Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Hauoni kama umeacha kuelezea hoja ya kukosa elimu kwa waafrika kuwa ni sababu ya wao kuamini habari za Mungu na sasa unaelezea sababu ya afrika kuwa nyuma kimaendeleo?
It's the same thing jamii zenye elimu kubwa haziwezi amini superstition.. tofautisheni Imani za watu wa Moshi bukoba na Arusha halafu ufananishe na shinyanga tanga sumbawanga...angalia jamii gani Ina elimu zaidi na nani anaamini maujinga zaidi
 
ndio mwanasayansi, vitu vingine vipo inje ya uwezo wetu kiakili, ushajiuliza kwanini mizimu ipo? wakati mtu ashakufa miaka milioni iliyopita? kama mungu hayupo wamewezaje kutengeneza roket za kufika mwezini wakashindwa kutengeneza roho ili tuishi milele? kama mizimu ina muonesha dawa mtu za kutibu ,umeshindwaje kutambua hata sayansi na teknoloji ni mafundisho tunayopata kutoka kwenye roho tusizozijua? kama mganga anavyooteshwa dawa usiku,umeshindwaje kutambua mtu anaoteshwa na roho isiyo na mwili kwamba tengeneza ndege fanya hivyo utafanikiwa akifatilia ina kuwa hivyo.MUNGU NI ROHO USHAWAHI IONA ROHO? .je hiyo teknolojia tunayo iona bila watu kuoteshwa na kufunuliwa na roho tusizo zijua tungefika hapa.kwanini muganga anaoteswa jins ya kutibu? vivyo hivyo na kwenye teknolojia,kama iko hivyo kwanin usiamini MUNGU yupo? kama majini ,mizimu,wachawi,mapepo yapo basi amin MUNGU yupo.akija mwanga ukakemea kwajina la yesu kwanini mwanga huyo anapotea.MUNGU yupo na ni roho nguvu isiyo onekana kwa macho ya nyama.
 
Nilizaliwa katika familia ya kipagani, nikajiunga na Ukristo ukubwani.

Mwanzoni mwa Ukristo wangu, usomaji wangu ulikuwa wa kawaida sana. Lakini miaka mingi baadaye, baada ya kukutana na changamoto zilizokosa majibu kwa wanadamu wasomi na wa kawaida, niliamini mahali pekee pa kupata majibu ni kwa Mungu. Ndiyo maana, kwa mara ya kwanza, niliamua kuisoma Biblia nzima, tena kwa "kuibugia".

Lengo kuu lilikuwa kupata ufumbuzi wa matatizo yaliyokuea yakinikabili. Nilitaka kupata majibu kutoka kwa Mungu. Nilichoka kuambiwa Mungu anaweza huku siouni utendaji wake kwangu.

Niliisoma Biblia na nikapita majibu yasiyotia shaka hata kidogo. Nikisema Mungu Yupo Hai na anaweza, si habari ya kuambiwa. Ni jambo nililolishuhudia maishani mwangu.

Hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufahamu kuwa BIBLIA ina majibu ya kila kitu maishani mwa mwanadamu.

Nimeshasoma Biblia nzima mara kadhaa, lakini lengo halikuwa kuisoma Biblia kwa lengo tu la kuisoma tu, la hasha. Ni kwa sababu inaniptaia majibu sahihi maishani mwangu.

Hata Sasa ningali ninaisoma, na nitaendelea kuisoma siku zote za maisha yangu.
Okay mi nakuletea kitabu na nakuambia humu ndani ni ukweli kila kitu ukisome Kama ukweli.... Utakuwa unasoma au unafanya unafki. Hizo contradictions elezea Basi ulisema saa sita cjui
 
Kama mtu anaamini kweli Mungu yupo, na anahesabu dhambi, na atatoa adhabu, hawezi kufanya kinyume na maagizo ya Mungu huyo.Mungu huyo alivyojengwa kidhana ni mkubwa sana na ana nguvu sana kumuasi.

Watu kufanya dhambi ni aina fulani ya kupiga kura ya kutokuwa na imani ya uwapo wa huyo Mungu.

Bado actions speaks louder than words, whether consciously or subconsciously.

Yani hata wewe ukifikiri unaamini Mungu yupo, ukajua kakataza kuiba, halafu ukaiba, hiyo ni rebellion inayotoa statement kwamba huamini sana kwamba Mungu yupo na atakuadhibu kwenda kwenye moto wa milele kwa dhambi zako. Watu wengi sana hawaamini Mungu yupo, wangeamini, dunia ingekuwa tofauti sana na ilivyo sasa.

In any case, huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Kwa sababu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo.
Hoja yako ni ya ajabu sana kwa sababu ni kana kwamba unataka kumfanya mtu anayeamini Mungu kuwa ni mtu wa tofauti kwamba hafanyi makosa katika mambo yake, mwenye kuamini Mungu kufanya yale yaliyokatazwa na Mungu kunaitwa dhambi na ndio maana kuna msamaha au kutubu.
 
Kwa Nini umechagua bible Kati ya vitabu vyote vya dini...why umeamini bible ni ya kweli na vingine vya uwongo na hata hujataka kuvisoma kujua story zao...wat if story za dini zingine ni za ukweli na kihistoria na zako za uwongo
Ni wapi nilkosema vingine ni vya uongo? Nimeiskma bible kwa sababu ndiyo nilivyokuwa nayo by that time, na ikanisaidia. Ndiyo maana naendelea kuisoma hata sasa.

Kama na wewe kuna uliyoisoma ya dini yoyote ile na ukabaini ni nzuri, tujuze ili kiweze kutafutwa na kusomwa.
 
ndio mwanasayansi, vitu vingine vipo inje ya uwezo wetu kiakili, ushajiuliza kwanini mizimu ipo? wakati mtu ashakufa miaka milioni iliyopita? kama mungu hayupo wamewezaje kutengeneza roket za kufika mwezini wakashindwa kutengeneza roho ili tuishi milele? kama mizimu ina muonesha dawa mtu za kutibu ,umeshindwaje kutambua hata sayansi na teknoloji ni mafundisho tunayopata kutoka kwenye roho tusizozijua? kama mganga anavyooteshwa dawa usiku,umeshindwaje kutambua mtu anaoteshwa na roho isiyo na mwili kwamba tengeneza ndege fanya hivyo utafanikiwa akifatilia ina kuwa hivyo.MUNGU NI ROHO USHAWAHI IONA ROHO? .je hiyo teknolojia tunayo iona bila watu kuoteshwa na kufunuliwa na roho tusizo zijua tungefika hapa.kwanini muganga anaoteswa jins ya kutibu? vivyo hivyo na kwenye teknolojia,kama iko hivyo kwanin usiamini MUNGU yupo? kama majini ,mizimu,wachawi,mapepo yapo basi amin MUNGU yupo.akija mwanga ukakemea kwajina la yesu kwanini mwanga huyo anapotea.MUNGU yupo na ni roho nguvu isiyo onekana kwa macho ya nyama.
Hamna mizimu
Hamna wachawi
Hamna mapepo
Hamna Mungu
Sayansi na technology kazi yake ni kuboresha maisha ya binadamu wakati anaishi...sio kufufua watu
Kama una ushahidi against any of this ulete.
Ukimaliza niambie roho Nini na ushahidi wake ni upi
 
Hamna mizimu
Hamna wachawi
Hamna mapepo
Hamna Mungu
Sayansi na technology kazi yake ni kuboresha maisha ya binadamu wakati anaishi...sio kufufua watu
Kama una ushahidi against any of this ulete.
Ukimaliza niambie roho Nini na ushahidi wake ni upi
Umeshawahi kusikia chochote kinachosu aliens?

Ni vitu gani hivyo?
 
Ni wapi nilkosema vingine ni vya uongo? Nimeiskma bible kwa sababu ndiyo nilivyokuwa nayo by that time, na ikanisaidia. Ndiyo maana naendelea kuisoma hata sasa.

Kama na wewe kuna uliyoisoma ya dini yoyote ile na ukabaini ni nzuri, tujuze ili kiweze kutafutwa na kusomwa.
Unajuaje vitabu vingine havitokusaidia, it means umechukua kilichopo karibu na wewe na hujafata ukweli, huo ni uvivu. Ni sawa na kupewa swali la shule ukaingia library ukachukua kitabu Cha kwanza unachokiona ukasema ndo majibu ya kila kitu...huo ni ujinga
 
It's the same thing jamii zenye elimu kubwa haziwezi amini superstition.. tofautisheni Imani za watu wa Moshi bukoba na Arusha halafu ufananishe na shinyanga tanga sumbawanga...angalia jamii gani Ina elimu zaidi na nani anaamini maujinga zaidi
Kwanza ieleweke kwamba kutokuamini uchawi na kujihusisha na imani za kichawi ni vitu vyenye utofauti kidogo, unaweza ukaamini uwepo wa uchawi na athari zake ila ukawa haujihusishi na mambo ya kichawi kwamba sio mtu mwepesi wa kuhusisha mambo na uchawi au kutegemea uchawi kupata mafanikio.

Kuna sehemu umetaja ina jamii ya watu wenye kujulikana kwa kujituma sana kwenye kupata mafanikio ila ni waumini wa Mungu na wanaamini mambo ya mizimu huko ya kwao.
 
🤣Sasa unasema waislamu matajiri wakati statistics zinaonyesha Islamic countries Zina low level of socioeconomic development kuliko non Islamic countries.. fuatilia sio unaona Dubai na Saudi Arabia na Qatar unasema waislamu matajiri kisa Mungu sijui.
Duh! Kuna sehemu nimesema waislamu ni matajiri?
 
Hivi ushawahi kukaa na mtu aliyesoma kabisa Kama daktari au mwanasayansi ukaongea nae on a personal level. Utaskia "haya mambo hayana logic na sense, Ila usiache kuamini", Ila wanaelewa kwa elimu Yao kwa sababu wanajua logic na reasoning Sana...Ila hawawezi kupayuka Mungu hayupo coz
1. Kuogopa kukataliwa na jamii
2. Kuogopa moto wa kufikirika
Nchi za nje madoctor na wanasayansi wapo more free kutoamini Mungu na wanaandika vitabu Wana engage in debates...bongo huwezi fanya hivyo coz serikali inahitaji watu wawe na dini ili ifunction so utafungwa tu ...huwezi omba kazi ukasema huamini Mungu ukapata, hata Mimi nitasema mi mkristo kwenye interview buh doesn't mean I honestly believe in those things. Ma atheists kibao wako jamii coz wapo free Ila mtaani kwao sidhani Kama Kuna watu wanajua ni ma atheists. Ndo hivyo, knowledge is power ndo maana mzungu ambae ameweza kutengeneza bomu la kuharibu dunia Kama Sodom, ameweza kupaa na kwenda mwezini, Leo hii huwezi mwambia story za nyoka kuongea na kulisha watu matunda coz ana maarifa mengi na anafuatilia vitu vya maana katika maendeleo ya jamii.
Wapo watu sio madaktari na hawana elimu kubwa ila pia hawaamini Mungu au kuamini hayo unayosema haya make sense, hivyo kama umekutana na wanasayansi na madaktari wenye mitazamo hiyo basi ni kawaida haina maana kwamba wanasayansi na madaktari wote hawaamini Mungu ila wanaigiza tu wanaamini.
 
Hamna mizimu
Hamna wachawi
Hamna mapepo
Hamna Mungu
Sayansi na technology kazi yake ni kuboresha maisha ya binadamu wakati anaishi...sio kufufua watu
Kama una ushahidi against any of this ulete.
Ukimaliza niambie roho Nini na ushahidi wake ni upi
mimi nina majini na mizimu utaniongopea nini,ila kama unataka uchanganyikiwe zaidi endelea kumjadili, ,kama teknolojia ime anza miaka mabilion watu wameanza kutumia ndege,simu, tv n.k hii hasa waganga na wachawi kwenye ulimwengu wa kiroho, MUNGU yupo na ni roho kwa sababu ushahid upo,nasa wameendele a mbabeli ya kumpeleleza MUNGU hata mwezini wameshindwa..usidanga nywe na teknolojia asili yake imetokana na miujiza, MUNGU ni roho na hana makazi maalumu,hachunguziki
 
😅🤣Hivi we hujiulizi Kama huyo Mungu yupo kila sehemu kwa Nini inabidi uletewe sheria zake na mtu ambae kaletewa na watu ambao wameletewa na watu wa sehemu fulani ndogo miaka 3000 iliyopita...mababu wa wayahudi kukatazana kuuana in a society that killing was normal na kulikuwa hamna police or legal system za maana so mtu anaweza kukufanya anachotaka so it was necessary utunge sheria uambie watu kwamba usipofata unaunguzwa...🤣Kodi ndo zilikuwa sadaka unalipia kwenda mbinguni... Ukifuatilia historia ya dini ni njama tu ya kucontrol binadamu Ila kweli hata Kama huyo Mungu angetengeneza dunia nzima na ulimwengu wote wenye sayari na nyota billions of billions ili juma asimwage nje coz atamind... Hebu😂
Naheshimu mitazamo yako kwa sababu naelewa kuwa suala la uwepo wa Mungu ni suala la imani hivyo kuwa na mitazamo tofauti tofauti ni kawaida, kwa sababu wewe hauamini kuwepo Mungu hivyo ni kawaida kuwa na hoja kama hizo ambazo kwako unaona ipo hivyo kwa sababu hakuna huyo Mungu na mwenye kuamini Mungu nae ni hivyo hivyo.
 
Kwanza ieleweke kwamba kutokuamini uchawi na kujihusisha na imani za kichawi ni vitu vyenye utofauti kidogo, unaweza ukaamini uwepo wa uchawi na athari zake ila ukawa haujihusishi na mambo ya kichawi kwamba sio mtu mwepesi wa kuhusisha mambo na uchawi au kutegemea uchawi kupata mafanikio.

Kuna sehemu umetaja ina jamii ya watu wenye kujulikana kwa kujituma sana kwenye kupata mafanikio ila ni waumini wa Mungu na wanaamini mambo ya mizimu huko ya kwao.
Ukishaamini uchawi upo automatically huna maarifa coz umeshindwa kureason na kutumia logic. Ndo maana unakuta hata Kuna watu ni wakristo Ila hawaamini uchawi na kulogana.. so why wewe unaamini uchawi au mizimu
 
Wapo watu sio madaktari na hawana elimu kubwa ila pia hawaamini Mungu au kuamini hayo unayosema haya make sense, hivyo kama umekutana na wanasayansi na madaktari wenye mitazamo hiyo basi ni kawaida haina maana kwamba wanasayansi na madaktari wote hawaamini Mungu ila wanaigiza tu wanaamini.
Mi sio daktari Ila naweza nikasoma basic biology nikaelewa Noah's story ni fake, Adam n Eve in the garden of Eden ni fake, heaven n hell and soul ni fake, coz naelewa hivi vitu haviwezekani in biology...Ila sio lazma niwe daktari
 
Back
Top Bottom