Uchaguzi 2020 Musoma: Tundu Lissu alala Butiama nyumbani kwa Mwalimu Nyerere

Uchaguzi 2020 Musoma: Tundu Lissu alala Butiama nyumbani kwa Mwalimu Nyerere

Waasisi wa taifa hili wapo pamoja na mkombozi Lisu.

Yale mafisadi na mauaji na matekaji mwisho wao ni October 28
 
Natumaini alitumia nafasi hio kuomba msamaha kwa kejeli na dharau alizokua anazitoa kuhusu mwalimu Nyerere.

Kuna familia zina moyo wa kusamehe
Wanasiasa hawa sio wa kuwatilia sana maanani wanayopayuka majukwaani.
 
Nakumbuka wakati muhula wa kwanza wa serikali ya awamu ya pili ya JK, KUB alikua Hamad Rashid Mohamed wa CUF. Siku ya Alhamisi ambayo ni siku ya maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, KUB alikua akipata kifungua kinywa nyumbani kwa PM na wakiondoka wote kwenda Bungeni.

Utamaduni huu umekomeshwa kikatili sana. Sasa hivi sio tu dhambi kumtembelea mtu mnae tofautiana itikadi za chama bali pia ni dhambi kumjulia hali mgonjwa hospitakini kama si wa chama chako! Na tunapoelekea hata kuzikana watu wa vyama tofauti itakua ni kosa la kimaadili la kuadhibiwa na chama. Nani katufikisha huku? Tusikubali.
Jiwe
 
Wakuu,

Tundu Lissu Siku ya Kuamkia leo alilala nyumbani kwa baba wa taifa Mwalimu Nyerere baada ya kuombwa na watoto wa Baba wa Taifa.

Watoto hao walijisikia furaha kubwa mno kupata ugeni mzito huo ambao wamesema hawajawahi kupata mgeni wa kulala kwao mkubwa kama Lissu na walijisikia kama wako na Baba yao Mzazi.,

Mmoja wa watoto hao Madaraka Nyerere amesema kuwa hawakuamini kama Lissu angewakubalia ombi lao hilo.

Kwenye Ukurasa wake wa Twitter, Tundu Lissu ameandika "In Mara we'd the honour of spending the night at Mwitongo, the birthplace & resting place of Mwl. J. K. Nyerere. We're privileged to be hosted by Madaraka, one of Mwalimu's sons, his sister Neema & her husband Carlo Giero both of whom treated us to a sumptuous dinner & breakfast."

View attachment 1582402View attachment 1582403View attachment 1582404View attachment 1582405
Bora Lisu kaenda kuwafariji maana wametengwa na maccm.
Kiufupi mwl angekuwa hai angefurahi pia maana alikuwa anapenda vijana wakosoaji kwa hoja Kama Lisu sio mambo ya kuabudiana
 
Wakuu,

Tundu Lissu Siku ya Kuamkia leo alilala nyumbani kwa baba wa taifa Mwalimu Nyerere baada ya kuombwa na watoto wa Baba wa Taifa.

Watoto hao walijisikia furaha kubwa mno kupata ugeni mzito huo ambao wamesema hawajawahi kupata mgeni wa kulala kwao mkubwa kama Lissu na walijisikia kama wako na Baba yao Mzazi.,

Mmoja wa watoto hao Madaraka Nyerere amesema kuwa hawakuamini kama Lissu angewakubalia ombi lao hilo.

Kwenye Ukurasa wake wa Twitter, Tundu Lissu ameandika "In Mara we'd the honour of spending the night at Mwitongo, the birthplace & resting place of Mwl. J. K. Nyerere. We're privileged to be hosted by Madaraka, one of Mwalimu's sons, his sister Neema & her husband Carlo Giero both of whom treated us to a sumptuous dinner & breakfast."

View attachment 1582402View attachment 1582403View attachment 1582404View attachment 1582405
Kifupi kulala bila kuomba msamaha mzimu wa Nyerere kwa Matusi ambayo Lisu alitukana Nyerere hakusaidii kitu laana ya Nyerere itamuanndama pili kupinga vitu ambavyo Nyerere alianzisha ikiwemo muungano huubuliopo na kuwa na taifa moja lisilo na majimbo haimsaidii hata alale kitanda alicholala Nyerere
Tatu kuona Lugha ya mkoloni mwingereza ndio muhimu kuliko kiswahili tofauti na Nyerere alivyosisitiza kuwa kama taifa tunabidi tujivunie lugha yetu yeye anaiponda haimusaidii hata angelala kitanda Nyerere alilala na Maria Nyerere au hata akilala kaburini alikozikwa Nyerere

NNE kuweka rehani madini kwa Mabeberu wakopeshaji Nyerere aligoma OK kalala ili apate Selfie!!! Ruksa.Nampongeza kwa Selfie!!

Amemkumbuka Nyerere kama mkumbuka shuka wakati kumekucha hakutakiwa kumponda Nyerere wala vitu vyake kama alikuwa na mpango wa kugombea uraisi

Ndio maana CCM tunasema wazi Lisu hakujiandaa kugombea uraisi .
 
Magufuli atakapotolewa madarani tutasikia mengi sana:

1. Watu hasa wana CCM watanena walivyozuiwa kuchangana na wapinzani.

2. Wataeleza nani alimpiga Lissu risasi

3. Wataeleza jinsi walivyopewa maelekezo kuwaengua wapinzani

Kea ujumla atafananisha na IDD AMINI DADA
Hapa unamzidishia hasira! Na kwa sababu hiyo, atalazimisha atangazwe yeye ndiye mshindi, hata kama amepata 36%. Na ndizo anazotegemewa kupata, ili aepuke hiyo HUKUMU!
 
Natumaini alitumia nafasi hio kuomba msamaha kwa kejeli na dharau alizokua anazitoa kuhusu mwalimu Nyerere.
Hiyo inaitwa kukumbuka shuka kujifunika wakati kumekucha haimusaidii kamtukana sana Nyerere Lisu mzimu wa Nyerere utahakikisha hashindi
 
Jiwe kafura kanuna kanyong'onyea,kalegea tepetepe baada ya kusikia watoto wa mwalimu wamemuomba Lissu akalale kwao,wakati Jiwe alimforce bi mkubwa wa taifa aende pale mkendo akaongeze idadi ya vichwa.
Kuna mambo unafanya binadamu unatakiwa ujiulize athari zake baadae. Huwezi kumburura kizee kile kikufate walitakiwa wamfate yeye na kama kuna neno la kusema basi walikuwa wamrikodi au wamtayarishie waandishi wamchukuwe mubashara akiwa nyumbani kwake! Jamaa wamejaa kiburi kiasi cha kuwapiga teke watoto wawili wa baba wa Taifa. Lakini hawara zao, wapwa zao, JK x3, Mwinyi×4, Pinda, Ditopile, Makamba hao wote wamepita lakini wa Baba wa Taifa wanalaumiwa wajumbe!
 
Hapo ni mwitongo Lodge sio nyumbani kwa nyerere, hiyo hotel inamilikiwa na madaraka na neema,

..Mwalimu Nyerere angekuwa hai asingefurahi unyama aliotendewa Tundu Lissu.
 
Back
Top Bottom