Nilizaliwa katika familia ya kipagani, nikajiunga na Ukristo ukubwani.
Mwanzoni mwa Ukristo wangu, usomaji wangu ulikuwa wa kawaida sana. Lakini miaka mingi baadaye, baada ya kukutana na changamoto zilizokosa majibu kwa wanadamu wasomi na wa kawaida, niliamini mahali pekee pa kupata majibu ni kwa Mungu. Ndiyo maana, kwa mara ya kwanza, niliamua kuisoma Biblia nzima, tena kwa "kuibugia".
Lengo kuu lilikuwa kupata ufumbuzi wa matatizo yaliyokuea yakinikabili. Nilitaka kupata majibu kutoka kwa Mungu. Nilichoka kuambiwa Mungu anaweza huku siouni utendaji wake kwangu.
Niliisoma Biblia na nikapita majibu yasiyotia shaka hata kidogo. Nikisema Mungu Yupo Hai na anaweza, si habari ya kuambiwa. Ni jambo nililolishuhudia maishani mwangu.
Hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufahamu kuwa BIBLIA ina majibu ya kila kitu maishani mwa mwanadamu.
Nimeshasoma Biblia nzima mara kadhaa, lakini lengo halikuwa kuisoma Biblia kwa lengo tu la kuisoma tu, la hasha. Ni kwa sababu inaniptaia majibu sahihi maishani mwangu.
Hata Sasa ningali ninaisoma, na nitaendelea kuisoma siku zote za maisha yangu.