Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mkuu hii ya magari ya deraya na farasi wa moto niliwahi kuona kwenye ndoto gari la farasi wa moto likitoka mashariki angani na kuelekea magharibi nilikuwa bado mtoto wa miaka kama tisa hivi lakini mpaka leo nakumbuka
Huyo farasi alikua anaenda wapi?
 
Yaani niliona anakayiza tu angani sijui alikua anaenda wapi bali ulikuwa ni uelekeo wa magharibi
 
NILIKUWA NIMELALA SIKU MOJA NIKAOTA NIMEFUNGWA KAMBA MIKONO YANGU YOTE MIWILI

NILISEMA NAKATA KAMBA HIZI KWA JINA LA YESU MIKONO YANGU ILIACHIA NA NIKASHITUKA USINGIZINI

Sent from my A37fw using JamiiForums mobile app
Mimi nakumbuka Kuna siku nliota tulikua mateka kwenye chumba hivi Niko Mimi Na wenzangu wengine siwajui tumekaa humo Kwa ajili Ya kuuawa Yani tuliwekwa humo ili tuuliwe.... tulikua tumekaa Kwa kupangwa Kwa line...mara Yule alikua anatakiwa kutuua akafika tulaogopa sana...maandalizi Ya kuuawa yakaanza akatokea mwanamke akawa anatuchapa bakora za mgongoni akaanzia line za mbele akawachapa watu bakora Iikafika zamu yangu Ila anataka kuanzia kunichapa nikawa nalia nasema Yesu wangu nlivotaja tu hivo nikajkuta nimeshtuka usingizini nahema.....nikama vile nilikua Brought to life maana nilikua niuawe
 
Ndugu mimi kumtafiti huyu Alfa na Omega ni suala endelevu,hapa ninashea tu na watu.Sikujua humu JF nikimzungumzia huyu Alfa na Omega nitapata watu wa kujadiliana nao...Lakini nikwambie kitu kimoja,yeye anawaona wote mnaomzungumzia na ni mkuu mwenye wivu.Hapo namaanisha ana wivu mkuu kwa wanamzungumzia yeye...WIVU WA ALFA NA OMEGA SIO WA KIBINADAMU.WIVU WAKE NI WA KIROHO SABABU ANAWATAKA WALOKOLE WAMTANGULIZE KATIKA KILA KITU MPAKA VILE VITU VIDOGO KABISA.KAMA YEYE ANAVYOWATANGULIZA KWENYE KILA KITU CHAKE..NA WALOKOLE WANAFANIKIWA SABABU WANAMTANGULIZA KWENYE KILA KITU CHAO
Tusaidie mtumishi hivo vitu vidogo uliyosema Ni kama nini
 
Haya ni maji ya upako yameombewa, kuyapata unanunua chupa ndogo 5000 ya kati 10000 dumu 20,000.

Pima mwenyewe kupitia maandiko ikiwa baraka za Mungu zinanunuliwa Kwa pesa.

Ingekuwa zinanunuliwa Kwa pesa, wezi, wazinzi na wachawi wangehonga Malaika kwenye GETI la Mbingu Ili waingie!!!
Hapohapo Kuna cake za upako zinauzwa Sio bure...Kuna kukanyaga Mafuta Kuna kipindi alikua anauza udongo wa upako kijiko buku...just imagine
 
Upo sahihi, Yesu hakutuachia maji, mafuta wala vitambaa alituambia jina lake. Matumizi ya maji, mafuta na vitambaa sasa yanachukua nafasi ya Jina la Yesu. Hii ndio changamoto.
Yesu alivoondoka alituachia Amani yake pia Na msaidizi ambaye Ni roho mtakatifu
 
Wale watu warefu wenye kuakisi mwanga wakimsogelea binadamu anahisi amani na raha katika mwili na huwezi kuielezea hiyo hali. Lakini wale watu warefu wengine wasioakisi mwanga wanaotokea baharini wakikusogelea unasisimkwa na mwili na kujawa na uoga mkubwa sana...Mkuu wewe ulitokewa na wale watu warefu wa angani wa kuakisi mwanga marafiki na walinzi wa walokole.
Kuna wakati unakuta nikiwa nasalii gafla mwili unasisimka Hasa nywele nakua Nahis kauwoga Ila Kadri navoendelea Na maombi Ile Hali inapotea kbs...au wakati mwingine unakuta usiku nakosa kabisa usingiz nakua ntagalagala tu kitandan kama nsipoamka Na kusali nikiforce kulala Hua napata mashambuliz Ya kiroho au sometimes unakuta Kuna hofu moyoni nkisema nilale nashambuliwa Ila nkisema nsilale nasalii Ile hofu huondoka Na Hua nalala Kwa amanii...hapo rohoni Ni Nini Hua kinaendelea
 
NINGEKUA NA UWEZO WA KUWAKUSANYA WALOKOLE WOTE NA KUWAWEKA SEHEMU MOJA NA NIWAAMBIE KAULI MOJA.BASI NINGEWAAMBIA HIVI""""""Haijalishi mnapitia hali gani kimwili ila kiroho nyinyi ni watawala na wamliki......kinachotakiwa kwenu ni imani tu
Tufafanunulie kiundani Zaidi kwenye hili kiongozi
 
Kuanzia mwaka 1997 mpaka mwaka 2019 nilikua kwenye research binafsi ya mambo yasiyoonekana kwa macho ya kawaida. Nimefanya mahojiano na watu wa fani hii,kuanzia watu wa kawaida mpaka viongozi wa fani hii katika nyanja mbalimbali.

Mambo yasiyoonekana kwa macho,watu wanaita""UCHAWI""na ni fani yenye kuchanganya kidogo sababu inajumuisha imani za dini za wanadamu na imani za dini zisizo za wanadamu. Pia inajumuisha watu ambao wanaitwa bin-adamu na inajumuisha watu wale wengine ambao hawana undugu na hawa watu wanaoitwa bin-adam.Nielezee kidogo hao watu wengine,nimewaita watu sababu wana maumbo kama binadamu ila vimo vyao vipo tofauti na wapo katika jamii mbili tofauti.

Kuna ile jamii ya wanaokaa angani ambapo bila ruhusa yao huwezi kuwafikia,na kuna ile jamii ambayo hata bila ruhusa yao unaweza kuwafikia na wanakaa chini ya bahari au mito au maziwa makubwa(Lakes).Ngoja nifafanue kidogo jamii za hawa watu.

Jamii ya watu wa angani inashuka sana duniani na sijui waga wanakuja kufanya nini ila mara nyingi wanajishugulisha na wale binadamu mnaowaita walokole,na ili uzungumze nao inategemea umekutana nao katika hali gani kwenye ulimwengu usio wazi kwa macho ya kawaida,kiasili sio waongeaji sana ila sura zao zinaakisi mwanga kwa namna ya tofauti na unaweza kujiuliza wanavaa mavazi gani, kwa mavazi wanavaa hizi nguo mnaita kanzu ila ni bwanga afu ndefu mpaka miguuni na ni nyeupe.

Jamii ile nyingine ya watu wasio na asili na binadamu ila wamefanana na binadamu kimuonekano lakini wana vimo vikubwa ni ile inayokaa chini ya bahari,maziwa(Lakes) na mito.Hii jamii wao ni wazungumzaji sana afu miili yao haiakisi mwanga na wanakuja sana duniani na unaweza kuwaona bila ridhaa yao kwa kufuata utaratibu wanaokupa wafuasi wao au wanajimu wa nyota mbao ni binadamu wa kawaida,na mavazi yao ni kanzu pia ila za rangi mbalimbali zaidi ya nyeupe.Na watu wanaojishugulisha nao sana ni wale watu ambao nyinyi binadamu mnawaita wanajimu na washirikina au wachawi ila inategemea ushirikina na uchawi wa wapi maana dunia ni kubwa kutoka bara moja mpaka lingine na ushirikina au uchawi unatofautiana.

Binadamu kuna vitu huwezi kuviona mpaka either uwe mshirika wa jamii mojawapo kati ya jamii hizo mbili nilizokutajia hapo juu.Lengo langu leo ni kuzungumzia mkuu wa jamii ile ya wale watu wa angani ambao wanapenda kushirikiana na walokole au watu wa kulia lia,maana huyo mkuu ana vitu vya tofauti kidogo ndio maana nikasema pale juu kua "Mungu wa walokole ana nguvu sana".

Katika utafiti wangu ndani ya ulimwengu usio,onekana inaonyesha kua walokole wanapendelewa sana na huyo mkuu wao,maana kuna vitu anawapa vya ziada wao hawavitumii sijui kwanini niligundua hilo huko mbele katika utafiti wangu.Nimemuita Mkuu au Mungu wa walokole sababu kila walokole wanapoanza kulialia""Kusali""wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wengine wana mabawa na wengine hawana wakitokea kwa mkuu wa walokole ama nilivyokuja kujua baadae huko huko angani wanawajia na wanawazunguka hawaondoki na lile eneo husika linakua na mwanga unaweza kupofusha macho (Ni kama mwanga wa jua au radi au shoti za umeme zile cheche) ila walokole waga hawawaoni nadhani waga wanalia(Kusali) kwa imani zaidi namaanisha meditation.

Nilisema hapo juu kua mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana nguvu sana maana wale walokole baada ya kulia kwa mkuu wao huwezi kuwasogelea katika hali ya nje ya ubinadamu au katika hali ya ushirika na jamii nyingine za kiroho zaidi ya mkuu wao na wale watu wa kuakisi mwanga.Kila mlokole anakua na yule mtu wa kuakisi mwanga na yule mtu haongei ila macho yake ni ishara tosha kua usimsogelee mlokole aliyenae.Cha ajabu wengi ya walokole hao katika hali ya ubinadamu wa kawaida hawana habari yoyote ile unawakuta sokoni au kwenye daladala au barabarani au ofisini au kwenye nyumba zao za ibada.

Sasa ikabidi nifanye uchunguzi juu ya huyo mkuu (Mungu) wa walokole,yupoje na ni nani, wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wanaishi nae vipi maana wana ushirika nae.Sababu ukitoka nje ya mwili kupitia(meditation) huwezi kuwasogelea hawa watu wa jamii ya kuakisi mwanga au hao walokole.Nikajikuta napata hamu ya kuchunguza mambo ya ulimwengu usionekana na hasa jamii za wale watu warefu wa angani na walokole hasa wale wa kulialia sisi binadamu tunaita kusali ila wao walokole wanaita kunena kwa lugha,na ni lugha ambayo inawafanya wawasiliane na wale watu warefu wa kuakisi mwanga.

Udadisi wangu ulijikita katika mambo makuu matano(5)
Mosi: Kwanini walokole wana uhusiano na wale watu wa kuakisi mwanga wanaotokea kule juu kusikofikika hata ukitoka nje ya mwili na kusafiri nje ya mzunguko wa sayari za kawaida kwa maelekezo ya wanajimu wa nyota?

Pili: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana uhusiano wa moja kwa moja na wale watu wa kuakisi mwanga na sio ile jamii ya chini ya bahari?

Tatu: Kwanini katika jamii za nje ya mwanadamu au mtu, hasa ile jamii ya watu wa kuakisi mwanga ina nguvu sana kuliko jamii za wale watu wanaokaa chini ya bahari na wasioakisi mwanga wa jua na mwezi?

Nne: Mkuu wa walokole kwanini yeye na wale watu wa kuakisi mwanga,hawana ukaribu na Mkuu wa wale watu wa jamii inayokaa baharini na chini ya maziwa na mito(Maana nayo ina mkuu wake) na hataki wafuasi wake wa dini yake wawe na ukaribu na walokole kwa namna yoyote ile?

Tano: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao pamoja na nguvu zoote ila hawapi utajiri wa kibinadamu hao walokole ila ukitoka nje ya mwili hawa walokole wana nguvu sana mpaka uñashindwa kuwaelezea labda uone kwa macho.Tofauti na mkuu wa ile jamii nyingine ambayo karibia robo ya wafuasi wake wana access ya kupata mali za dunia hii tunayoishi binadamu wote.

Basi nikajikuta naanza utafiti kufuatilia nguvu za mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao.Ni nani na yupoje na anaishi wapi..Utafiti wangu ukanipelekea kuja na kichwa cha habari hapo juu kua Mungu wa walokole ana nguvu sana maana nilishuhudia mengi kumuhusu huyu Mungu wa hawa watu wa kulialia mnawaitaga walokole.

Safari yangu ya utafiti ilinikutanisha na wazee wa kibantu,wanajimu,viongozi wa dini za wanadamu zinazoonekana na zisizoonekana na watu wa jamii zile za nje ya ulimwengu wa mwanadamu.

ITAENDELEA
taka aka taka taka takataka takataka
 
Mungu wa watu yukoje?
Elezea kwa Maandiko matakatifu ndo tutaelewana.

Sio kwa maneno matupu.
MUNGU aliyeumba mbingu na nchi, Mtakatifu wa Watakatifu haabudiwi na kila mtu. Ndo maana alijiita " Mungu wa Israeli" mara nyingi katika agano la Kale na wakati pale Middle east kulikuweko na Wafilisti, Wayebusi, Wagibeon, Waamaleki, Waamori, Wamoabu , Waamoni. Unajua kwanini hakujiita "Mungu wa Wafilisti "? Je Wafilisti sio watu? Ni kwasababu walikataa kumuabudu wakaamua kumuabudu Dagon kama Mungu wao.
 

Attachments

  • Screenshot_20231009-213833_Chrome.jpg
    Screenshot_20231009-213833_Chrome.jpg
    82.5 KB · Views: 17
  • Screenshot_20231009-220601_Facebook.jpg
    Screenshot_20231009-220601_Facebook.jpg
    76.1 KB · Views: 20
  • Screenshot_20231009-213943_Chrome.jpg
    Screenshot_20231009-213943_Chrome.jpg
    76.3 KB · Views: 20
  • Screenshot_20231009-213934_Chrome.jpg
    Screenshot_20231009-213934_Chrome.jpg
    94.2 KB · Views: 18
  • Screenshot_20231009-213928_Chrome.jpg
    Screenshot_20231009-213928_Chrome.jpg
    79.8 KB · Views: 18
  • Screenshot_20231009-213903_Chrome.jpg
    Screenshot_20231009-213903_Chrome.jpg
    76.9 KB · Views: 19
BAADA YA KUANZA HII SIMULIZI NILIPITIA MENGI,,,,,,UNAJUA MUNGU WA WALOKOLE HAITAKIWI WATU WA DUNIANI WAMJUE NA NDIO MAANA NIKAPITIA CHANGAMOTO MPAKA NIKAKAA PEMBENI KIDOGO JAMII FORUM....!!!LAKINI NAMSHUKURU HUYU MUNGU WA WALOKOLE AMBAE NI MKUU WA ANGA ZA JUU NA NI MUNGU MMILIKI ALINIAMBIA MANENO HAYA
MOSI: MIMI NI MUNGU NINAESAMEHE NA HAKUNA MUNGU KAMA MIMI UKITAKA KUTOA USHUHUDA WATU WANIFAHAMU USIOGOPE MATOKEO SABABU MIMI NI ROHO IWAKAYO MOTO NA WANAONIAMINI WANANIAMINI KATIKA ROHO NA UJASIRI WA IMANI WAOGA HAWANA NAFASI.
PILI: ANASEMA YEYE NI MUNGU MWENYE WIVU KWA WATU WAKE HASA WAMJUAO (HAPA NAMAANISHA WALOKOLE) NA ANAWALINDA KWA HIYO WASIOGOPE KUMTAJA.
KWA HIYO BAADA YA MANENO HAYA NA CHANGAMOTO ZA KIROHO ZILIZONIANDAMA TAKRIBANI MWAKA NIMERUDI TENA KUMZUNGUMZIA MUNGU WA WALOKOLE.YULE MUNGU MWENYE USHARIKA NA WALE WATU WAREFU WA NURU WENYE MABAWA NA AMBAE MTOTO WAKE WA KIPEKEE NDIE MFALME PEKEE WA ULIMWENGU WA KIMWILI NA ULIMWENGU WA KIROHO.
MKUBALI AU MKATAE ILA KWENYE ULIMWENGU WA KIROHO,,HUYU MTU MREFU MWENYE ALAMA YA ALFA NA OMEGA KIFUANI WALOKOLE WANAMUITA YESU AU IMANUELI AMBAE WALOKOLE WAKILIA ANATUMA WALE WATU WAREFU WENYE KUAKISI MWANGA WA JUA KUWALINDA,NDIE MUNGU WA KWELI NA ULIMWENGU WOTE WA KIROHO UNAJUA HIVYO.
MIMI BINAFSI WAKATI NAANDIKA KUHUSU MUNGU WA WALOKOLE NILIAMUA KUMSUJUDIA MAANA LEO NI MWAKA WA KENDA YUPO ANANITIZAMA TU KWA MACHO YA REHEMA..PAMOJA NA DHAMBI ZANGU BADO NINAISHI KWA REHEMA ZAKE ZA ULE USO WA KUNGAA NA KWA REHEMA ZA BABA YAKE AMBAE ANAWAKA KAMA JUA NA BILA KIBALI PENDEKEZI WALOKOLE WANAITA(UTAKATIFU) HUWEZI KUMTIZAMA AU KUMSOGELEA.
HAKUNA KITU KINATISHA KAMA KUMZUNGUMZA AU KUMUONGELEA MUNGU WA WALOKOLE ANATISHA MAANA ANA GRAVITY'S YA AJABU SANA INAKUTETEMESHA ROHO NA MWILI.NILIPOAMUA KUMZUNGUMZIA MUNGU WA WALOKOLE NILIPATA VITISHO VYA KIROHO ILA NIMERUDI TENA KUMZUNGUMZIA HUYU MUNGU MAANA NIMEMUONA KATIKA UKUU WAKE NA SI KWA MACHO YA NYAMA BALI MACHO YA KIROHO
MUNGU WA WALOKOLE YUPO HAI NA ANASHUKA DUNIANI KWA WASJIRIKA WAKE MDA WOTE NA KAMA AMEGAWANYIKA MAANA MAHALI POPOTE YUPO NA KAMA WALOKOLE MNGEFUNGULIWA MACHO YENU YA KIROHO BASI HAKUNA HATA MLOKOLE MMOJA AMBAE ANGEACHA USHARIKA NAE..YEYE NI MUNGU WA NURU NA VIUMBE VYOOOTE VYA KIROHO VINAMUABUDU NA ANA WASHIRIKA ZAKE WATU WAREFU WENYE KUAKISI MWANGA WA JUA WANAOWALINDA WALOKOLE NA MAPANGA YA MOTO POPOTE WAENDAKO.
KABLA SIJAENDELEA NAOMBA WALOKOLE POPOTE MLIPO MNIOMBEE ILI NIPATE KIBALI MBELE YA MUNGU WENU NIENDELEE KUWALETEA USHUUDA HUU KUMUHUSU YEYE AMBAE NI MUNGU MMLIKI WA ULIMWENGU WA KIROHO NDANI NA NJE YA MFUMO WA SAYARI ZA ULIMWENGU.
MUNGU WA WALOKOLE ANA NCHI YAKE SAYARI ZA MBALI AMBAYO NI WALOKOLE TU WENYE NEEMA YAKE MNAITA UTAKATIFU NDIO WATAFIKA HU

Tuko tunasililizia muendelezo

Mimi Kuna jamii ya watu nilikuwa nawasaidia wafanikiwe kimawazo ya kipesa ,
Kumbe wao lengo lao ni baya ,kumbe Nia nikuniona nafeli nashindwa siendelei,

Nakaa nao kumbe wao wanawivu mpaka wanakuwa na chuki nzito mioyoni mwao, Sasa Mimi nafanya wema kumbe wao wanawaza watanizidi vipi ,


Sasa Kuna siku Mungu akaanza kinuonyesha nilikuwa NACHEKA nao ni watu Gani, nilikuwa kugundua kumbe ni jamii ya uzao wa nyoka ,
Kilinikutaga pia Mimi nlikua namsaidia Sana Kwa Upendo Mungu alikuja kunifunilia Ni watu wa Aina Gani...ili nibidi nisitishe msaada Kwa Hao watu Ila Kwa wengine misaada kama kawaida
 
Hakuna Mungu wa walokole kuna wokuvu tu basi Mungu ni wawote na ukimwihitaji yupo
Wokovu unahubiriwa na akina nani?
Si Walokole ndo wanahubiri?
Ujue kuokoka sio tu kutubu na kumkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi, hiyo ni step ya kwanza ya Imani, step ya pili ni kumpokea Roho Mtakatifu, step ya tatu ni kuishi maisha Matakatifu Ili uendane na Roho Mtakatifu, Roho Mtakatifu atakuwa mwalimu wako mzuri sana , na ukitia bidii na nidhamu, utaenda in a high dimension, kuishi kama Mwana wa Mmiliki alivoishi hapa duniani..
 
NAENDELEA.............!!!
Kuna nyakati baadhi ya walokole wanajihisi kuchoka na kukata tamaa kwa masahibu mbalimbali katika maisha,,na kiroho inakua hv wanapoanza kuomba kwa kulia.....
Wale watu warefu wenye mabawa wanashuka na kukaa karibu yao na kuwatazama kwa upendo huku wakiwazunguka pande zote.Lakini wakiendelea kulia zaidi basi mbingu zinafunguka na Mwana wa mmiliki anashuka mwenyewe mpaka chini kuwatazama na wakizidi kulia na yeye analia na kuwaambia NIPO HAPA USILIE ISHI KWA IMANI NIPO HAPA DAIMA.
Na hata kama wapo sehemu tofauti tofauti duniani yeye anajigawa kwa sekunde hiyo hiyo anafika kote.Hakuna kitu kinachomshusha duniani kwa haraka mwana wa mmiliki kama maombi.
Walokole hawajui ila maombi ni silaha kuu sababu chochote utakachokisema kwenye maombi basi kwenye ulimwengu wa kiroho kinatokea hivyo hivyo.
WAKISEMA WANAFUNGA BASI NJIA ZOTE ZOTE ZA ANGA ZINAFUNGWA NA WAKISEMA MOTO KWELI MOTO HUTOKEA NA WAKIIMBA ILE NYIMBO YA ROHO YA MUNGU WAO ISHUKE BASI INASHUKA KWELI NA WINGU ZIIITO LA MWANGA MKALI KULIKO JUA LINAWAFUNIKA MPAKA WAMALIZE MAOMBI.
Mungu wa walokole huwezi kumtizama kwa macho ya kawaida ila anafanana na binadamu kimuonekano ni kama mzee hivi aliyekula chumvi za miaka usoni ila sio kwa ukubwa wa kimwili,,sababu yeye ni mkubwa mno kuliko dunia LAKINI ANASEMA ALIMUUMBA MTU KWA MFANO WAKE KIMUONEKANO ILA SIO KWA SIZE.Mwana wa mmliki na yeye anafanana na binadamu kimuonekano ila na yeye ni mkubwa mno kimuonekano.Na wale watu warefu wenye mabawa wanafanana na binadamu ila ni wakubwa mno kimuonekano..
Basi walokole wakiendelea kulia na kusali anga lote linafunguka na inakua ni uwanja wa mawasiliano kati yao na mwana wa mmliki,ambae anashuka na kukaa nao huku akiwatizama ila wao hawamuoni.
CHA AJABU WATOTO WOTE WA KIBINADAMU WANAMUONA NA WANAONGEA NAE NA KUCHEKA NA ANAWABEBA KIFUANI WAKATI WAKIWA NA WAZAZI WAO AU WALEZI WAO NA HAIJALISHI NI WATOTO WA WALOKOLE AU LA....YEYE MWANA WA MMLIKI NA WALE WATU WAREFU WENYE KUAKISI MWANGA RAFIKI ZAO WAKUBWA NI WATOTO WA KIBINADAMU KUANZIA UMRI WA SIKU MOJA MPAKA MIAKA KUMI NA NNE MPAKA KUMI NA SITA.
NB: KUNA WATOTO WASIO WA KIBINADAMU PIA IKUMBUKWE
Basi walokole wanapomaliza kuomba wanakua hawaoni wala kujua kua wamezungukwa na viumbe vya kiroho vinavyowatizama ila waga wanajihisi amani sana na utulivu wa moyo.Haijalishi kanisa gani wanatokea ila walokole wote wana alama sawa,,iwe wasabato au wakatoliki au waangilikana au walutheri au wapentekoste,,kwa mwana wa mmliki wote ni kitu kimoja na anawalinda sawa sawa.
Wachawi ni wabishi sana ndio wanaoongoza kwa kuwasumbua walokole wakiamini kua walokole ni wachawi kama wao ila wamewazidi maarifa ya kiuchawi.Na ndio wanaoongoza kwa kuwadhuru walokole kimwili.
KUNA ALAMA SABA ZA WALOKOLE KIROHO ZINAONEKANA WAZIWAZI
1: TUNDA LA UPENDO ( NJIWA WA MOTO)
2: WALINZI WATU WAREFU WENYE MABAWA NA PANGA ZA MOTO
3:NDIMI ZA MOTO JUU YA VICHWA VYAO
4: NGUZO ZA MOTTO ZINAZOZUNGUKA
5: WINGU LA MANUKATO NA MOSHI MWEUPE
6:MAGARI YA DERAYA NA FARASI WA MOTO
7:UTIIFU WA MOYO ULIO WAZI KIMUONEKANO KIROHO KWA MUNGU WA WALOKOLE.
Nitaendelea....................!!!!
 
NAENDELEA.............!!!
Kuna nyakati baadhi ya walokole wanajihisi kuchoka na kukata tamaa kwa masahibu mbalimbali katika maisha,,na kiroho inakua hv wanapoanza kuomba kwa kulia.....
Wale watu warefu wenye mabawa wanashuka na kukaa karibu yao na kuwatazama kwa upendo huku wakiwazunguka pande zote.Lakini wakiendelea kulia zaidi basi mbingu zinafunguka na Mwana wa mmiliki anashuka mwenyewe mpaka chini kuwatazama na wakizidi kulia na yeye analia na kuwaambia NIPO HAPA USILIE ISHI KWA IMANI NIPO HAPA DAIMA.
Na hata kama wapo sehemu tofauti tofauti duniani yeye anajigawa kwa sekunde hiyo hiyo anafika kote.Hakuna kitu kinachomshusha duniani kwa haraka mwana wa mmiliki kama maombi.
Walokole hawajui ila maombi ni silaha kuu sababu chochote utakachokisema kwenye maombi basi kwenye ulimwengu wa kiroho kinatokea hivyo hivyo.
WAKISEMA WANAFUNGA BASI NJIA ZOTE ZOTE ZA ANGA ZINAFUNGWA NA WAKISEMA MOTO KWELI MOTO HUTOKEA NA WAKIIMBA ILE NYIMBO YA ROHO YA MUNGU WAO ISHUKE BASI INASHUKA KWELI NA WINGU ZIIITO LA MWANGA MKALI KULIKO JUA LINAWAFUNIKA MPAKA WAMALIZE MAOMBI.
Mungu wa walokole huwezi kumtizama kwa macho ya kawaida ila anafanana na binadamu kimuonekano ni kama mzee hivi aliyekula chumvi za miaka usoni ila sio kwa ukubwa wa kimwili,,sababu yeye ni mkubwa mno kuliko dunia LAKINI ANASEMA ALIMUUMBA MTU KWA MFANO WAKE KIMUONEKANO ILA SIO KWA SIZE.Mwana wa mmliki na yeye anafanana na binadamu kimuonekano ila na yeye ni mkubwa mno kimuonekano.Na wale watu warefu wenye mabawa wanafanana na binadamu ila ni wakubwa mno kimuonekano..
Basi walokole wakiendelea kulia na kusali anga lote linafunguka na inakua ni uwanja wa mawasiliano kati yao na mwana wa mmliki,ambae anashuka na kukaa nao huku akiwatizama ila wao hawamuoni.
CHA AJABU WATOTO WOTE WA KIBINADAMU WANAMUONA NA WANAONGEA NAE NA KUCHEKA NA ANAWABEBA KIFUANI WAKATI WAKIWA NA WAZAZI WAO AU WALEZI WAO NA HAIJALISHI NI WATOTO WA WALOKOLE AU LA....YEYE MWANA WA MMLIKI NA WALE WATU WAREFU WENYE KUAKISI MWANGA RAFIKI ZAO WAKUBWA NI WATOTO WA KIBINADAMU KUANZIA UMRI WA SIKU MOJA MPAKA MIAKA KUMI NA NNE MPAKA KUMI NA SITA.
NB: KUNA WATOTO WASIO WA KIBINADAMU PIA IKUMBUKWE
Basi walokole wanapomaliza kuomba wanakua hawaoni wala kujua kua wamezungukwa na viumbe vya kiroho vinavyowatizama ila waga wanajihisi amani sana na utulivu wa moyo.Haijalishi kanisa gani wanatokea ila walokole wote wana alama sawa,,iwe wasabato au wakatoliki au waangilikana au walutheri au wapentekoste,,kwa mwana wa mmliki wote ni kitu kimoja na anawalinda sawa sawa.
Wachawi ni wabishi sana ndio wanaoongoza kwa kuwasumbua walokole wakiamini kua walokole ni wachawi kama wao ila wamewazidi maarifa ya kiuchawi.Na ndio wanaoongoza kwa kuwadhuru walokole kimwili.
KUNA ALAMA SABA ZA WALOKOLE KIROHO ZINAONEKANA WAZIWAZI
1: TUNDA LA UPENDO ( NJIWA WA MOTO)
2: WALINZI WATU WAREFU WENYE MABAWA NA PANGA ZA MOTO
3:NDIMI ZA MOTO JUU YA VICHWA VYAO
4: NGUZO ZA MOTTO ZINAZOZUNGUKA
5: WINGU LA MANUKATO NA MOSHI MWEUPE
6:MAGARI YA DERAYA NA FARASI WA MOTO
7:UTIIFU WA MOYO ULIO WAZI KIMUONEKANO KIROHO KWA MUNGU WA WALOKOLE.
Nitaendelea....................!!!!
Mkuu vipi kuhusu kusikiliza nyimbo za gospel kitu Gani Hua kinatokea MTU anapokua anaimba au kusikiliza wimbo wa gospel Uwe wa kuabudu au kusifu....binafsi Hua najikuta nabubujikwa sanyingine nanena Kwa lugha Yan nkiomba huku nimefungulia gospel Hua Naona maombi nakua spiritual zaid tofaut nkiomba bila kufungulia gospel
 
Nikili tu ya kuwa Huu uzi umenifanya nikue kiimani
Maana umenikumbusha mambo mengi sana sana tangu nikiwa mtoto mpaka kijana.
Kuna wakati nilipokuwa nimetekwa kupelekwa mererani kutolewa kafara,
Kuna mambo ya ajabu niliona yakishuka angani kwa macho yangu, kuna siku nikipata muda nitaweka, wakati huo nikiwa mtoto wa miaka 8.
Sio tu hili, nilipishana na makundi ya wanyama hatari kama Nyati, majoka makubwa ambayo yalikuwa yanauwezo wa kunimeza kwa dakika 0, simba, chui, lkn hawakuweza kunidhuru, nilikuwa najiona nipo kwenye kundi la watu wenye moto mkali ambao pumzi zao zinawasukuma na kuwapumbaza wale wanyama. Rohoni nilikuwa nina amani kubwa mnoo japo kuwa nipo katikati ya hatari.

Kupitia andiko hili sasa nimejua mengi
Asante mwandishi[emoji91][emoji91][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom