Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

"Siyo kila anayemuamini Mungu yupo, anamwamini Mungu", Rudi la kwanza ujifunze kuandika ukimaliza ndo uje ueleweke naona unatype shit tu hapa
Umemnukuu nani? Mimi sujaandika hivyo! Kama unafikiri meandika hivyo, soma vizuri
 
Ushawahi kumuona jibu swali?
Jibu lolote nitakalokupa haliwezi kukusaidia. Nafikiri, lengo lako kuu ni kubisha. Huna Nia ya kujifunza. Sioni afya kuenedelea kuuchangia huu uzi. Maadam umeamua kubisha huku ukijua unachokifanya, Bora Mimi niendelee na mambo mengine.

Mwanzoni nilifikiri ulikuwa unataka kujifunza kutoka kwa wengine, lakini kutokana na mwenendo wa majibu yako, ni dhahiri kuwa lengo kuu ni ubishi, jambo ambalo kwa wengine ni kama kupoteza muda.
 
Hata nikikujibu, haitakuwa na msaada wowote kwako. Nimeshajieidhisha kuwa lengo lako si kufahamu, ni kubisha. Sioni sababu ya kuendelea kubishana kwa jambo ambalo mtu ameshafanya maamuzi yake.

Wewe umeshaamua ulivyoamua, kwa hiyo naona kama ni kupoteza muda kuendelea kukuelekeza kitu ambacho ulishaamua unavyotaka iwe.

Ingelikuwa ni mtu ambaye lengo lake ni kujifunza, ingekuwa sawa. Lakini kwa mtu ambaye anafahamu anachokifanya, kuwa anabisha kwa lengo la kuhakikisha kuwa alichoamua linakuwa
Basi skia ukimwona niletee na Mimi sawa nataka niongee nae. Naona una bwabwaja
 
Ni maneno ya Mungu? Una uhakika ni maneno ya Mungu na si maneno ya wayahudi wa kale waliosema hivyo ili kutishia na kutawala watu wafate sheria zao? Una uhakika Hilo ziwa la moto lipo?
Kwani Mungu wako wewe anasemaje? hakuna ziwa la moto?
 
Kwani Mungu wako wewe anasemaje? hakuna ziwa la moto?
Sina Mungu, sijawahi skia maneno ya Mungu na sijawahi pata ushahidi wa Hilo ziwa la moto, so siwezi amini kuwa ni ya kweli
 
Utajiri mtu anaweza kupata hata kwa bahati nasibu tu.

Unapinga hilo?

Nitajie jamii ya watu walio na umasikini mpaka wamemsahau Mungu kwa umasikini wao, mimi siongelei watu mmoja mmoja, naongelea jamii za watu.
Nimeshaeleza kwamba point sio wamepataje utajiri bali hawana changamoto za umasikini ambazo masikini wanazo.
 
Nimeshaeleza kwamba point sio wamepataje utajiri bali hawana changamoto za umasikini ambazo masikini wanazo.
Nani kakupa wewe cheo cha kuamua point ni ipi?

Hujathibitisha Mungu yupo.

Hujaondoa contradictions zilizopo katika dhana ya kuwapo Mungu.

Kwa sababu Mungu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo na ondoa contradictions hizo.
 
Huna Mungu una nini? Unadhani kwanini waliokutangulia walifikia maamuzi kuwa pawepo na imani ya uwepo wa Mungu?
Hawakuwa na maarifa niliyonayo now. Leo hii huamini jua kuzunguka dunia au jua kuzama kwenye tope, Wala huamini mbinguni ni mawinguni unaweza enda na farasi wa kupaa au mvua Ni maji ya mbinguni. Kulikuwa na haja ya Imani kipindi hicho coz watu hawakujua vitu vingi. Lakini kusema vitu hivyo ndo maneno ya Mungu na hayabadiliki, ndo walipokosea.
 
Hawakuwa na maarifa niliyonayo now. Leo hii huamini jua kuzunguka dunia au jua kuzama kwenye tope, Wala huamini mbinguni ni mawinguni unaweza enda na farasi wa kupaa au mvua Ni maji ya mbinguni. Kulikuwa na haja ya Imani kipindi hicho coz watu hawakujua vitu vingi. Lakini kusema vitu hivyo ndo maneno ya Mungu na hayabadiliki, ndo walipokosea.
Watu wa zamani hawakuwa na maarifa uliyonayo ndo maana wakawa na imani kuwa yupo MUNGU na sasa wewe huamini uwepo wa MUNGU sababu umewazidi maarifa. Okey, embu tuambie kwa kutumia hayo maarifa waliyoyakosa wazee wetu, hakuna MUNGU kuna nini?
 
Nani kakupa wewe cheo cha kuamua point ni ipi?

Hujathibitisha Mungu yupo.

Hujaondoa contradictions zilizopo katika dhana ya kuwapo Mungu.

Kwa sababu Mungu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo na ondoa contradictions hizo.
Kusema hakuna MUNGU bila kusema kuna nini ni sawa na hawa chawa ndani ya ngozi ya mbwa wakitaka uthibitisho kuwa kuna Mbwa.

Screenshot_20230614-064804_Facebook.jpg
 
Watu wa zamani hawakuwa na maarifa uliyonayo ndo maana wakawa na imani kuwa yupo MUNGU na sasa wewe huamini uwepo wa MUNGU sababu umewazidi maarifa. Okey, embu tuambie kwa kutumia hayo maarifa waliyoyakosa wazee wetu, hakuna MUNGU kuna nini?
Kuna Nini kivipi Tena?
 
Kusema hakuna MUNGU bila kusema kuna nini ni sawa na hawa chawa ndani ya ngozi ya mbwa wakitaka uthibitisho kuwa kuna Mbwa.

View attachment 2663728
So Mungu ni dunia au ..Kama Mungu ni dunia Sayansi imetufanya tuone dunia nzima kuwa ni round kupitia picha za satellite na sio vitabu vya dini ambavyo hawakujua dunia ipoje. So kama umemtumia chawa na mbwa basi Mungu ni dunia. Haya kakuambia ukifa unaenda mbinguni au Motoni, kakuambia anataka umuabudu, kakuambia anataka Nini, kakuambia sifa zake, why uassume, why utunge story, why utishie watu,
 
So Mungu ni dunia au ..Kama Mungu ni dunia Sayansi imetufanya tuone dunia nzima kuwa ni round kupitia picha za satellite na sio vitabu vya dini ambavyo hawakujua dunia ipoje. So kama umemtumia chawa na mbwa basi Mungu ni dunia. Haya kakuambia ukifa unaenda mbinguni au Motoni, kakuambia anataka umuabudu, kakuambia anataka Nini, kakuambia sifa zake, why uassume, why utunge story, why utishie watu,
Kwa hiyo tatizo lako si imani ya uwepo wa MUNGU ni uwepo wa dini inayoamini uwepo wa mwisho wa dunia na adhabu? Dini huja baada ya imani ya uwepo wa MUNGU.

Imani ya uwepo wa MUNGU ipo sababu hakuna kiumbe kinachofahamu siri ya uumbaji, kama wewe unaijua hiyo siri njoo ufute imani ya uwepo wa MUNGU.

Huo mfano wa Chawa wanaosema hakuna Mbwa sababu hawana maarifa na uwezo wa kumwona ni sawa na yoyote asemaye hakuna MUNGU sababu hana uwezo na maarifa ya kumwona.

Ukisema hakuna MUNGU sema kuna nini sio uje na porojo. Binadamu hawezi kuacha imani yenye matumaini ya uwepo wa nguvu ya MUNGU kama chanzo cha yote tuliyoyakuta wafuate porojo kutoka kwa kiumbe dhaifu unayekisubiri kifo ambacho hata hufahamu ni nini.
 
Hakuna MUNGU kuna nini? Nini chanzo cha haya tuliyoyakuta baada ya kuzaliwa?
Kama hujui kitu chake ni Mungu si ndio...Kama hujui nani kaiba mkoba wako jibu litakuwa Mungu mpaka umpate aliyekuibia, kama hujui rais wa Nicaragua ni nani anakuwa Mungu mpaka ujue rais wa Nicaragua ni nani ndo anaacha kua Mungu, hii Ni argument from ignorance, Kama kitu hukijui unakitafuta mpaka upate jibu hauanzi na kukipa jibu na kusema Hilo tu ndo jibu, hii sio logic na ni dhana ya kivivu katika kufikiria na kujenga hoja katika mdahalo wowote
 
Kwa hiyo tatizo lako si imani ya uwepo wa MUNGU ni uwepo wa dini inayoamini uwepo wa mwisho wa dunia na adhabu? Dini huja baada ya imani ya uwepo wa MUNGU.

Imani ya uwepo wa MUNGU ipo sababu hakuna kiumbe kinachofahamu siri ya uumbaji, kama wewe unaijua hiyo siri njoo ufute imani ya uwepo wa MUNGU.

Huo mfano wa Chawa wanaosema hakuna Mbwa sababu hawana maarifa na uwezo wa kumwona ni sawa na yoyote asemaye hakuna MUNGU sababu hana uwezo na maarifa ya kumwona.

Ukisema hakuna MUNGU sema kuna nini sio uje na porojo.
Soma message yangu kuhusu kutokujua kitu. Kusema kwamba god did it, instead of kutafuta jibu ni dhana ya kivivu wa kufikiria
 
Back
Top Bottom