Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Umenikumbusha jambo moja kuu kuhusu waamini katika Mungu wa mbingu na nchi ambao wanaomwamini hupitia jina lake la utambulisho la wakati yaani Yesu Kristo hata wakaitwa wakristo kwa maana ya ufuasi wao kwa Kristo. Miongoni mwao ni hao walipachikwa jina walokole au wa kulialia.
Jambo lenyewe ni hili kuna siri kuu katika mambo ya ulimwengu wa roho ambayo wanajimu, waganga na wachawi wanayafahamu kumhusu Mungu mara mia elfu zaidi ya wakristo. Hata hivyo kwa kuyafahamu hakuwafanyi kujisalimisha maisha yao kwake kwa sababu ya maslahi binafsi.
Adamu kabla ya kuwekwa katika mwili ule wa udongo kwa kazi ya kuilima nchi na kuitiisha, aliishi ulimwengu zote mbili yaani wa kiroho na kimwili hata alipoanguka na kupoteza haki ya umiliki.
Maana yake kumbe uwezo wa kumiliki ya kiroho na kimwili haitoshi tu kuwa sababu pekee ya ushindi dhidi ya kumuasi Mungu.
Mama jusi ambao ni wanajimu ndio walioiona na kuitambua nyota ya Yesu na kufunga safari ya miaka kadhaa kutoka huko kwa wakaldayo(mashariki ya mbali) kuifuata hata ilipowafikisha mahali mtoto alizaliwa ambaye walimsujudia maana walinjua kuwa mfalme tena juu ya wafalme wote maana nyota yake ilizidi zote.
Daniel alipokuwa utumwani huko babeli miaka kama miatano kabla ya Yesu kuzaliwa aliwahi kuwekwa kuwa kiongozi juu ya hawa wanajimu, wenye hekima, waganga na wachawi wa huko. Na ni baada ya kumshuhudia na kuhakiki kuwa yeye alikuwa mshiriki wa miungu mitakatifu isiyo na ushirika na wanadamu yenye uwezo wa juu mara mamilioni kuwazi.
Hawa wanajimu waliotoka huko mashariki ya mbali pamoja na magombo yao lakini walihitaji muongozo wa magombo ya manabii kama kina Danieli kufikia ufanisi wa kuzisoma nyota na kuelewa maana yake.
Kingine cha ajabu Yesu alijulikana na wafuasi tena hohehahe wa wakati wao na sii wakuu wa kidini.
Mfano wa mtu aitwae simion na nabii mke kwa jina la Ana. Hawa walipo muona mtoto Yesu ameletwa hekaluni waliingiwa na roho na kutabiri juu yake.
Mapepo nayo yalimtambua kila aendako kabla ya wengine na mengi yalipiga kilele kwa kuomba rehema na kusihi asiyaangamize kabla ya wakati wao.
Wakati yakipaaza sauti kuwa wewe ndiye mtakatifu wa Mungu, hekaluni makuhani na wakuu wa dini walimwita Yesu belzebuli yaani mkuu wa pepo kwa kumdhihaki.
Yesu asingeweza kuwaangamiza wale mapepo kabla ya wakati. Aliyafukuzia baharini ambako Mungu ndiko alikompa Lewiathani kuwa makazi yake hata siku ya kuangamizwa.Zaburi 104:25-26
[25]Bahari iko kule, kubwa na upana,
Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika,
Viumbe hai vidogo kwa vikubwa.
So is this great and wide sea, wherein are things creeping innumerable, both small and great beasts.
[26]Ndimo zipitamo merikebu,
Ndimo alimo lewiathani uliyemwumba acheze humo.
There go the ships: there is that leviathan, whom thou hast made to play therein.

Na maangamizi yake Isaya aliyanenea
Isaya 27:1
[1]Katika siku hiyo BWANA, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.
In that day the LORD with his sore and great and strong sword shall punish leviathan the piercing serpent, even leviathan that crooked serpent; and he shall slay the dragon that is in the sea.

Natamani kuongelea wale mwenye uzi anawaita watu warefu.
Lakini ukweli wake ni walinzi wa kile kiti cha rehema cha Mungu ambacho kwa sasa kipo katika moyo wa mwamini halisi wa Yesu Kristo.
Zamani kilikuwa katika hekalu patakatifu pa patakatifu(utukufu wa shekina) kikilindwa na makerubi.
Sasa hivi ni zile injili nne yaani Matayo, Marko, Luka na Yohana zikilinda matendo ya roho mtakatifu ndani ya mitume ambapo waandishi waliyaita MATENDO YA MITUME .
Mbona unachagua maswali ya kujibu?Nimekuuliza kama Yesu ni Mungu,je Mama yake aliyemzaa yaani Bikira Maria alikuwa anamuitaje?
 
Mbona unachagua maswali ya kujibu?Nimekuuliza kama Yesu ni Mungu,je Mama yake aliyemzaa yaani Bikira Maria alikuwa anamuitaje?
Hutapata jibu ikiwa tayari una Islamic perception ya Mungu.
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili kila amwaminie asipotee bali awe na uzima wa Milele.
Bikira Maria alijua Yesu ni mwana wa Mungu kwa sababu alitokewa na Malaika akaambiwa kuwa atamzaa mwana.Soma Luka 1:26 - 45
 
Hutapata jibu ikiwa tayari una Islamic perception ya Mungu.
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili kila amwaminie asipotee bali awe na uzima wa Milele.
Bikira Maria alijua Yesu ni mwana wa Mungu kwa sababu alitokewa na Malaika akaambiwa kuwa atamzaa mwana.Soma Luka 1:26 - 45
Tatizo mnashindwa kujibu maswali mepesi kama hayo,utaweza kuwafundisha watu vitu vigumu?dini siyo ya kukalilishwa labda nikuulize tena swali jingine Yesu alikuwa Dini gani?mimi nataka vitu vikubwa
 
INAENDELEA...........
Tulikutana na mzee Matata na tukaendelea na utafiti wetu kuhusu walokole,ila sikumuambia kuhusu yule mtu mrefu aliyenishika bega na kunitamkia yale maneno ya kirafiki.Ila kuna siku moja mzee Matata akaniambia""Kijana wangu wale watu warefu walikugusa"""nikamwambia ndio.Akaniambia mbona hukuniambia????? Basi nikamuelezea tukio lile la siku ile pale nyumbani kwa mzee Karugala nilipoenda kufanya ibada.Akaniambia wale watu warefu wamekuachia alama kwenye bega lako haifutiki,lakini nikamwambia ni kitendo cha sekunde ishirini tu yote hayo yalitokea Akajibu akasema wale watu warefu wameshakuweka alama yao ila hakuna madhara.
Bas tukaendelea na utafiti wetu kwa kutumia elimu ya unajimu kuwadadisi hao watu warefu na walokole.Akanipa mtihani nisome kitabu cha sala cha walokole kinaitwa biblia na humo ndani akaniambia nisome kitabu kinaitwa isaya na kitabu kinaitwa ufunuo.Pia nisome kitabu cha kinajimu kinaitwa Al azif na nisome humo ndani sura inaitwa miliki ya anga,nikimaliza tutaendelea na utafiti wetu wa kinajimu.Basi ilikua kila jioni tunakaa na kuanza kusoma kitabu kimoja baada ya kingine na tunaunganisha doti kwenye utafiti wetu.Kuna kitu mzee wangu alinionyesha,ilikua ikifika ijumaa usiku walokole wengi wanakua kwenye mikesha na wakiwa wanasali anga inafunguka unaona wale watu warefu wanashuka kuwaendea.Mimi nakua nimekaa mkekani nje uwani kaniacha pale mzee wangu nashangaa maajabu ya anga na viumbe vyake namaanisha wale watu warefu.
Ikifika asubuhi tunaingia darasani kuwachambua ni akina nani na asili yao ni wapi na ni kwanini wana mahusiano ya moja kwa moja na walokole..Vile vitabu ndio vilikua muongozo,maana mzee alisema ukitaka kuwajua walokole na hawa watu warefu wa angani basi tumia vitabu vyao
UTAFITI WETU UKAIBUA MAMBO 3
MOSI: Ikatuonyesha katika vitabu vya walokole hasa kitabu cha isaya kuna ibara imetaja kwa upana zaidi kuhusu hizi jamii mbili za watu warefu (Wale wa kutokea angani na wale wa kutokea baharini) na ikazungumzia vita yao ya miaka trion elfu kugombea anga.Pili kitabu cha Al azif kuna sura inasema wale watu warefu wa baharini ni ndugu na wale watu warefu wa angani ila walifanyiana fitina wakatawanyika na kuja duniani kabla ya binadamu kuanzisha makazi.Tukapata jibu kua wale watu warefu wote wa angani na baharini wametokana na mionzi ya nguvu kani za jua kuu nje ya ulimwengu wa nyota kwenye ule mduara wenye uhai wa moto ndani ya pumzi za moto zenye uhai zinazowazunguka walokole.
PILI:Kupitia hivi vitabu tukagundua kua hawa walokole wana uhusiano wa moja kwa moja na wale watu warefu wa angani sababu wanazungumza lugha moja yenye herufi zisizotamkika kibinadamu ila wao walokole wakiwa wanasali ni kama wanazungumza na wale watu warefu.Na hii ndio maana inaleta uhusiano wa moja kwa moja kati yao.
TATU:Jinsi tunavyowachunguza ndio kama tunajikuta tunavutiwa nao ili tuwachunguze zaidi kwa namna yoyote ile.Tujue je wanakula,je wana familia,je wanakufa,je wanazaliwa?????
Kitabu cha Al azif kinawataja kama wana wa angani na kitabu cha biblia kinawataja kama wana wa Mungu(Mungu wa walokole).
Nikamuuliza mzee Matata mbona nikiwa nawatazama mkekani anakimbia????Yeye akanijibu kua ananipa mda mzuri wa kutulia na kutafakari peke yangu.Bas tuliendelea na utafiti wetu na lengo likiwa baada ya kuwasoma kwenye vitabu basi twende kwenye makazi yao kuwapeleleza mimi na mnajimu mzee Matata.Lakini sasa ili kuwafikia inabidi tujenge urafiki nao namaanisha tuwe walokole au tuwavizie wakiwa wanatoka kwa walokole tuwafuatie kwa nyuma nyuma.Nilipotoa hayo mawazo mzee matata akachekaaa akasema wao ukisema uwafuatie kwa nyuma hutowapata wanatembea kwa kasi ya zaidi ya umeme utapotea angani ila kujenga urafiki nao unaweza ukiwa mlokole.
Bas tukaendelea na udadisi wetu huku vitu vipya vya kustaabisha na kushangaza vinatokea kila siku.Unaweza kuuliza nilipataje uwezo wa kuwaona hao watu warefu,nitaelezea hapo mbele
ITAENDELEA........................!!!!
 
Umenikumbusha jambo moja kuu kuhusu waamini katika Mungu wa mbingu na nchi ambao wanaomwamini hupitia jina lake la utambulisho la wakati yaani Yesu Kristo hata wakaitwa wakristo kwa maana ya ufuasi wao kwa Kristo. Miongoni mwao ni hao walipachikwa jina walokole au wa kulialia.
Jambo lenyewe ni hili kuna siri kuu katika mambo ya ulimwengu wa roho ambayo wanajimu, waganga na wachawi wanayafahamu kumhusu Mungu mara mia elfu zaidi ya wakristo. Hata hivyo kwa kuyafahamu hakuwafanyi kujisalimisha maisha yao kwake kwa sababu ya maslahi binafsi.
Adamu kabla ya kuwekwa katika mwili ule wa udongo kwa kazi ya kuilima nchi na kuitiisha, aliishi ulimwengu zote mbili yaani wa kiroho na kimwili hata alipoanguka na kupoteza haki ya umiliki.
Maana yake kumbe uwezo wa kumiliki ya kiroho na kimwili haitoshi tu kuwa sababu pekee ya ushindi dhidi ya kumuasi Mungu.
Mama jusi ambao ni wanajimu ndio walioiona na kuitambua nyota ya Yesu na kufunga safari ya miaka kadhaa kutoka huko kwa wakaldayo(mashariki ya mbali) kuifuata hata ilipowafikisha mahali mtoto alizaliwa ambaye walimsujudia maana walinjua kuwa mfalme tena juu ya wafalme wote maana nyota yake ilizidi zote.
Daniel alipokuwa utumwani huko babeli miaka kama miatano kabla ya Yesu kuzaliwa aliwahi kuwekwa kuwa kiongozi juu ya hawa wanajimu, wenye hekima, waganga na wachawi wa huko. Na ni baada ya kumshuhudia na kuhakiki kuwa yeye alikuwa mshiriki wa miungu mitakatifu isiyo na ushirika na wanadamu yenye uwezo wa juu mara mamilioni kuwazi.
Hawa wanajimu waliotoka huko mashariki ya mbali pamoja na magombo yao lakini walihitaji muongozo wa magombo ya manabii kama kina Danieli kufikia ufanisi wa kuzisoma nyota na kuelewa maana yake.
Kingine cha ajabu Yesu alijulikana na wafuasi tena hohehahe wa wakati wao na sii wakuu wa kidini.
Mfano wa mtu aitwae simion na nabii mke kwa jina la Ana. Hawa walipo muona mtoto Yesu ameletwa hekaluni waliingiwa na roho na kutabiri juu yake.
Mapepo nayo yalimtambua kila aendako kabla ya wengine na mengi yalipiga kilele kwa kuomba rehema na kusihi asiyaangamize kabla ya wakati wao.
Wakati yakipaaza sauti kuwa wewe ndiye mtakatifu wa Mungu, hekaluni makuhani na wakuu wa dini walimwita Yesu belzebuli yaani mkuu wa pepo kwa kumdhihaki.
Yesu asingeweza kuwaangamiza wale mapepo kabla ya wakati. Aliyafukuzia baharini ambako Mungu ndiko alikompa Lewiathani kuwa makazi yake hata siku ya kuangamizwa.Zaburi 104:25-26
[25]Bahari iko kule, kubwa na upana,
Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika,
Viumbe hai vidogo kwa vikubwa.
So is this great and wide sea, wherein are things creeping innumerable, both small and great beasts.
[26]Ndimo zipitamo merikebu,
Ndimo alimo lewiathani uliyemwumba acheze humo.
There go the ships: there is that leviathan, whom thou hast made to play therein.

Na maangamizi yake Isaya aliyanenea
Isaya 27:1
[1]Katika siku hiyo BWANA, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.
In that day the LORD with his sore and great and strong sword shall punish leviathan the piercing serpent, even leviathan that crooked serpent; and he shall slay the dragon that is in the sea.

Natamani kuongelea wale mwenye uzi anawaita watu warefu.
Lakini ukweli wake ni walinzi wa kile kiti cha rehema cha Mungu ambacho kwa sasa kipo katika moyo wa mwamini halisi wa Yesu Kristo.
Zamani kilikuwa katika hekalu patakatifu pa patakatifu(utukufu wa shekina) kikilindwa na makerubi.
Sasa hivi ni zile injili nne yaani Matayo, Marko, Luka na Yohana zikilinda matendo ya roho mtakatifu ndani ya mitume ambapo waandishi waliyaita MATENDO YA MITUME .
Taratibu nitaekezea mkuu udadisi wangu na utafiti wangu...Tuvumiliane nitakua naandika kidogo kidogo ili nisipoteze maana na kuchosha wasomaji.... wa huu uzi
 
15 Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?
2 Wafalme 6:15

16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.
2 Wafalme 6:16

17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.
2 Wafalme 6:17
FaizaFoxy jisomee uone Mungu weti alivyo Mkuu sana
 
Na kuna wale wanaozurura hewani hawagusi chini kama wanaelea hivi na panga zao mikononi.

Hilo ni kundi la malaika wa vita, na kiongozi wao ndiye malaika Mikaeli kama ambavyo amekuwa akielezwa kwenye Biblia...

Ufunuo wa Yohana 12
7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
 
Mbona umesharogwa? Unajiona unadunda wala hudundi🤣🤣🤣! Shetani kakufunga ufahamu, umekosa maarifa ya kimungu na wala hutaki kujua! Umerogwa, hawana shida ya kukuroga maana wewe ni wa kwao tayari!
Kama si hivyon basi inawezekanapia huna wanachotaka! Wewe ni makapi!

🤣 🤣 🤣 nyie watu huwa mnakuja na excuses zote duniani but the actual thing. Umeambiwa niroge unaanza story nyingi badala ya kuokoa nguvu na muda na kuniroga, inabidi uwe zwazwa A1 kuamini mambo ya ushirikina.
 
Kuanzia mwaka 1997 mpaka mwaka 2019 nilikua kwenye research binafsi ya mambo yasiyoonekana kwa macho ya kawaida. Nimefanya mahojiano na watu wa fani hii,kuanzia watu wa kawaida mpaka viongozi wa fani hii katika nyanja mbalimbali.

Mambo yasiyoonekana kwa macho,watu wanaita""UCHAWI""na ni fani yenye kuchanganya kidogo sababu inajumuisha imani za dini za wanadamu na imani za dini zisizo za wanadamu. Pia inajumuisha watu ambao wanaitwa bin-adamu na inajumuisha watu wale wengine ambao hawana undugu na hawa watu wanaoitwa bin-adam.Nielezee kidogo hao watu wengine,nimewaita watu sababu wana maumbo kama binadamu ila vimo vyao vipo tofauti na wapo katika jamii mbili tofauti.

Kuna ile jamii ya wanaokaa angani ambapo bila ruhusa yao huwezi kuwafikia,na kuna ile jamii ambayo hata bila ruhusa yao unaweza kuwafikia na wanakaa chini ya bahari au mito au maziwa makubwa(Lakes).Ngoja nifafanue kidogo jamii za hawa watu.

Jamii ya watu wa angani inashuka sana duniani na sijui waga wanakuja kufanya nini ila mara nyingi wanajishugulisha na wale binadamu mnaowaita walokole,na ili uzungumze nao inategemea umekutana nao katika hali gani kwenye ulimwengu usio wazi kwa macho ya kawaida,kiasili sio waongeaji sana ila sura zao zinaakisi mwanga kwa namna ya tofauti na unaweza kujiuliza wanavaa mavazi gani, kwa mavazi wanavaa hizi nguo mnaita kanzu ila ni bwanga afu ndefu mpaka miguuni na ni nyeupe.

Jamii ile nyingine ya watu wasio na asili na binadamu ila wamefanana na binadamu kimuonekano lakini wana vimo vikubwa ni ile inayokaa chini ya bahari,maziwa(Lakes) na mito.Hii jamii wao ni wazungumzaji sana afu miili yao haiakisi mwanga na wanakuja sana duniani na unaweza kuwaona bila ridhaa yao kwa kufuata utaratibu wanaokupa wafuasi wao au wanajimu wa nyota mbao ni binadamu wa kawaida,na mavazi yao ni kanzu pia ila za rangi mbalimbali zaidi ya nyeupe.Na watu wanaojishugulisha nao sana ni wale watu ambao nyinyi binadamu mnawaita wanajimu na washirikina au wachawi ila inategemea ushirikina na uchawi wa wapi maana dunia ni kubwa kutoka bara moja mpaka lingine na ushirikina au uchawi unatofautiana.

Binadamu kuna vitu huwezi kuviona mpaka either uwe mshirika wa jamii mojawapo kati ya jamii hizo mbili nilizokutajia hapo juu.Lengo langu leo ni kuzungumzia mkuu wa jamii ile ya wale watu wa angani ambao wanapenda kushirikiana na walokole au watu wa kulia lia,maana huyo mkuu ana vitu vya tofauti kidogo ndio maana nikasema pale juu kua "Mungu wa walokole ana nguvu sana".

Katika utafiti wangu ndani ya ulimwengu usio,onekana inaonyesha kua walokole wanapendelewa sana na huyo mkuu wao,maana kuna vitu anawapa vya ziada wao hawavitumii sijui kwanini niligundua hilo huko mbele katika utafiti wangu.Nimemuita Mkuu au Mungu wa walokole sababu kila walokole wanapoanza kulialia""Kusali""wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wengine wana mabawa na wengine hawana wakitokea kwa mkuu wa walokole ama nilivyokuja kujua baadae huko huko angani wanawajia na wanawazunguka hawaondoki na lile eneo husika linakua na mwanga unaweza kupofusha macho (Ni kama mwanga wa jua au radi au shoti za umeme zile cheche) ila walokole waga hawawaoni nadhani waga wanalia(Kusali) kwa imani zaidi namaanisha meditation.

Nilisema hapo juu kua mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana nguvu sana maana wale walokole baada ya kulia kwa mkuu wao huwezi kuwasogelea katika hali ya nje ya ubinadamu au katika hali ya ushirika na jamii nyingine za kiroho zaidi ya mkuu wao na wale watu wa kuakisi mwanga.Kila mlokole anakua na yule mtu wa kuakisi mwanga na yule mtu haongei ila macho yake ni ishara tosha kua usimsogelee mlokole aliyenae.Cha ajabu wengi ya walokole hao katika hali ya ubinadamu wa kawaida hawana habari yoyote ile unawakuta sokoni au kwenye daladala au barabarani au ofisini au kwenye nyumba zao za ibada.

Sasa ikabidi nifanye uchunguzi juu ya huyo mkuu (Mungu) wa walokole,yupoje na ni nani, wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wanaishi nae vipi maana wana ushirika nae.Sababu ukitoka nje ya mwili kupitia(meditation) huwezi kuwasogelea hawa watu wa jamii ya kuakisi mwanga au hao walokole.Nikajikuta napata hamu ya kuchunguza mambo ya ulimwengu usionekana na hasa jamii za wale watu warefu wa angani na walokole hasa wale wa kulialia sisi binadamu tunaita kusali ila wao walokole wanaita kunena kwa lugha,na ni lugha ambayo inawafanya wawasiliane na wale watu warefu wa kuakisi mwanga.

Udadisi wangu ulijikita katika mambo makuu matano(5)
Mosi: Kwanini walokole wana uhusiano na wale watu wa kuakisi mwanga wanaotokea kule juu kusikofikika hata ukitoka nje ya mwili na kusafiri nje ya mzunguko wa sayari za kawaida kwa maelekezo ya wanajimu wa nyota?

Pili: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana uhusiano wa moja kwa moja na wale watu wa kuakisi mwanga na sio ile jamii ya chini ya bahari?

Tatu: Kwanini katika jamii za nje ya mwanadamu au mtu, hasa ile jamii ya watu wa kuakisi mwanga ina nguvu sana kuliko jamii za wale watu wanaokaa chini ya bahari na wasioakisi mwanga wa jua na mwezi?

Nne: Mkuu wa walokole kwanini yeye na wale watu wa kuakisi mwanga,hawana ukaribu na Mkuu wa wale watu wa jamii inayokaa baharini na chini ya maziwa na mito(Maana nayo ina mkuu wake) na hataki wafuasi wake wa dini yake wawe na ukaribu na walokole kwa namna yoyote ile?

Tano: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao pamoja na nguvu zoote ila hawapi utajiri wa kibinadamu hao walokole ila ukitoka nje ya mwili hawa walokole wana nguvu sana mpaka uñashindwa kuwaelezea labda uone kwa macho.Tofauti na mkuu wa ile jamii nyingine ambayo karibia robo ya wafuasi wake wana access ya kupata mali za dunia hii tunayoishi binadamu wote.

Basi nikajikuta naanza utafiti kufuatilia nguvu za mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao.Ni nani na yupoje na anaishi wapi..Utafiti wangu ukanipelekea kuja na kichwa cha habari hapo juu kua Mungu wa walokole ana nguvu sana maana nilishuhudia mengi kumuhusu huyu Mungu wa hawa watu wa kulialia mnawaitaga walokole.

Safari yangu ya utafiti ilinikutanisha na wazee wa kibantu,wanajimu,viongozi wa dini za wanadamu zinazoonekana na zisizoonekana na watu wa jamii zile za nje ya ulimwengu wa mwanadamu.

ITAENDELEA
Ulifanya utafiti huo Ukiwa team ipi?

Maana kuwaona hao watu warefu Walio angani wenye mavazi meupe wenye urafiki na walokole ni LAZIMA uwe katika team moja wapo kati ya mbili.

Asiyejishughulisha na team hizo, ngumu sana kufanya utafiti na kupata findings za Kweli.

Anyway,1997 INJILI ya uamsho wa Moses Kulola ndo ulikuwa on fire, na Hadi sasa wapo wanaoendelea moto huo.

Soon, wale wa CHINI Baharini ,watakosa Makao ktk Nchi yetu nzuri TANZANIA.

Amen
 
INAENDELEA.....!!!!!
Ulifanya utafiti huo Ukiwa team ipi?

Maana kuwaona hao watu warefu Walio angani wenye mavazi meupe wenye urafiki na walokole ni LAZIMA uwe katika team moja wapo kati ya mbili.

Asiyejishughulisha na team hizo, ngumu sana kufanya utafiti na kupata findings za Kweli.

Anyway,1997 INJILI ya uamsho wa Moses Kulola ndo ulikuwa on fire, na Hadi sasa wapo wanaoendelea moto huo.

Soon, wale wa Baharini watakosa Makao ktk Nchi yetu nzuri TANZANIA.

Amen
Ukisoma vizuri utanielewa na mtu niliyeshirikiana nae kwenye utafiti
 
Sijajua ila nazungumziwa watu warefu wa jamii ya kuakisi mwanga wa jua na wana mahusiano ya moja kwa moja na walokole.Ukitaka kugombana nao nje ya mwili wako wa kibinadamu basi uwaguse walokole wao hasa wakiwa wanalialia,nyie binadamu mnaita kunena kwa lugha.Hawana mzaha
Kumbe,Naokoka leo,nakua Mlokole!..sitaki kuonewa hapa Duniani
 
Back
Top Bottom