Hali hiyo) ambaye Ndiye mjadala wenyewe na ambaye Ndiye maswali yanaelekezwa kwake, umetokana na ni nini.

Ndugu zangu:-

Ni nini hutufanya tuseme Mungu? Yaani ni nini tunakirejelea tunapoita Mungu? Neno Mungu au wazo Mungu; au wazo kuna Mungu tumelitoa wapi? Sababu gani zimetusababisha kusema kuna Mungu; au wazo Mungu limesababishwa na nini?

Aidha, wazo hakuna Mungu limetoka wapi na limetokana na sababu gani? Na linapendekeza au linaelezea nini vitu vilivyopo?

Lakini pia, hii elimu tunayokwenda kusoma shuleni na vyuoni: kufundishwa na kusoma, (fizikia, hisabati, bailojia, kemia, jogorafia, sheria, uraia, historia, lugha, uhandisi, taalimungu (theology), elimu ya mtima (psychology), nakadhalika), imetoka wapi? Nani aliileta? Nani aliipangilia na kuiweka katika utaratibu huo? Kwa nini?

Kwa sababu kama ikiwa kila binadamu anapelekwa shule na chuo kujifunza na kusoma, maana yake hayo masomo tunayo kwenda kusoma au hiyo elimu tunayofundishwa shuleni na vyuoni hatukuwa tunaijua au tunaifahamu. Na hii maana yake ni kwamba kuna mtu aliyeijua hiyo elimu ambayo sisi tunakwenda kusoma na kufundishwa.

Sasa basi, huyo mtu aliipata wapi hiyo elimu au hayo masomo tunayofundishwa shuleni na vyuoni yalitoka wapi?

Na je, ni kweli kwamba hiyo ndio elimu (yaani hayo masomo) na kwamba hakuna kitu kingine bora zaidi au utaratibu mwingine wa kupima na kuelewa ulimwengu, ila isipokuwa kwa masomo au elimu hiyo tu?

Unauelezeaje ulimwengu: vitu vyote vilivyopo

Kadiri ya ufahamu wako na kadiri ya unavyoona na unavyoelewa, unaona vitu vilivyopo (ulimwengu ) vimefanyika kwa akili au havijafanyika kwa akili? Na je, unagundua hilo kwa jinsi gani? Je, ni baada ya kufundishwa au ni kabla? Au hugundui hivyo, badala yake unagundua nini?

Na hali hiyo ya vitu vya asili kuwa au kufanyika hivyo vilivyofanyika, inaashiria nini au unaieleza kuwa ni hali gani: yenye ufahamu au haina ufahamu?

Kwa binadamu, vitu vyote vilivyopo angalau vitu vyote anavyoweza kuviona akiwemo na mtu mwenyewe, anaona kuwa vitu hivyo au viumbe hivyo kuanzia na miundo yao ya nje na ya ndani, mpangilio wao, na jinsi yao ya utendaji kazi; ama ni kiungo kimoja kimoja katika kitu au kiumbe kimoja; au ni vitu mbalimbali, vinaonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.

Kwa lugha rahisi, binadamu anaona ulimwengu kuwa umefanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana. Hali hiyo ya mtu ya kufikiri au ya kuona kuwa ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na akijiangalia na yeye mwenyewe - asijuwe ni hali gani hiyo imesababisha vitu sio tu kuwa kwa akili lakini na kwa jinsi gani, anajitiisha na kutambua hali hiyo kwa kuiita "Mungu".

Tunapojiuliza kuna Mungu au hakuna Mungu, tunapaswa kimsingi kufahamu kuwa neno hilo (Mungu) tunaita uwepo wa hali ya akili ambao hauonekani lakini tumeufahamu au tumeujua kwa jinsi tunavyoona vitu vyote vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.

Hivyo basi, "Mungu", ni nini? Au Mungu maana yake ni nini? Mungu maana yake ni, Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili. Kumbe, tunaposema Mungu au tunaposema kuna Mungu, ni Neno tunaloita "Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili". Na maana hii inatokana na jinsi tunavyoona na kustaajabia vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.

Tunasikia mara zote watu wakizungumza juu ya akili na kuhusu akili. Kwa hakika watu huzungumza kuhusu akili wakielezea mpangilio na miundo na ufanyaji kazi wa vitu na upatano wao jinsi ulivyo na unavyoeleweka, mkamilifu na wenye matokeo chanya.

Na tunasema akili kuelezea uwezo wa hali ya juu wa kujua, wa kufahamu, wa kuelewa, wa ujuzi, wa maarifa na wa kufanya vitu, yaani kutatua matatizo na kufanya mageuzo yenye maendeleo. Lakini hatahivyo akili ni nini? Je, akili ipo wapi? Je, akili inaonekana?

Akili ni kipawa kinachomwezesha mtu kufikiri kujifunza, kuwasiliana kuamua na kutatua matatizo. Kwa maneno mengine, akili ni ufahamu. Kwa kuchukua wanyama na hata mimea kama viumbe wenye ufahamu tunaweza kuelewa akili ya wanyama na mimea, akili ya binadamu, na tunaposema Mungu - Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili.

Kimsingi wanyama wote wana ubongo ambamo mna ufahamu yaani akili. Lakini hatahivyo, wote tunakubali kwamba ubongo wa binadamu una akili kuliko ubongo wa wanyama wengine.

Kwa hiyo hatuwezi kuhitimisha kuwa akili ni shughuli au kazi za ubongo kwa sababu ubongo wa wanyama wengine nao vile vile unafanya shughuli za ufahamu. Lakini hatahivyo, wanyama wameendelea kubaki katika mstali wa ulalo (horizontal) wanadamu wako katika msatali wa wima (vertical).

Na kwa kweli binadamu pia anaweza kutokuwa na akili. Akabaki tu na ufahamu wa kawaida kama wanyama. Akawa tu kama wanyama anatekeleza kile mwili unamuasilishia kupitia milango yake mitano ya fahamu.

Kimsingi, akili ni ile hali ya kuwa na ufahamu wa kina wa mambo jinsi yalivyo na elimu ya vitu, yaani maarifa kamilifu au ushahidi wao wa ndani, na hivyo akili ni tofauti na ufahamu unaotokana na unaotegemea mwili, yaani milango mitano ya fahamu, ambao huo hautupatii maarifa kamilifu ya kitu au vitu, ya jambo au mambo jinsi yalivyo na yanavyotakiwa kuwa. Lakini hatahivyo, kama bado tungali hapa duniani tunahitaji mwili (hali safi ya ndani na ya mwili), ili kuunganika na Mungu, yaani Uwepo wa Hali ya Juu Wenye.

Unaweza kujiuliza au kufikiri ni nini kinakufanya uone au usema kitu hiki au jambo hili au hali fulani ni ya kiakili au imefanyika kwa akili; au jambo hili haliingii akilini? Unaposema kwa mfano, kitu hiki au jambo hili haliingii akilini unakuwa unajaribu kueleza nini?

Pengine wewe mwenyewe unaweza usijue jinsi mwili wako ulivyofanyika na unavyofanya kazi, labda ni vigumu sana. Lakini fikiria kwa mfano, kama umewahi kuona mitambo mbalimbali iwe ni ya viwandani au hospitalini ilivyotengenezwa na inavyofanya kazi, ni hali gani hiyo, na unaweza kuielezeaje?

Iwe ni mashine rahisi mpaka tata. Vivyo hivyo kuanzia na viumbe vidogo kabisa mpaka vikubwa kabisa vinaeleza hali ambayo mtu anaona na anaiita akili. Ingawa hakuna aliyeona akili ila ubongo ambao ni mahali pa ufahamu lakini hatahivyo, tunakubali kuwa vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu.

Kwa hiyo kama hivi ndivyo binadamu anaona ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na vimefanyika kwa akili, na sayansi haikatai hilo la vitu vya asili kuonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu isipokuwa inatafuta hali hiyo, na kwa jinsi gani.

Basi wazo kwamba kuna Mungu (idea that there is God is absolutely true), ni la kweli na hakika kwa sababu ambazo ni wazi na bayana. Kwanza vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu. Na Pili mtu alivyo bora angalau katika viumbe wanaoonekana. Ubora huo ndio unaoelezwa katika biblia ikimtaja mtu kuwa "amefanyika kwa mfano na sura ya Mungu."

"Mfano na sura ya Mungu", mwandishi wa simulizi hilo la kweli za akili anamaanisha kuwa mtu amefanyizwa kwa mwili na roho - anayo hali ya akili hivi kwamba anaweza kuunganika na Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili, yaani Mungu.

Dini inafundisha kuwa Mungu ndiye amesababisha uhai na ulimwengu kuwepo na kwamba Yeye ndiye tokeo la uhai na ulimwengu na ulimwengu unatawaliwa na uwepo Wake. Sayinsi inasema mianzo ya vitu vilivyopo: ulimwengu, umesababisha na mlipuko mkubwa uliotokea zamani. Nadharia hii ambayo ni msingi mkuu wa nadharia zote za sayansi na ambayo inakubalika na wanasayansi wengi jinsi vitu vilivyotokea inafundisha kuwa vitu vilitokana na nishati au nguvu (energy).

Kwa sababu sayansi inashughulikia jinsi vitu vilivyopo vilitokea, katika muktadha huo imetusaidia sio tu kuelewa ulimwengu, lakini pia kumjua Mungu. Na hivyo kwa sababu inashughulika na vitu vinavyoonekana na vinavyoweza kupimika, sayansi haitufundishi kwamba nishati hiyo ambayo imesababisha vitu kutokea ni kama nishati tunayoitumia kwa mitambo au inayopatikana kwa vyakula, jua nakadhalika. Lakini (Sayansi) inatufundisha kwamba nishati hiyo ni zaidi ya hali tunayoweza kuielezea kama mlipuko au kama nishati inayoupa mwili nguvu, au inayowezesha mitambo kufanya kazi au jua kustawisha na kuwezesha uhai wa viumbe duniani, ni Nishati Yenye Ufahamu wa Hali ya Juu wa Akili.

Kitabu cha Mwanzo kinasema kuwa Mungu aliumba ulimwengu pasipo kutumia kitu chochote. Simulizi hilo linachoeleza ni kuwa ulimwengu uliumbwa au ulifanyizwa kwa kutumia akili. Na hii ni sayansi iliyowazi kwamba vitu vyote vilivyopo vinaonekana na vimefanyika kwa akili.

Kwa jinsi ufahamu wetu ulivyo na unavyotokana na kujifunza au kusoma au kufuatilia vitu vilivyopo kwa karibu yaani maarifa yetu yanayotuwezesha kuelewa na hatimaye kupima ulimwengu, haiwezekani kukataa au hata kukana kwamba ulimwengu yaani vitu vyote vilivyopo havionekani kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.

Labda kama kutakuja utaratibu mwingine, yaani elimu au ufahamu au uelewa mwingine, ambao utaeleza kwa namna nyingine isiyo hii tunayoiona au tulionao kwamba, ulimwengu kuonekana na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu, unaashiria Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili tunaouita Mungu.
Mungu ni roho kamili na ukamilifu wake hauna mipaka
 
Mkuu. Sio nia yangu kumshawishi yeyote. Lakini kama wanyama wenye busara, umakini unapaswa kuzingatia akili kutuongoza sio tu kuelewa ulimwengu, bali kwa jinsi gani tunafikia hatua hiyo.

Pamoja na kwamba mtu ana wajibika kwa mambo mbalimbali, nyajibu hizo ni pia kujifunza. Kama mtu unataka kuwa salama; unataka kuendelea, unalazimika kufuatilia kwa karibu vitu mbalimbali - elimu ya vitu mbalimbali, kujifunza.

Watu huenda shule na vyuo kujifunza. Watu hufanya tafiti na utafiti wa kisayansi kujifunza. Kujifunza ni kutafuta ukweli au kujua ukweli - jinsi vitu au mambo yalivyo na jinsi gani ya kutenda au kufanya mambo au vitu.

Kabla ya kusema sayansi inafanyaje kazi zake na kazi hizo lengo lake ni nini; kwa sababu si kweli kwamba sayansi inajishughulisha tu na vitu vinavyoonekana na vinavyoweza kupimika, bila ya lengo lolote, ni vema tukajua kwanza sayansi maana yake ni nini kabla ya kuangalia msingi wake mkuu, nadharia.

Sayansi ni maarifa yanayopatikana kwa kufanya vitendo, kutazama na kujaribu kweli mbalimbali zilizobainishwa hazijathibitishwa. Kuna misamiati msingi katika maana hiyo ya sayansi. Nayo ni hii hapa chini:-

Moja, sayansi ni maarifa - hili ni muhimu sana kujua kwa sababu hili la maarifa ndiyo linatengeneza msingi mkuu wa sayansi, Nadharia (Theory). Kwa hiyo ni muhimu sana kujua maarifa maana yake ni nini. Kwa sababu kwa kujua maarifa ni nini unaweza kuelewa msingi wa sayansi, nadharia.

Mbili ni "kweli zilizobainishwa hazijathibitishwa" . Hii inamaanisha kwamba sayansi inashughulika na kuthibitisha kweli zilizobainishwa hazijathibitishwa, kwa kufanya vitendo, kwa kutazama, na kwa kufanya majaribio.

Lakini hatahivyo, kweli zilizobainishwa ni nini au maana yake ni nini hadi sayansi idhithibitishe?

Kweli zilizobainishwa maana yake ni ulimwengu wote - mwanzo wake na mwisho wake. Yaani vitu vinatoka wapi, vinaenda wapi? Mtu anatoka wapi, anaenda wapi? Mtu anatakiwa aishije - jinsi gani ya kutenda katika maisha? Ouvu ni nini? Kwa nini duniani kuna ouvu? Unatoka wapi? Wema ni nini? Na kwa nini wema na si ouvu? Kifo ni nini? Nini huendelea baada ya kifo?

Kwa lugha rahisi, sayansi inafanya kazi ya kuthibitisha kama mambo hayo (kweli zilizobainishwa hazijathibitishwa), ni kweli au si kweli, yapo au hayapo.

Sasa, kwa jinsi gani tunathibitisha jambo hili au jambo fulani ni ukweli au sio ukweli, lipo au halipo. Kwa maneno mengine, tunaelezaje katika utaratibu unaoeleweka (kiakili) wenye mpangilio ulionyooka (kimantiki) na kupimika (kuonekana) kuwa jambo hili au jambo fulani lipo au halipo, ni ukweli au sio ukweli. Hii ndio huitwa nadharia - msingi mkuu wa sayansi.

Na kama nilivyoandika kwamba nadharia maana yake ni ujuzi wa kuunda mfumo wa mawazo au wa maelezo; au muongozo uliopangwa ili kuelezea ukweli wa jambo fulani.

Jambo muhimu katika maana hiyo ya nadharia ni, ujuzi kama ilivyo sayansi ni, maarifa (Fuatilia maarifa na ujuzi).

Jambo moja muhimu kuhusu sayansi. Sayansi ni kama mwili - una viungo mbalimbali. Maana yake sayansi imegawanyika katika elimu (matawi) mbalimbali (Natural sciences, social sciences, formal sciences)na kila elimu (tawi) nayo limegawanyika katika elimu (aina) mbalimbali. Hizo zote ni sayansi -sawa ulivyo mwili mmoja viungo mbalimbali, inaelezea upi ni ukweli na upi sio ukweli kuhusu ulimwengu, ukweli ambao tuko nao (bayana), ila bado hatujui waziwazi.
Mkuu nikuulize swali
Hivi wewe Huyu “Mungu” umemjulia wapi hadi “ukajua” yupo?
Reference gani zilitumika ili kupata “kumjua” Mungu?
 
Sasa hata kama wewe hujijui ni binadamu, sidhani uthibitisho upi utakufaa ujue kwamba wewe ni binadamu.

Ukitaka uthibitisho, look at yourself.

Ukijiona wewe ni roboti basi wahi kituo cha afya.
Soma nlichondika, Then angalia majibu yako


Nadhani unajishangaa hata wewe mwenyewe, Wewe umeshindwa kuthibitisha kama wewe ni Binadamu ila unataka mimi nkuthibitishie kuhusu Mungu hahaha
 
Soma nlichondika, Then angalia majibu yako


Nadhani unajishangaa hata wewe mwenyewe, Wewe umeshindwa kuthibitisha kama wewe ni Binadamu ila unataka mimi nkuthibitishie kuhusu Mungu hahaha
Mkuu umeanza kwa kumuuliza anataka ushahidi gani kuwa kuna Mungu ili umthibitishie.
Na ukataka akuthibitishie kama yeye ni binadamu.
Akikwambia aje sehemu ulipo mkutane na ujiridhishe kuwa ni binadamu Je wewe utaweza kuthibitisha kama Mungu yupo?
Utaweza kumpeleka kwa Mungu akamuome kama ulivyo muona yeye?

Mnaulizaga maswali ya kitoto sana badala ya kutoa uthibitisho tu
 
Mkuu nikuulize swali
Hivi wewe Huyu “Mungu” umemjulia wapi hadi “ukajua” yupo?
Reference gani zilitumika ili kupata “kumjua” Mungu?
Mkuu.

Swali lako linanirudisha wakati wa umri wangu wa kuanza kutumia akili. Wakati ule nilipoanza kufikiri, kujifunza, kuwasiliana na kutafuta maana ya vitu mbalimbali. Ukiacha vitu vingine vyote vilivyopo, ukiacha na ufanyaji kazi wao na jinsi yao, mtu pia ni kitu kilichonistajaabisha na bado ananistaajabisha sana.

Hivi ndivyo nilivyojua kuna Mungu - jina tunaloita Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili.

Swali langu daima lilikuwa: Je! Vitu hivi yaani ulimwengu upo tu, bila kusababishwa na hali fulani au nguvu fulani? Yaani ulimwengu ndio wenyewe vitu na ndiyo wenyewe nguvu au hali iliyosababisha ulimwengu au vitu vyote vilivyopo kutokea na kuwepo na kuendelea kuwepo?

Na kama ulimwengu upo tu, yaani hauna mwanzo wala mwisho; haujasababishwa na nguvu yoyote au hali yoyote kutokea au kuwepo-wenyewe ndio hiyo hali au ndiyo hiyo nguvu ya kutokea, kuwepo na kuendelea kwake: moja, hii hali ya viumbe kuwa tofauti, kwa mfano mtu na viumbe wengine inaashiria nini au inaelezea nini?

Mbili, ikiwa kama ulimwengu wenyewe upo tu hauna chanzo wala mwisho, haujasababishwa na nguvu yoyote au hali yoyote - wenyewe ndio hiyo nguvu au ndiyo hiyo hali ya kutokea, kuwepo na kuendelea kwake, kwa nini vitu au viumbe vingine vinatoweka kabisa?

Hivyo nimejua kwamba ulimwengu yaani vitu vyote vilivyopo as material things hauna mamlaka dhidi yake kama ulimwengu. Yaani kwa mfano, mwili kama mwili asa material things hauwezi kufanya au kutengeneza kitu. The mental processes that is the power of mind can create things.

Kwa kurejelea ulimwengu kama vitu vyote vilivyopo. Iwe ni kama baadhi ya wanafalsafa waliosema ulimwengu ndio Mungu Mwenyewe au vyovyote vile watu wanavyoelewa na kufafanua ulimwengu, haimanishi chochote isipokuwa Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Utambuzi yaani Akili.
 
Mkuu.

Swali lako linanirudisha wakati wa umri wangu wa kuanza kutumia akili. Wakati ule nilipoanza kufikiri, kujifunza, kuwasiliana na kutafuta maana ya vitu mbalimbali. Ukiacha vitu vingine vyote vilivyopo, ukiacha na ufanyaji kazi wao na jinsi yao, mtu pia ni kitu kilichonistajaabisha na bado ananistaajabisha sana.

Hivi ndivyo nilivyojua kuna Mungu - jina tunaloita Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili.

Swali langu daima lilikuwa: Je! Vitu hivi yaani ulimwengu upo tu, bila kusababishwa na hali fulani au nguvu fulani? Yaani ulimwengu ndio wenyewe vitu na ndiyo wenyewe nguvu au hali iliyosababisha ulimwengu au vitu vyote vilivyopo kutokea na kuwepo na kuendelea kuwepo?

Na kama ulimwengu upo tu, yaani hauna mwanzo wala mwisho; haujasababishwa na nguvu yoyote au hali yoyote kutokea au kuwepo-wenyewe ndio hiyo hali au ndiyo hiyo nguvu ya kutokea, kuwepo na kuendelea kwake: moja, hii hali ya viumbe kuwa tofauti, kwa mfano mtu na viumbe wengine inaashiria nini au inaelezea nini?

Mbili, ikiwa kama ulimwengu wenyewe upo tu hauna chanzo wala mwisho, haujasababishwa na nguvu yoyote au hali yoyote - wenyewe ndio hiyo nguvu au ndiyo hiyo hali ya kutokea, kuwepo na kuendelea kwake, kwa nini vitu au viumbe vingine vinatoweka kabisa?

Hivyo nimejua kwamba ulimwengu yaani vitu vyote vilivyopo as material things hauna mamlaka dhidi yake kama ulimwengu. Yaani kwa mfano, mwili kama mwili asa material things hauwezi kufanya au kutengeneza kitu. The mental processes that is the power of mind can create things.

Kwa kurejelea ulimwengu kama vitu vyote vilivyopo. Iwe ni kama baadhi ya wanafalsafa waliosema ulimwengu ndio Mungu Mwenyewe au vyovyote vile watu wanavyoelewa na kufafanua ulimwengu, haimanishi chochote isipokuwa Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Utambuzi yaani Akili.
Huo "uwepo wa hali ya juu wenye utambuzi yaani Akili" ulikujaje au ulitokeaje?

Au ulitokea tu from no where?
 
Theory za kisayansi hazitengenezwi from nowhere au kwa mtu kusema tu kuna kitu fulani halafu sayansi ianze kutengene nadharia based na ulichoropoka tu....... science doesn’t work that way mkuu.
Nadharia Zinatangenezwa pale physical data(accessible) zilizo kusanywa zinapokua hazitoshelezi kutoa hitimisho ndio inatengenezwa NADHARIA
Big Bang imetengenezwa baada ya ku access data zilizopo ambazo ni kila kitu kilichopo duniani na angani, zikachakatwa ikatengenezwa Bing Bang.
Nadharia ya Solar system ilianza kwa kukusanya data za sayari zingine zilizo kua accessible kwa darubini hadi ilipokuja kuwa proven..... haikuanza kwa Hadithi za alfa ulela wa ulela
Nadharia ya mlipuko mkubwa (big bang theory) ni mawazo (kama ulivyosema physical data) zinazoelezea tokeo la ulimwengu: vitu vyote vilivyopo vilitokeaje. Physical data za nadharia ya big bang zinaeleza vitu vilivyopo vilivyotokea

Nadharia ya big bang inasema ulimwengu ulitokea kwa sababu ya mlipuko mkubwa. Kwa maneno mengine, nadharia ya big bang anasema mlipuko mkubwa (nishati - energy) ndio ulioumba ulimwengu. Na Dini inasema Mungu Ndiye aliyeumba ulimwengu. Sasa, ni nini usichoelewa hapo? Kama sio sayansi?
 
Mungu amefafanuliwa kinaga ubaga kwenye scriptures.
Kwa mujibu wa maandiko (Tanakh, Bible,Quran)Mungu hafananishwi wala kulinganishwa na chochote..... NI KUFURU.
Njia zake sio njia zetu wanadamu.......... Halafu wewe unataka tuanze kumtengenezea NADHARIA?
Sasa kama na wewe umekuja na Mungu wako mpya ambaye hatumjui ni nini au nani na anayeweza kuchakatwa kisayansi basi utupe hizo data zake tuzichakate..... Ila Mungu wa kwenye scriptures tajwa ameelezwa wazi kabisa ni nani na kwanini katuumba na anataka tufanye nini na hachunguziki
Maandiko matakatifu yanahusu maadili - jinsi gani ya kutenda. Ndiyo jinsi gani ya kuishi: nini unatakiwa kufanya na nini hutakiwi kufanya na kuwafanyia wengine. They're all about natural law or moral law.
 
Wewe hata kuandika huwezi una bwabwaja bwabwaja tu..

Wala huelewi hata unacho andika.

Unafanya a lot of logical fallacies kuanza kutaka ziwe fact kumbe hakuna kitu.

Unaruka ruka tu.
Kwa sababu wewe uwezo wako wa kuchakata taarifa na kung'amua mambo ni hafifu.

Wewe ni mnyama ambaye unatawaliwa na mwili si busara.
 
Kwa sababu wewe uwezo wako wa kuchakata taarifa na kung'amua mambo ni hafifu.

Wewe ni mnyama ambaye unatawaliwa na mwili si busara.
Umeishiwa hoja unaanza Viroja.

Umebaki kutapatapa..

Bure kabisa.
 
Umeishiwa hoja unaanza Viroja.

Umebaki kutapatapa..

Bure kabisa.
Uko sahihi kusema viroja kwa sababu uwezo wako wa kuchakata taarifa, kuona uwezekano na kutafisiri ni hafifu sana hivi kwamba nakuweka kundi moja na mnyama asiye na busara.

Ovyo kabisa.
 
Mkuu umeanza kwa kumuuliza anataka ushahidi gani kuwa kuna Mungu ili umthibitishie.
Na ukataka akuthibitishie kama yeye ni binadamu.
Akikwambia aje sehemu ulipo mkutane na ujiridhishe kuwa ni binadamu Je wewe utaweza kuthibitisha kama Mungu yupo?
Utaweza kumpeleka kwa Mungu akamuome kama ulivyo muona yeye?

Mnaulizaga maswali ya kitoto sana badala ya kutoa uthibitisho tu
Umeniuliza vizuri kuwa akija akanithibitishia yeye ni binadamu je nitaweza kumthibitishia kuhusu Mungu ? Lakini kabla hujasubiri jibu langu umemaliza kwa kuita ni swali la kitoto,,

Lakini vile vile haujafahamu mantiki ya mimi kutaka uthibitisho kuhusu yeye, Huoni kama wewe ndio unaleta utoto ?
 
Mi kwa mtizamo wangu. Huyu Mungu tunaemzungumzia atakuwa kaumba viumbe vingi sana na madunia mengi sana. Sasa kila dunia kaiwekea viumbe vyake tofauti tofauti na kanuni za asili zinazoviongoza hivyo viumbe.
Mfano wanyama kila mnyama unaemuona anaongea na mwenzie wa jamii yke kabisa wanautaratibu wa asili unaoongoza dunia yao. Na vile tunavyoona labda paka hana akili sio kweli wana akili zinazoishia kwenye levo yao. Sisi binadamu pia tunajiona tuna ufahamu sio kweli ni ufahamu unoishia levo yetu. Sasa sisi juu yetu utakuta tena Kuna malaika. wanatuona tunamapungufu na tu wadhaifu na levo yao iko juu kuliko sisi. Na ndio maana unakuta ukisoma Biblia unakuta kuna mahali Mungu anamtuma kunguru ampelekee Eliya chakula. Sasa utajiuliza tangu lin kunguru akatumwa. Ni kwamba Mungu kila kiumbe kakiwekea kinafuata kanuni ile ile ya asili bila kuingiliana japo yeye vinamjua japo kwa kuhisi na vikitumwa vinajua mamlaka ya Mungu na kutii. Ukimsikiliza Yesu anasema amepewa mamlaka juu ya wote wenye mwili yaan ishu ya kwenda Mbinguni kwa wnadam Yesu kaachiwa. Kingine viumbe vyote vya Mungu vinamjua kwa asilimia 00000.01. na tena utamjua tu kwa yeye kukufunulia katika ile levo anayotaka yeye. Tena ukisoma Biblia utagundua badhi ya siri nzito kwamb kuna wenye uhai wanne wamekizunguka kiti kikuu Mbinguni na biblia haijatuambia ni viumbe gan hivyo. So kma alivyosema mleta muda ishu ya Mungu ni kubwa mno kiasi kwamba uwezo wa mwanadam kuelewa ni mdogo sana. Bado hujaweka ule mstar Yesu aliosema nina kwenda kwa Baba kuwaandalia makao. It means kuna madunia kibao bdo unaendelea kujengwa. Hayo ni machache kuhusu ufahamu wangu. Ila kuhusu Mwenyezi Mungu ni kweli yupo. Ni kma vile giza na mwanga au mema na mabaya. So dunia imeumbwa kuwili hasi na chnya so kama unawez kuwaza au kutenda mema basi unaweza kufanya hivyo vibaya pia so huo ubaba wa huo ubaya ni shetan na ubaba wa huo wema ni Mungu. Asanten
 
Back
Top Bottom