Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Status
Not open for further replies.
Wakuu Eiyer, JingalaFalsafa na Mleta mada hii na wachangiaji wote wanaokubali uwepo wa Mungu, Hawa akina Kiranga na wenzake hawana jipya Zaidi ya kubisha kwa hoja zao zilezile!

Ambazo hazijapata majibu, zimepata ubabaishaji tu.
 
Kabla sijazungumzia chochote kuhusiana na maelezo yako ya ajabu hebu thibitisha kwanza hilo hapo

Unaweza kuwa hujanielewa
Yaani namaanisha utupe ushahidi wa hayo maneno yako hapo juu kuwa "complexity kubwa iliyoumba comlexity ndogo nayo ni lazima iumbwe"
Kisha utupe na njia uliyotumia kufikia hayo majibu yako
Maana inawezekana hata hujui unachoandika hapa!

Na ndipo tutajua mbwiga ni nani kati yako wewe na mkuu uliemquote!

Premise imeanza "kama complexity ni lazima iumbwe".

Unajua kusoma wewe?

Una kifaduro cha ubongo?
 
Kuna kujibu na kubabaisha.
Ukitoa jibu lisilo sahihi hujajibu.
Umebabaisha.

Unazidi kujiingiza kwenye kinyesi wewe
Umeleta ngonjera nyingine tena
Hebu niambie

Nimejibu
AU
Sijajibu
Au
Nimebabaisha?

Lakini pia kubabaisha na kutokujibu kwako ni sawa?
Halafu unasema ukitoa jibu lisilo sahihi hujajibu umeshasahau hii kauli yako?
Kwamba jibu lako si sahihi.
Hii kauli yako inathibitisha kuwa umeshapewa jibu
Few hours later unakana kupewa jibu
Soon you'll end up in the mental hospital
Halafu nani amekuambia jibu lisilo sahihi sio jibu ni nani[maana bora hata uwe umeambiwa maana kama umefikiri hivyo ni hatari zaidi]

Hukufundishwa tofauti ya kujibu na kujibu jibu lisilo sahihi?

Ni sawa uamuambie mwanao aweke mchanga kwenye gunia halafu akaweka mapumba ya mpunga
Kwako wewe mtoto huyo hajaweka kitu kwenye gunia!

Yaani hujui tofauti kati ya gunia lenye mapumba ya mchele na gunia lisilokuwa na kitu,kwako wewe kwakuwa uliagiza gunia liwekwe mchanga na likawekewa mapumba linabakia kuwa halina kitu!
Hii inaonesha vile ambavyo hujui hata unaandika nini!
 
Again, umepiga blaa blaa tu. Swali Kuu hapa ni: IWEJE MUNGU AACHILIE DHAMBI ITOKEE, THEN APANGE MPANGO MGUMU WA UKOMBOZI ULIOGHARIMU MAISHA YA MWANAYE WA PEKEE? UNAJUA SABABU HASA YA MUNGU KURUHUSU DHAMBI IINGIE? JE, KAMA ALIACHIA DHAMBI IINGIE, TUNA UHAKIKA GANI KUWA HAITAJIRUDIA TENA IWAPO NI MUNGU YULE YULE WA KALE, LEO NA HATA MILELE ZOTE? AU KABADILI MAWAZO NA MTAZAMO KUHUSU UHURU ALIOMPATIA MWANADAMU WA KWANZA? Au uhakika wako unaoutoa kwenye huo mkusanyiko wa novels mnaouita BIBLIA?

Swali la kwanini dhambi iwepo linatakiwa liulizwe na yule anaekubali uwepo wa Mungu

Wewe unaekana uwepo wake inabidi tukuulize ni kwanini unadhani kuna dhambi na ni kwa tafsiri ipi?
 
Kama complexity ni lazima iumbwe, complexity kubwa inayoumba complexity ndogo nayo ni lazima iumbwe.
Ok,
First thing first,unakubali kuwa binadamu aliumbwa ili tuanze safari nyingie ya kutafiti kama aliyemuumba binadamu nae kaumbwa?
 
Ni sawa na kusema kama wewe unabisha kuwa risasi haiui na mimi nasema inaua inabidi mimi niruhusu unirarue nayo ili tuone kama inaua ama la!
Funny,isn't it?

Kwanini utoke kwenye msimamo wako?
Unataka tufanye majadiliano kutokakwenye msimamo fake,kwanini?

Kama unasema Mungu hayupo halafu ukapose kama gnostic inamaana wewe ni kigeugeu na hujui kama hujui Mungu yupo ama la!

Kwanini "tuseme Mungu yupo"?
Kwanini tufanye majadiliano kwa kutumia assumption?
Sisi hapa atu-assume bali tunaamini yupo kama wewe UNAVYOAMINI hayupo!


Haya ni maswali ambayo anatakiwa aulize mtu ambae anaamini Mungu yupo sio anae-assume Mungu yupo
Maswali yako hayana maana kwakuwa una-assume tu!

Sisi hatusemi let x be,sisi tunasema x ni ......
Wewe ndio unasema let x be ....
Huoni kuwa tuko nchi mbili tofauti?
Tutajadilije jambo ambalo hata uwepo wake hatujakubaliana?

Nimeshakujibu hii

How do you "distinguish" bad from good?
Unatumia kipimo gani?

Sio kweli

Kwanini hupendi?

Kwanini unapenda?

Umekosa tafakuri wewe
Ukishasema jema tayari umeshamtaja Mungu
Au na hili hujui?

Kwahiyo "wakijadili" tayari wanakuwa wamemfanya Mungu kutokuwepo?
Huoni hata hapa tunajadili?
AAu kwa mimi kujadili morality inayothibitisha kuwepo kwa Mungu nakuwa nimemthibitisha tayari,right?

Halafu Moral ni nini?
Imetoka wapi?
Kwanini tunayo?

Hebu tuambie kwanza baya na jema ni nini ili tujadili kama tunaweza kujua kama Kuna ubaya na wema nje ya Mungu

Maana naona unarukia mambo tu!
Kiranga hujaona kama kuna maswali unayotakiwa kujibu hapo?
Au hakuna maswali?
 
Ok,
First thing first,unakubali kuwa binadamu aliumbwa ili tuanze safari nyingie ya kutafiti kama aliyemuumba binadamu nae kaumbwa?

Sikubali,

Ila katika kuonesha kwamba habari ya "binadamu ni lazima kaumbwa" haiko logical, natumia "immanent criticism".

Kwa kuwa nikisema "binadamu hajaumbwa" na wewe ukisema "binadamu kaumbwa" kutakuwa na stalemate, hatutafika popote.

Kwa hiyo nakubali "for the sake of argument" kusema "let's say binadamu kaumbwa kwa sababu kitu complex kama binadamu hakiwezi kutokea bila kuumbwa".

Key words are "suppose" "let's say".

Mtu anayesema "suppose" au "let's say" hajakubali. Huyu ni mtu anayekubali kufanya thought experiment na/au immanent critique.

Sasa ndio tunaendelea kutoka hapo.

Suppose complexity ni lazima iwe imeumbwa, haiwezi kutokea yenyewe.

If follows kwamba, as long as complexity ni lazima iumbwe, complexity ndogo haiwezi kuumbwa na complexity ndogo.

Kwa hiyo complexity ndogo ni lazima iumbwe na complexity kubwa.

Lakini tushaona kwamba complexity lazima iumbwe.

Kwa hiyo tukishasema tu kwamba "mwanadamu kaumbwa na mungu", tunaona kwamba mungu ni complex kuliko mwanadamu.

Kwa hiyo, sheria ile ile iliyotufanya tufikiri kwamba mwanadamu kaumbwa (kwa sababu yuko complex) itatutaka tufikiri kwamba mungu naye kaumbwa.

Kwa sababu uwezi kusema kwamba ni lazima complexity ndogo iwe imeumbwa, lakini complexity kubwa iweze kutokea bila kumbwa.

Huwezi kusema kiti ni lazima kiwe kimeumbwa, halafu ukasema Jumbo Jet linaweza kutokea tu.

Huwezi kusema binadamu ni lazima awe ameumbwa, halafu mungu hajaumbwa.

Kwa sababu sheria ile ile iliyokufanya uone binadamu ni lazima awe ameumbwa (kwa sababu ni complex) zitakutaka ulazimike kufikiri kwamba mungu naye ni lazima awe ameumbwa, tena haja ya mungu kuumbwa inakuwa kubwa zaidi.

Kwa sababu kama complexity ni lazima iumbwe, complexity kubwa zaidi ni lazima zaidi iwe imeumbwa.

The argument from design falls on its face due io it's logical absurdity.

Kwa sababu mungu atahitaji muumbaji wake, na muumbaji wake atahitaji muumbaji wake, ad infinitum, ad absurdum.
 
Mimi nasema hujaelewa ulichokiandika
Kama umeelewa thibitisha!

Wewe hata hujaelewa kama sijaelewa.

Kama ungeelewa usingeomba uthibitisho.

Hata hujaelewa kwamba sijaelewa kama sijaelewa.

Na hujaelewa tofauti ya kuelewa kwamba sijaelewa kama sijaelewa na kutoelewa kwamba sijaelewa kuwa nimeelewa.
 
Kabla sijazungumzia chochote kuhusiana na maelezo yako ya ajabu hebu thibitisha kwanza hilo hapo

Unaweza kuwa hujanielewa
Yaani namaanisha utupe ushahidi wa hayo maneno yako hapo juu kuwa "complexity kubwa iliyoumba comlexity ndogo nayo ni lazima iumbwe"
Kisha utupe na njia uliyotumia kufikia hayo majibu yako
Maana inawezekana hata hujui unachoandika hapa!

Na ndipo tutajua mbwiga ni nani kati yako wewe na mkuu uliemquote!
That follows from LOGIC, haiwezekani kitu rahisi kama kiberiti kitengenezwe halafu jitu kubwa na tata kama Air Bus / Boeing 747 iwe iliibuka tu from no where! Kama hadi hapa na kwa analogy hii simple kabis hutakuwa umeelewa basi sitakuwa na cha kukusaidia maana huenda hutaki tu kuelewa au huyo mungu wako hakufanikiwa kukupa akili yenye upeo mdogo tu wa kuelewa mambo marahisi kama hili! Hilo sasa halitakuwa kosa langu tena, you will need to consult your creator!
 
Swali la kwanini dhambi iwepo linatakiwa liulizwe na yule anaekubali uwepo wa Mungu

Wewe unaekana uwepo wake inabidi tukuulize ni kwanini unadhani kuna dhambi na ni kwa tafsiri ipi?

This is ridiculous, kwani nani aliyekuambia kuwa ili kujua JEMA na BAYA ni sharti ukubali kuna Mungu? Una uthibitisho wowote kuwa chanzo cha JEMA ni Mungu??????????? Ulete hapa huo ushahidi!
 
Wewe hata hujaelewa kama sijaelewa.
Kama ungeelewa usingeomba uthibitisho.
Hata hujaelewa kwamba sijaelewa kama sijaelewa.
Na hujaelewa tofauti ya kuelewa kwamba sijaelewa kama sijaelewa na kutoelewa kwamba sijaelewa kuwa nimeelewa.
Thibitisha hili na lile lingine

Hii mambo yako ya kuleta longolongo inaonesha hata hujui kithibitisha ni nini
Tutakesha hapa!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom