Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mbona unachagua maswali ya kujibu?Nimekuuliza kama Yesu ni Mungu,je Mama yake aliyemzaa yaani Bikira Maria alikuwa anamuitaje?
 
Mbona unachagua maswali ya kujibu?Nimekuuliza kama Yesu ni Mungu,je Mama yake aliyemzaa yaani Bikira Maria alikuwa anamuitaje?
Hutapata jibu ikiwa tayari una Islamic perception ya Mungu.
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili kila amwaminie asipotee bali awe na uzima wa Milele.
Bikira Maria alijua Yesu ni mwana wa Mungu kwa sababu alitokewa na Malaika akaambiwa kuwa atamzaa mwana.Soma Luka 1:26 - 45
 
Tatizo mnashindwa kujibu maswali mepesi kama hayo,utaweza kuwafundisha watu vitu vigumu?dini siyo ya kukalilishwa labda nikuulize tena swali jingine Yesu alikuwa Dini gani?mimi nataka vitu vikubwa
 
INAENDELEA...........
Tulikutana na mzee Matata na tukaendelea na utafiti wetu kuhusu walokole,ila sikumuambia kuhusu yule mtu mrefu aliyenishika bega na kunitamkia yale maneno ya kirafiki.Ila kuna siku moja mzee Matata akaniambia""Kijana wangu wale watu warefu walikugusa"""nikamwambia ndio.Akaniambia mbona hukuniambia????? Basi nikamuelezea tukio lile la siku ile pale nyumbani kwa mzee Karugala nilipoenda kufanya ibada.Akaniambia wale watu warefu wamekuachia alama kwenye bega lako haifutiki,lakini nikamwambia ni kitendo cha sekunde ishirini tu yote hayo yalitokea Akajibu akasema wale watu warefu wameshakuweka alama yao ila hakuna madhara.
Bas tukaendelea na utafiti wetu kwa kutumia elimu ya unajimu kuwadadisi hao watu warefu na walokole.Akanipa mtihani nisome kitabu cha sala cha walokole kinaitwa biblia na humo ndani akaniambia nisome kitabu kinaitwa isaya na kitabu kinaitwa ufunuo.Pia nisome kitabu cha kinajimu kinaitwa Al azif na nisome humo ndani sura inaitwa miliki ya anga,nikimaliza tutaendelea na utafiti wetu wa kinajimu.Basi ilikua kila jioni tunakaa na kuanza kusoma kitabu kimoja baada ya kingine na tunaunganisha doti kwenye utafiti wetu.Kuna kitu mzee wangu alinionyesha,ilikua ikifika ijumaa usiku walokole wengi wanakua kwenye mikesha na wakiwa wanasali anga inafunguka unaona wale watu warefu wanashuka kuwaendea.Mimi nakua nimekaa mkekani nje uwani kaniacha pale mzee wangu nashangaa maajabu ya anga na viumbe vyake namaanisha wale watu warefu.
Ikifika asubuhi tunaingia darasani kuwachambua ni akina nani na asili yao ni wapi na ni kwanini wana mahusiano ya moja kwa moja na walokole..Vile vitabu ndio vilikua muongozo,maana mzee alisema ukitaka kuwajua walokole na hawa watu warefu wa angani basi tumia vitabu vyao
UTAFITI WETU UKAIBUA MAMBO 3
MOSI: Ikatuonyesha katika vitabu vya walokole hasa kitabu cha isaya kuna ibara imetaja kwa upana zaidi kuhusu hizi jamii mbili za watu warefu (Wale wa kutokea angani na wale wa kutokea baharini) na ikazungumzia vita yao ya miaka trion elfu kugombea anga.Pili kitabu cha Al azif kuna sura inasema wale watu warefu wa baharini ni ndugu na wale watu warefu wa angani ila walifanyiana fitina wakatawanyika na kuja duniani kabla ya binadamu kuanzisha makazi.Tukapata jibu kua wale watu warefu wote wa angani na baharini wametokana na mionzi ya nguvu kani za jua kuu nje ya ulimwengu wa nyota kwenye ule mduara wenye uhai wa moto ndani ya pumzi za moto zenye uhai zinazowazunguka walokole.
PILI:Kupitia hivi vitabu tukagundua kua hawa walokole wana uhusiano wa moja kwa moja na wale watu warefu wa angani sababu wanazungumza lugha moja yenye herufi zisizotamkika kibinadamu ila wao walokole wakiwa wanasali ni kama wanazungumza na wale watu warefu.Na hii ndio maana inaleta uhusiano wa moja kwa moja kati yao.
TATU:Jinsi tunavyowachunguza ndio kama tunajikuta tunavutiwa nao ili tuwachunguze zaidi kwa namna yoyote ile.Tujue je wanakula,je wana familia,je wanakufa,je wanazaliwa?????
Kitabu cha Al azif kinawataja kama wana wa angani na kitabu cha biblia kinawataja kama wana wa Mungu(Mungu wa walokole).
Nikamuuliza mzee Matata mbona nikiwa nawatazama mkekani anakimbia????Yeye akanijibu kua ananipa mda mzuri wa kutulia na kutafakari peke yangu.Bas tuliendelea na utafiti wetu na lengo likiwa baada ya kuwasoma kwenye vitabu basi twende kwenye makazi yao kuwapeleleza mimi na mnajimu mzee Matata.Lakini sasa ili kuwafikia inabidi tujenge urafiki nao namaanisha tuwe walokole au tuwavizie wakiwa wanatoka kwa walokole tuwafuatie kwa nyuma nyuma.Nilipotoa hayo mawazo mzee matata akachekaaa akasema wao ukisema uwafuatie kwa nyuma hutowapata wanatembea kwa kasi ya zaidi ya umeme utapotea angani ila kujenga urafiki nao unaweza ukiwa mlokole.
Bas tukaendelea na udadisi wetu huku vitu vipya vya kustaabisha na kushangaza vinatokea kila siku.Unaweza kuuliza nilipataje uwezo wa kuwaona hao watu warefu,nitaelezea hapo mbele
ITAENDELEA........................!!!!
 
Taratibu nitaekezea mkuu udadisi wangu na utafiti wangu...Tuvumiliane nitakua naandika kidogo kidogo ili nisipoteze maana na kuchosha wasomaji.... wa huu uzi
 
FaizaFoxy jisomee uone Mungu weti alivyo Mkuu sana
 
Na kuna wale wanaozurura hewani hawagusi chini kama wanaelea hivi na panga zao mikononi.

Hilo ni kundi la malaika wa vita, na kiongozi wao ndiye malaika Mikaeli kama ambavyo amekuwa akielezwa kwenye Biblia...

Ufunuo wa Yohana 12
7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
 

🤣 🤣 🤣 nyie watu huwa mnakuja na excuses zote duniani but the actual thing. Umeambiwa niroge unaanza story nyingi badala ya kuokoa nguvu na muda na kuniroga, inabidi uwe zwazwa A1 kuamini mambo ya ushirikina.
 
Ulifanya utafiti huo Ukiwa team ipi?

Maana kuwaona hao watu warefu Walio angani wenye mavazi meupe wenye urafiki na walokole ni LAZIMA uwe katika team moja wapo kati ya mbili.

Asiyejishughulisha na team hizo, ngumu sana kufanya utafiti na kupata findings za Kweli.

Anyway,1997 INJILI ya uamsho wa Moses Kulola ndo ulikuwa on fire, na Hadi sasa wapo wanaoendelea moto huo.

Soon, wale wa CHINI Baharini ,watakosa Makao ktk Nchi yetu nzuri TANZANIA.

Amen
 
INAENDELEA.....!!!!! Ukisoma vizuri utanielewa na mtu niliyeshirikiana nae kwenye utafiti
 
Kumbe,Naokoka leo,nakua Mlokole!..sitaki kuonewa hapa Duniani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…