Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Mi najiuliza maswali mengi. Mungu Ni Nini, anataka Nini na Yuko wapi.

Ukifuatilia historia ya binadamu tokea tukiwa wawindaji maporini miungu ilikuwepo. Wazee walikuwa wanaongoza vijana kwa kuwaambia kuwa Mungu anataka mfanye hivi, na hio miungu ilikuwepo pangoni ambapo wazee tu wanaingia, baadae vijana wakajitoa akili kwenda wakaona wazee ni waongo na hamna kitu mule. Wagiriki wakaja na miungu yao wakasema ipo ya milima ya Olympus, Leo hii watu wamepanda milima yote ugiriki hawajaona miungu hio.

Wakaja wayahudi, wakasema Mungu yupo mawinguni. Ukifuatilia hata Yesu alipaa mawinguni, Mungu alifungua madirisha ya mbinguni kuleta mafuriko, alichungulia kutoka mawinguni kwenye mnara wa babel, etc. Waislamu nao wakaja na mbingu Saba sijui. Anyways wazungu wametengeneza ndege na rocket zimeenda mawinguni, nje ya dunia, mpaka mwezini. Sasa hivi watu wa dini wanasema yupo nje ya ulimwengu.

So nikagundua trend, wanamficha, wanamweka mbali ili watu wasiweze kumfikia, why? Kwa sababu hayupo? Kwa sababu hajasema hizo sheria? Why wanamficha. Afu wanakuambia anataka uamini yupo ndo utapona usipoamini unaunguzwa. Ukiuliza nikimwona afu nikamwamini, anasema no, lazma usimwone ndo uamini. Na wanaweka kifo mwisho wa kumuani ili waweze kuendelea kutunga sheria kwa jina lake na kuweza kuendelea kutawala watu kwa sababu hamna mtu Ashawahi kurudi akasema baada ya kifo kipo hivi.

Mwanasayansi mi nauliza Mbinguni Kuna Nini. Hamna njaa hamna maumivu hamna ndoa hamna chochote zaidi ya kumuabudu Mungu. Watu kanisani na msikitini hawapendi kwenda unategemea watapenda milele ya Ibada. So wakaamua kuanzisha motoni kutishia watu kwamba wataunguzwa milele. Sasa, ukifa unaacha mwili wako hapa, wanasema una roho, roho ni Nini, hoo mawazo sijui pumzi, ukiuliza unajua kazi ya ubongo ni Nini mtu hajui, haya tufanye roho ni ka upepo kanaenda motoni ehe kanaunguaje, hakana nyama, hakana nervous system hakana ngozi, hakana pain receptors, hakana ubongo au spinal cord, maumivu unayasikiaje, na bado hatujauliza huu Moto upo wapi, walisemaga chini kisa mavolcano lakini now hawasemi Tena coz of elimu.

Tukienda kwenye sheria zenyewe sijui usivae nguo tofauti, usile shellfish, usichanganye mazao, usimwage nje, usiabudu sanamu lakini abudu kitu Cha kufikiriwa na myahudi, hivi kwa Nini mtu atengeneze nyota billion 60 na sayari trillion afu aje kujali binadamu wewe ambae ni Kama vumbi kwa huu ulimwengu unamwaga wapi. Na kwa Nini sheria hizi zinaonekana Kama sheria za kabila ya la zamani huko kwenye majangwa na haziendani na sheria za binadamu kuishi na watu vizuri. Na Wanavyosema tumuabudu siku ya Saba.

Siku zimekuja kutengenezewa baadae Sana na zimebadilika badilika Mara kwa Mara katika historia ya Mayans na Romans. Na wamechagua sun day coz ni siku ya pagans kuabudu jua. Ila yote haya tuyaache, why Mungu muweza yote anataka hela, mwisho wa siku wote mnabidi mgundue kuwa binadamu walitengeneza miungu ili kujibu maswali magumu yasiyojibika kipindi kile na ku
Wewe sio mwili wewe ni nafsi yaani roho... Kama unabisha sema Mungu yupo ukiwa umefumba mdomo.....


Baada ya kutekeleza hilo zoezi mtafute nani aliye sema hivyo ilijali wewe umefumba mdomo wako ujakenue hata punje ya jino lako moja kuonekana nje.... Ukimpata aliye sema hivyo njoo kwenye huu uzi unitag ukimkosa tena sema huku umefumba mdomo kuwa mimi ni mbumbavu... Afu mtafute tena nani kasema Mpaka umpate....
 
Kuna watu zaidi wanalala na kuamka kuliko watu ambao wameona mbingu na Moto. So mtu mwenye akili timamu anajua ana chance kubwa kuamka kesho kuliko kwenda sehemu fikirishi baada ya kufa
Ndio hauna uthibitisho wala uhakika wa kuamka hiyo kesho, ukisema una chance tena kubwa ya kuamka kesho itabidi utupe sababu za msingi za kuwa na hiyo chance huwezi kusema et kwa sababu nimeona wengi waliyolala na kuamka.
 
Hivi jamani naomba kuuliza kile kilichotokea brazili baada ya kumziaki YESU na kumtukuza shetani ilikuwa ni mambo ya hali ya hewa tu ya liangukia siku Ile au ni MUNGU mwenyewe alishusha Ile dhoruba

Maana naona watu hawazingatii kabisa hili swala yani
 
Watu wanapenda kujidanganya kwamba wanajua kila kitu.

Na pale ambapo hawana jibu, wanapenda kuweka jibu la Mungu, ambaye hayupo.

Nia yao wawe na jibu tu, hata kama si la kweli.

Hawataki kukosa jibu.

Ukiwauliza maswali kuhusu mambo ambayo hawana majibu, kama kifo, waseme "kazi ya Mungu, haina makosa".

Dhana ya kuwepo Mungu ni hadithi ya kutunga ili liwepo chaka la kutupia maswali yote ambayo hatuna majibu yake.

Halafu tukipata majibu, tunayatoa katika chaka hilo polepole.

God of the gaps.

Ndiyo maana jamii zilizopiga maendeleo ya kielimu kama Ulaya ya Kaskazini, watu wanaacha kumuamini huyu Mungu kwa kasi kubwa sana.

Hawahitaji hili chaka tena, elimu yao imeondoa maswali mengi kutoka kwenye hili chaka.

Wakati huohuo, jamii ambazo zina matatizo ya elimu kama Africa, imani ya Mungu iko juu sana.

Mtu wa Ulaya Kaskazini anapata elimu kirahisi, anajua mengi, akiumwa ana mfumo wa afya ya jamii anaoweza kuutegemea. Hahitaji kuomba Mungu.

Wewe mtu masikini wa Africa, huna elimu, huna huduma bora za afya, ukiumwa ni lazima uombe Mungu tu.
Umegusa mule mule yaani Asante.
 
Ni sahihi kabsa ulivyofikiri kulinganisha na ulicho aminishwa .
Sijaaminishwa...Mungu Kama ni mmoja kwa Nini kila mtu anakuja na yake. Ni kitu ambacho ukikaa mwenyewe unaweza fikiria ukajua ni uvushaji tu
 
Waarabu ni matajiri sana ila sidhani kama waislamu wa afrika wanawafikia waarabu kwa imani ya Mungu, hakuna muarabu anayetoka huko arabuni kuja kujifunza dini afrika bali tunaona waafrika ndio wanaenda huko kwa matajiri kujifunza masuala ya Mungu.

Mtu kama Professor Assad asingekuwa bado anaamini Mungu ukizingatia elimu anayo na hana umasikini wa kukosa chakula na huduma bora ya afya. Na wapo wengi kama Prof Assad.
Nitajie nchi ya kiislamu ambayo haina mafuta na haina partnership na marekani afu Ina maendeleo na amani. Ukipata, niite mbwa nimekaa pale.
 
Tofauti inakuja kwenye nini? Maana umetoka kusema kwamba imani(faith) ni kuamini(kukubali) kitu bila uthibitisho, haya hebu eleza huko kuamini unayemuona na kuona anachofanya.
Mi Nikiona mtu ni mwizi mwizi sitamuamini katika vitu vyangu coz najua ye Ni mwizi. Ila we unaamini kitu ambacho hakina uthibitisho wowote tofauti ndo hiyo.
 
Ushawahi skia mtanzania anatoka kuwa mkristo anakuwa mhindu au mbudha, au anaamini Zeus au mithra. If not elewa maana yangu ya dini ambazo zipo katika jamii yetu ambazo ni Christian na Muslim. Dunia Ina dini zaidi ya 10k...ukiona wabongo wanahama ni Kati ya hizi mbili na sio coz wanaamini chochote ni kutafuta wepesi katika kuishi, ndoa, ajira au siasa. Prove me wrong
Hapo umeleta hoja mpya kama unazungumzia hao wanaoenda kwenye imani fulani kwa sababu za wepesi wa kimaisha tu hawana imani basi hilo ni suala lengine.
 
Wewe sio mwili wewe ni nafsi yaani roho... Kama unabisha sema Mungu yupo ukiwa umefumba mdomo.....


Baada ya kutekeleza hilo zoezi mtafute nani aliye sema hivyo ilijali wewe umefumba mdomo wako ujakenue hata punje ya jino lako moja kuonekana nje.... Ukimpata aliye sema hivyo njoo kwenye huu uzi unitag ukimkosa tena sema huku umefumba mdomo kuwa mimi ni mbumbavu... Afu mtafute tena nani kasema Mpaka umpate....
Bro..hiyo ni akili yako..ndo maana tuna mawazo tofauti...Kama hiyo akili ndo Mungu bac binadamu wote tungekuwa na dini moja lakini dini zipo 10k, coz hizi ni fikra za watu. Hamna kitu kiitwacho roho, fikra zipo katika ubongo. Hizo dhana za roho nafsi moyo ni dhana za watu wa kale wasioelewa mwili wa binadamu, Kama unabisha tikisa ubongo kidogo tu uone Kama utakuwa sawa. Soma biology form 2 itakusaidia
 
Ndio hauna uthibitisho wala uhakika wa kuamka hiyo kesho, ukisema una chance tena kubwa ya kuamka kesho itabidi utupe sababu za msingi za kuwa na hiyo chance huwezi kusema et kwa sababu nimeona wengi waliyolala na kuamka.
It's a better explanation than kusema naamini Mungu yupo coz Kuna kitabu Cha miaka 3000 Cha mababu wayahudi au waarabu wamesema yupo. Na uthibitisho kuwa nitaamka kesho coz najiskia vizuri Leo. That is a better explanation than kusema ni by chance, sio chance,
 
Maswali yako ni mengi sana yanahitaji darasa ili upate majibu yako
 
Mi najiuliza maswali mengi. Mungu Ni Nini, anataka Nini na Yuko wapi.

Ukifuatilia historia ya binadamu tokea tukiwa wawindaji maporini miungu ilikuwepo. Wazee walikuwa wanaongoza vijana kwa kuwaambia kuwa Mungu anataka mfanye hivi, na hio miungu ilikuwepo pangoni ambapo wazee tu wanaingia, baadae vijana wakajitoa akili kwenda wakaona wazee ni waongo na hamna kitu mule. Wagiriki wakaja na miungu yao wakasema ipo ya milima ya Olympus, Leo hii watu wamepanda milima yote ugiriki hawajaona miungu hio.

Wakaja wayahudi, wakasema Mungu yupo mawinguni. Ukifuatilia hata Yesu alipaa mawinguni, Mungu alifungua madirisha ya mbinguni kuleta mafuriko, alichungulia kutoka mawinguni kwenye mnara wa babel, etc. Waislamu nao wakaja na mbingu Saba sijui. Anyways wazungu wametengeneza ndege na rocket zimeenda mawinguni, nje ya dunia, mpaka mwezini. Sasa hivi watu wa dini wanasema yupo nje ya ulimwengu.

So nikagundua trend, wanamficha, wanamweka mbali ili watu wasiweze kumfikia, why? Kwa sababu hayupo? Kwa sababu hajasema hizo sheria? Why wanamficha. Afu wanakuambia anataka uamini yupo ndo utapona usipoamini unaunguzwa. Ukiuliza nikimwona afu nikamwamini, anasema no, lazma usimwone ndo uamini. Na wanaweka kifo mwisho wa kumuani ili waweze kuendelea kutunga sheria kwa jina lake na kuweza kuendelea kutawala watu kwa sababu hamna mtu Ashawahi kurudi akasema baada ya kifo kipo hivi.

Mwanasayansi mi nauliza Mbinguni Kuna Nini. Hamna njaa hamna maumivu hamna ndoa hamna chochote zaidi ya kumuabudu Mungu. Watu kanisani na msikitini hawapendi kwenda unategemea watapenda milele ya Ibada. So wakaamua kuanzisha motoni kutishia watu kwamba wataunguzwa milele. Sasa, ukifa unaacha mwili wako hapa, wanasema una roho, roho ni Nini, hoo mawazo sijui pumzi, ukiuliza unajua kazi ya ubongo ni Nini mtu hajui, haya tufanye roho ni ka upepo kanaenda motoni ehe kanaunguaje, hakana nyama, hakana nervous system hakana ngozi, hakana pain receptors, hakana ubongo au spinal cord, maumivu unayasikiaje, na bado hatujauliza huu Moto upo wapi, walisemaga chini kisa mavolcano lakini now hawasemi Tena coz of elimu.

Tukienda kwenye sheria zenyewe sijui usivae nguo tofauti, usile shellfish, usichanganye mazao, usimwage nje, usiabudu sanamu lakini abudu kitu Cha kufikiriwa na myahudi, hivi kwa Nini mtu atengeneze nyota billion 60 na sayari trillion afu aje kujali binadamu wewe ambae ni Kama vumbi kwa huu ulimwengu unamwaga wapi. Na kwa Nini sheria hizi zinaonekana Kama sheria za kabila ya la zamani huko kwenye majangwa na haziendani na sheria za binadamu kuishi na watu vizuri. Na Wanavyosema tumuabudu siku ya Saba.

Siku zimekuja kutengenezewa baadae Sana na zimebadilika badilika Mara kwa Mara katika historia ya Mayans na Romans. Na wamechagua sun day coz ni siku ya pagans kuabudu jua. Ila yote haya tuyaache, why Mungu muweza yote anataka hela, mwisho wa siku wote mnabidi mgundue kuwa binadamu walitengeneza miungu ili kujibu maswali magumu yasiyojibika kipindi kile na ku
Mungu yupo mkuu ila habari za yesu, mhamedi sijui manabii mm ndo huniambii kitu huwa sielewi kabisa sababu manabii hadi sasa wapo wanaendele kujitokeza tu
 
Hivi jamani naomba kuuliza kile kilichotokea brazili baada ya kumziaki YESU na kumtukuza shetani ilikuwa ni mambo ya hali ya hewa tu ya liangukia siku Ile au ni MUNGU mwenyewe alishusha Ile dhoruba

Maana naona watu hawazingatii kabisa hili swala yani
We mjuaje niambie kilichotokea Brazil. Maana Kama unaweza amini bikra kazaa unaweza amini chochote kile. Event ya 2019 rio mafuriko yametokea 2023 mkoa mwingine mbali kabisa. Leo hii dar wamtukane Mungu afu 2028 litokee bukoba tetemeko utasema kisa dar wamemtukana Mungu. Jifunze kutafuta habari za ukweli sio story za mtaani, hio issue hata ITV hawajatangaza nor BBC na wewe unakubalikubali tu Kama ulivyokubali mtu kutembea kwenye maji...tumia akili sio matako
 
Waarabu ni matajiri sana ila sidhani kama waislamu wa afrika wanawafikia waarabu kwa imani ya Mungu, hakuna muarabu anayetoka huko arabuni kuja kujifunza dini afrika bali tunaona waafrika ndio wanaenda huko kwa matajiri kujifunza masuala ya Mungu.

Mtu kama Professor Assad asingekuwa bado anaamini Mungu ukizingatia elimu anayo na hana umasikini wa kukosa chakula na huduma bora ya afya. Na wapo wengi kama Prof Assad.
Umeongelea utajiri na umasikini wa kiuchumi lakini hujaongelea elimu.

Waarabu wakiamini Mungu hapo hakuna contradiction na hoja yangu, kwa sababu hawana elimu.

Na hata hao waarabu kadiri wanavyoongeza uchumi na elimu, imani ya Mungu inashuka.



 
Hapo umeleta hoja mpya kama unazungumzia hao wanaoenda kwenye imani fulani kwa sababu za wepesi wa kimaisha tu hawana imani basi hilo ni suala lengine.
Ndo ukweli...mtu anataka adake pisi ya kiislamu anasilimu anavaa makanzu anadaka pisi. Mtu hawezi ajiriwa au kupandishwa cheo katika institution ya kiislamu anasilimu anapata...fikiria bac
 
Mi Nikiona mtu ni mwizi mwizi sitamuamini katika vitu vyangu coz najua ye Ni mwizi. Ila we unaamini kitu ambacho hakina uthibitisho wowote tofauti ndo hiyo.
Hapo umeeleza upande wa kutokuamini na si kuamini, umetoa sababu za kutokumuamini huyo mtu. Sasa mtu ambaye hujui kama ni mwizi utamuamini kwa uthibitisho upi?
 
Ndo ukweli...mtu anataka adake pisi ya kiislamu anasilimu anavaa makanzu anadaka pisi. Mtu hawezi ajiriwa au kupandishwa cheo katika institution ya kiislamu anasilimu anapata...fikiria bac
Ndio nasema hicho ni kitu tofauti si suala la imani hilo.
 
Back
Top Bottom