Musukuma: SGR inawahudumu kama Ndege, tutapata hasara waondolewe

Musukuma: SGR inawahudumu kama Ndege, tutapata hasara waondolewe

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku Musukuma amesema haina haja ya kuweka wahudumu wanaotoa huduma za ndani ya treni ya Mwendokasi (SGR) ili kuepuka shirika kupata hasara kwakuwa ndio kwanza mradi huo umeaanza hivyo haina haja ya kuweka gharama kubwa za uendeshaji.

"Hakuna haja ya kuwa na wahudumu wanaopita kuuliza abiria kama wanakunywa chai au kahawa. Treni inapaswa kuwa na behewa rasmi la chakula, kama ilivyo kwenye huduma za kimataifa, ambapo abiria ana uhuru wa kwenda kununua chakula au kinywaji bila kusubiri kuulizwa."

Mbunge Musukuma ameyasema hayo leo Februari 03, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya Kamati za Kudumu za Bunge za Miundombinu na Nishati na Madini

 
Usafirishaji na customer care ni biashara
Achana nae tumvumilie
 
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma, ameikosoa mifumo ya huduma katika reli ya kisasa (SGR), akipendekeza kuondolewa kwa wahudumu wa ndani ya treni kwa sababu huduma wanazotoa hazina umuhimu wa msingi. Akizungumza bungeni, Musukuma alieleza kuwa badala ya kuwa na wahudumu wanaopita kuuliza abiria kama wanahitaji chai au vinywaji, SGR inapaswa kuwa na behewa maalum la huduma za chakula na vinywaji, ambako abiria wanaweza kwenda kujipatia wanachohitaji bila usumbufu.
 

Attachments

  • musukuma.mp4
    53.8 MB
Katika takataka ambazo huwa azieleweki kama zina jisaidia haja gani ni huyu jina la kabila lake ukiondoa erufi za mwanzoni mbili unapata kiungo cha uzazi.
Umezingua sana,unayemsema vibaya hivyo,ukute akili zake ndo zimemfanya hadi kapata mali alizonazo na si ajabu anakuzidi maarifa ya utafutaji pesa.
 
Kwa hiyo wanazidiwa hata na MV - KILINDONI, utoaji huduma za ndani ya chombo 🤔🤔??
 
Aliyeshiba hamjui mwenye njaa gharama zipo kwenye SGR tu na siyo kule walikojaza wabunge wa viti maalum wasio na kazi yoyote au kujaza wakuu wa mikoa. Wilaya na Wakurugenzi hiyo siyo gharama
Kote huko kufanyike REVIEW ya ki-Trumptrump...
 
Mwambie hata ATCL inawafanyakazi kibao na kila siku inaajiri, idadi ya wabunge nayo ni kubwa sana kama ilivyo idadi ya mawaziri pia.
 
Hawa ndo watunga sera za nchi na kutunga sheria,hakika waafrika tunapaswa kujitafakari kuhusu tabia zetu.
 
Back
Top Bottom