Musukuma: Maprofesa wanatuchanganya; wakati wa Magufuli walisema hakuna Corona na wakati huu wa Samia wanasema tuchanjwe

Musukuma: Maprofesa wanatuchanganya; wakati wa Magufuli walisema hakuna Corona na wakati huu wa Samia wanasema tuchanjwe

Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
Kama kweli aliamini hivyo mbona alikuwa mbele kupiga na kufagilia nyungu...!!
 
Ule haukuwa utafiti kuwa Tanzania hakuna korona, isipokuwa ulikuwa utafiti kuwa korona hata kwenye mapapai inaonekana. (Labda mchato alitaka kuiaminisha dunia kuwa corona is a Hoax)
Mkuu, leta basi matokeo ya utafiti kwamba Tanzania kuna korona
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
Waziri wa afya, Katibu MKUU WA wizara ya afya, mganga Mkuu wa serikali, wote ni jirani zako . Waulize hayo maswali. Ila chato wanawalaumu sana.
 
Form seven ni Shida, yaani yeye anadhani kipindi cha utawala ULE yale maamuzi ya kupinga na Kuficha kuwa Corona haikuwepo yanaweza ku-hold water kwa kiongozi wa sasa mwenye Maono (uongozi sikivu). Hivi ni kweli huyo form Seven hajui hasara ya kupoteza wapendwa wetu kwa Maamuzi ya ajabu ajabu. Mimi Ilikuja kunizidishia machungu na niliuchukia utawala ule zaidi tena Zaidi pale tu Dada yangu Daktari alipofariki kwa corona and was the only Dr in our family. Baba alikuwa anatuambia alimsomesha kwa gharama kubwa. Tumwombe tu huyo form seven hasiturudishe matesoni,kwani maamuzi ya uongozi wa sasa kuhusu Corona (task force ya kumshauri SSH kuhusu Corona) ni sahihi na yaheshimiwe. Anachojifanya hajui ni kuwa, Watawala uliopita Ulikuwa unaogopwa, ulikuwa utawala wa YES BOSS or ONE MAN SHOW kila alichokisema mtawala ndicho wasaidizi wake walikitenda na kutuaminisha kuwa tuko sahihi ili mradi tu Maisha na familia zao vilineemeka na utawala ule.
hujamuelewa msukuma-anahosema kwa nini prof A anatoa jib tofauti na prof b
 
Mkuu, leta basi matokeo ya utafiti kwamba Tanzania kuna korona
Utafiti mwepesii kabisa ambao hata mtoto anaukubali ni kuona vifo sababu ya korona. Sasa nikuulize wewe, Tanzania hakuna mtu hata mmoja aliyekufa na korona?
 
Acha uongo kwahyo yale mapapai ni ww uliyafanyia utafiti?
Haukua utafiti wa kujua kama kuna korona.

Alikua amefanya vile ili kujua kama majibu wanayotoa maabara ni halisi siyo ya kupikwa.
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
Huyu muheshimiwa Msukuma yaani kila anapotoa hoja haachi kabisa kuwadhihaki wana taaluma sijui kana kwamba walimkosea nini au wao ndio walikuwa namemzuia asisome?

Hakuna Professor hata mmoja aliyesema hakuna korona na wala hakuna Daktari yoyote aliyesema hayo kwanza hakukuwa na platform ya kufanya hivyo.

Ushauri tuu kwa Msukuma basi huna budi kupeleka watoto shule
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
amuulize Dr Ndungulile kilichompata
 
Hii nchi imepitia mengi Sana[emoji848]
IMG_20210517_174844.jpg
 
Maprofesa sampuli ya Muongo, na yule Wa kafu aliyetengua barua unaweza kutegemea nini kutoka kwao? Wanaangalia upepo ubwabwa unatokea wapi? Huko huko wanapiga pambio!! Hata hao maprofesa wa tiba upepo ulishabadilika!! SAA hii wanavalia kininja ni mwendo wa kufunika pua na midomo kama hawana akili nzuri! Wabongo kwa unafiki!! Ikitokea ( najua haiwezekani) JPM akafufuka na kurudi kwenye kiti chake na mama kurudi kwenye kiti chake cha awali, hao wanaosemà less government watapiga pambio za more government!! Na barakoa hutakaa uione imetorokea wapi!! halafu watu ni wàle wàle!! Wabongo kwa unafiki!!
 
Hahahaaaa...... Msukuma ni la 7 lakini anaongoza kwa kujenga hoja mwanana bungeni!
Musukuma kajenga hoja nzuri sana ila kuna watu watampinga lakini ukweli uko palepale-maprofesa ao hao walisema hakuna corona Tanzania lakini pia wakaenda mbali kwa kusema hata vifaa vya kupimia vinanganya ndio maana mbuzi, fenesi na mapapai yalipatikana na korona hivyo huo ni uzushi mtupu ila leo wamebadili gia angani wanasema korona ipo na chanjo inahitajika.
Kwa hili namuunga mkono Musukuma.
 
Wataalam wetu hawana jipya zaidi ya copy and paste.Msukuma yupo sawa waje na chanjo ya kitanzania na siyo kutusomea vitu walivyoandikiwa.
 
WANAFIKI wanataka kujitoa sasa kwenye legacy.😂😂
Huyo msukuma ni mpumbavu sana, kama aliamini kua Corona haipo wakati wa Mwendawazimu mwenzie, imekuaje nayale MANYUNGU aliokua anajifukiza.
MaCCM ni hovyo kabisa
 
Chanjo ya corona ni ufisadi tu. wakowapi wanaoumwa korona Tanzania? Kama korona inawafuta wavaa barakoa hao wa high profile ambao wakati Hayati yupo walikuwa hawavai na wala hawakufa, basi wachanjwe wao. Yawezekana virusi vinaambatana na mawazo ya kiutawala utawala na ndiyo maana hata chanjo inagusa hadi DNA na RNA ili pengine iwaondolee hisia za utawala ili corona wasiwafuate.

Sisi tusio viongozi hatuna korona na hatuvai mabakkoa na hiyo korona haijatufuata, watuache.

Si rahisi kuelewa mpangi huu ni ufisadi wa aina gani.
Usiseme "sisi", sema wewe, usiwapangie wengine
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
Uzuri maprofesa wote waliofanya utafiti ni makada wa ccm
 
Msukuma ana ugomvi mkubwa sana na wasomi sijui kwanini.

Na anageuza habari! Hao maprofesa wakati wa JPM ni lini walifanya utafiti wakagundua Tanzania hakuna korona? Hakukuwa utafiti wowote isipokuwa kulikuwa na matamko kuwa Tanzania hakuna korona
Usimlaani sana, anayo sababu. Kuna kitu kinaitwa REDET pale UD, Mlimani, Chuo kikuu. Kilianzishwa na huyo anayejiita Profesa Mkandara. Kila leo REDET ikawa ni kusema uongo tu! Leo hii bado anaaminika hadi kupewa kuzungumzia mambo ya kitaifa. Aibu tu!
 
Back
Top Bottom