Mungu Yuko wapi?

Ndio maana nikasema kuamini kuna sababu na dalili zake, hata wewe usiyeamini hizo hekaya za waarabu na wayahudi kuna ambayo unayaamini.
Siamini hekaya yoyote...elewa, ndo maana Sina dini...coz naona zote ni story za watu wa kale tu siwezi ishi maisha yangu According to maisha Yao ya kizamani na ya kuamini vitu vya ajabu Kama dragons giants unicorns angels demons etc
 
Mkuu imani ina sababu za kuamini na ndio maana watu hutofautiana tunavyoviamini, kwahiyo mtu anapoamini jambo fulani anakuwa na sababu za kuamini hilo jambo.

Mimi hapa sizungumzii dini bali nazungumzia neno imani.
Imani ni kuamini kitu bila udhibitisho. Dini pekee ndo imepewa hii haki...nikiamini Leo kwamba usiku nalindwa na wadada wa mwezini wanaoniangalia nitaitwa chizi Ila ukiamini kwamba ukiinama Mara 9 na kuongea kiarabu ndo unaongea na alitengeneza ulimwengu unaitwa muislam...
 
Mkuu pamoja na hizo sababu ulizozieleza bado watu wanahama au kubadili imani moja(ya tokea udogoni) na kuhamia imani nyengine. Kwamba pamoja na kukulia kwenye familia na jamii yenye imani A na kuahidiwa pepo na kutishwa na moto kwenye hiyo imani ila bado anakuja kuacha hiyo imani na kubadili kuwa imani B, kama ingekuwa wanaamini kisa tu kalelewa katika mazingira ya hiyo imani na kutishiwa moto basi tusingeona watu kufikia uamuzi wa kubadili imani ikiwa hakuna sababu na dalili za kuamini imani fulani.
 
Mkuu Naomba unitofautishie haya maneno mawili yani Nadharia na Imani.
 
Siamini hekaya yoyote...elewa, ndo maana Sina dini...coz naona zote ni story za watu wa kale tu siwezi ishi maisha yangu According to maisha Yao ya kizamani na ya kuamini vitu vya ajabu Kama dragons giants unicorns angels demons etc
Ni tatizo tu katika uelewa kwa sababu hata kusingekuwa na dini kabisa wala habari za Mungu/miungu bado hilo neno imani lingetumika katika maisha ya kila siku ya watu.

Kusema mtu fulani namuamini au sina imani nae, kuamini utafanikiwa, kuamini utashinda.

Hayo mambo hayahusiani na dini ila ni katika mambo ambayo yapo kila siku kwenye maisha yetu.
 
Ushawahi skia mtanzania anatoka kuwa mkristo anakuwa mhindu au mbudha, au anaamini Zeus au mithra. If not elewa maana yangu ya dini ambazo zipo katika jamii yetu ambazo ni Christian na Muslim. Dunia Ina dini zaidi ya 10k...ukiona wabongo wanahama ni Kati ya hizi mbili na sio coz wanaamini chochote ni kutafuta wepesi katika kuishi, ndoa, ajira au siasa. Prove me wrong
 
Wangapi wamelala na hawakuamka?
 
Wangapi wamelala na hawakuamka?
Kuna watu zaidi wanalala na kuamka kuliko watu ambao wameona mbingu na Moto. So mtu mwenye akili timamu anajua ana chance kubwa kuamka kesho kuliko kwenda sehemu fikirishi baada ya kufa
 
Believing sio sawa na faith. Trust sio sawa na faith.. kiswahili kina maneno machache na we unajua Hilo...Kuna maneno mengi ya kingereza yenye maana tofauti kidogo Ila kiswahili wamefanya ni neno moja.. so tumia context ya kingereza uelewe. Mi kumuamini Mtu ambae yupo na ninaona anachofanya ni tofauti na kuamini hekaya za waarabu kuhusu mtu aliyetokewa na malaika pangoni na kuongea nae kiarabu... Hata we unaweza ona tofauti hapo
 
Kama yupo ndani yako huyo si Mungu huyo ni akili yako na fikra zako na ukifa na ye anakufa
Watu wanapenda kujidanganya kwamba wanajua kila kitu.

Na pale ambapo hawana jibu, wanapenda kuweka jibu la Mungu, ambaye hayupo.

Nia yao wawe na jibu tu, hata kama si la kweli.

Hawataki kukosa jibu.

Ukiwauliza maswali kuhusu mambo ambayo hawana majibu, kama kifo, waseme "kazi ya Mungu, haina makosa".

Dhana ya kuwepo Mungu ni hadithi ya kutunga ili liwepo chaka la kutupia maswali yote ambayo hatuna majibu yake.

Halafu tukipata majibu, tunayatoa katika chaka hilo polepole.

God of the gaps.

Ndiyo maana jamii zilizopiga maendeleo ya kielimu kama Ulaya ya Kaskazini, watu wanaacha kumuamini huyu Mungu kwa kasi kubwa sana.

Hawahitaji hili chaka tena, elimu yao imeondoa maswali mengi kutoka kwenye hili chaka.

Wakati huohuo, jamii ambazo zina matatizo ya elimu kama Africa, imani ya Mungu iko juu sana.

Mtu wa Ulaya Kaskazini anapata elimu kirahisi, anajua mengi, akiumwa ana mfumo wa afya ya jamii anaoweza kuutegemea. Hahitaji kuomba Mungu.

Wewe mtu masikini wa Africa, huna elimu, huna huduma bora za afya, ukiumwa ni lazima uombe Mungu tu.
 
Waarabu ni matajiri sana ila sidhani kama waislamu wa afrika wanawafikia waarabu kwa imani ya Mungu, hakuna muarabu anayetoka huko arabuni kuja kujifunza dini afrika bali tunaona waafrika ndio wanaenda huko kwa matajiri kujifunza masuala ya Mungu.

Mtu kama Professor Assad asingekuwa bado anaamini Mungu ukizingatia elimu anayo na hana umasikini wa kukosa chakula na huduma bora ya afya. Na wapo wengi kama Prof Assad.
 
Tofauti inakuja kwenye nini? Maana umetoka kusema kwamba imani(faith) ni kuamini(kukubali) kitu bila uthibitisho, haya hebu eleza huko kuamini unayemuona na kuona anachofanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…