Myebusi Mweusi
JF-Expert Member
- Jan 23, 2022
- 671
- 1,543
Dini ni chombo cha kufubaza akili
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Issue sio kwenda kanisani au msikitini bali tunajua uwepo wa Mungu kupitia watu kwa bila kujali watu hao wa dini au sio wanadini.Mungu hata usipoenda kanisani au msikitini utajua tu yupo...Mungu anaongea na sisi muda wote..ni vile tunsjitoa ufahamu...Ndo maana huhitaji mtu akuambie hiki ni kibaya, kuna sauti ndani iko wazi sana...
Hata babu zetu kabla ya ukristu au uislam walijua kuna nguvu ipo ndo maana wakawa wanaenda kutambika kwenye miti, mapango, wanaomba mvua n.k
Mkuu kuna akili na elimu/maarifa.Dini ni chombo cha kufubaza akili
Mungu ni asili, yeye ndiyo chanzo cha vyote vinavyoonekana na visivyo onekana.
Ili Mungu akure maarifa, hana haja ya kukuandikia kiatabu.
Jiulize maarifa makubwa waliyonayo wanyama mbalimbali, wameyasoma kwenye kitabu gani kitakatifu?
Mungu yupo, hasomi, haandiki, wala hana dini. Dini ni mpango wa mwanadamu. Dini imejaa vitisho, Mungu hana haja ya kumtisha mtu.
Dini zimeenezwa kwa kufanya mauaji makubwa. Mungu wetu anachukia mauaji.
Dini ni mpango halisi wa shetani, kuwadanganya watu, wajione wanamfuata Mungu kumbe wako maili nyingi sana na mpango wa Mungu kwa mwanadamu.
Kama dini haiwezi kukupeleka Kariakoo, itawezaje kukupelela mbinguni?
Ukiweza kumpenda jirani yako kama nafsi yako mwenyewe wewe utakuwa bora kuliko mtu anayesali kuanzia asubuhi hadi usiku wa manane.
Upendo ndio kusudi la mwanadamu kuwepo duniani. Tukipendana kwa dhati, dunia ndio Paradiso yenyewe
Dini ni elimu haramuMkuu kuna akili na elimu/maarifa.
Naona umeishia njianiKaka..., au basi!
MUmeona
Mie nilimuona jamaa mmoja kutoka DRC alikuwa anaitwa MUNGU WA UBEMBE alijitangaza kwenye tv na sikuona aliyebisha mi nkajua labda ndo yeyeJe wewe unaweza kuthibisha uwepo wa Mungu?
Kwani mafunzo ya dini hutoka wapi?Dini ni elimu haramu
Critical thinkingHivi ulisha wahi kujiuliza viumbe vilivyomo mwilini mwako huwa vinakutambua ww km nani??.Unaweza kuta navyo vinakuita Mungu ama vinakutambua kama muumbaji maana km vikisikia kiu,njaa,kulala,kutoa uchafu,kustarehe ww lazima huku nje upate shida,mfano ni lazima ule ulale unywe maji ili tu viumbe walioko ndani yako wapate mahitaji yao waishi.Ww mtu ukiacha kufanya hivyo viumbe walioko ndabi yako wanaanza kufa na ww pia mtu lazima ufe tunaishi kwa kutegemeana.
Jambo fikirishi..na sisi inaweza tukawa tunaishi ndani ya kiumbe kikubwa ndo maana na sisi hiki kiumbe dunia kisipo tupa mazao ama mvua ama hewa safi kwa wakati lazima sisi viumbe ndani yake tunakufa.
Wazo langu mm ni kwamba inawezeka Mungu ..ama huyo mwenye vyote yuko nje ya uishi wetu sisi viumbe wadogo na hana mda kabisa na sisi km sisi tusivo na mda na viumbe wa mwilini mwetu.maana hakuna anaejua kua vinasali sala tano ama jumapili.Chanzo cha vyote anacho jali ni kwamba tupo kuendeleza uwepo wetu..Inawezekana pia kuna viumbe wakubwa zaidi yetu hao sasa ndo hua wanamuomba huyo Mwenye vyote.
Mungu anajulikana kabla hizi dini za kutoka mashariki ya kati hazijatufikia. Kila jamii na kabila walikuwa na Mungu wao. Bahati mbaya hawa wanakuja walipokuja wakawadanganya mababu na mabibi zetu kwamba wao wanaabudu na kuamini mizimuNaona swali la msingi unalikwepa kila ukijaribu kuulizwa.
Swali:
Mungu na Concept mzima ya Mungu imeletwa na kuelezewa na hizo Dini na sisi wote tumejua kuna Mungu kupitia hizo Dini, kwa kifupi God issues is religious things, sasa wewe hapa unasema unaamini kuna Mungu ila huamini Dini hizo zilizokuletea Cocept ya huyo Mungu mbona kama haingii akilini.
Muelezee huyo mungu anayemuamini wewe ambae si wadini yeyote, umemjulia wapi, ameamrisha nini, kupitia nini umepata hayo maamrisho au miongozo yake na nini ESSENCES ya hio miongozo wa huyo mungu unayemuamini wewe....na inakuwaje huyo mungu awe na miongozo fulani bila kuwa na mfumo unayesimamia hio miongozo ambapo pale juu mfumo huo unaitwa Dini.
nadhani ungeeleza mambo haya kwa kina tukuelewe.
Wanadai kwamba alifunuliwa kujajua mambo yalitotukia kabla yeye hajazaliwaNAJIULIZA KITU KIMOJA HIVI ALIYEANDIKA KWAMBA HAPO MWANZO MUNGU ALIWAUMBA ADAM NA HAWA YEYE ALIJUAJE NA KIPINDI HAO ADAM NA HAWA WANAUMBWA YEYE ALIKUWA WAPI NA ALIUMBWA NA NANI.
Hoja yako inamaanisha kwamba kila kilichopo kimetengenezwa na kilichokuwepo kabla. Ndio maana unasema Mungu yupo kwasababu dunia haiwezi kujitengeneza yenyewe. Je, huyo Mungu ilikuwaje akatokea? Alitoka wapi na lini? Je huyo Mungu alitokea mwenyewe bila kuwa na chanzo?Mungu yupo maana Dunia haiwezi kujitengeneza yenyewe na viumbe vyake na kila kiumbe kina sababu yake...
Ila uwepo wa Mungu yapo Mataifa makubwa na baadhi ya watu wanafanya fursa ndio maana wengine wanabaki kutokuamini...
Utapeli mtupuWanadai kwamba alifunuliwa kujajua mambo yalitotukia kabla yeye hajazaliwa
Labda nikuulize huyo Mungu wewe ulimjua tu mwenyewe uwepo wake( kama ulivyojua kunyonya titi la mama) au uwepo wa anayeitwa Mungu ulijua kupitia watu?
Mkuuu Kama nakuelewa hiiv
Nikiunganisha na Lesson ya kitabu Cha Rhonda Byrne "THE POWER"
Sent using Jamii Forums mobile app
Binafsi sitoweza kufanya hivyo,Je wewe unaweza kuthibisha uwepo wa Mungu?
Umejuaje?🙂…Mungu yupo, hasomi, haandiki, wala hana dini….
Freedom of speech.Anyway kuna kitu hujakifahamu bado about human nature to his/her Creature.Ukiwa mkubwa utaelewa.Mungu ni asili, yeye ndiyo chanzo cha vyote vinavyoonekana na visivyo onekana.
Ili Mungu akure maarifa, hana haja ya kukuandikia kiatabu.
Jiulize maarifa makubwa waliyonayo wanyama mbalimbali, wameyasoma kwenye kitabu gani kitakatifu?
Mungu yupo, hasomi, haandiki, wala hana dini. Dini ni mpango wa mwanadamu. Dini imejaa vitisho, Mungu hana haja ya kumtisha mtu.
Dini zimeenezwa kwa kufanya mauaji makubwa. Mungu wetu anachukia mauaji.
Dini ni mpango halisi wa shetani, kuwadanganya watu, wajione wanamfuata Mungu kumbe wako maili nyingi sana na mpango wa Mungu kwa mwanadamu.
Kama dini haiwezi kukupeleka Kariakoo, itawezaje kukupelela mbinguni?
Ukiweza kumpenda jirani yako kama nafsi yako mwenyewe wewe utakuwa bora kuliko mtu anayesali kuanzia asubuhi hadi usiku wa manane.
Upendo ndio kusudi la mwanadamu kuwepo duniani. Tukipendana kwa dhati, dunia ndio Paradiso yenyewe.