Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Hivyo ni visingizio ili usikosoe dini, Mara hoo Mungu hachunguzwi, 🤣ujinga mtupu...kiumbe chenye nguvu kuliko kingetengeneza dunia isiyo na dhambi na shida, na Kama anatujali na anajua yote hamna haja ya kuumba watu afu awachome baadae, Mungu wa hivi ni wa kutungwa ili watu waogope watoe sadaka na kufata sheria za waliotunga, Mungu anajali unamwaga wapi kweli
Mungu aliiumba dunia safi isiyo na dhambi, akamkabidhi mwanadamu aitawale kwa niaba Yake. Kwa maneno mengine, Mungu alimfanya mwanadamu kuwa mungu wa dunia hii. Kila kitu alikiweka chini yake. Alimpa mwanadamu mamlaka kamili juu ya ulimwengu wote. Zaburi 115:16.

Shetani alipofanikiwa kumdanganya mwanadamu, alimpindua Adamu kwenye nafasi yake ya kuwa mungu wa dunia hii, badala yake, yeye Shetani ndiyo akawa mungu wa dunia hii. 2Wakorintho 4:4.

Jehanamu haijaandaliwa kwa ajili ya mwanadamu. Ni kwa ajili ya Shetani. Ikiwa mwanadamu ataenda motoni, si kwa sababu Mungu kampeleka huko, ila kachagu yeye mwenyewe kwa kuamua kutokumwamini Mungu.

Kukataa kumwamini Mungu ni kuchagua kumfuata Shetani kwa hiari.

Mungu anawapenda watu wote, hata wanaokataa kumwamini. Japo kumkataa Mungu kutampelekea mtu kuishia Jehanamu ya milele, hakumfanyi Mungu kumchukia.

Mungu anayaheshimu maamuzi ya kila mtu. Ndiyo maana amemjulisha mwanadamu faida ya kumwamini Yeye na hasara ya kutokumwamini. Hampangii mtu, anachofanya ni kukujulisha faida na hasara na kukuacha uchague mwenyewe kumfuata kwa faida yako au kumkataa kwa hasara yako. Kumbukumbu la Torati 30:19-20.

Mungu hachomi watu. Mungu hapeleki watu motoni. Mtu akienda motoni ni kwa sababu kachagua yeye mwenyewe kwa kukataa kumwamini Mungu.
 
Ni kweli, Mpagani si mtu asiye na dini, hata kuiabudu mizimu ni dini.

Ndiko nilikoanzia, kwenye dini ya asili. Kabla ya kuwa Mkristo, nilikuwa nikishiriki hata ibada za kipagani. Nakumbuka, nilishawahi kuhudhuria tukio ambalo kabla ya jambo lolote kufanyika, kulifanyika maombi kwanza. Maombi yalielekezwa kwa mti. Kwamba, mti ndiyo uliokuwa kama mungu.

Lakini baadaye nilikuja kugundua kuwa kuna Mungu MKUBWA kuliko mababu zetu. Nilipogundua huo utofauti, niliamua kuachana na kamungu na kumfuata MUNGU MKUU!!!

Kuwepo kwa madhehebu mengi si tatizo, muhimu tu wawe wanamwamini Kristo. Hata kukiwepo na madhehebu bilioni kumi, kama wanamwamini Kristo, wote watakuwa ni Wakristo.

Wakristo wa Kweli wanajulikana. Hata humu jukwaani, bila shaka, kuna nyuzi ambazo kwa kuzisoma tu, unajua huyo ni Mkristo au la.

Kwani wewe unashindwa kumfahamu Mkristo wa Kweli? Mbona ni rahisi tu! Hata Shetani hasumbuki kumtofautisha Mkristo wa Kweli na anayeuigiza Ukristo. Mkristo wa Kweli anafahamika, si makanisani tu, hata katika maeneo mengine. Imeandikwa, "Mtawatambua kwa matendo yao"

Hao waliogeka atheist mimi siwafahamu! Ukweli ni kuwa mtu akishaouonja utamu wa Kristo, hatatamani tena kitu kingine.
Kama kuna waliokuwa wakienda , labda makanisani lakini baadaye wakaamua kugeukia uatheist, ni kwa sababu hawajawahi kukutana na Mungu Halisi mioyoni mwao. Waliingia kwenye dini kwa kufuata mkumbo. Hawakumwamini Mungu!
Why we ndo unaamua nani mkristo wa kweli na sio wa kweli, we Kama nani, ni sawa na kusema Kama we hufaulu shule we sio mwanafunzi wa kweli, unalazimisha hoja yako iwe juu, we onja utamu hata watoto wadogo wamaenjoy kuambiwa wameokotwa baharini na wamenunuliwa dukani Ila wakikuwa wanajua ukweli wametoka wapi. Assume Mimi ndo nimekuwa kifikra nimeachana na story za kuambiwa na mababu
 
Hujiulizi why vinatokea kigoma a place ambao Ina watu wenye low level of economic status na low level of education. Why not Moshi, dar, Arusha na bukoba. Why places za tanga, sumbawanga, shinyanga na kigoma places zenye watu wenye maisha duni na wasio na elimu
Ni viwango tu ndiyo vinatofautiana. Hata Dar , Arusha, Bukoba, Moshi n.k. kuna ushirikina na kuna wanaoamini katika Mungu.
 
Why we ndo unaamua nani mkristo wa kweli na sio wa kweli, we Kama nani, ni sawa na kusema Kama we hufaulu shule we sio mwanafunzi wa kweli, unalazimisha hoja yako iwe juu, we onja utamu hata watoto wadogo wamaenjoy kuambiwa wameokotwa baharini na wamenunuliwa dukani Ila wakikuwa wanajua ukweli wametoka wapi. Assume Mimi ndo nimekuwa kifikra nimeachana na story za kuambiwa na mababu
Nimeteuliws na nani na lini kuwaainisha Wakristo wa Kweli na wasio wa Kweli?

Ni wapi nilikosema mimi ndiye ninayeamua nani Mkristo wa Kweli na kinyume chake?

Sijawahi kupewa hilo jukumu na wala sijawahi kusema nina hayo mamlaka.
 
Unataka nikueleze? Utanielewa? Hautaanza kuleta ubishi? Lengo lako ni kuelewa au kutafuta kupinga?

Nitakuambia! Mungu alipomwumba mwanadamu, alimwumba katika hali ya ukamilifu. Asingeweza kuugua wala kufa. Lakini kupitia anguko la Adamu, dhambi iliingia duniani. Kitu kinachoitwa Sheria ya dhambi na mauti ikaingia duniani. Warumi 8:1-2.

Hiyo ndiyo sababu mojawapo ya kuwepo kwa magonjwa.

Lakini pamoja na hayo, Mungu hajawaacha watu Wake bila ya msaada. Madhalani, kwa upande wa magonjwa, mtu anaweza kupata msaada, ama kwa njia ya kutibiwa na madaktari, au kwa kuamua kumwamini Mungu akapokea uponyaji.

Madaktari wana usemi wao usemao, "Sisi tunatibu, lakini Mungu Ndiye anayetibu". Hata madaktari wanajua kuwa Mungu ni Mponyaji.

Magonjwa hayatoki kwa Mungu! Mungu ni Mponyaji!!!
1. Magonjwa hayatoki kwa Mungu? Ye anajua yote anaweza yote na anatupenda, why Kuna magonjwa? Kwa Nini hayazui?
2. Hiyo story ya Adam na Eve imetungwa kuelezea mambo yameanzaje na pia imeibwa ideas from epic of Gilgamesh ya mesapotemia na Pandora's box ya ugiriki na pia haina ushahidi wa kihistoria.
3. Madaktari mpaka wanalipwa mamillion kufanya upasuaji ni kwa sababu wagonjwa wanamshukuru Mungu badala ya kuwashukuru wao ambao wamesoma miaka 7 na kufanya upasuaji masaa 20 ili we upone, so ni Kama hasira coz anafanya kazi kubwa bila kupewa shukrani.
4. Mungu ni kama group partner ambae kazi unafanya wewe ukikosea anakulaumu ukipatia sifa anachukua yeye ni kama mpenzi ambae anakuonea(abusive husband)
 
Hiyo imeitofautishaje na Tanzania? What's the difference?
Marekani Kuna atheists wengi kuliko Tanzania. So kusema kwamba ni watu wa dini Sana it's not realistic coz kule mpaka wanakuwa na public debates kuhusu atheism na religion na atheists wanapewa freedom kutoa views zao.
 
Kwani Mzungu hana dini? Unajua Tanzania hain dini lakini Marekani ina dini? Unafahamu Marekani ni Taifa la Kidini?

Pamoja na kwamba wamegundua dawa za Corona, na vitu vingine vingi, bado pia wanaamini katika Mungu.

Unafahamu kuwa Marekani inayo mpaka siku ya Kitaifa ya Maombi?

Wamarekani wenyewe wanaamini kuwa wao kuwa Super Power duniani ni kwa sababu wanamwamini Mungu. Japo siku hizi idaidi ya wanaoamini katika Mungu nchini Marekani inapungua, bado ni Taifa lenye watu wengi wanaomwamini Mungu.

Umeshawahi kuiona noti ya dola ya Marekani? Imeandikwaje?
"In God We Trust" Tusaidie tafsiri ya hiyo sentensi kwa Kiswahili, tafadhali.

Wana na kauli yao maarufu isemayo, GOD WE TRUST, BUT MONEY WE AUDIT! Ukiweza, utusaidie na hii pia tafsiri yake kwa Kiswahili.

Ujue tu kuwa Mungu hajawazuia watu kutumia akili. Ndiyo maana kawapa watu akili.

Kumwamini Mungu hakumwondolei mtu wajibu wa kuitumia akili yake panapohitajika kutumia. Mungu anataka watu Wake watumie kwa usahihi akili alizowapa ili wafanye mambo makubwa mazuri.
Acha uwongo marekani sio taifa ka kidini na sheria zake hazifavour dini yoyote ndo maana ya 1st amendment kwenye katiba Yao. Ndo maana Wana ruhusu abortion, ushoga, pornography, etc coz wanavalue individual freedom na sio religion. Tanzania ni nchi ya kidini kuliko marekani in terms of sheria, ila tunatumia mwamvuli wa "utamaduni wetu" ili tusiseme tu tunafata dini. Marekani hawaruhusu kusali kwa lazima shuleni, na kuanzisha vipindi vya dini katika shule za serikali. Wazungu ambao wanafanya uvumbuzi katika Karne ya 21 ni wanasayansi ambao wengi hawana dini kwa sababu wametumia logic na reason kugundua kua dini zote ni story tu za kale za mababu wa jamii fulani na hamna moja special kuliko wenzako so wanazitreat Kama tamaduni tu na kuzipa heshima.
 
1. Magonjwa hayatoki kwa Mungu? Ye anajua yote anaweza yote na anatupenda, why Kuna magonjwa? Kwa Nini hayazui?
2. Hiyo story ya Adam na Eve imetungwa kuelezea mambo yameanzaje na pia imeibwa ideas from epic of Gilgamesh ya mesapotemia na Pandora's box ya ugiriki na pia haina ushahidi wa kihistoria.
3. Madaktari mpaka wanalipwa mamillion kufanya upasuaji ni kwa sababu wagonjwa wanamshukuru Mungu badala ya kuwashukuru wao ambao wamesoma miaka 7 na kufanya upasuaji masaa 20 ili we upone, so ni Kama hasira coz anafanya kazi kubwa bila kupewa shukrani.
4. Mungu ni kama group partner ambae kazi unafanya wewe ukikosea anakulaumu ukipatia sifa anachukua yeye ni kama mpenzi ambae anakuonea(abusive husband)
Mtafute daktari yeyote mwenye akili umwulize kuhusu Mungu. Naamini atakusaidia pa kubwa sana.
 
Kuamini kuwa Mungu Yupo ni jambo moja. Na watu wengi wanaliamini hilo. Hata Shetani na mapepo yote yanaamini hivyo pia, tena, wanaamini mpaka wanatetemeka.

Lakini kuamua kumwamini Mungu ni jambo jingine. Siyo kila anayeamini Mungu Yupo anamwamini Mungu. Lakini hakuna anayemwamini Mungu asiyeamini kuwa Mungu Yupo.

Suala la kumwamini Mungu si kwa ajili ya maisha ya baadaye tu, baada ya kufa , bali ni kuanzia sasa. Amwaminiye Mungu hunufaika katika maisha ya sasa na ya baadaye.
"Siyo kila anayemuamini Mungu yupo, anamwamini Mungu", Rudi la kwanza ujifunze kuandika ukimaliza ndo uje ueleweke naona unatype shit tu hapa
 
Wazinzi, walevi, wasengenyaji, Sehemu yao ni ziwa la moto. Haya ni maneno yangu?
Ni maneno ya Mungu? Una uhakika ni maneno ya Mungu na si maneno ya wayahudi wa kale waliosema hivyo ili kutishia na kutawala watu wafate sheria zao? Una uhakika Hilo ziwa la moto lipo?
 
Umetumia methodology gani kwenye hizo tafiti? Wewe unaweza kumtafiti Mungu?

Vipi na mtoto aliyeko tumboni naye akisema hakuna mtu kama yeye kwa vile tu hajamwona, itahesabiwa kuwa ni Kweli?

Mungu hana njaa ya wewe kujua kuwa Yupo. Usipomtambua ni hasara yako.
Sijamtafiti Mungu coz hayupo, we umemtafiti Babu Christmas? Unajuaje hayupo? Nimetafiti story ambazo wanaziita ni za Mungu za dini tofauti tofauti. Angalia movie inaitwa religulous utaelewa.
 
Mungu aliiumba dunia safi isiyo na dhambi, akamkabidhi mwanadamu aitawale kwa niaba Yake. Kwa maneno mengine, Mungu alimfanya mwanadamu kuwa mungu wa dunia hii. Kila kitu alikiweka chini yake. Alimpa mwanadamu mamlaka kamili juu ya ulimwengu wote. Zaburi 115:16.

Shetani alipofanikiwa kumdanganya mwanadamu, alimpindua Adamu kwenye nafasi yake ya kuwa mungu wa dunia hii, badala yake, yeye Shetani ndiyo akawa mungu wa dunia hii. 2Wakorintho 4:4.

Jehanamu haijaandaliwa kwa ajili ya mwanadamu. Ni kwa ajili ya Shetani. Ikiwa mwanadamu ataenda motoni, si kwa sababu Mungu kampeleka huko, ila kachagu yeye mwenyewe kwa kuamua kutokumwamini Mungu.

Kukataa kumwamini Mungu ni kuchagua kumfuata Shetani kwa hiari.

Mungu anawapenda watu wote, hata wanaokataa kumwamini. Japo kumkataa Mungu kutampelekea mtu kuishia Jehanamu ya milele, hakumfanyi Mungu kumchukia.

Mungu anayaheshimu maamuzi ya kila mtu. Ndiyo maana amemjulisha mwanadamu faida ya kumwamini Yeye na hasara ya kutokumwamini. Hampangii mtu, anachofanya ni kukujulisha faida na hasara na kukuacha uchague mwenyewe kumfuata kwa faida yako au kumkataa kwa hasara yako. Kumbukumbu la Torati 30:19-20.

Mungu hachomi watu. Mungu hapeleki watu motoni. Mtu akienda motoni ni kwa sababu kachagua yeye mwenyewe kwa kukataa kumwamini Mungu.
According to ur story
1. Why Mungu ameumba Malaika ambae alijua beforehand atakuja kuwa shetani na atakuja kutesa watu, Kama kweli ni muweza yote mjua yote na mpenda wote asingeruhusu Hilo.
2. Kulikuwa na haja Gani ya kuweka matunda ambao angewakataza kula na anajua watakula afu awaadhibu wao na uzao wao. Ni sawa na mwalimu ampe mtoto mtihani mgumu ambao anajua atafeli afu ampe adhabu Kali
3. Shetani alikuwa anafanya Nini katika bustani Ile, Mungu mweza yote na mjua yote asingeruhusu Hilo ni either alikuwa Hana Nia njema na binadamu au alikuwa Hana uwezo wa kumzidi shetani.
4. Why Mungu awaadhibu uzao mzima kwa kosa la watu wawili. Je Ni haki Kama baba kaua na wewe ukizaliwa unyogwe pia?
5. No matter how u look at it hii story haimake sense kwa akili ya kawaida ndo maana wakristo wengine hukimbilia kusema ni mafumbo
 
Nimeteuliws na nani na lini kuwaainisha Wakristo wa Kweli na wasio wa Kweli?

Ni wapi nilikosema mimi ndiye ninayeamua nani Mkristo wa Kweli na kinyume chake?

Sijawahi kupewa hilo jukumu na wala sijawahi kusema nina hayo mamlaka.
Basi usiseme kwamba huyu mkristo wa kweli huyu sio ..
 
Back
Top Bottom