Musukuma: Maprofesa wanatuchanganya; wakati wa Magufuli walisema hakuna Corona na wakati huu wa Samia wanasema tuchanjwe

Musukuma: Maprofesa wanatuchanganya; wakati wa Magufuli walisema hakuna Corona na wakati huu wa Samia wanasema tuchanjwe

Muda mwingine bora msomi aliyeishia darasa la saba kuliko hao Maprofesa wanaoendeshwa na matumbo yao!
(Kusoma sana sio kuwa na akili)
Ni kauli za walioshindwa kuendelea kusoma. Msomi ni msomi tu, mfumo wa kumfanya mwanasiasa awe juu ya mwanataaluma ndio unaowafanya walazimishwe kutoka nje ya weledi wao
 
Form seven ni Shida, yaani yeye anadhani kipindi cha utawala ULE yale maamuzi ya kupinga na Kuficha kuwa Corona haikuwepo yanaweza ku-hold water kwa kiongozi wa sasa mwenye Maono (uongozi sikivu). Hivi ni kweli huyo form Seven hajui hasara ya kupoteza wapendwa wetu kwa Maamuzi ya ajabu ajabu. Mimi Ilikuja kunizidishia machungu na niliuchukia utawala ule zaidi tena Zaidi pale tu Dada yangu Daktari alipofariki kwa corona and was the only Dr in our family. Baba alikuwa anatuambia alimsomesha kwa gharama kubwa. Tumwombe tu huyo form seven hasiturudishe matesoni,kwani maamuzi ya uongozi wa sasa kuhusu Corona (task force ya kumshauri SSH kuhusu Corona) ni sahihi na yaheshimiwe. Anachojifanya hajui ni kuwa, Watawala uliopita Ulikuwa unaogopwa, ulikuwa utawala wa YES BOSS or ONE MAN SHOW kila alichokisema mtawala ndicho wasaidizi wake walikitenda na kutuaminisha kuwa tuko sahihi ili mradi tu Maisha na familia zao vilineemeka na utawala ule.
Kwahiyo sasa hivi kimefanyika kuhusu na corona?
 
Ule wa mapapai ulikuwa ni nini bwashee?
Ulifanyika maabara ya Chato.
Ukiwaambia watu waliopoteza wapendwa wao kwamba Tanzania haijawahi kuwa na Corona kwa sababu ya vipimo vya mapapai alivyotangaza yule kiongozi mwongo kuwahi kutokea nchini watakupiga mawe. Bora hata Nyerere alikuwa anaangalia TV peke yake usiku, asubuhi anatutangazia yatakayotokea nje ya nchi na jioni tunatangaziwa BBC tunamwona mnajimu.
 
Mbunge wa Geita vijijini mh Joseph Kasheku aka Msukuma amesema maprofesa wa Tanzania wanafeli sana na hii inasikitisha ndio maana aliwaripua bungeni.

Msukuma amesema kwa mfano tafiti za Corona zilizofanywa na maprofesa wakati wa hayati Magufuli wakitumia mapapai mbuzi, sungura, mafenesi na oil ilionyesha Tanzania hakuna Corona lakini alipoingia Rais Samia maprofesa walewale wameshauri tuanze kuchomwa " masindano" na kuvaa mabarakoa.

Msukuma anajiuliza hawa maprofesa wetu wamesoma kweli?

Msukuma amemshauri Rais Samia kutumia wanasayansi wa nje kama anaona hawa wa kwetu wamejaa longo longo.

Chanzo: Clouds Digital
Kwa mara ya kwanza kabisa leo namuunga mkono huyu #teamla7
 
Msukuma ana ugomvi mkubwa sana na wasomi sijui kwanini.

Na anageuza habari! Hao maprofesa wakati wa JPM ni lini walifanya utafiti wakagundua Tanzania hakuna korona? Hakukuwa utafiti wowote isipokuwa kulikuwa na matamko kuwa Tanzania hakuna korona
Hata sasa hao Maprofesa hawajafanya utafiti zaidi ya kuja na mapendekezo tu.
 
Yeye kipindi cha mwendazake akili aliipeleka wapi?

Juzi kati hapa si kasema watu walinyang'anywa viwanda kimakosa?
Enzo hizi lazima akili zimrudi,na hao aliowakandia wakati fulani nizamu yao kumburuza,awe mpole kutesa kwa zamu.
 
Muda mwingine bora msomi aliyeishia darasa la saba kuliko hao Maprofesa wanaoendeshwa na matumbo yao!
(Kusoma sana sio kuwa na akili)
Endelea kujifariji,pia kumbuka hayo yananafasi kwa mazingira ya Tz na zaidi Afrika
 
Ule wa mapapai ulikuwa ni nini bwashee?
Ule haukufanywa na ma Professa ulifanywa na Magu mwenyewe, alikusanya zile sample akazipa majina ya uongo na kupeleka maabara ya taifa, majibu yakaja positive, ndio yeye mwenyewe akapinga...wala hakuna Profesa aliyefanya vile....pengine Kabu..
 
Ule haukuwa utafiti kuwa Tanzania hakuna korona, isipokuwa ulikuwa utafiti kuwa korona hata kwenye mapapai inaonekana. (Labda mchato alitaka kuiaminisha dunia kuwa corona is a Hoax)
Ule utafiti ulikuwa unahusu utata wa vipimo vya corona.
 
Musukuma kajenga hoja nzuri sana ila kuna watu watampinga lakini ukweli uko palepale-maprofesa ao hao walisema hakuna corona Tanzania lakini pia wakaenda mbali kwa kusema hata vifaa vya kupimia vinanganya ndio maana mbuzi, fenesi na mapapai yalipatikana na korona hivyo huo ni uzushi mtupu ila leo wamebadili gia angani wanasema korona ipo na chanjo inahitajika.
Kwa hili namuunga mkono Musukuma.
Msiwalishe maneno ma Profesa, aliyesema hivi ni Hayati Magu...maprofesa walikaa kimya hawakusema...
 
Msiwalishe maneno ma Profesa, aliyesema hivi ni Hayati Magu...maprofesa walikaa kimya hawakusema...
Magu alisema kutokana na waliyoyasema matokeo ya utafiti uliofanywa na wachunguzi/maprofesa/doctors na wanausalama aliowatuma
 
Wameambiwa na Rais Samia kuwa ni ruksa kuikosoa serikali.sasa Msukuma alitakiwa tu ajiulize wakati wa magufuli kwanini haikusa ruksa kuikosoa serikali?
 
Form seven ni Shida, yaani yeye anadhani kipindi cha utawala ULE yale maamuzi ya kupinga na Kuficha kuwa Corona haikuwepo yanaweza ku-hold water kwa kiongozi wa sasa mwenye Maono (uongozi sikivu). Hivi ni kweli huyo form Seven hajui hasara ya kupoteza wapendwa wetu kwa Maamuzi ya ajabu ajabu. Mimi Ilikuja kunizidishia machungu na niliuchukia utawala ule zaidi tena Zaidi pale tu Dada yangu Daktari alipofariki kwa corona and was the only Dr in our family. Baba alikuwa anatuambia alimsomesha kwa gharama kubwa. Tumwombe tu huyo form seven hasiturudishe matesoni,kwani maamuzi ya uongozi wa sasa kuhusu Corona (task force ya kumshauri SSH kuhusu Corona) ni sahihi na yaheshimiwe. Anachojifanya hajui ni kuwa, Watawala uliopita Ulikuwa unaogopwa, ulikuwa utawala wa YES BOSS or ONE MAN SHOW kila alichokisema mtawala ndicho wasaidizi wake walikitenda na kutuaminisha kuwa tuko sahihi ili mradi tu Maisha na familia zao vilineemeka na utawala ule.
Yeye si alikuwa anapiga nyugu alikuwa anajikinga na nini kwani ? Aendelee na uganga wake wa kienyeji awaache wataalamu wavae barakoa na chanjo
 
Wameambiwa na Rais Samia kuwa ni ruksa kuikosoa serikali.sasa Msukuma alitakiwa tu ajiulize wakati wa magufuli kwanini haikusa ruksa kuikosoa serikali?
Kwani walikatazwa, mbona Bashe alikuwa anakosoa?
 
Back
Top Bottom