Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Status
Not open for further replies.

Mtangoo

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2012
Posts
6,167
Reaction score
5,613
Nimeifuatilia kwa Muda kiasi nyuzi hii https://www.jamiiforums.com/jamii-i...-maswali-haya-ili-nikubaliane-na-kiranga.html ambayo imekutanisha watu wa aina mbalimbali. Kwa kuwa nina ufahamu kiasi fulani ningependa kuanzisha mjadala huu tena. Swali unaloweza kujiuliza ni kwa nini nianzishe mjadala mpya? Majibu ni kama ifuatavyo

Moja, mjadala husika una mambo anuai ambayo mwandishi wake anataka majibu na ni kutoka kwa mtu fulani (Kiranga). Pili ni mjadala mbao ni "too general" yaani "kuhusu Mungu". Kama nitakavyoaiisha baadae hili linafanya mjadala uwe mgumu kama unavyoonekana na usifikie tamati. Lakini mwisho pia binafsi sijaona swali maalum au lengo ambalo likipata majibu mjadala unafika ukingoni.

a. Ufafanuzi
Kabla sijaweka pwenti zangu ningependa kuweka msingi wa tunachokijadili hapa na mipaka yake. Suala la Mungu ni pana sana na hata vitabu vyote havitoshi kujadili, kwa hiyo kwa nafasi fnyu kama forum, tunahitaji kuweka mipaka.

Kwanza ninaposema Mungu ninaongelea "Mungu kama anavyoelezwa ndani ya Biblia". Hapa hatutazungumzia (ktk mada hii) kuhusu Biblia, ila Mungu wa Biblia. Usiniulize kuhusu imani nyingine maana mimi nakubali Mungu wa Biblia na ninaweza kukujibu kuhusu Mungu kama inavyoeleza Biblia. Kwa habari ya imani nyingine, subiri wafungue uzi au fungua kuwauliza watakujibu vizuri tu (ninaamini hivyo).

Pili ninaposema asiyeamini nina maana yeyote asiyekubali kuwa Mungu kama Biblia inavyomsema aliumba Ulimwengu wote, Mbingu na Nchi (Universe) ikiwajumuisha "atheists" na "agnostics". Hawa wawili ni walengwa wakuu ingawa sio pekee wa uzi huu.

Tatu ninaposema sayansi nina maana ya sayansi iliyotuletea ndege, Tv, upasuaji, n.k. Hii ni ile sayansi inayofuata hatua tano za kisayansi (Identification of problem, Hypothesis formulation, Experimentation, Observation, Data analysis Conclusion).

b. Ninachotaka kufikia katika Uzi Huu
Ninachotaka kuonesha katika uzi huu ni kuwa watu hawa wasioamini katika Mungu wa biblia wako hawawezi kupinga uwepo wake kwa kutumia mantiki (logic) ingawa hujificha sana nyuma ya logic. Sababu nitazitoa hapo chini. Ultimately watu hawa hukataa uwepo wa Mungu wa biblia kwa kuwa IMANI yao haiwaruhusu kukubali na si kwa sababu za kisayansi au kimantiki. Kusisitiza tu ninachotaka kuonesha ni kuwa watu hawa wana Imani, kama ambavyo wakristo wana imani. Tatizo lao ni kuwa kwanza wanakataa kuwa "Mungu hayupo" ni tamko la imani ya dini yao na kuwa wanaliamini pasipo sababu za kimantiki au kisayansi bali kiimani. Imani ya Wakristo ni juu ya Mungu wa biblia lakini wao imani yao ni imani upofu na haina pa kuegemea. Ni imani katika utupu (void faith/faith in nothing). "Argument" zao ni matamko ya imani kwa kiasi kikubwa.

Kifupi katika uzi huu nimelenga kuonesha kuwa:
  1. Wakristo na wasioamini Mungu wa biblia wote wanafanya haya kwa imani
  2. Imani katika Mungu wa Biblia ni "sound and solid" na inakubaliana na sayansi asilimia zote
  3. Imani ya hawa wandugu ni ya upofu, inayopingana na sayansi na mantiki kwa namna zote

c. "Arguments" zangu Kinyume nao
1. Ndugu zangu hawa hawaamini kama Mungu yupo wakisema kuwa hakuna ushahidi wa kuonesha uwepo wake. Na wanafikia hitimisho kuwa kwa sababu hii (kuwa hakuna ushahidi) Mungu hayupo na hivyo wote wanasema yupo wanasema kwa imani tu. Tukibadili juu-chini na kuwadai ushahidi thabiti (absolute evidence) ya kuthibitisha hakuna Mungu, hawana. Kwa kufuata mantiki yao wenyewe wao pia wanaamini kuwa hakuna Mungu...ni tamko la Imani

2. Watu hawa wanaamini kuwa kuamini Mungu yupo ni kukosa mantiki, na ni jambo la kiimani lililo kinyume na sayasi kabisa na hazivumiliki kwa yeyote aliye na akili ya kufikiri. Lakini watu hawa hawa wenye akili za kufikiri baadhi yao wanaamini kuwa ghafula kulikuwa na mpasuko, utupu (nothing) ulipasuka na katika mpasuko huu tunapata mpangilio wa sayari na jua, na wanadamu na mito na maziwa.

Watu hawa wengine wao huamini kuwa mercedes benz ilitengenezwa kiwandani na haikutokea tu, lakini watu hawahawa ambao tungetarajia watumie mantiki na fikra za juu sana wanaamini mwanadamu na wanyama wote wenye mifumo tata kuliko mercedes benz aina yeyote ile walitokea kwa bahati tu. Hii ni kinyume na mantiki na sayansi. Kwa nini watu hawa wanaamini mambo haya? Je ni wajinga wasioweza kufikiri? Si kweli kabisa...Tamko la dini yao, "hakuna Mungu" linawazuia wasikubaliane na ukweli na hivyo hawaruhusiwi na dini yao kutoka nje ya fundisho lao (doctrine of no God).


3. Watu hawa ambao wengine wanadiriki kusema "Mungu hayupo, na shetani ni hadithi" wanaamini kuwa hata kesho akiruka na ndege itatua chini na kuwa akipanda juu ya mwembe atashuka tu. hafikirii katika ulimwengu ambapo hakuna Mungu (the central coordinator) hakuna ulandano (uniformity). Kwa nini kuwe na ulandano katika dunia ambayo vitu vyaenda bila mpangilio (random/chance)? Kama kuna siku kulikuwa hakuna kitu ghafla bila mtu kusababisha vitu vikatokea kwa nini asiwe na shaka kuwa kuna siku ndege inaweza kwenda isirudi? Nani anayefanya vitu hivi viendelee hivi hivi? Watu hawa wanaongelea sheria za uvutano, mwendokasi n.k. bila kutuambia mtunga hizo sheria ni nani? Wanaamini zilitokea tu bila kutungwa. Je watu hawa wana ufahamu mfinyu sana kuweza kuelewa kukataa uwepo wa Mungu ni upuuzi unaopingana na mantiki na hata sayansi? Hapana...wanajua sana ila fundisho la dini yao ni kuwa hawaruhusiwi kukubali "Mungu yupo", kwa gharama yeyote!

4. Watu hawa wasioamini Mungu yupo huamini kuwa kama Mungu angaikuwepo kusingelikuwa na magonjwa na maumivu haya yote. Hawa watu wanaamini kuwa magonjwa ni kitu kibaya, na hata maumivu. Lakini swali wanaloliruka ni kuwa ili utofautishe kati ya mazuri na mabaya lazima kuwe na sheria iliyo juu ya wanadamu wote (absolute law) iliyo juu ya wanadamu wote. viginevyo bay kwa huyu laweza lisiwe baya kwa yule. Na ili kuwepo na sheria hiyo lazima awepo mtunga sheria aliye juu ya wanadamu wote. Watu hawa wanamkataa mtunga sheria huyu (Mungu) na hivyo wanapoteza sheria yenyewe na kimantiki mambo yote yanapaswa kuwa na hali sawa (hakuna baya au zuri). sasa wanpolalamika juu ya magonjwa na matatizo wanapimaje ubaya na uzuri? Je watu hawa hawawezi kuwaza haya yote? Je ni wajinga? Hapana, ni werevu sana. Ila tamko la dini yao linadai "Mungu hayupo" na wao kukiri kinyume na hivyo ni kuikana imani yao. Wanaenda kidini zaidi na sio kisayansi wala kimantiki!

5. Nimalizie kwa sasa (japo nina mengi bado) kusema kuwa watu hawa wanadai hawaamini uwepo wa Mungu wa kuwa Yeye haonekani, wala si wa ulimwengu huu wa damu na nyama (immaterial being). Wanadai hakuna kitu zaidi ya ulimwengu huu (nothing exist beyond material world). watu hawa wanatumia mantiki kuonesha kuwa kuamini vinginevyo ni kuvunja sheria za mantiki. lakini wanasahau kuwa sheria haijitungi na kwa sheria kuwa juu a wanadamu wote (absolute to all humans) lazima itoke kwa mamlaka juu ya wanadamu kwa namna ambayo wanadamu hawawezi kuivunja bila kuwa tasked kama ilivyo kwa sheria za mantiki. lakini pili watu hawa na dai lao hili wanajisahaulisha kuwa sheria ya mantiki haionekani wala sio ya ulimwengu wa damu na nyama (Logic laws are immaterial and invisible/intangible). Watu hawa kutumia mantiki kuipinga mantiki hawaoni ni kinyume na mantiki? Je watu hawa ni wajinga kiasi hiki? La Hasha! Ila dini yao haiwaruhusu kukubali uwepo wa Mungu wala ulimwengu mwingine tofauti na "material world".

d. Kwa Nini naamin Mungu Yupo?
1. Naamini kuna Mungu kwa kuwa naona uumbaji. DNA inabeba taarifa nyingi kuliko pengine vitabu vyote ulivyowahi kusoma tangu uzaliwe hata leo. Itakuwa ni upumbavu kuamini vitabu hivyo vilijiandika vyenyewe au kuwa post hii unayoisoma haikuandika na yeyote bali ilijitokeza bahati mbaya. Je si zaidi kuamini kuwa DNA ilijifanya yenyewe na mifumo yake tata ya kurekebisha makosa?

Ninaona Jua mwezi na mifumo ya jua jinsi inavyofanya kazi kwa ustadi na naungana na Daudi Mfalme kumtukuza Mungu nikikubali kuwa "Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake"(Zaburi 19). Kwa kweli siwezi kusoma sayansi ya anga na nisione mkono wa Mungu stadi na mwenye Nguvu ukiyatenda hayo. Sioni ni kwa namna gani haya yote yanaweza tokea bila Mungu na kwangu mimi Mungu ndio jibu linaloleta mantiki na linakubalika kisayansi!

2. Naamini Mungu yupo kwa kuwa hata uwepo wa sayansi unadai Mungu awepo kwanza. Sayansi inategemea ulandano i.e Uniformity (kuwa ukifanya vipimo chini ya "condition" zilezile majibu yanapaswa kuwa yaleyale). Tunajua kuwa ili kuwe na ulandano tunahitaji kuwe na Mtu au sheria (itakayodai mtunga sheria) ya kuvifanya vikae vilivyo. Kama hakuna Mungu hakuna haja ya ulandano kuwepo bali vitu vilipaswa kuwa shaghala bhagala. inachoona ni ulandano wa hali ya juu unaoiwezesha sayansi iwepo. Hivyo huwezi sema sayansi ukamtoa Mungu. Mungu ndiye anayefanya sayansi iwezekane. Hakika naungana na mwandishi wa Waraka kwa Waebrania kuwa Mungu "akivichukua [upholding] vyote kwa amri ya uweza wake" (waebrania 1:3). Bila Mungu hakuna sayansi na bila sayansi hakuna ndege, kompyuta n,k. Kwa kuwa vyote hivi vipo, Mungu yupo pasi na shaka.

3. Ninaamini Mungu yupo kwa kuwa maumivu na mateso, na mabaya yote yanadai uwepo wake. Mungu ndiye anayeweka kiwang cha nini ni kibaya na nini ni chema. Tunajua mema na mabaya kwa kuwa tumeumbwa kwa mfano wake ajuaye mema na mabaya. Tunafikiri kwa mantiki kwa kuwa tuna sura fulani ya Yeye Mungu Muumba. Hatukuumbwa tukiwa sokwe tukabadilika bali wanadamu wenye utashi ili tutawale viumbe wengine. Kila nikiangali jinsi mwanadamu anavyotawala viumbe wengi, anavyowafunga simba kwenye "cage" au anavyowadaka mamba kwa mitego yake sina cha kusema ila kukubaliana na Musa kuwa Mungu alituumba kwa mfao wake tutawale uumbaji wake (Mwanzo 1:26-27)

4. Mwisho, Ninaamini Mungu yuo kwa kuwa Mungu mwenyewe alitembelea sayari yetu akiuchukua mwili kama wetu katika utu wa Yesu Mnazarethi, akaishi katikati yetu akijithibitisha kwa nama ambayo kila atakaye kuujua ukweli atajua, akafanyiwa ukatili na watu ambao hawakutaka kukiri kuwa Mungu amewatembelea wakidai ni mwanadamu tu wa kawaida, akauawa kifo cha aibu na viumbe wake. Katika kufa kwake akalipa gharama ya mwanadamu kuifikia ile mbingu ambayo maumivu na mabaya ambayo yaliingia kwa sababu ya uasi wa mwanadamu hayatakuwepo. Je nihitaji nini tena kuamini kuwa Mungu yupo zaidi ya hili? Si tu kwamba alitutembelea, na si kwamba tu alifanya mambo yaliyomtenga na wanadamu wengine (kurudisha uhai, kufufuka toka wafu n.k) bali alikufa ili mimi siku moja niione mbingu...what a proof!

e. Hitimisho
Kwa kumalizia ni kuwa, imani katika Mungu ni imani sahihi inayokubaliana na sayansi, mantiki na hata akili ya kawaida. Imani katika dini ya "hakuna Mungu" ni imani potofu na ya kiupofu amabayo inapingana na kila aina ya ufahamu (sayansi) na mantiki na hata akili ya kawaida tu....

Wanaosema hakuna Mungu ni dini yao na sio kwamba ni kweli hakuna Mungu....usidanganywe!
Peace,
S.

[UPDATED] My Final Words after good debate
Kila mjadala huwa una mwisho wake, na kwangu mimi naona inatosha. Lengo langu limetimia kwa asilimia zote.
Ya kuwa Wasioamini uwwepo wa Mungu wanafanya hivyo kwa sababu za kiimani na sio kisayansi au kimatiki. Ya kuwa Imani katika Mungu wa Biblia ndio pekee "reasonable" na kuwa wakana Mungu na dini yao sio tu wako kinyume na sayansi, bali pia wako kinyume na Mantiki na hata fikra za kawaida.

Lengo limetimia kwa kuwa waliokuwa wakisombwa na mafundisho ya dini hii potofu ya Hakuna Mungu hata wakadhani ndio sayansi wameujua ukweli kuwa ni dini ambayo inapingana na sayansi na mantiki. Kipekee niwashukuru wote mliosoma na mliochangia, hasa Kiranga na wafuasi wote wa dini hii kongwe kabisa kwa kunisaidia kuthibitisha madai yangu pasipo na shaka. pia niwashukuru wote mliojadili kwa kuheshimiana na kwa staha.

Sijafunga mjadala huu (utaendelea kuwepo mpaka utakapoacha kuwepo) lakini kwa kuwa kusudi langu limetimia ninatundika daluga. Nitakuwa nikipita na pengine kujibu hapa na pale lakini sio kwa kiasi cha kwanza. Kama kuna boiling issue nai miss, fanya wema kuni mention
smile.png


Kwa mnaoamini Mungu wa biblia, imani yenu ni solid and reasonable, ishikilieni. Kwa msioamini Mungu naomba niwaache na zawadi hii hapa chini.

For the wrath of God is revealed from heaven against all ungodliness and unrighteousness of men, who hold the truth in unrighteousness; Because that which may be known of God is manifest in them; for God hath shewed it unto them. For the invisible things of him from the creation of the world are clearly seen, being understood by the things that are made, even his eternal power and Godhead; so that they are without excuse:

Because that, when they knew God, they glorified him not as God, neither were thankful; but became vain in their imaginations, and their foolish heart was darkened. Professing themselves to be wise, they became fools....Who changed the truth of God into a lie, and worshipped and served the creature more than the Creator, who is blessed for ever. Amen... And even as they did not like to retain God in their knowledge, God gave them over to a reprobate mind, to do those things which are not convenient...haters of God (Romans 1)

Mungu awabariki na mjadala uendelee
 
Hujajibu swali la "the problem of evil".

Kama kuna mungu mwenye uwezo wote na upendo wote, kwa nini katengeneza ulimwengu ambao uovu unawezekana?

Hapa umejaribu.

4. Watu hawa wasioamini Mungu yupo huamini kuwa kama Mungu angaikuwepo kusingelikuwa na magonjwa na maumivu haya yote.

Kwanza hujaelewa suala.Suala si kwamba "kama kungekuwa na mungu kusingelikuwa na magonjwa". Swala ni, kwa nini magonjwa yamewezekana kuwepo. Mawili haya ni tofauti.

Hawa watu wanaamini kuwa magonjwa ni kitu kibaya, na hata maumivu. Lakini swali wanaloliruka ni kuwa ili utofautishe kati ya mazuri na mabaya lazima kuwe na sheria iliyo juu ya wanadamu wote (absolute law) iliyo juu ya wanadamu wote.

Sheria iliyo juu ya wanadamu wote wewe mwanadamu utaijuaje? Na ukiijua kweli itakuwa juu ya wanadamu wote?

viginevyo bay kwa huyu laweza lisiwe baya kwa yule. Na ili kuwepo na sheria hiyo lazima awepo mtunga sheria aliye juu ya wanadamu wote.

Inakuwaje sheria iliyo juu ya wanadamu wote iliyotungwa na mtunga sheria aliye ju ya wanadamu wote iwe na compassion, logic, ethics, responsibility ndogo kuliko sheria za kibinadamu?

Watu hawa wanamkataa mtunga sheria huyu (Mungu) na hivyo wanapoteza sheria yenyewe na kimantiki mambo yote yanapaswa kuwa na hali sawa (hakuna baya au zuri).

Hali sawa kwa nani? Utaweza kumwambia mtoto anayezaliwa kipofu kwamba hii ni "hali sawa" na hakuna zuri au baya?

sasa wanpolalamika juu ya magonjwa na matatizo wanapimaje ubaya na uzuri?

Kwa vipimo vya ubinadamu, ambavyo vinakataza baba kuwanyima watoto wake chakula kama anacho.

Vipimo vya kibinadamu vina standards za chini kwa sababu binadamu hana uwezo wa juu na upendo wa juu. Mungu ambaye tunamtegemea awe na upendo wa juu kabisa, tulitegemea asiache viumbe vyake vife kwa magonjwa na njaa, visizaliwe na upofu.

Imekuwaje Bill Gates amsaidie kazi mungu kwa kupelekea chanjo watoto masikini Afrika?

Mungu kashindwa kuwapa afya nzuri viumbe wake?

Je watu hawa hawawezi kuwaza haya yote? Je ni wajinga? Hapana, ni werevu sana. Ila tamko la dini yao linadai "Mungu hayupo" na wao kukiri kinyume na hivyo ni kuikana imani yao. Wanaenda kidini zaidi na sio kisayansi wala kimantiki!

Hujajibu "the problem of evil".

Kama mungu ni mwenye uwezo wote na upendo wote, imekuwaje kaumba ulimwengu mbaya kama huu wenye matetemeko ya ardhi, magonjwa, vilema vya maisha, njaa, vita etc?

Mngesema hana uwezo angalau tungesema alitaka kuumba ulimwengu mzuri zaidi akshindwa, kama yule baba ambaye anataka kuwapa watoto chakula lakini hana kipato. Tungeelewa.

Mngesema ana uwezo ila hana upendo, tungeelewa. Ni kwamba hatujali tu, labda yuko busy na projects zake za kuumba ulimwengu mwingine.

Lakini mmesema ana uwezo wote na upendo wote, tena kaona ulimwengu wote ulivyokuwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho wakati akiuumba.

Sasa kama kaumba ulimwengu mbaya kama huu, ni kwa nini?

Haiyumkiniki!

Swali umelikwepa kwa kuweka "deus ex machina" na ku tip toe around it.

Ila hujasema ni kwa nini ulimwengu huu ambao hata mawazo madogo ya kibinadamu yashauona mbaya, unaweza kuwa kazi ya mungu.

Habari ya kusema sijui baya na zuri kwa mungu ni tofauti na hatuwezi kujua mawazo yake ni "deus ex machina" kwa sababu hata kama hatujui, tunategemea mungu awe na standards kubwa kuliko zetu binadamu.

Hivi kweli mungu muumba vyote mwenye uwezo wa yote na mapenzi yote ashindwe kwenye ethics, responsibility na compassion akilinganishwa na kwa mfano, the medical profession?

Inaingia akilini?
 
Hujajibu swali la "the problem of evil".
Huwa siwaelewi mnapomkana Mungu na kuleta "problem of evil". hili swali nimelijibu katika uzi huu na kama hujaelewa nitarudia. Kiranga , unaposema "problem of evil" huoni unafanya "assumption" zinazodai/zinazolazimu uwepo wa Mungu? Unatofautishaje mema na mabaya katika ulimwengu ambao hakuna Mungu? Maana kusema tu "evil" una "imply" aina fulani ya sheria ya maadili (Moral Law) na hivyo Mtoa/Mtunga sheria hiyo (Mungu). Sasa kama wewe huamini kuwa Kuna Mungu, unatofautishaje kati ya zuri na baya? utuambie hili kwanza kabla hata hujauliza kuhusu "problem of evil". maana kama huwezi kutuambia tofauti ya jema na baya, then kwanini tuendelee zaidi ya hapo?

Kama kuna mungu mwenye uwezo wote na upendo wote, kwa nini katengeneza ulimwengu ambao uovu unawezekana?
Wewe ulitaka afanyeje? atengeneze watu ambao hawana uhuru wa kuchagua? Kama angefanya unavyotaka unafikiri angekuwa ameumba watu kwa mfano wake? Unafikiri kuna upendo bila kuchagua?

Imagine mke wako ukitaka akubusu anakubusu hata kama yeye hataki. Utakwenda mtaani kifua mbele kuwa kuna upendo kati yenu?

Mungu yuko sahihi kabisa kuumba ulimwengu wa namna hii na ndio maana Yesu ni mwanakondoo aliyechinjwa kabla ya misingi ya ulimwengu kuwekwa. Hii ni kwa sababu Mungu aliamua (in his Sovereign choice) kuumba ulimwengu ambao si tu kwamba alijua maovu yanawezekana bali alijua pia Mwaadamu huyu ataasi. Na akaamua kuonyesha ni wa Upendo zaidi kwa kufanya njia ya kumwokoa toka katika uovu wake: Mpango ambao wewe Kiranga unaukana leo hii.

Kwa kuumba ulimwengu wa namna hii Mungu amedhihirisha upendo mkuu sana (Yohana 3)


Kwanza hujaelewa suala.Suala si kwamba "kama kungekuwa na mungu kusingelikuwa na magonjwa". Swala ni, kwa nini magonjwa yamewezekana kuwepo. Mawili haya ni tofauti.
Simple! Kuna Magonjwa kwa sababu kuna dhambi. Kuna dhambi kwa sababu Mwanadamu aliamua kumwasi Mungu. Mwanadamu alimwasi Mungu kwa sababu ya kutumia vibaya utashi wake. Mwanadamu alikuwa na utashi kwa sababu Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua. Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua kwa sababu Mungu nu pendo. Kwa hiyo "ultimately" kuna magonjwa kwa sababu kuna Mungu!



Sheria iliyo juu ya wanadamu wote wewe mwanadamu utaijuaje? Na ukiijua kweli itakuwa juu ya wanadamu wote?
Unadhani kuna mahali popote ambapo ni sahihi kwa mtu kumbaka mtoto mchanga na kumkatakata vipande kisha kula nyama yake? Jibu lako lina maana gani (what does your answer imply)?



Inakuwaje sheria iliyo juu ya wanadamu wote iliyotungwa na mtunga sheria aliye ju ya wanadamu wote iwe na compassion, logic, ethics, responsibility ndogo kuliko sheria za kibinadamu?
Hili tatizo lingine la wasioamini Mungu! Kama unaamini katika naturalism (kama ambavyo nimekusoma katika nyuzi kadhaa) kwa nini utumie "compassion, logic, ethics," vitu ambavyo havionekaniki wala kushikika? Na pia hapa unajaribu kusema kuwa "God is morally wrong" na mimi nauliza "Under which Moral Law is God wrong?". Unapimaje ethics za Mungu na kuzithibitisha kuwa ziko chini? What are the scales?



Hali sawa kwa nani? Utaweza kumwambia mtoto anayezaliwa kipofu kwamba hii ni "hali sawa" na hakuna zuri au baya?
Katika ulimwengu/Dini unayoiamini ya "random and chance" kuna tatizo gani mtoto kuzaliwa kipofu? Katika dini yako ya "Hakuna Mungu" na hivyo hakuna "Ultimate Law" kuna tofauti gani kati ya mema na mabaya? Hitler aliona ni jambo Jema kuua wayahudi Mil 6+ na Stallin akaona ni jambo zuri tu kuua mamilioni ya Warusi. Kuna watu wanaona ni vyema wakibaka au kuua. Katika dini yenu ya hakuna Mungu, unawahukumu wana kosa? Kwa sheria ipi?


Kwa vipimo vya ubinadamu, ambavyo vinakataza baba kuwanyima watoto wake chakula kama anacho.
Baba A akiona ni vyema kuwapa watoto chakula na Baba B akaona ni vyema watoto wake wakafa na njaa, na wote hawa ni binadamu, nani atakuwa amekosea? Kwa sheria ipi hiyo ya ubinadamu maana hawa wote ni wanadamu!

Hujatuambia pa sheria hiyo mtunzi wake ni nani na kwa mamlaka gani aliitunga sheria hii!

Vipimo vya kibinadamu vina standards za chini kwa sababu binadamu hana uwezo wa juu na upendo wa juu. Mungu ambaye tunamtegemea awe na upendo wa juu kabisa,
You are right na ndivyo alivyo!

tulitegemea asiache viumbe vyake vife kwa magonjwa na njaa, visizaliwe na upofu.
Una maana hata pale viumbe hawa wanapochagua mauti badala ya uzima Mungu awalazimishe? Mfano, wewe Kiranga leo umemkataa Mungu mbele yetu sote, halafu unatarajia kwa sababu ya upendo wake akuachie tu uende, are you kidding? Hakimu anapotoa hukumu huitoa kwa upendo kwa kuwa ni haki stahili. Haya Magonjwa ni haki stahili ya Mwanadamu kwa sababu ya kuukaribisha uasi (dhambi). Huwezi kukaribisha adui halafu ukalalamikia madhara yake. Each choice have its consequence!

Imekuwaje Bill Gates amsaidie kazi mungu kwa kupelekea chanjo watoto masikini Afrika?
Bill hajawahi kumsaidia Mungu kazi hata siku moja. kupeleka chanjo Afrika haijawahi kuwa kazi ya Mungu. Umelipata wapi hili?

Mungu kashindwa kuwapa afya nzuri viumbe wake?
Jibu la swali hili nimeshalijibu hapo juu...madhara ya kukaribisha adui si kazi ya Mungu kuyabeba. Ukweli hata kama unauma ndio ukweli wenyewe!



Hujajibu "the problem of evil".

Kama mungu ni mwenye uwezo wote na upendo wote, imekuwaje kaumba ulimwengu mbaya kama huu wenye matetemeko ya ardhi, magonjwa, vilema vya maisha, njaa, vita etc?
Check the answer above! Huna haki ya kudai habari ya mabaya wakati unasema hakuna Mungu!

Mngesema hana uwezo angalau tungesema alitaka kuumba ulimwengu mzuri zaidi akshindwa, kama yule baba ambaye anataka kuwapa watoto chakula lakini hana kipato. Tungeelewa.

Mngesema ana uwezo ila hana upendo, tungeelewa. Ni kwamba hatujali tu, labda yuko busy na projects zake za kuumba ulimwengu mwingine.

Lakini mmesema ana uwezo wote na upendo wote, tena kaona ulimwengu wote ulivyokuwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho wakati akiuumba.

Sasa kama kaumba ulimwengu mbaya kama huu, ni kwa nini?
Haiyumkiniki!

Swali umelikwepa kwa kuweka "deus ex machina" na ku tip toe around it.

Ila hujasema ni kwa nini ulimwengu huu ambao hata mawazo madogo ya kibinadamu yashauona mbaya, unaweza kuwa kazi ya mungu.

Habari ya kusema sijui baya na zuri kwa mungu ni tofauti na hatuwezi kujua mawazo yake ni "deus ex machina" kwa sababu hata kama hatujui, tunategemea mungu awe na standards kubwa kuliko zetu binadamu.

Hivi kweli mungu muumba vyote mwenye uwezo wa yote na mapenzi yote ashindwe kwenye ethics, responsibility na compassion akilinganishwa na kwa mfano, the medical profession?

Inaingia akilini?

Swali hili unabadili tu namna ya kuliuliza na nimeshalijibu hapo juu!


Anyway hujaweka ushahidi wowote kuwa hakuna Mungu zaidi ya kuhoji kwa nini Mungu kama yupo alifanya A B C. Hakuna mahali umefuta point zangu na kwa ukweli umehakikisha nilichokisema kuwa ni dini yako tu inayokataa uwepo wa Mungu inakulazimisha kufika uliko. Si kwa sababu hakuna Mungu bali kwa sababu hutaki kukubali uwepo wake ambao pia wajua ni halisi

Umeruka na kukimbia point zangu badala ya kuzijibu moja baada ya nyingine.
Mungu yupo, alikuweko na ataendelea kuwepo!
Huu ndio ukweli mchungu!
 
Mungu yupo,na suala la Kiranga eti kwa nini kuna maovu,Mungu amemuumba mwanadamu then akamwekea
utashi wa kuchagua mema au mabaya,na wala hilo halimfanyi asiwe Mungu eti kwa sababu anao uwezo wa
kuzuia maovu yasiwepo,kwa sababu Yeye ni Mungu hakuna wa kumhoji kwa nini iwe hivi au iwe vile'
Narudia Kiranga kutokuamini kwako hakuwezi kumfanya MUNGU asiwepo na wala asiwe Aliyeumba Mbingu na
nchi na vyote vilivyomo.Nikushauri usisubiri Mungu kujidhirisha kwako kwa namna nyingine'
 
Kwahy kiranga kwa akili yako kwasab unabaka,unzin unaiba!!! jibu lake Mungu hayupo! Huwa nasema kila siku hapa wewe ni sawa na kibuyu kilichowekwa jangwani,halaf upepo ukiwa unapita unatoa ule mlio!

Swali langu hujawahi kujibu"kwanini huwa unabishia jambo ambalo halipo"?
 
Nitachangia mara moja tu hapa kwa sababu mleta mada kaweka wazi kuwa 'anaamini' juu ya uwepo wa mungu, na kuamini au IMANI (FAITH) ndio key word ya mjadala wake wote.

Siwezi kujadili tena kwa sababu hatuwezi kuipima imani ya mtu katika mizani ya mantiki au hizo njia za kisayansi mleta mada kaziorodhesha, kwa sababu maana halisi kabisa ya neno sayansi ni KNOWLEDGE (UJUZI) na sio IMANI, kwa hiyo hatuwezi kutumia njia za kisayansi kuipima imani.

Wewe unaamini, mimi nataka kujua, huwezi kunisaidia kwa sababu na wewe haujui kama mimi ila umeamua kuamini kile ambacho wote hatukijui.
 
Nitachangia mara moja tu hapa kwa sababu mleta mada kaweka wazi kuwa 'anaamini' juu ya uwepo wa mungu, na kuamini au IMANI (FAITH) ndio key word ya mjadala wake wote.

Siwezi kujadili tena kwa sababu hatuwezi kuipima imani ya mtu katika mizani ya mantiki au hizo njia za kisayansi mleta mada kaziorodhesha, kwa sababu maana halisi kabisa ya neno sayansi ni KNOWLEDGE (UJUZI) na sio IMANI, kwa hiyo hatuwezi kutumia njia za kisayansi kuipima imani.

Wewe unaamini, mimi nataka kujua, huwezi kunisaidia kwa sababu na wewe haujui kama mimi ila umeamua kuamini kile ambacho wote hatukijui.
Point yangu ni kuwa hata wewe unaamini kuwa hakuna/kuna Mungu.
Vitu vingine vyote vitakavyofuata vinatafsriwa kulingana na moja kati ya imani hizi mbili.
Hakuna namna mwanadamu anaweza epuka hili Mourinho

God or No God must be settled before you take any further step. Na katika post hii nimeonesha kuwa "No God" ni Imani inayokwenda kinyume na ufahamu (sayansi) na hata mantiki (logic). Kwa hiyo huwezi kusema hakuna Mungu halafu ukatumia mantiki au sayansi. Ukikataa Mungu maana yake umeikataa mantiki na sayansi na unapoteza uhalali wa kuvitumia vyote!
 
Last edited by a moderator:
what a joke... yaan wewe vitu usivyo na majibu navyo ndio unaviita vya mungu??? y would ur god give freedom where by human nature to do the so called bad things is easier than to do the so called good... kwa nn yesu alisema kama atachelewa kurud hakuna atayebaki ina maana its impossible kutokufanya dhambi!!!
 
what a joke... yaan wewe vitu usivyo na majibu navyo ndio unaviita vya mungu???
Umeitoa wapi hii? It have nothing to do with the topic... Please stick to what we are discussing!

y would ur god give freedom where by human nature to do the so called bad things is easier than to do the so called good...
Majibu yake yapo hapo juu, soma tena!

kwa nn yesu alisema kama atachelewa kurud hakuna atayebaki ina maana its impossible kutokufanya dhambi!!!
Fungua uzi wake wapo wajuzi wengi tu watakupa majibu. Huu sio mjadala wa uzi huu!

Once again, umehakikisha pwenti yangu Muhimu kabisa kuwa watu wanaokana Mungu hawafanyi hivyo kwa sababu za kisayansi wala kimantiki. Bali ni sababu za kiimani. Imani yako kuwa hakuna Mungu ndiyo imekusukuma kuziita "arguments" zangu joke bila kuzijibu... naam kwa sababu hauna majibu ila imani katika dini yako ya "hakuna Mungu"

Once again pangua hoja zangu na sio kufanya "rhetorics" zisizo na mashiko!
 
Mkuu Stefano Mtangoo naona unashindwa kabisa kuamini big bang theory kwa sababu unaamini hakuna kitu kinachoweza kutokea kutokana na utupu, JE UNAWEZA KUTUELEZA CHANZO CHA MUNGU?
 
Last edited by a moderator:
Mungu yupo,na suala la Kiranga eti kwa nini kuna maovu,Mungu amemuumba mwanadamu then akamwekea
utashi wa kuchagua mema au mabaya,na wala hilo halimfanyi asiwe Mungu eti kwa sababu anao uwezo wa
kuzuia maovu yasiwepo,kwa sababu Yeye ni Mungu hakuna wa kumhoji kwa nini iwe hivi au iwe vile'
Narudia Kiranga kutokuamini kwako hakuwezi kumfanya MUNGU asiwepo na wala asiwe Aliyeumba Mbingu na
nchi na vyote vilivyomo.Nikushauri usisubiri Mungu kujidhirisha kwako kwa namna nyingine'

Ni Mungu wa namna gani huyo anayeweza kuwafanya wanawe watumwa? Ni baba wa namna gani huyo anayeweza kuwaweka wanawe katika majaribu anayojua kabisa kuwa yatawashinda halafu mwisho akawaadhibu kwa kuwatundika motoni? Ni Mungu wa namna gani huyo anayeshindwa kumteketeza shetani na kumwacha awapotoshe viumbe wake na mwisho yeye mwenyewe awatupie lawama watoto na kuwateketeza katika moto wa milele? Kwa mujibu wa vitabu mnavyoamini mungu ana uwezo wa kila jambo, kwa nini asiamuru kila kitu kiende sawa na kiwe hivyo? Je, Mungu anafurahia picha anayoigiza shetani na wanadamu hapa duniani, Kwa nini anaangalia na kuchekelea?
 
Mkuu Stefano Mtangoo naona unashindwa kabisa kuamini big bang theory kwa sababu unaamini hakuna kitu kinachoweza kutokea kutokana na utupu, JE UNAWEZA KUTUELEZA CHANZO CHA MUNGU?
Mungu akishakuwa na chanzo anakuwaje Mungu?
Mungu ninayemwongelea essentially ni wa Milele (Eternal Being) na eternity by definition mean no time which means no beginning nor end!

Ukisoma Big bang, wanasayansi wenyewe wanakubali sio eternal na hivyo basi kwa kuwa BB sio eternal wanapaswa watupe maelezo ya mwanzo wake.

BTW,ili kuja na BB theory ilihitajika sayansi iwepo na ili sayansi iwepo lazima mazingira ya kufanyia hiyo sayansi yawepo. No moja kati ya mahitaji (prerequisites) ni ulandano (uniformity). Ili kuwe na ulandano kunadai uwepo wa Mungu (alternative yake ni randomness and chances ambayo inafanya science isiwezekane). Sasa hao wanaoamini BB wanapaswa kwanza kutuambia kwa nini kuwa na "uniformity" badala ya "randomness/chances". halafu watuambie kwa kuwa BB na element zake sio eternal, ni wapi zilitoka na ilikuwaje vitu vikalipuka.
 
Is Uniformity one of the key elements to justify God's existence, siyo? Good, sasa hapo mwanzo biblia yako inatuambia hakukuwa na dhambi. Mungu Aliumba viumbe vyake vyote akiwemo Malaika Mkuu wake Lusifa a.k.a. Shetani wa leo akiwa mkamilifu. Ila ghafla bin vuu bwana mkubwa huyu akaota kiburi na kutaka kujifananisha na Muumba wake! Is this what you refer to be uniformity, one of your poor proof of God's existence? Okay, following the same trend, Mungu Alijua kuwa Ulimwengu aliouumba baadaye ungetumbukia dhambini, sasa akaandaa mpango mkubwa, mgumu, wa gharama kubwa na tena usiofikirika eti wa kumkomboa mwanadamu kutoka dhambini! Sasa two issues here to be addressed, 1. Ikiwa ni kweli kuwa Mungu Alimpa mwanadamu uhuru wa kuchagua mema na mabaya (sawa na Baba unavyoweza kumpa uhuru mwanao aende Mzumbe Secondary au Ikinabushu Secondary), iweje tena Baba huyu aanze kumtishia mwanaye kuwa ukichagua kwenda Ikinabushu Secondary nitakufukuza kwangu tena na kukuchoma moto? Iweje mtu anapo-exercise uhuru wake uliompatia wewe mwenyewe aonekane adui yako kisa tu hakuchagua vile ulivyotaka wewe? Je, katika viwango vya kibinadamu, huo kweli ni uhuru au ni udikteta zaidi ya Idd Amin? By the way, iweje motto wako achague kwenda IkinabushU Secondary halafu wewe uanze njama za kuandaa mpango wa kumuhamisha mara tu atakapokuwa amejiunga na Ikinabushu Secondary? Sasa hapo ulimpa achague kweli anachokitaka yeye mwenyewe au ulikuwa unamfanyia usanii tu? Na hata kama ulitaka asiende Ikinabushu Secondary kwa kuwa ni shule ya kata tena isiyo na vifaa wala walimu wazuri, kwa nini usisubirie hadi atakapoona madhara/matokeo ya uchaguzi wake huo? Badala yake wewe Baba unayependa Mzumbe Secondary unatoka huko uliko na kwenda kumuadhibu mwanao aliyeko Ikinabushu Secondary? Kwa nini usingemuacha tu na wewe ukabaki na chaguo lako, na iwapo una watoto wawili na bahati "nzuri" kwako mmoja amekukubalia chaguo lako basi uwashindanishe wote wawili tena kwa usawa kuliko kumtisha yule wa Ikinabushu kuwa atafeli, utamnyima ada, hela ya matumizi na hutakwenda kumsalimia huko shuleni na mbaya zaidi asije akarudi nyumbani kwako wakati wa likizo???????? Back to Uniformity: Kama mwanadamu naye alikuwa mkamilifu, baadaye akaasi, mpango wa kumuokoa dhambini ukasukwa, sasa tuna uhakika gani kuwa mwanadamu yule yule atakayekuwa ameokolewa dhambini hataasi ktk paradise/akhera/mbingu/dunia ijayo? Na nini mpango wa Mungu endapo tena mwanadamu atakuja kuasi akifika huko mbinguni? Maana hapo mwanzo Mungu Alijua kuwa kiumbe wake mkamilifu angeasi, akajiandaa, lakini this time tunaambiwa kuwa huko mbinguni hakutakuwa na dhambi wa kifo tena (just as it was in the beginning) lakini hatuambiwi nini kitatokea endapo hali ikigeuka kuwa ndivyo sivyo! Au wanadamu watakaokuwepo kule hawatakuwa tena na uchaguzi wa kuamua njia waitakayo kama wale wa awali walivyopewa fursa hiyo? If that is the case, kwa maana hiyo Mungu atakuwa amewafunga, wasiwe na any other choice except him, na kama hivi ndivyo basi huyo Mungu hajiamini, ni dikteta na hajali athari za mabavu yake kwa watoto wake maana kama angelikuwa na upendo basi asingewanyima uhuru wao ule ule! Pili, wewe (Mungu) ni Mwalimu wa Sanaa (Arts), unafundisha wanafunzi, kutunga mitihani, kusahihisha na mwisho kutoa matokeo. Sasa iweje tena wewe huyo huyo ukatoe matokeo ya wanafunzi waliofanya somo la Hisabati ilhali halikuhusu, hukusomea, hukuwafundisha na wala hukutunga mtihani huo? Maana yangu ni kwamba, kwanini Mungu asi-deal na wale wanaofuata sharia zake tu (yaani awalinde, awatunze, awahudumie na hatimaye siku atakayoona inafaa awapeleke anakotaka yeye basi) na badala yake ana-cross over na kuwafuata wale wasiomuamini na kujifanya ndiye Jaji wao? Kwanini wale wasiomuamini (kwa maana nyingine ni wafuasi wa Mzee Mzima Shetani) asiwaache nao walindwe, watunzwe, wahudumiwe na hatimaye wapelekwe kule ambako Master wao atataka wawe? Hayo ya Ngoswe yanamhusu nini yeye huyo Mungu wenu? MWISHO: Eti kuna Mungu au Shetani ni nadharia tu zisizo na mantiki wala mashiko kwa kutumia akili ndogo kabisa za kibinadamu maana hata yasemwayo kuhusu hao wawili hayawezi kuthibitishwa pasipo kuacha chembe ya shaka! So, what for? Leave this Topic alone, don't waste your precious time at all!
 
Mungu akishakuwa na chanzo anakuwaje Mungu?
Mungu ninayemwongelea essentially ni wa Milele (Eternal Being) na eternity by definition mean no time which means no beginning nor end!

Ukisoma Big bang, wanasayansi wenyewe wanakubali sio eternal na hivyo basi kwa kuwa BB sio eternal wanapaswa watupe maelezo ya mwanzo wake.

BTW,ili kuja na BB theory ilihitajika sayansi iwepo na ili sayansi iwepo lazima mazingira ya kufanyia hiyo sayansi yawepo. No moja kati ya mahitaji (prerequisites) ni ulandano (uniformity). Ili kuwe na ulandano kunadai uwepo wa Mungu (alternative yake ni randomness and chances ambayo inafanya science isiwezekane). Sasa hao wanaoamini BB wanapaswa kwanza kutuambia kwa nini kuwa na "uniformity" badala ya "randomness/chances". halafu watuambie kwa kuwa BB na element zake sio eternal, ni wapi zilitoka na ilikuwaje vitu vikalipuka.
Weweee, hapo kwenye Bold, ni nani alikuambia kuwa ili kuwepo na Uniformity lazima iwe ni kwa sababu ya Mungu? Kwanini isiwe kinyume chake (kwamba Uniformity has nothing to do with God's Control)? Unaweza ukathibitisha pasipo kuacha chembe ya shaka kuwa Uniformity >>> God? How, Why and Why not?
 
Weweee, hapo kwenye Bold, ni nani alikuambia kuwa ili kuwepo na Uniformity lazima iwe ni kwa sababu ya Mungu? Kwanini isiwe kinyume chake (kwamba Uniformity has nothing to do with God's Control)? Unaweza ukathibitisha pasipo kuacha chembe ya shaka kuwa Uniformity >>> God? How, Why and Why not?
Why should things be uniform in random universe where things just run themselves through chance?
Why? As for me God withholds all things by the Word of His power. That speaks why things are uniform!

As for you how do you account for uniformity?

Halafu ungerekebisha post ya hapo juu in paragraphs. Napata shida kidogo kupata mtiririko wako uzuri 🙂
 
the book that u so trust has a lot of inconsistency y would a rational person trust it??? even from early chapters lots of ambiguities!! kwa mfano wakat cain amemuua ndugu yake anafukuzwa akawa anamlalamikia mungu kua uko anakoenda anaogopa watu watamuua? swali ni kwamba nani hao watu anaowaogopa? kulikua na town ingine apart from eden? watu hao walitoka wapi? and funny enough uko alikoenda akapata na mke!!!
 
Why should things be uniform in random universe where things just run themselves through chance?
Why? As for me God withholds all things by the Word of His power. That speaks why things are uniform!

As for you how do you account for uniformity?

Halafu ungerekebisha post ya hapo juu in paragraphs. Napata shida kidogo kupata mtiririko wako uzuri 🙂

Is Uniformity one of the key elements to justify God's existence, siyo? Good, sasa hapo mwanzo biblia yako inatuambia hakukuwa na dhambi. Mungu Aliumba viumbe vyake vyote akiwemo Malaika Mkuu wake Lusifa a.k.a. Shetani wa leo akiwa mkamilifu. Ila ghafla bin vuu bwana mkubwa huyu akaota kiburi na kutaka kujifananisha na Muumba wake! Is this what you refer to be uniformity, one of your poor proofs of God's existence? Okay, following the same trend, Mungu Alijua kuwa Ulimwengu aliouumba baadaye ungetumbukia dhambini, sasa akaandaa mpango mkubwa, mgumu, wa gharama kubwa na tena usiofikirika eti wa kumkomboa mwanadamu kutoka dhambini! Sasa two issues to be addressed here:-

  1. Ikiwa ni kweli kuwa Mungu Alimpa mwanadamu uhuru wa kuchagua mema na mabaya (sawa na wewe Baba/Mama unavyoweza kumpa uhuru mwanao aende Mzumbe Secondary au Ikinabushu Secondary), iweje tena Baba/Mama huyu huyu aanze kumtishia mwanaye kuwa "ukichagua kwenda Ikinabushu Secondary nitakufukuza kwangu tena na kukuchoma moto"? Iweje mtu anapo-exercise uhuru wake uliompatia wewe mwenyewe aonekane adui yako kisa tu hakuchagua vile ulivyotaka wewe? Je, katika viwango vya kibinadamu, huo kweli ni uhuru au ni udikteta zaidi ya ule wa Idd Amin Dada? Halafu tena, iweje mtoto wako ambaye amechagua kwenda Ikinabushu Secondary wewe mzazi uanze "njama"(maana humshirikishi) za kuandaa mpango wa kumuhamisha mara tu atakapokuwa amejiunga na Ikinabushu Secondary? Sasa hapo ulimpa achague kweli alichokitaka yeye mwenyewe au ulikuwa unamfanyia usanii tu? Na hata kama ulitaka asiende Ikinabushu Secondary kwa madai kuwa ni Shule ya Kata tena isiyo na vifaa wala walimu wazuri, kwa nini usisubirie hadi atakapoona madhara/matokeo ya uchaguzi wake huo iwapo tu ulifanya kazi ya kumshauri lakini hakusikia? Badala yake wewe Mzazi unayependa Mzumbe Secondary ndiye unayetoka huko uliko na kukurupuka kwenda kumuadhibu mwanao aliyeko Ikinabushu Secondary tena kwa mapenzi na utashi wake mwenyewe? Kwa nini usingemuacha tu na wewe ukabaki na chaguo lako, na iwapo una watoto wawili na bahati "nzuri kwako" mmoja amekukubalia chaguo lako (la kwenda Mzumbe Secondary) basi uwashindanishe wote wawili tena kwa usawa (pasipo upendeleo) kuliko kumtishia yule wa Ikinabushu kuwa atafeli, utamnyima ada, hela ya matumizi na hutakwenda kumsalimia huko shuleni na wala asije akarudi tena nyumbani kwako wakati wa likizo????????


  1. Back to Uniformity: Kama mwanadamu naye alikuwa mkamilifu, baadaye akaasi na mpango wa kumuokoa kutoka dhambini ukasukwa, sasa tuna uhakika gani kuwa mwanadamu yule yule atakayekuwa ameokolewa dhambini hataasi tena ktk paradise/akhera/mbingu/dunia ijayo? Kwa nini hapa usione kuwa kuna Non-uniformity katika plans za huyo Mungu wako? Iweje Duniani pa likuwa Patakatifu, Kisha Dhambi na Tunaambiwa Baadaye tena patakuwa Patakatifu lakini hatuelezwi kuwa yawezekana ikaja kuwa tena Dhambi na kufanya iwe Loop inayoonyesha hiyo Uniformity yako? Sasa Utakatifu >>> Dhambi >>> Utakatifu ndio hiyo Uniformity unayoizungumzia hapa? Na ni nini mpango wa Mungu endapo tena mwanadamu atakuja kuasi akifika huko mbinguni? Maana hapo mwanzo Mungu Alijua kuwa kiumbe wake mkamilifu angeasi, akajiandaa, lakini this time tunaambiwa kuwa huko mbinguni hakutakuwa na dhambi wala kifo tena (just as it was in the beginning) lakini hatuambiwi nini kitatokea endapo hali ikigeuka kuwa ndivyo sivyo! Au wanadamu watakaokuwepo kule hawatakuwa tena na uchaguzi wa kuamua njia waitakayo kama wale wa awali walivyopewa fursa hiyo? If that is the case, ina maana huyo Mungu atakuwa amewafunga watu wake wasiwe na any other choice except him? Na kama hivi ndivyo basi huyo Mungu hajiamini, ni dikteta wa hali ya juu na hajali athari za mabavu yake kwa watoto wake mwenyewe maana kama angelikuwa na upendo basi asingewanyima uhuru wao kama ule aliowapa hapo mwanzo!


  1. By the way, wewe (Mungu) ni Mwalimu wa Sanaa (Arts), unafundisha wanafunzi, kutunga mitihani, kusahihisha na mwisho kutoa matokeo. Sasa iweje tena wewe huyo huyo ulazimishe kutoa matokeo ya wanafunzi waliofanya somo la Hisabati ilhali halikuhusu, hukusomea, hukuwafundisha na wala hukutunga mtihani huo? Maana yangu ni kwamba, kwanini Mungu asi-deal na wale wanaofuata sheria zake tu (yaani awalinde, awatunze, awahudumie na hatimaye siku atakayoona inafaa awapeleke anakotaka yeye basi) na badala yake ana-cross over na kuwafuata wale wasiomuamini na kujifanya ndiye Jaji wao? Kwanini wale wasiomuamini (kwa maana nyingine ni wafuasi wa Mzee Mzima Shetani) asiwaache nao walindwe, watunzwe, wahudumiwe na hatimaye wapelekwe kule ambako Master wao atataka wawe halafu mwishoni ndio atoe ushuhuda kuwa "Niliwaambia hamkusikia, oneni jinsi uchaguzi wenu ulivyowagharimu"? Hayo ya Ngoswe yanamhusu nini yeye huyo Mungu wenu? Mbona huyo Kiongozi wa hilo kundi lingine (Shetani) yuko kimya tu, hajatangaza adhabu kwa wale wasiomtii (kama wewe unayejidai ni mfuasi wa Mungu)? Iweje huyu muungwana (Shetani) asiwe na noma kwenu nyie mnaokesha na kumtukana mchana na usiku kucha lakini kinyume chake huyo Mungu wenu mnayempamba ni mwenye haki na upendo atangaze shari kwa wasiomfuata? Yaani ni sawa na Kikwete (Rais wa Nchi na Watz wote + M/Kiti wa Magamba) atangaze kiama na majanga kwa watu wote wasio wafuasi wa Magamba lakini Dr. Slaa/Mbowe/Lipumba/Cheyo/Mrema/Mbatia/Mtikila/et al wao wabaki kimya wala hawawalalamikii watu ambao hawawaungi mkono/ni wafuasi wa Magamba, sasa kati ya pande hizi mbili ni upi unaoonekana kutenda haki na uungwana kwa standards za kibinadamu? Sasa iwapo kwa stabdards za kibinadamu imekuwa hivyo, habari gani kwa standards za huyo Mungu? Kwanini isiwe hivyo?????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


  1. Kwa hali ya kibinadamu, wanasema "wengi wape". Ninyi licha ya Shetani kutolalamika wala kuomba kutukuzwa kama vile Mungu wenu anavyotaka atukuzwe mchana na usiku kucha, lakini hata hivyo watu wengi (naamini na wewe ukiwemo) mnaimba mko kwa Mungu lakini matendo yenu hayana tofauti na ya Mzee Mzima Shetani! Hata huyo Yesu wenu aliwahi kukiri, kuwa vinywa vyenu vinaimba Mungu lakini miondoko na midundo ya matendo yenu ni ya Mzee mzima ambaye mnakesha mchana kutwa mkimpiga vijembe! Hii ina maana gani?????? Maana yake ni kwamba huyo Mungu wenu kimantiki hayupo maana kaweka vigezo vigumu sana vya kumfikia, na hata yeye mwenyewe anakiri kuwa njia yake ni nyembamba na waionao ni wachache! Yohana aliona idadi ya watakaourithi ufalme wa mbinguni ni mia moja arobaini na nne elfu tu! Sasa kati ya Watu zaidi ya 2 billion tuliopo, wateule ni sawa na asilimia 0.0072 tu! Anyway, sasa kama hivyo ndivyo itakavyokuwa, kwa nini nisiamini kuwa kitendo cha Mungu kuamua kuja kuchoma moto dunia hii (na wakati wa Nuhu kugharikisha dunia nzima) ni wivu tu baada ya Sera zake kukataliwa na watoto wake wa kuumba yeye mwenyewe? Kwanini isiwe hivyo iwapo hata kule mbinguni alivyotaka kupima ubavu na Lusifa Mzee Mzima alijinyakulia theluthi 1 ya malaika wote tena kwa mkupuo pasipo kufanya kampeni? BY LOGIC: Iwapo hao malaika na hata Lusifa mwenyewe aliyekuwepo kule mbinguni na akawa karibu sana na huyo Mungu waliasi, habari gani wewe Mnyalukolo mwenzangu ambaye hukuwahi hata kwenda juu ya haya mawingu tunayoyaona ujiaminishe kiasi hicho kuwa Mungu wako unayemtumainia ni mwenye upendo, huruma na msamaha? Hivi mwanao akikaidi ushauri wako na akaamua kufanya maamuzi yake anayoona ni sahihi kwake utamwadhibu au utamsikitikia na kumuonea huruma kwa kitakachompata? Sasa iweje kwa standards za Mungu JEHANAMU ndio iwe kusudio kwa wale watakaomkataa badala ya kuwahurumia, kuwasikitikia na ikiwezekana kuwaepushia majanga hayo????? Hivi bado tu hujaona mantiki hapa, au unaendelea kuimba na kukariri tu kama ambavyo wajanja fulani waliwataka muendelee kuamini hivyo milele? Unachekesha aiseee!!!!!!!!!!!


  1. MWISHO: Eti kuna Mungu au Shetani ni nadharia tu zisizo na mantiki wala mashiko yoyote katika viwango viwavyo vyovyote vile, hata iwe ni kwa kutumia akili ndogo kabisa za kibinadamu maana hata yasemwayo kuhusu hao wawili hayawezi kuthibitishwa pasipo kuacha chembe ya shaka! So, what for? Leave this Topic alone, don't waste your precious time at all!
 
the book that u so trust has a lot of inconsistency y would a rational person trust it??? even from early chapters lots of ambiguities!! kwa mfano wakat cain amemuua ndugu yake anafukuzwa akawa anamlalamikia mungu kua uko anakoenda anaogopa watu watamuua? swali ni kwamba nani hao watu anaowaogopa? kulikua na town ingine apart from eden? watu hao walitoka wapi? and funny enough uko alikoenda akapata na mke!!!

Sasa cheki nyingine hapa chini:Is Uniformity one of the keyelements to justify God's existence, siyo? Good, sasahapo mwanzo biblia yako inatuambia hakukuwa na dhambi. Mungu Aliumba viumbevyake vyote akiwemo Malaika Mkuu wake Lusifa a.k.a. Shetani wa leo akiwamkamilifu. Ila ghafla bin vuu bwana mkubwa huyu akaota kiburi nakutaka kujifananisha na Muumba wake! Is this what you refer to be uniformity,one of your poor proofs of God's existence? Okay, following the same trend,Mungu Alijua kuwa Ulimwengu aliouumba baadaye ungetumbukia dhambini, sasaakaandaa mpango mkubwa, mgumu, wa gharama kubwa na tena usiofikirika eti wakumkomboa mwanadamu kutoka dhambini! Sasa two issues to be addressed here:-1. Ikiwa ni kwelikuwa Mungu Alimpa mwanadamu uhuru wa kuchagua mema na mabaya (sawa na wewe Baba/Mamaunavyoweza kumpa uhuru mwanao aende Mzumbe Secondary au Ikinabushu Secondary),iweje tena Baba/Mama huyu huyu aanze kumtishia mwanaye kuwa "ukichagua kwendaIkinabushu Secondary nitakufukuza kwangu tena na kukuchoma moto"? Iweje mtuanapo-exercise uhuru wake uliompatia wewe mwenyewe aonekane adui yako kisa tuhakuchagua vile ulivyotaka wewe? Je, katika viwango vya kibinadamu, huo kwelini uhuru au ni udikteta zaidi ya ule wa Idd Amin Dada? Halafu tena, iweje mtotowako ambaye amechagua kwenda Ikinabushu Secondary wewe mzazi uanze "njama"(maanahumshirikishi) za kuandaa mpango wa kumuhamisha mara tu atakapokuwa amejiungana Ikinabushu Secondary? Sasa hapo ulimpa achague kweli alichokitaka yeyemwenyewe au ulikuwa unamfanyia usanii tu? Na hata kama ulitaka asiendeIkinabushu Secondary kwa madai kuwa ni Shule ya Kata tena isiyo na vifaa walawalimu wazuri, kwa nini usisubirie hadi atakapoona madhara/matokeo ya uchaguziwake huo iwapo tu ulifanya kazi ya kumshauri lakini hakusikia? Badala yake weweMzazi unayependa Mzumbe Secondary ndiye unayetoka huko uliko na kukurupuka kwendakumuadhibu mwanao aliyeko Ikinabushu Secondary tena kwa mapenzi na utashi wakemwenyewe? Kwa nini usingemuacha tu na wewe ukabaki na chaguo lako, na iwapo unawatoto wawili na bahati "nzuri kwako" mmoja amekukubalia chaguo lako (la kwendaMzumbe Secondary) basi uwashindanishe wote wawili tena kwa usawa (pasipoupendeleo) kuliko kumtishia yule wa Ikinabushu kuwa atafeli, utamnyima ada,hela ya matumizi na hutakwenda kumsalimia huko shuleni na wala asije akarudi tenanyumbani kwako wakati wa likizo???????? 2. Back to Uniformity: Kama mwanadamu nayealikuwa mkamilifu, baadaye akaasi na mpango wa kumuokoa kutoka dhambiniukasukwa, sasa tuna uhakika gani kuwa mwanadamu yule yule atakayekuwaameokolewa dhambini hataasi tena ktk paradise/akhera/mbingu/duniaijayo? Kwa nini hapa usione kuwa kuna Non-uniformity katika plans za huyo Munguwako? Iweje Duniani pa likuwa Patakatifu, Kisha Dhambi na Tunaambiwa Baadayetena patakuwa Patakatifu lakini hatuelezwi kuwa yawezekana ikaja kuwa tenaDhambi na kufanya iwe Loop inayoonyesha hiyo Uniformity yako? Sasa Utakatifu>>> Dhambi >>> Utakatifu ndio hiyo Uniformity unayoizungumziahapa? Na ni nini mpango wa Mungu endapo tena mwanadamu atakuja kuasi akifikahuko mbinguni? Maana hapo mwanzo Mungu Alijua kuwa kiumbe wake mkamilifuangeasi, akajiandaa, lakini this time tunaambiwa kuwa huko mbinguni hakutakuwana dhambi wala kifo tena (just as it was in the beginning) lakini hatuambiwinini kitatokea endapo hali ikigeuka kuwa ndivyo sivyo! Au wanadamuwatakaokuwepo kule hawatakuwa tena na uchaguzi wa kuamua njia waitakayo kamawale wa awali walivyopewa fursa hiyo? If that is the case, ina maana huyo Munguatakuwa amewafunga watu wake wasiwe na any other choice except him? Na kamahivi ndivyo basi huyo Mungu hajiamini, ni dikteta wa hali ya juu na hajaliathari za mabavu yake kwa watoto wake mwenyewe maana kama angelikuwa na upendobasi asingewanyima uhuru wao kama ule aliowapa hapo mwanzo! 3. By the way, wewe (Mungu) ni Mwalimu waSanaa (Arts), unafundisha wanafunzi, kutunga mitihani, kusahihisha na mwishokutoa matokeo. Sasa iweje tena wewe huyo huyo ulazimishe kutoa matokeo yawanafunzi waliofanya somo la Hisabati ilhali halikuhusu, hukusomea,hukuwafundisha na wala hukutunga mtihani huo? Maana yangu ni kwamba, kwaniniMungu asi-deal na wale wanaofuata sheria zake tu (yaani awalinde, awatunze,awahudumie na hatimaye siku atakayoona inafaa awapeleke anakotaka yeye basi) nabadala yake ana-cross over na kuwafuata wale wasiomuamini na kujifanya ndiyeJaji wao? Kwanini wale wasiomuamini (kwa maana nyingine ni wafuasi wa MzeeMzima Shetani) asiwaache nao walindwe, watunzwe, wahudumiwe na hatimayewapelekwe kule ambako Master wao atataka wawe halafu mwishoni ndio atoeushuhuda kuwa "Niliwaambia hamkusikia, oneni jinsi uchaguzi wenuulivyowagharimu"? Hayo ya Ngoswe yanamhusu nini yeye huyo Mungu wenu? Mbona huyoKiongozi wa hilo kundi lingine (Shetani) yuko kimya tu, hajatangaza adhabu kwawale wasiomtii (kama wewe unayejidai ni mfuasi wa Mungu)? Iweje huyu muungwana(Shetani) asiwe na noma kwenu nyie mnaokesha na kumtukana mchana na usiku kuchalakini kinyume chake huyo Mungu wenu mnayempamba ni mwenye haki na upendoatangaze shari kwa wasiomfuata? Yaani ni sawa na Kikwete (Rais wa Nchi na Watz wote + M/Kiti wa Magamba) atangazekiama na majanga kwa watu wote wasio wafuasi wa Magamba lakini Dr.Slaa/Mbowe/Lipumba/Cheyo/Mrema/Mbatia/Mtikila/et al wao wabaki kimya walahawawalalamikii watu ambao hawawaungi mkono/ni wafuasi wa Magamba, sasa kati yapande hizi mbili ni upi unaoonekana kutenda haki na uungwana kwa standards zakibinadamu? Sasa iwapo kwa stabdards za kibinadamu imekuwa hivyo, habari ganikwa standards za huyo Mungu? Kwanini isiwe hivyo?????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
4. Kwa hali yakibinadamu, wanasema "wengi wape". Ninyi licha ya Shetani kutolalamika walakuomba kutukuzwa kama vile Mungu wenu anavyotaka atukuzwe mchana na usikukucha, lakini hata hivyo watu wengi (naamini na wewe ukiwemo) mnaimba mko kwaMungu lakini matendo yenu hayana tofauti na ya Mzee Mzima Shetani! Hata huyoYesu wenu aliwahi kukiri, kuwa vinywa vyenu vinaimba Mungu lakini miondoko namidundo ya matendo yenu ni ya Mzee mzima ambaye mnakesha mchana kutwa mkimpigavijembe! Hii ina maana gani?????? Maana yake ni kwamba huyo Mungu wenukimantiki hayupo maana kaweka vigezo vigumu sana vya kumfikia, na hata yeyemwenyewe anakiri kuwa njia yake ni nyembamba na waionao ni wachache! Yohanaaliona idadi ya watakaourithi ufalme wa mbinguni ni mia moja arobaini na nne elfu tu! Sasa kati ya Watu zaidi ya 2billion tuliopo, wateule ni sawa na asilimia 0.0072 tu! Anyway, sasa kama hivyondivyo itakavyokuwa, kwa nini nisiamini kuwa kitendo cha Mungu kuamua kujakuchoma moto dunia hii (na wakati wa Nuhu kugharikisha dunia nzima) ni wivu tubaada ya Sera zake kukataliwa na watoto wake wa kuumba yeye mwenyewe? Kwaniniisiwe hivyo iwapo hata kule mbinguni alivyotaka kupima ubavu na Lusifa MzeeMzima alijinyakulia theluthi 1 ya malaika wote tena kwa mkupuo pasipo kufanyakampeni? BY LOGIC: Iwapo hao malaika na hata Lusifa mwenyewe aliyekuwepo kulembinguni na akawa karibu sana na huyo Mungu waliasi, habari gani wewe Mnyalukolo mwenzangu ambaye hukuwahi hatakwenda juu ya haya mawingu tunayoyaona ujiaminishe kiasi hicho kuwa Mungu wakounayemtumainia ni mwenye upendo, huruma na msamaha? Hivi mwanao akikaidiushauri wako na akaamua kufanya maamuzi yake anayoona ni sahihi kwakeutamwadhibu au utamsikitikia na kumuonea huruma kwa kitakachompata? Sasa iwejekwa standards za Mungu JEHANAMU ndio iwe kusudio kwa wale watakaomkataa badalaya kuwahurumia, kuwasikitikia na ikiwezekana kuwaepushia majanga hayo????? Hivibado tu hujaona mantiki hapa, au unaendelea kuimba na kukariri tu kama ambavyowajanja fulani waliwataka muendelee kuamini hivyo milele? Unachekeshaaiseee!!!!!!!!!!!
5. MWISHO: Eti kuna Mungu au Shetani ninadharia tu zisizo na mantiki wala mashiko yoyote katika viwango viwavyovyovyote vile, hata iwe ni kwa kutumia akili ndogo kabisa za kibinadamu maanahata yasemwayo kuhusu hao wawili hayawezi kuthibitishwa pasipo kuacha chembe yashaka! So, what for? Leave this Topic alone, don't waste your precious time atall!
 
.....Sheria iliyo juu ya wanadamu wote wewe mwanadamu utaijuaje? Na ukiijua kweli itakuwa juu ya wanadamu wote?

....
Hapa ndipo na mimi naungana na Mtoa mada kuwa kwa mujibu wa
tamko la dini yenu linalodai "Mungu hayupo" na nyinyi kukiri ni kinyume na hivyo ni kuikana imani yenu.

Naungana naye kwa sababu kitendo cha kutilia mashaka hata kile ambacho unaeleza kuwa kuna uwezekano kikawa kweli (rejea...Na ukiijua kweli itakuwa juu ya wanadamu wote?) inaonyesha jinsi gani umepofushwa na Tamko la dini yenu.

Maana kama utajua kweli kuna sheria iliyojuu ya wanadamu wote ...mashaka mengine yatatoka wapi ? vinginevyo unieleze pia kuwa imani yenu haotambui uwepo wa Ukweli na Uongo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom